Nina Milioni 45, msaada wanaJF

Kuwa wakala mdogo wa kuuza pombe/vilevi
  • Tafuta fremu ya kuridhisha
  • Sajili jina la biashara
  • Tafuta leseni
  • Nunua kirikuu 5M
  • Anza na kreti 500 za bia
  • Anza kuuza rejareja na jumla
  • Anza kula faida na kurudisha mkopo
 
Biashara ni kipaji mkuu
 
Sio kila mtu anafit
 
kisumapai nunua tata mpya peleka mwanza kuna kjj nmetoka huko kina dala dala mbili tu nauli 5000 per head
 
huo uzoefu unaupatia wapi? ndotoni au? this is 2020 sio 80's , kuna njia maelfu ya kuendesha biashara, technology imerahisisha sana kila kitu
 
Kwanza ni kosa kuchukua mkopo kwa madhumuni ya biashara ilihali hauna hiyo biashara bado na wala hujui biashara,cha msingi hapo chukua milion 30 nzima ifungie kwa account usiitoe kwa faida ya baadae,then 15M ndo anza nayo kulingana na ushauli wa watu utakao ona unakufaa,biashara nyingi zina changamoto sana unaweza kukaanga hiyo milion 45 kwa mwaka mmoja tu,amini usiamini..biashara siyo mtaji kwanza,biashara ni fikra kwanza na uthubutu..biashara ni tabia,waweza fanya biashara hata ya mtaji wa laki tano mpaka uzoee biashara ndo uwe unaongeza kidogo kidogo
 
Hapo kwenye kujifungia ndani kuangalia CD

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Anapigwa mtu asubuhi asubuhi hapa.
 
Sio bongo hii....africa bila kusimamia kitu chako mwenyewe au kama huna uzoefu nacho basi we subiri maumivu au kama ukifanikiwa shukuru Mungu.
huo uzoefu unaupatia wapi? ndotoni au? this is 2020 sio 80's , kuna njia maelfu ya kuendesha biashara, technology imerahisisha sana kila kitu
 
Je nifanye nini ndugu maana na hela nshaichukua

Upo mkoa gani mkuu nunua mpunga na mahind weka stoo hela utakayopiga mwezi wa 12 hadi 1 kwenda3 utakuja nikumbuka .note kwenye mpunga inahitaji umakini wahali ya juu kununua
 

Njoo tabora ununue mpunga kisha unauacha stoo mindugu wangu anagodown lakuhifadhia pia anamashine anakoboa mpunga
 

Gunia la mpunga hivi sasa ni 42000 anaekununulia anakula 2000 kwakila gunia pia ushuru kila gunia1500 usafiri kwakila gunia kutoa porin hadi stoo2000 vibega kupakia na kushusha1000 mfuko wakuhifadhia tsh800 wafuata mpunga polini ndani ndani kila gunia1000 kuhifadhi stoo1500 kwaiyo gharama zote pamoja ununuzi gunia litakua ni 51800 utakuja kuuza kila gunia ifikikapo december kwa kima cha chini soko likiwa baya utauz tsh 80000 kwaiyo utakua na faida ya tsh 28200 kwa kila gunia.ila ukitaka usiuze mpunga uje uuze mchele yaan ukoboe huo mpunga uwauzie walanguz wa mchele wanaotaka dar uganda nakwingneko gharama itaongezeka kwenye kukoboa ambayo kila kilo utakobolea tsh50 kwaiyo gunia la kilo tisini utalikoboa kwa tsh3000 hapo mchele bei ya jumla utakuta imefika 1700 kwaiyo utazidisha mara kilo60 kila gunia ndo litao hizo kilo za mchele kwaiyo utapata faida ya tsh 47200 sasa zidisha mara gunia utakazo kua na zo stoo utaona faida kias gani umepata ndani ya miez isiyo zidi 10
 
Asante sana kwa mawazo yako naendelea kujifunza mengi kupitia jukwaa ili japo kuna wengine wananibeza na kuona kama sina akili .Ndugu zangu Tambua sisi binadamu tumezidiana uelewa wa mambo ata mimi ukija katika upande wangu wa kazi basi najua kila kitu mpka nisipokuwepo kazini dhairi ofisi inaona pengo langu pia ndo hivyo hivyo kwa maisha ya mtaani kuna watu wanajua mambo mengi kulingana na sector mtu anayoitegemea kuingizia kipato kwahiyo msinibeze na kuona kama nimekurupuka kuchukua huo mkopo. Ndo maana nimesema kuwa hizi hela sio kama narudisha mkononi hapana nakatwa moja kwa moja kwenye mshahara kwahiyo ata ningefeli au kufanikiwa sio kama benki itanifilisi hapana
 
kisumapai nunua tata mpya peleka mwanza kuna kjj nmetoka huko kina dala dala mbili tu nauli 5000 per head
Ndugu mimi niko Dar na sina uzoefu na mwanza pia kwa pesa niliyo nayo ni ndogo kununua ilo gari may be kununua kwa mtu na ni kitu katu ambacho siwezi kufanya
 
Njoo tabora ununue mpunga kisha unauacha stoo mindugu wangu anagodown lakuhifadhia pia anamashine anakoboa mpunga
Kwa kazi yangu si ruhusa kusafir nje ya mkoa pasi na likizo ndugu
 
Kuwa wakala mdogo wa kuuza pombe/vilevi
  • Tafuta fremu ya kuridhisha
  • Sajili jina la biashara
  • Tafuta leseni
  • Nunua kirikuu 5M
  • Anza na kreti 500 za bia
  • Anza kuuza rejareja na jumla
  • Anza kula faida na kurudisha mkopo
Asante kwa ushauri ndugu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…