cariha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2015
- 22,077
- 46,549
Ushauri wako mzuri Tena akienda nje ya mkoa Kuna maeneo ka kibaigwa huko watu Wana magala na wanalipia kuweka mahindi kwa ushuruNimejaribu kufuatilia namna unavyo respond kwenye baadhi ya comment za wanaokushauri nimegundua vitu vifuatavyo:-
1. Una uoga wa asili
2. Hauna uwezo wa kukabili changamoto
3. Umekulia mazingira ya wasomiwasomi wengi au
4. Umesoma sana
Nianze na namba 3 na 4, watu wengi waliokulia mazingira ya wasomi wasomi au waliosoma sana (hata degree ya kwanza ni kusoma sana pia) na mazingira hayo yakawa hayana hata mfanyabiashara au mjasiriamali tunakosa uzoefu wa kufanya kitu nje ya ajira.
Namba 1 na 2 vinaweza kuwa matokeo ya namba 3 na 4.
Mtu muoga anaogopa kuanza.
Mtu muoga anawaza hasara kwanza badala ya faida
Mtu muoga hataki usumbufu
Mtu muoga hataki kukosana na watu
Kwenye biashara hivyo vitu HAVIKWEPEKI!
Hakuna biashara isiyo na hasara
Hakuna biashara isiyo na changamoto
Hakuna biashara isiyo na usumbufu
Na biashara nyingi lazima kuna kutofautiana hata na mteja tu achilia mbali uliowaajiri
Ukishajihisi ni muoga wa kupoteza, muoga wa usumbufu, muoga wa kukosana na watu achana na biashara zinazohusisha watu kwasababu kwanza sio lazima kila mtu afanye biashara na wala si kila mmoja anaweza kufanya biashara
Ni kweli kabisa tunahitaji kuwa na kipato cha ziada ila kuna vitu havifanywi na kila mtu.
Ushauri wangu kwako
Kwasababu angalau mwenzetu unauwezo wa kupata mamilioni yote hayo, kuna uwekezaji ambao unaweza kufanya usio na usumbufu
Mimi huwa naamini uwekezaji ni tofauti kidogo na biashara japo vinashabihiana
Unaweza kufanya moja kati ya vifuatavyo:
1. Tafuta kampuni inayopata faida kanunue hisa huko
2. Tafuta eneo (sio lazima iwe dsm), jenga stoo (sijui ndo godown) ambapo wakulima watakuwa wanatunza mazao yao huko kwa kulipia ushuru
3. Nunua mashine ya kusaga na kukoboa weka kwenye hiyo stoo kupanua wigo wa mapato
Katika hivyo vitatu sio rahisi kuibiwa pesa kizembe, hazina stress, hazina purukushani wala hazikuhitaji kuwepo kila siku japo kwenye mashine hapo utahitajika kuweka ndugu yako au mtu unayemuamini atukuibia ila hatakuibia sana