Nina Mil.10 Nikianza ujenzi wa nyumba itafika wapi??

Nina Mil.10 Nikianza ujenzi wa nyumba itafika wapi??

Ungeweka ramani ya nyumba yako wadau humu watakushauri vizuri zaidi.
Hapo umenena mkuu, kwa maana Thamani ya Nyumba wakati mwingine inategemea na aina ya Nyumba unayotaka kujenga, ya kisasa au Nyumba yenye vyumba tu, je unataka vyumba au sebure zenye ukubwa gani, unataka kupaua au finishing ya aina gani? Hayo maswali yakipata majibu ndipo unaweza kufanya tathimini nzuri zaidi.
 
yuko poa sana mkuu, sema tu inategemea anaongea akiwa jukwaa gani, huwa unamsikia akiwa siasani nini, teh teh teh!!
Labda kama akiwa huku huwa anabadilika, lakini akiwa kule siasani anajitoa akili kabisa na anatema pumba za kutosha.
 
Tuko busy na mambo ya mtwara tutarudi baadaye bana..lakini usijenge nyumba njoo tulewee hiyo hela nyumba kitu gani
 
Hapo umenena mkuu, kwa maana Thamani ya Nyumba wakati mwingine inategemea na aina ya Nyumba unayotaka kujenga, ya kisasa au Nyumba yenye vyumba tu, je unataka vyumba au sebure zenye ukubwa gani, unataka kupaua au finishing ya aina gani? Hayo maswali yakipata majibu ndipo unaweza kufanya tathimini nzuri zaidi.
Ni kweli kabisa mkuu, kwani lengo langu lilikuwa hilo hilo.
 
Labda kama akiwa huku huwa anabadilika, lakini akiwa kule siasani anajitoa akili kabisa na anatema pumba za kutosha.

hiyo kwa red inawahusu karibia wote kule siasani (si ccm wala chadema), wote wanatetea itikadi zao na hiyo per day (sijui elfu 7) yao wanayolipwa. Baada ya kugundua hilo nimeamua kuwa msomaji tu manake mi sina chama, so siwezi kuegemea upande wo wote ule.

Loh, hapa tuna-dilute thread ya watu mkuu
 
Itafika mpaka level ya lenta kabla ya kuezeka. Hii ni iwapo hautacomplicate msingi. Ukicomplicate itaishia kwenye msingi tu.

acha kudanganya japo hali ya uchumi si nzuri Tz haiwezi kuwa hivyo
 
Mkuu inategemea ukubwa wa nyumba, vyumba na ubora wake. Kuna nyumba ya rafiki yangu nilikuwa naangalia juzi, msingi peke yake umegharimu kama milioni 5, kwa kuwa kiwanja kipo kwenye eneo lenye undongo wa mfinyanzi. Ukiangalia matofali unaona matofali yameshiba kweli, sio yale ya kupukutika ambayo ukijenga leo baada ya miaka kumi yanaanza kupukutika,

Kwa hiyo kimsingi milioni 10 inaweza kutosha kama unataka kujenga nyumba ya mbavu za mbwa, milioni 10 inaweza kutosha nyumba mbili, lakini kama ni nyumba ya kisasa ya karne hii, milioni 10 bado hela ndogo, inaweza kukujengea nyumba nzuri ndogo kwa asilimia 30 au 40 hivi.

Asante sana Mkuu, nahitaji nyumba yangu iwe standard na isiwe mbavu za mbwa, ila nitajikuna ninapofikia
 
Habari wa JF , naomba msaada wa kimawazo na ushauri, Nina Mil.10 ninaplan ya kujenga nyumba yenye vyumba 3,

Je kwa hiyo pesa nyumba yangu itaishia wapi?

Kwa wenye uzoefu wa mambo ya ujenzi tafadhari....

Jenga mkuu, kama kama kiwanja chako kiko kwenye eneo la flat na la kichanga ambalo sio mfinyazi basi kwa kifupingharama zako zitakuwa hivi

Msingi: tofali 500 x 1200tsh= 600000/= msingi wako utakwa wa tofali tano (height)
Cement: msingi 15x17000= 255000
Nondo za mkanda (10 mm) 15x15000=225000
Cement za mkanda 15x 17000 = 255000
binding wire, mbao, misumari, ring, maji na dharura: 500,000/=
Kokoto unanunua mende moja 300000, kokoto zitabakia mingi za kuwekea mkanda wa juu rental
mchanga mende moja 300000
JUMLA YA MSINGI BILA HELA YA FUNDI = 2,455,000/=

Boma: Tofali 1040 x 1200= 1,248,000
Cement 20x 17000= 340000
Mchanga mende2 =600000
Maji na mengineyo= 500,000
JUMLA YA BOMA BILA HELA YA FUNDI = 2,688,000

Mkanda wa juu, hapo inakuwa ni nafuu kidogo kwani mbao utakuwa nazo, kokoto zitakuwepo, mchanga utakuwepo na size yake itakuwa ndogo kwani tofali zitakuwa za wima na gharama yake itakuwa hivi
Nondo (mm10) 15x 15000= 225000
cement za mkanda 15x 17000= 255000
Binding wire, ringi, misumali, mbao za sahani, maji na dharura=500000
JUMLA JUMLA YA MKANDA WA JUU BILA FUNDI = 980000

JUMLA KUU BILA FUNDI = 6,123,000/=
KIFUSI CHA KUJAZA NDANI NA KAZI ZA DHARURA= 2,000,000/
FUNDI MAKUBALIANO LAKINI ISIZIDI = 2,000,000

JUMLA YA MWISHO 10,123,000/=

mimi sio fundi ila nina uzoefu sana wa ujenzi hasa wa Dar,
hiyo gharama imezingatia kuwa , kiwanja chako kiko tambarare, na ground ni ya kichanga au udongo unaofanan na kichanga sio mfinyanzi
pia hesabu hiyo itapatikana tu ikiwa kila kitu unanunua mwenyewe na wewe ndio msimamizi mkuu wa show nzima
 
acha kudanganya japo hali ya uchumi si nzuri Tz haiwezi kuwa hivyo

Kuna watu mnapenda kila kitu kubishana. Hayo mambo ya jukwaa la siasa. Hili ni jujkwaa lingine. Haya majukwaa yana maana yake.


Unachotakiwa kusema kama unaona nilichosema mimi si sahihi ni wewe kutoa makadirio unayoona sahihi.

Kulingana na uzoefu wangu wa kujenga Dar es Salaam nyumba kadhaa nina uhakika kuwa iwapo msingi hautakuwa complicated na iwapo mdau atasimamia asiibiwe na mafudi, basi pesa hiyo inafikisha lenta kwa nyumba aliyotaja.

Kunä mdau Kituko ameenda mbali zaidi na kupiga mahesabu hatua kwa hatua. Yaangalie mahesabu yake halafu uonyeshe kama kuna kasoro.
 
Last edited by a moderator:
Kuna watu mnapenda kila kitu kubishana. Hayo mambo ya jukwaa la siasa. Hili ni jujkwaa lingine. Haya majukwaa yana maana yake.


Unachotakiwa kusema kama unaona nilichosema mimi si sahihi ni wewe kutoa makadirio unayoona sahihi.

Kulingana na uzoefu wangu wa kujenga Dar es Salaam nyumba kadhaa nina uhakika kuwa iwapo msingi hautakuwa complicated na iwapo mdau atasimamia asiibiwe na mafudi, basi pesa hiyo inafikisha lenta kwa nyumba aliyotaja.

Kunä mdau Kituko ameenda mbali zaidi na kupiga mahesabu hatua kwa hatua. Yaangalie mahesabu yake halafu uonyeshe kama kuna kasoro.

Kaka ZeMarcopolo,
kuna watu wanakuwa na ubishi wa ukoo, hata kama kitu hajuhi na hajahi kufanya atabishatu, we nadhani hatutofautiani sana kwenye ujenzi, hiyo pesa inatosha sana kwa kupandiasha nyumba mpakamusawa wa rental
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kituko kwa mchanganuo mzuri uliotoa, hebu elezea vipimo vya vyumba ulivyotumia ili iwe msaada zaidi!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Kituko kwa mchanganuo mzuri uliotoa, hebu elezea vipimo vya vyumba ulivyotumia ili iwe msaada zaidi!

Mkuu@Soki,
ni Nyumba ya standard za kawaida kabisa isiyo vikolombwezo vingi,
vyumba havitazidi 11x11ft, sebule inaweza kuwa hata14x12ft na utapata choo cha 1.5m na bafu 1.5m utapata jiko dogo la 2m to 2.5m, cha muhimu ni kucontrol vicorridor vingi ambavyo havina maana, mara nyingi corridor zinapanua jengo na zinakuwa space zilizopotea

inawezekana mkuu, sio kwa dhana bali kwa ushahidi wangu mimi mwenyewe wa kuona, nyumba kubwa kuliko hiyo na maeneo hayohayo ya tabata kwa hiyo hiyo 10m
 
Asante! Hebu nisaidie tena kuanzia hapo ilikofika, mil 10 zingine zitaifikisha wapi?
 
miilioni kumi hadi kuezeka inatosha kasoro madirisha, milango na mengineyo endapo kiwanja kipo flati
 
Ndugu we anza tu mil 10 unajenga mpaka level ya lenta na kubakiwa na vijisent vyako

Sidhani, ilinigharimu Mil. 24 kuifikisha nyumba hiyo level ya lental tena ni nyumba ya kawaida tu, wala si ya manjonjo; Ukiingia kwenye ujenzi tofauti na unavyofikiria, pesa ya ki-tz ni uhuni mtupu inaondoka bila kutaraji. Na mahitaji yote nilisimamia mwenyewe kwenye malipo so hakukuwa na fix. Hata hivyo miaka minne iliyopita nyumba inayofanana na hivyo ilichukua mil. 14; hii ni kuonyesha kuwa kwa sasa gharama za ujenzi ziko juu mno, wala usipime. Kwa hesabu za haraka akijumuisha Tofali, Saruji, Nondo (4lines beam+lental, sahau habari ya kumwaga zege chini), maji, mafundi, kokoto, kama itakuwa na nguzo za zege, mchanga et al; kwa uchache walau awe na 18-20m. Hata hivyo suala la msingi yeye aanze tu then mengine atayaona ndani ya safari
 
Jenga mkuu, kama kama kiwanja chako kiko kwenye eneo la flat na la kichanga ambalo sio mfinyazi basi kwa kifupingharama zako zitakuwa hivi

Msingi: tofali 500 x 1200tsh= 600000/= msingi wako utakwa wa tofali tano (height)
Cement: msingi 15x17000= 255000
Nondo za mkanda (10 mm) 15x15000=225000
Cement za mkanda 15x 17000 = 255000
binding wire, mbao, misumari, ring, maji na dharura: 500,000/=
Kokoto unanunua mende moja 300000, kokoto zitabakia mingi za kuwekea mkanda wa juu rental
mchanga mende moja 300000
JUMLA YA MSINGI BILA HELA YA FUNDI = 2,455,000/=

Boma: Tofali 1040 x 1200= 1,248,000
Cement 20x 17000= 340000
Mchanga mende2 =600000
Maji na mengineyo= 500,000
JUMLA YA BOMA BILA HELA YA FUNDI = 2,688,000

Mkanda wa juu, hapo inakuwa ni nafuu kidogo kwani mbao utakuwa nazo, kokoto zitakuwepo, mchanga utakuwepo na size yake itakuwa ndogo kwani tofali zitakuwa za wima na gharama yake itakuwa hivi
Nondo (mm10) 15x 15000= 225000
cement za mkanda 15x 17000= 255000
Binding wire, ringi, misumali, mbao za sahani, maji na dharura=500000
JUMLA JUMLA YA MKANDA WA JUU BILA FUNDI = 980000

JUMLA KUU BILA FUNDI = 6,123,000/=
KIFUSI CHA KUJAZA NDANI NA KAZI ZA DHARURA= 2,000,000/
FUNDI MAKUBALIANO LAKINI ISIZIDI = 2,000,000

JUMLA YA MWISHO 10,123,000/=

mimi sio fundi ila nina uzoefu sana wa ujenzi hasa wa Dar,
hiyo gharama imezingatia kuwa , kiwanja chako kiko tambarare, na ground ni ya kichanga au udongo unaofanan na kichanga sio mfinyanzi
pia hesabu hiyo itapatikana tu ikiwa kila kitu unanunua mwenyewe na wewe ndio msimamizi mkuu wa show nzima

mkuu nimependa tathmin yako, lakini ila napenda kujua hii nyumba inavyumba vingapi kwa ujumla. Mimi nina ramani yenye vyumba vya kulala vinne dining, store, living room. Inaweza gharimu kiasi gani roughly.
 
Asante! Hebu nisaidie tena kuanzia hapo ilikofika, mil 10 zingine zitaifikisha wapi?

Kenchi na bati na huenda kufunika; Ila baada ya hapo sasa, kwa maana kwenye finishing, jiandae kugombana na mafundi. Pesa inayokwenda ni nyingi na huoni kilichofanyika; finishing ni noma
 
Back
Top Bottom