Nina milion 10 nahitaji kujenga nyumba Mwanza

Nina milion 10 nahitaji kujenga nyumba Mwanza

Kama uko mbali na site kuibiwa kupo mkuu.

Yawezekana 20+ imepigwa au zaidi hali ni mbaya sana mafundi na hata watu wengine siyo waaminifu hapo unakuta wameiba material na hela.
Ujenzi ni gharama sana mkuu,kama jamaa hapo juu anakwambia katumia mil 23 ndio kwana anapaua na kasimamia kila kitu. Hapo ndio ujenzi unaanza aandae milion 50 nyingine.
 
Heshima kwenu wataalam, nimehamia kikazi hapa Mwanza.

Sasa nimekuja kugusa bei za nyumba nikaona kama nitawapa faids tu washkaji. Maana nyumba ya standards zangu naambiwa 3,600,000/= kwa mwaka nimeona ni hela ndefu sana. Nikaamua kutafuta kiwanja nikapata cha 10mil nimebakia mfukoni na 10 mil.

Kiwanja nakigawa mara mbili kimoja nitajenga appartment na kingine nusu najenga nyumba ya familia yangu. Sasa nahitaji nianze na appartment ambayo ni vyumba viwili kimoja self na jiko na sebule nitapaua tu simple kama darasa.

Ninachoomba mlio na ramani inayomeet requirements zangu mnisaidie muweke hapa nitakayoipenda nitaona namna tunawezeshanakidogo ili unipatie.

Pia naomba usauri namna nitaweza kufanya ujenzi rahisi zaidi.

Plan yangu nitumie msingi wa tofali tu.

Nitatumia bati za kawaida za rangi vyumba vyote ni vidogo 3.5m na sebule 4m jiko3m.

Kama kuna mtu anaweza kunipigia gharama ya hii nyumba utakuwa umenisaidia sana. Nataka nitumia likizo ya sensa kukamilisha project hii maana nimejiegesha kwa jamaa yangu na familia yangu yote.

Kiwanja nlichopata kina 1090sqm
njoo nikupe kiwanja
 
Inawezekana,lakini hela sio rahisi kuiba,nilifanya manunuzi mwenyewe ya kila kitu. Dunia imekuwa kijiji,fundi alikuwa akinipa mahitaji ya Rangi nawasiliana na mafundi wengine wanipe makadirio yao,mara nyingi yalikuwa yanacheza mule mule,nikijiridhisha naweka oda kiwandani mzigo ukiwa tayari unaenda Site. Nimefanya hivyo kwa kila kitu,kuanzia Bati,tiles,Vifaa vya umeme,vifaa vya mabomba, Aluminium n.k...
Nilitaka kuleta uzi humu kuwaambia watu Dunia imekuwa kijiji sa hivi,mfano tiles fundi alinipa vipimo vyake,nikatuma kwa jamaa yangu Engineer akasema viko sawa,Ishu ilikuwa kwenye bei,nilitafuta namba za Twyford kwenye website,nikawapigia wakanipa namba za wakala wao aliye jirani na site,nikaweka oda kisha nikamwambia fundi akakague,akasema ziko sawa,mzigo ukaenda Site. Nimefanya hivyo kwa kila kitu.Kitu pekee ambacho nahisi kupigwa ni cement na Tofali...maana walikuwa wanatoka nje ya hesabu wanazonipa wanaomba nyongeza.
Ni kweli mkuu kwenye cement hapo siyo rahisi kuwazuia kuiba maana wanaweza kuiba hata mchanga uliochanganywa na cement wakauza, hata tofari ni hivyo hivyo.
 
Ujenzi ni gharama sana mkuu,kama jamaa hapo juu anakwambia katumia mil 23 ndio kwana anapaua na kasimamia kila kitu. Hapo ndio ujenzi unaanza aandae milion 50 nyingine.
Hata mimi niko hatua za kupaua nimeshatoboka 16 tayari.
 
Ni kweli mkuu kwenye cement hapo siyo rahisi kuwazuia kuiba maana wanaweza kuiba hata mchanga uliochanganywa na cement wakauza, hata tofari ni hivyo hivyo.
Yeah kweli Cement inawezekana waliiba lakini walikuwa wanajitetea,wanasema kiwanja kina slope kwahiyo Tofali zimeenda nyingi,na msingi waliochimba wanasema mtu alikuwa anazama haonekani,nyumba imenyanyuka juu balaa.Nilielewa.
 
Hata mimi niko hatua za kupaua nimeshatoboka 16 tayari.
Hapo ndio ujenzi unaanza mkuu,ila gharama za kutoka hapo na kuendelea inategemea na wewe ni muumini wa brand ama la. Kama mie kila kitu niliweka brand,bati nilipiga ALAF,rangi PLASCONE, tiles TYWFORD ,vifaa vya plumbing na masink nilichukua twyford pia,kwahiyo gharama huwa zinatofautiana kulingana na brand unazochagua,ukichukua brand cheap utamaliza nyumba kwa hela ndogo.
 
Kama uko mbali na site kuibiwa kupo mkuu.

Yawezekana 20+ imepigwa au zaidi hali ni mbaya sana mafundi na hata watu wengine siyo waaminifu hapo unakuta wameiba material na hela.

Mmm hawez kupigwa kiasi chote hicho mkuu kwenye 70m ndo tunasema Hamna uzoefu mnatisha tu watu
 
Inawezekana,lakini hela sio rahisi kuiba,nilifanya manunuzi mwenyewe ya kila kitu. Dunia imekuwa kijiji,fundi alikuwa akinipa mahitaji ya Rangi nawasiliana na mafundi wengine wanipe makadirio yao,mara nyingi yalikuwa yanacheza mule mule,nikijiridhisha naweka oda kiwandani mzigo ukiwa tayari unaenda Site. Nimefanya hivyo kwa kila kitu,kuanzia Bati,tiles,Vifaa vya umeme,vifaa vya mabomba, Aluminium n.k...
Nilitaka kuleta uzi humu kuwaambia watu Dunia imekuwa kijiji sa hivi,mfano tiles fundi alinipa vipimo vyake,nikatuma kwa jamaa yangu Engineer akasema viko sawa,Ishu ilikuwa kwenye bei,nilitafuta namba za Twyford kwenye website,nikawapigia wakanipa namba za wakala wao aliye jirani na site,nikaweka oda kisha nikamwambia fundi akakague,akasema ziko sawa,mzigo ukaenda Site. Nimefanya hivyo kwa kila kitu.Kitu pekee ambacho nahisi kupigwa ni cement na Tofali...maana walikuwa wanatoka nje ya hesabu wanazonipa wanaomba nyongeza.
Ujenzi wa mbali tunaibiwa sana. Miaka ya nyuma nilifanya ujenzi Morogoro nikiwa naishi Arusha, nyumba ya 75m zilitumika zaidi ya mia. Hata ukinunua materials yote,wanaiba na kuyauza
 
Back
Top Bottom