Nina milioni 22, nahitaji wazo zuri la biashara kwa mkoa wa Arusha

Nina milioni 22, nahitaji wazo zuri la biashara kwa mkoa wa Arusha

Ningekushauri igawe hiyo hela utoe kiwango kidogo cha mtaji nyingine iweke kwenye nyumba biashara zimekuwa ngumu mzunguko wa hela haujakaa poa Sana hasa kwa arusha wekeza hiyo hela kwny kujenga hata nyumba za kupanga ntafute kwa maswala ya ujenzi ntakusaidia napatikana arusha mm ni mhandisi wa ujenzi nmba zangu 0783166050
 
Umefanya kazi miaka miwili umesave million 22?

Aisee
Kawaida au wewe mwalimu umezoea mishahara haikutani? Salary tar. 22 inaisha tar. 29 mwezi huohuo!! Maana mwalimu mshahara lakitatu yaani pea mbili za viatu.

Mshahara wamwezi haununui hata suit moja ya kawaida ya mbunge ya lakinne...alafu ndo wanatoa elimu yaani ufunguo wa maisha!! Poleni walimu wote Tz
 
Tafuta business consultant ama business planners mzuri hapo chuga umkatie kama lakitatu akuchoree biashara itayokulipa!! Haya mawazo ya Bure utajaingia choo shimofupi bureee utoke unanuka mimafii!
 
Kawaida au wewe mwalimu umezoea mishahara haikutani? Salary tar. 22 inaisha tar. 29 mwezi huohuo!! Maana mwalimu mshahara lakitatu yaani pea mbili za viatu... Mshahara wamwezi haununui hata suit moja ya kawaida ya mbunge ya lakinne...alafu ndo wanatoa elimu yaani ufunguo wa maisha!! Poleni mwalimu wote Tz
Humu jf mnajikuta mnamishahara minono hahaaa

Kwa mwezi mnapata mamilioni kumbe njaa tupu

Nina uhakika kwa mwezi huna mshahara hata wa 1.5milion wewe

Wapo wenye pesa sawa ila ,nikikutana na watu kama nyie mitandaoni mnaojishaua mnapesa ,Mara nyingi mna njaa Kali
 
Chukua milioni 18 weka fixed account mwaka mmoja. Baki na milioni 4 ambazo ndio utafanyia pilot.

Ingia chimbo tafuta elimu, maarifa, taarifa sahihi na kila kitu kuhusu biashara flani. Ukishapata kwa kushirikiana na waozefu na wadau wengine (ambao hawajui kama una hela) anza hiyo biashara kwa kiasi kidogo ulichobakiza.

Ukishapata uzoefu nido baada ya mwaka utoe kiasi flani kati ya hizo 18M ndio uendelee.
Huu ndio ushauri wa kupita nao mkuu [emoji457]
 
Habari wanajukwaa.

Ee Bwana ee, nimekuja kwenu wana jukwaa, kuomba tusaidiane mawazo kama kichwa cha habari kinavyosomeka.

Baada ya kumaliza chuo 2019, Mungu alinifungulia mlango nikapata kazi ya miaka miwili na NGO x hapa Nchini, kutokana na msoto uliopo kitaa niliona ni vyema nijibane niweze kusave pesa walau nifanye kitu kitakacho nisaidia. Mkataba wangu umefika tamati na namshukuru Mungu nimeweza kusave takribani milion 22.

Nilikuwa na mawazo mawili, la kwanza ni kujenga nyumba kwa kuwa nilishanunua kiwanja.

La pili, ni kufanya biashara, ila kwa bahati mbaya bado sijawa na wazo zuri la biashara.

Naombeni mawazo yenu, nijenge au nifanye biashara, kama ni biashara Je, unahisi biashara gani nzuri katika mkoa wa Arusha?

========
Baadhi ya mawazo ya wadau




Pia soma:
Nina mtaji wa Milioni 35 nataka kufanya biashara Kariakoo
Mkuu ,nimekusoma nimekuelewa...nipo Arusha hapa moshono,kama utapenda ushauri wangu tuonane,nipigie +255716060677.

USHAURI WANGU .

FANYA BIASHARA,FANYA BIASHARA...,SAWA BIASHARA NI RISK,ILA IKIENDA VIZURI MIAKA MITATU TU KWA MTAJI HUO TU UNAWEZA KUJA KUJENGA NYUMBA ZAKO ZA KIWANGO NA BIASHARA IKAWEPO NA MAISHA MENGINE YAKAENDELEA.

DUNIANI HAPA KILA KITU NI HATARI (RISK),UWE UNA KAZI,..UNAWEZA KUFUKUZWA AU KUACHA KWA SABABU YOYOTE TU,UNAWEZA KUJENGA NYUMBA IKAISHA VIZURI THEN IKAJA KUWAKA MOTO,UNAWEZA KUOA AU KUOLEWA NDOA IKAWA YA MATESO UKAAMUA KUACHANA NA NDOA,...YAANI, USIOGOPE RISK,SEMA FANYA KITU (BIASHARA) ILIYO NA HATARI KIDOGO(VERY CALCULATED RISK).

BIASHARA ZIPO NYINGI TU MKUU,..MFANO NAFAKA AINA ZOTE,...DAGAA, N.K...ZAIDI SANA TUWASILIANE TUONANE TUSHAURIANE MAANA UZOEFU NA MAARIFA YA BIASHARA NILIZOKUTAJIA HAPO NINAO WA KUTOSHA. YOU NEVER KNOW TUNAWEZA KUSHARE UZOEFU NA TUKAONA NAMNA YA KUSHIRIKIANA PIA.(kama utapenda lakini).

Mwisho usiogope ,BIASHARA ndo njia pekee inayoweza kukupa Uhuru wa kiuchumi, yaan ukawa mtu miongoni mwa Watu.,,,Eti ujenge NYUMBA ubaki na zero...,hapana aisee,,,labda kama utajenga harafu ubaki na pesa ya kufanya biashara.
NIMESOMEKA.!
 
Pikipiki mtumba 6 za million 1.5 jumla ni 9,000,000.

Mimi nilifanyaga hii pesa yangu ya deal ya kwanza kabisa katika miradi ila lazima uwe mjanja sana.

Nilikuwa na uhakika na m 1-1.2 kwa mwezi hapo ukifungua biashara yeyote ile ukawa unailealea wakati unaingiza hiyo pesa hautakuwa na pressure sana.

Biashara ya chakula sio kichaa sana km ukijipangana kujua wapi utanunua debe la mahindi kwa 4000 au gunia la mpunga kwa 45000.Huwezi kufirisika.

Ingiza million 7 kwenye biashara ya chakula,mgahawa wa kisasa.
 
Njoo na milioni kumi Nina shamba Naberera maharage miezi minne utakua na 50.
 
Nakushauri vet mechi za champions league wiki ijayo.
- jumanne na jumatano kutakuwa na champions league , mpe man City, mpe Bayern, alafu weka over 1.5 kwenye mechi ya Madrid vs liver.
Hapo hukosi odds ya 2.5 ambapo ukiweka mil 22 inakuja mil 45.
Fanya hivyo and thank me later
Nimetoka kusoma uzi wako kua umejenga nyumba ya million 78 ndani ya miaka mitano na ulikua una save 1.8 million kwa mwenzi.

Ila kama haya ndo mawazo yko mkuu natilia mashaka kua ule uzi ni wauongo mtu mwenye akili ya kufanya jambo kubwa kama lile hawez kua na mawazo yaki pumbavu kama haya kwa mtu ambae yupo serious anahitaj ushauri.
 
Mkuu, 22Mil, sio haba na sio nyingi. Aina ya biashara inategemea ulipo, interest zako, life style yako na malengo yako. Kwa ujumla inakubidi kwanza utulie uiweke hela yako kwenye FIXED DEPOSIT na kisha uanze sasa kujenga wazo la biashara.

Katika kutafiti wazo la biashara hakikisha unazingatia kutumia wataalamu ili kupata picha kamili ya aina ya biashara unayofikiri kufanya .Kuna aina nyingi za biashara unazoweza kufanya ila jambo la muhimu ni kuwa innovative ili uweze kuleta ushindani. Hilo ni muhimu sana.

Usishawishike kufanya biashara bila kuwa na taarifa sahihi kwani hatari yake ni wewe kupoteza na kukata tamaa.
iweke UTT sio bank wakati unaendelea kuchakata cha kufanya ikuzalishie faida. chagua mfuko wa liquid fund ukipata dill zuri waweza kuchukua in 3 days. tena siku zote unakusanya zingekua huko ungekua ushapata riba nzuri sana ya 12-14% per year.
 
Nakushauri vet mechi za champions league wiki ijayo.
- jumanne na jumatano kutakuwa na champions league , mpe man City, mpe Bayern, alafu weka over 1.5 kwenye mechi ya Madrid vs liver.
Hapo hukosi odds ya 2.5 ambapo ukiweka mil 22 inakuja mil 45.
Fanya hivyo and thank me later
Mancity na madrid washatoa over 1.5, ngoja tumsikilizie bayern.
 
Nunua ngo'ombe ndama kisha nenepesha kwa mwaka uza.dume laki2 ukimnenepesha utauza kuanzia laki 6.Hawana risk kama miradi ya kuuza na kununua bidhaa. Milioni 10 ndama,kumi chakula na madawa na mbili balance yako.Waone mabwana mifugo.
 
Hongera Sana kaka kwa ku-save...,
Nakushauri weka Mobile money hiz tgo pesa,mpesa, eatel money, mpesa, halopesa, ezypesa,TTcl pesa, NMB, CRDB, NBC,Amana mtaani nk..,
Ongezea na super agent ya voda na eatel...
Tafuta site nzuri ie sokoni, stend, eneo karbu na hospital au sehem yoyote yenye wng wa watu... baada ya miez mitano utakua unatengeneza zaid ya 5,000,0000..,
Nimekushaur biashara ambayo nina uzoefu nayo
 
ni
Fanya mchakato wa tin namba na leseni ya biashara. Tafuta kijiwe kilicho changamka, anzisha biashara ya miamala ya huduma nyingine za kibenki. Simamia mwenyewe. Kila mwezi utakuwa unakula tu kamisheni.

Katika hicho kijiwe, uza na vitu vingine vya ziada kama kuuza na akubadilisha mitungi ya gesi, weka friji yenye mlango wa kioo kwa ajili ya kuuza vinywaji baridi, nk.

Usiwe na uoga wa maisha kwa kukimbilia kujenga nyumba, kama sisi watumishi wa umma wenye umri mkubwa na tulio na wategemezi lukuki. Nyumba haizalishi! Na kama utajenga ya kukuzalishia, bado itakuzalishia kiasi kidogo sana kwa mwezi ukilinganisha na pesa uliyo izika!
nimelipenda hili wazo pia its my dream bussiness
 
Milioni 22.. unaweza fanya yote. Jenga nyumba ya bajeti ya milioni 15. Hakikisha unamaliza chumba walau kimoja uhamie. Milion 15 ni nyumba nzuri ya kuishi. Inabakia 7. Nunua bajaj ya milion 5 used naimani inaweza ikawa nzuri sanaa. Alafu milioni 2 weka akiba.

Bajaj haiwezi kukutupa. Na utamalizia nyumba na utapata mtaji wa kufanyia biashara zingine. Bajaj iwe kama ajira ya kutafuta mtaji wa mbeleni. Minimize risk. Maana tumefanya biashara za fremu tunazijua tofauti na bajaj haina kodi ya mwisho wa mwezi.

Ina bima, sumatra na tra ambazo hazizidi laki 3. Ila biashara inabidi uangalie na fremu, kuna fremu mpaka milioni kwa mwezi, kuna tra leseni, usafi, ulinzi, shelf za dukani na vingine vingi.

At the end of the day choice is yours. Angalia what you like and what you're capable off.

Minimize risk that is my advice to you. Usiweke mayai yote kwa trei moja. If you understand what i am saying...
 
Back
Top Bottom