Nina milioni 22, nahitaji wazo zuri la biashara kwa mkoa wa Arusha

Nina milioni 22, nahitaji wazo zuri la biashara kwa mkoa wa Arusha

GREAT INVESTOR

Senior Member
Joined
Nov 13, 2018
Posts
128
Reaction score
297
Habari wanajukwaa.

Ee Bwana ee, nimekuja kwenu wana jukwaa, kuomba tusaidiane mawazo kama kichwa cha habari kinavyosomeka.

Baada ya kumaliza chuo 2019, Mungu alinifungulia mlango nikapata kazi ya miaka miwili na NGO x hapa Nchini, kutokana na msoto uliopo kitaa niliona ni vyema nijibane niweze kusave pesa walau nifanye kitu kitakacho nisaidia. Mkataba wangu umefika tamati na namshukuru Mungu nimeweza kusave takribani milion 22.

Nilikuwa na mawazo mawili, la kwanza ni kujenga nyumba kwa kuwa nilishanunua kiwanja.

La pili, ni kufanya biashara, ila kwa bahati mbaya bado sijawa na wazo zuri la biashara.

Naombeni mawazo yenu, nijenge au nifanye biashara, kama ni biashara Je, unahisi biashara gani nzuri katika mkoa wa Arusha?

========
Baadhi ya mawazo ya wadau

Mkuu, 22Mil, sio haba na sio nyingi. Aina ya biashara inategemea ulipo, interest zako, life style yako na malengo yako. Kwa ujumla inakubidi kwanza utulie uiweke hela yako kwenye FIXED DEPOSIT na kisha uanze sasa kujenga wazo la biashara.

Katika kutafiti wazo la biashara hakikisha unazingatia kutumia wataalamu ili kupata picha kamili ya aina ya biashara unayofikiri kufanya .Kuna aina nyingi za biashara unazoweza kufanya ila jambo la muhimu ni kuwa innovative ili uweze kuleta ushindani. Hilo ni muhimu sana.

Usishawishike kufanya biashara bila kuwa na taarifa sahihi kwani hatari yake ni wewe kupoteza na kukata tamaa.

Wewe fanya mpango ujenge ila nyumba iwe nzuri hata ukiweza kupangisha kwa familia moja iwezekane, biashara sasa hivi hazieleweki na pia ukijenga pesa ya biashara huwa tunakutana nazo tena ila hela ya kujenga ukafanya biashara kipindi hiki ambacho hakieleweki kabisaa utabaki na picha ya nyumba kwenye kichwa maana biashara inataka utulivu wa kichwa na pia usitafute biashara za haraka ili ujenge daah.

Pia soma: Nina mtaji wa Milioni 35 nataka kufanya biashara Kariakoo
 
Wewe fanya mpango ujenge ila nyumba iwe nzuri hata ukiweza kupangisha kwa familia moja iwezekane, biashara sasa hivi hazieleweki na pia ukijenga pesa ya biashara huwa tunakutana nazo tena ila hela ya kujenga ukafanya biashara kipindi hiki ambacho hakieleweki kabisaa utabaki na picha ya nyumba kwenye kichwa maana biashara inataka utulivu wa kichwa na pia usitafute biashara za haraka ili ujenge daah.
 
Mkuu, 22Mil, sio haba na sio nyingi. Aina ya biashara inategemea ulipo, interest zako, life style yako na malengo yako. Kwa ujumla inakubidi kwanza utulie uiweke hela yako kwenye FIXED DEPOSIT na kisha uanze sasa kujenga wazo la biashara.

Katika kutafiti wazo la biashara hakikisha unazingatia kutumia wataalamu ili kupata picha kamili ya aina ya biashara unayofikiri kufanya .Kuna aina nyingi za biashara unazoweza kufanya ila jambo la muhimu ni kuwa innovative ili uweze kuleta ushindani. Hilo ni muhimu sana.

Usishawishike kufanya biashara bila kuwa na taarifa sahihi kwani hatari yake ni wewe kupoteza na kukata tamaa.
 
Habari wanajukwaa.

Ee Bwana ee, nimekuja kwenu wana jukwaa, kuomba tusaidizane mawazo kama kichwa cha habari kinavyosomeka.

Baada ya kumaliza chuo 2019, Mungu alinifungulia mlango nikapata kazi ya miaka miwili na NGO x hapa Nchini, kutokana na msoto uliopo kitaa niliona ni vyema nijibane niweze kusave pesa walau nifanye kitu kitakacho nisaidia. Mkataba wangu umefika tamati na Namshukuru Mungu nimeweza kusave takribani milion 22.

Nilikuwa na mawazo mawili, la kwanza ni kujenga nyumba kwa kuwa nilishanunua kiwanja.

La pili, ni kufanya biashara, ila kwa bahati mbaya bado sijawa na wazo zuri la biashara.

Naombeni mawazo yenu, nijenge au nifanye biashara, kama ni biashara Je, unahisi biashara gani nzuri katika mkoa wa Arusha?
Daah usisahau kunifundisha ulisave save vipi? Maana naamini ni zaidi ya kuweka tu hela bank na kuisahau.
 
Chukua milioni 18 weka fixed account mwaka mmoja. Baki na milioni 4 ambazo ndio utafanyia pilot.

Ingia chimbo tafuta elimu, maarifa, taarifa sahihi na kila kitu kuhusu biashara flani. Ukishapata kwa kushirikiana na waozefu na wadau wengine (ambao hawajui kama una hela) anza hiyo biashara kwa kiasi kidogo ulichobakiza.

Ukishapata uzoefu nido baada ya mwaka utoe kiasi flani kati ya hizo 18M ndio uendelee.
 
Ushawahi kufanya biashara? Kutumbukiza mzigo wote huo kwenye biashara yanaweza kuja kuwa majuto baadae.

Weka lengo anza na biashara ya mtaji usiozidi mil5 kwanza uusome mchezo. Me si mtaalamu wa biashara, ila kazi kwako kutafuta biashara isiyozidi mtaji wa hiyo mil5. Ila kwa siku ikuingizia faida ya walau 20k na kuendelea.
 
Fanya mchakato wa tin namba na leseni ya biashara. Tafuta kijiwe kilicho changamka, anzisha biashara ya miamala ya huduma nyingine za kibenki. Simamia mwenyewe. Kila mwezi utakuwa unakula tu kamisheni.

Katika hicho kijiwe, uza na vitu vingine vya ziada kama kuuza na akubadilisha mitungi ya gesi, weka friji yenye mlango wa kioo kwa ajili ya kuuza vinywaji baridi, nk.

Usiwe na uoga wa maisha kwa kukimbilia kujenga nyumba, kama sisi watumishi wa umma wenye umri mkubwa na tulio na wategemezi lukuki. Nyumba haizalishi! Na kama utajenga ya kukuzalishia, bado itakuzalishia kiasi kidogo sana kwa mwezi ukilinganisha na pesa uliyo izika!
 
Back
Top Bottom