Nina Milioni 45, msaada wanaJF

Nina Milioni 45, msaada wanaJF

Nimejaribu kufuatilia namna unavyo respond kwenye baadhi ya comment za wanaokushauri nimegundua vitu vifuatavyo:-

1. Una uoga wa asili

2. Hauna uwezo wa kukabili changamoto

3. Umekulia mazingira ya wasomiwasomi wengi au

4. Umesoma sana

Nianze na namba 3 na 4, watu wengi waliokulia mazingira ya wasomi wasomi au waliosoma sana (hata degree ya kwanza ni kusoma sana pia) na mazingira hayo yakawa hayana hata mfanyabiashara au mjasiriamali tunakosa uzoefu wa kufanya kitu nje ya ajira.

Namba 1 na 2 vinaweza kuwa matokeo ya namba 3 na 4.

Mtu muoga anaogopa kuanza.
Mtu muoga anawaza hasara kwanza badala ya faida
Mtu muoga hataki usumbufu
Mtu muoga hataki kukosana na watu

Kwenye biashara hivyo vitu HAVIKWEPEKI!

Hakuna biashara isiyo na hasara
Hakuna biashara isiyo na changamoto
Hakuna biashara isiyo na usumbufu
Na biashara nyingi lazima kuna kutofautiana hata na mteja tu achilia mbali uliowaajiri

Ukishajihisi ni muoga wa kupoteza, muoga wa usumbufu, muoga wa kukosana na watu achana na biashara zinazohusisha watu kwasababu kwanza sio lazima kila mtu afanye biashara na wala si kila mmoja anaweza kufanya biashara

Ni kweli kabisa tunahitaji kuwa na kipato cha ziada ila kuna vitu havifanywi na kila mtu.

Ushauri wangu kwako

Kwasababu angalau mwenzetu unauwezo wa kupata mamilioni yote hayo, kuna uwekezaji ambao unaweza kufanya usio na usumbufu

Mimi huwa naamini uwekezaji ni tofauti kidogo na biashara japo vinashabihiana

Unaweza kufanya moja kati ya vifuatavyo:

1. Tafuta kampuni inayopata faida kanunue hisa huko

2. Tafuta eneo (sio lazima iwe dsm), jenga stoo (sijui ndo godown) ambapo wakulima watakuwa wanatunza mazao yao huko kwa kulipia ushuru

3. Nunua mashine ya kusaga na kukoboa weka kwenye hiyo stoo kupanua wigo wa mapato

Katika hivyo vitatu sio rahisi kuibiwa pesa kizembe, hazina stress, hazina purukushani wala hazikuhitaji kuwepo kila siku japo kwenye mashine hapo utahitajika kuweka ndugu yako au mtu unayemuamini atukuibia ila hatakuibia sana
Ushauri wako mzuri Tena akienda nje ya mkoa Kuna maeneo ka kibaigwa huko watu Wana magala na wanalipia kuweka mahindi kwa ushuru
 
Namtakia mafanikio mema lakini kuna kila dalili ya mtu kulizwa hizo fedha hata kabla hajaanza biashara. Dalili zote zinaonyesha hivyo. Kweli dunia ya leo unaonyesha nyama uliyobeba kwenye kundi lenye mafisi?

Hata kama hatalizwa (tena na member(s) kutoka hapa hapa) akifanya biashara uwezekeno wa kufanikiwa ni mdogo.

kisumapai ni bora kama huna wazo lolote kwa sasa basi chukuwa fedha zote, tafuta benki yenye riba nzuri, weka fixed kwa muda wa mwaka au miezi sita, ili upate muda wa ku-research utafazifanyia nini.
Good advice
 
Mimi pamoja na mke wangu ni watumishi wa serikali tumekaa pamoja tumeshauliana tumeamua kuchukua mkopo wa mil 45 lakini tatizo tulilonalo hatuna idea yoyote ya biashara maana kazini tunaenda asubuhi na kurudi jioni.

Japo mungu ametujalia tumeweza kujikwamua na kujenga nyumba ya kuishi maeneo ya boko chasimba.

Shida yangu kwenu je ni biashara gani naweza kufanya ili tuweze kujipatia kipato cha ziada bila kuaribu utaratibu wa kazi maana ikifika tarehe 14 wote tunakuwa tumeishiwa tunabakia ndani kuangalia CD za kikorea na kijapani.
Mawazo niliyokuwa nayo ni÷

1. Ninunue daladala ya habiria.
2. Ninunue bodaboda 5
3. Ninunue bajaji mbili
4. Nifuge kuku wa nyama

Maana siwezi kuweka fixed account kwakuwa pesa yenyew ni ya mkopo ushauri wenu ndugu zangu lakini wazo la daladala ndo tumelipa kipau mbele kikubwa naomba kwa mwenyewe uzoefu na iyo biashara ya daladala anipe msaada kwa umakini maana makato ya miaka 5 sio powa kabisa
Achana kabisa na daladala zitakufilisi njoo Pwani kuna sehemu uhitaji wa nyumba za kupanga uko juu sana
Kiwanja 20 kwa 20 4M
Jenga vyumba 10 kwa mtindo wa madarasa
Kila chumba ni elfu 30
Kila mwezi una hakika ya laki 3 isiyo na makato
Ngarama ya ujenzi haizidi 25M

Jr[emoji769]
 
Sio uchawi, lakini naona ukienda kuanguka.
Mmechukua mkopo bila kuwa na plan.
Halafu ni risk sana kuanzisha biashara kwa kuutegemea mkopo 100℅

Mna uzoefu na biashara gani?
Kwa usalama wa hiyo pesa kama una kiwanja ni heri ujengee nyumba upangishe.

Neno langu si sheria. Zaidi labda wataalamu waje
Hii sawa kabisa

Jr[emoji769]
 
Duh, pole!
I did the same mistake nilipokuwa nacjukua mkopo wangu wa kwanza, sitasahau miaka ile mi4 ya kupoteza pesa na kuendelee kupokea nusu mshahara. yaani ilokuwa miaka migumu sana ktk maisha yangu.
 
Milioni 45 ushindwe kujenga na kumaliza?

Unaweza nunua hata pagala kuna mapagala unanunua 20 unatumia million 10 kumalizia..

Naona wewe ulivyojenga mwanzo ulipigwa Sana na mafundi..
Hivi mkuu, eti ni kweli kujenga nyumba ukiwa unajua gharama na ufatiliaji pia unajenga kwa pesa nafuu? Hua naskia tu wakisema kujenga sio mchezo
 
Mimi pamoja na mke wangu ni watumishi wa serikali tumekaa pamoja tumeshauliana tumeamua kuchukua mkopo wa mil 45 lakini tatizo tulilonalo hatuna idea yoyote ya biashara maana kazini tunaenda asubuhi na kurudi jioni.

Japo mungu ametujalia tumeweza kujikwamua na kujenga nyumba ya kuishi maeneo ya boko chasimba.

Shida yangu kwenu je ni biashara gani naweza kufanya ili tuweze kujipatia kipato cha ziada bila kuaribu utaratibu wa kazi maana ikifika tarehe 14 wote tunakuwa tumeishiwa tunabakia ndani kuangalia CD za kikorea na kijapani.
Mawazo niliyokuwa nayo ni÷

1. Ninunue daladala ya habiria.
2. Ninunue bodaboda 5
3. Ninunue bajaji mbili
4. Nifuge kuku wa nyama

Maana siwezi kuweka fixed account kwakuwa pesa yenyew ni ya mkopo ushauri wenu ndugu zangu lakini wazo la daladala ndo tumelipa kipau mbele kikubwa naomba kwa mwenyewe uzoefu na iyo biashara ya daladala anipe msaada kwa umakini maana makato ya miaka 5 sio powa kabisa
Ulipataje iyo pesa bila kujua matumizi. Kama ni ya urithi itaisha bila kujua
 
Kabisa Bagamoyo panafaa kujenga tena mitaa uliko mradi wa malaria sababu viwanja vimeshapimwa na ni sqm 1 tsh 12,000(max) ,ukiingia kichwa kichwa mitaa isiyopimwa umepigwa.

Kujenga andaa m25,jenga nyumba pangisha nzima iwe na fensi ni tsh 250,000 kwa mwezi
 
Gunia la mpunga hivi sasa ni 42000 anaekununulia anakula 2000 kwakila gunia pia ushuru kila gunia1500 usafiri kwakila gunia kutoa porin hadi stoo2000 vibega kupakia na kushusha1000 mfuko wakuhifadhia tsh800 wafuata mpunga polini ndani ndani kila gunia1000 kuhifadhi stoo1500 kwaiyo gharama zote pamoja ununuzi gunia litakua ni 51800 utakuja kuuza kila gunia ifikikapo december kwa kima cha chini soko likiwa baya utauz tsh 80000 kwaiyo utakua na faida ya tsh 28200 kwa kila gunia.ila ukitaka usiuze mpunga uje uuze mchele yaan ukoboe huo mpunga uwauzie walanguz wa mchele wanaotaka dar uganda nakwingneko gharama itaongezeka kwenye kukoboa ambayo kila kilo utakobolea tsh50 kwaiyo gunia la kilo tisini utalikoboa kwa tsh3000 hapo mchele bei ya jumla utakuta imefika 1700 kwaiyo utazidisha mara kilo60 kila gunia ndo litao hizo kilo za mchele kwaiyo utapata faida ya tsh 47200 sasa zidisha mara gunia utakazo kua na zo stoo utaona faida kias gani umepata ndani ya miez isiyo zidi 10
Kulingana namazingira yako yakaz naupeo wako wabiashara hii ndo biashara sahihi ambayo haitakutesa ninaiamin asilimia 100% kama sio mpunga nunua mahindi weka stoo hiyo pesa kama isipojidouble itaongezeka zaidi ya asilimia Sabin, nalogic ni ndogo tu saiv mahind bado yan 7000.

Nunua mifuko yakinga njaa yakuhifadhia yasibunguliwe kwa bei yajumla inauzwa 4000 @ inabeba debe sita ko pigia umenunua kwa 10000jumla ukusanyaji nausafir mwez kuanzia wakumi mahind debe co chini ya 15 (minimum) hyo ni faida 50% nabila stress kama unavyotaka ukichanganya nampunga hapo faida kotekote. Mimi nimtumishi pia hii business imeniweka mjin trust utakuja shukuru baadae
 
Dah! Basi tu yani. Kwa kuwa huna uzoefu na biashara ila unatamani kuingia kwenye daladala mimi ngoja nikushauri ila utaamua mwenyewe.
Badala ya daladala agiza IST zako za tu Japan ambapo utatumia kama mil 35 hivi halafu zifanye kazi ya uber ambapo utazikatia na bima kubwa jumlisha ma GPS. Hesabu yake ipo hivi. Kwa wiki huwa malengo ni 200000 so kwa gari tatu itakua 600 ambapo kwa mwezi itakua unafunga 2m. Hiyo nadhani sio haba kwani usimamizi sio mkubwa pia gari inakua kwenye hali nzuri katika upande wa makenika hivyo mwaka wa kwanza itakua ni nafuu zaid kiuendeshaji wa bashara. Risk zipo kiasi.
Wewe ni jiran kabisa, ukipata nafasi pita hapa ANDO unisalimie
Kwa nadharia uko sawa lakini practically ni tofauti sana naweza sema kwa sasa bora taxi ya kawaida kuliko uber
 
Hujui bei ya Tata ni zaidi ya 100mil?
Hujui kwa mwezi atapata 2.4mil kama atafanya siku 30 ambacho hakiwezekani?
Hapo hujatoa service
Hujatoa emergencies

Kwa mwezi akabakisha sana ni 1mil je atalipia vipi hizo hela zilizobakia kununua gari
Nunua tata mpya lipia sumatra weka barabaran tafuta dereva mzoefu piga kazi....kwa siku hukosi 80....ngariba haogopi mikojo wanaoogopa biashara ya abiria na gari walinunua gari mbovu....

Ungekuwa uko free ungechukua ya mizigo cantre uingie mikoa ya uzalishaji wa mazao hukosi hela ila unatakiwa uwe na moyo wa kitajiri hesabu unayoletewa ni sawa na pasu ya dereva na konda....yaani ukiletewa laki ni laki mbili zilipatikana....piga kazi...
 
Hii kauri sio Valid kwenye huu ulimwengu wa sasa hakuna Biashara ambayo akimbilii kilamtu karne hii.

1)kila mtu anakimbilia biashara ya bodaboda √
2)kila mtu anakimbilia biashara y uwakala √
3)kilamtu anakimbilia biashara ya bajaji √
4)kilamtu anakimbilia kulima √

Kwa kauri hiyo utatafuta Biashaara ambayo watu wengi wajaikimbia huipati na hutafanya biashara.

Sijakataa bali nimempa angalizo kukimbilia biashara iliyopo pasipo ubunifu ni 0 yani mtu unakua wakala haufanyi ubunifu ata wa ofisi?

Sasa wacha wakimbilie iyo biashara ya kuku wataona mziki wake sokoni wateja walewale wauzaji wengi wa kuku, chakula kinauzwa gari n ukizingua bei wanunuzi uwaoni kbxa na kuku muda wa kutok umefik wanakul tu chakula ambapo ni hasara, kutan n chngamoto ya magonjwa kuku wanakua mpk siku 1 watoke wanakufa karibia nusu banda.

Hii business nimeifanya miaka 4 naijua in and out sio namtisha mtu ila inabidi uwe na capita haswa unaweza pata faida mara tano ukaanza na kuku 200 ukafika kuku 1000 ukapata majanga kama ulikua hauna Contigency plan utajuta alafu kumbuka hii biashara imeingiliwa na Macelebrite kama Nandy, Mc pilipili kutake over market inabid uwe smart so kama mtu hajafanya reserch ya kutosha kupata masoko mapya atajuta sana
 
Milioni 45 ushindwe kujenga na kumaliza?

Unaweza nunua hata pagala kuna mapagala unanunua 20 unatumia million 10 kumalizia..

Naona wewe ulivyojenga mwanzo ulipigwa Sana na mafundi..
Huwa nachukia idea ya kununua nyumba iliyojengwa, kwanini usianze yako na ramani yako jinsi unavyopenda,
 
Nani ana michoro mizuri ya banda la kuku lenye usalama wezi wasiweze kuiba na lenye mipangilio mizuri
 
Kwa pesa yako hiyo inabidi kuwa makini sana mkuu kwani hizi hela za mikopo asilimia 95 watu wanazipiga blanda alafu inabaki majuto kwenye makato.
Cha kufanya kwanza usimwage hela yote kwenye biashara moja.

Mimi nakushauri kwa sababu una mtaji mrefu chukua hata m30 au 25 hv wekeza kwenye e-money business na hakikisha unampata kijana mzoefu kabisa na maslahi utampa mazuri kulingana na mwenendo wa biashara.Hapa uchaguzi wa location ndio mchawi mwenyewe ukipata sehemu nzuri then weka M pesa,tigo pesa,aitel money halopesa nmb,crdb,equity kiujumla wakala wa benki zote.

Hakuna muamala utakupita hapa na uzuri wa biashara hii kila siku mtaji wako uko pale pale.Hapa tu zingatia eneo lenye liquidity kubwa na kijana mzoefu plus ofisi iwe rahisi kuonekana.

Kiasi kinachobaki hicho angalia hata kununua longterm asset kama kiwanja na vinginevyo.
 
Madalali wamekaba kila sehemu kuleta ugumu tu ..mbavu zao 😡
Angalizo kwenye hii biashara ya mpunga.

Ni kweli kabisa kwa mahesabu uliyompigia sehemu nyingi ununuzi wa mpunga uko hivyo na siku hizi kila eneo linalolimwa mpunga kuna dalali (sijui kama ni kote ila Morogoro sehemu nyingi wapo) ambapo bila huyo inakuwa changamoto kupata mpunga

Chakufanya ni kutenga muda kuzunguka na huyo dalali ili ujihakikishie upimaji na aina ya mpunga ili kuepuka kununua mpunga mbaya na kupunja kwenye upimaji

Pili ni vizuri kuwa makini kuchagua sehemu ya kutunzia maana baadhi ya magodauni kuna wafanyakazi wasio waaminifu siku ya kuja kuuza mpunga wako kupoteza gunia tano na kuendelea ni kawaida halafu mnarudi kusumbuana kwenye kudaiana

Tatu, wanunuzi wengi wa mpunga uliotunzwa stoo wanalazimisha kununua kwa kilo wakati wewe ulinunua kwa kupima kwa ndoo, hapa mara nyingi inakula kwako maana kwenye zile ndoo mara nyingi kilo hazitoshi hivyo ni vizuri wakati wa kuuza ukoboe uuze mchele

Na mwisho kabisa mpunga ukishafika elfu 60 kwa gunia ukijumlisha na hizo gharama nyingine inafika hadi elfu 71 au elfu 72 usijisumbue kununua labda kama unatunza fedha maana mara nyingi mpunga unaishia elfu 90 au laki moja lakini kwa kupima kwenye mzani ambapo hata kwa dawa gunia moja halitimii

Pamoja na yote hayo biashara ya mpunga ni ngumu kupata hasara ya kupoteza mtaji wote. Utarudisha hela au utapoteza kidogo kama soko litakuwa baya hasa hasa kwa miaka ya hivi karibuni ambapo Tanzania inazuia kuuza chakula nje

Kwa vile yuko DSM afanye survey ya maeneo wanakotunza mpunga na wanunuzi hasa wa kutoka nje wanaenda kununua pale kisha ajisogeze Morogoro maeneo ya dakawa au ifakara kupeleka dsm sio mbali sana japo anaweza kutunzia huko huko
 
Nimejaribu kufuatilia namna unavyo respond kwenye baadhi ya comment za wanaokushauri nimegundua vitu vifuatavyo:-

1. Una uoga wa asili

2. Hauna uwezo wa kukabili changamoto

3. Umekulia mazingira ya wasomiwasomi wengi au

4. Umesoma sana

Nianze na namba 3 na 4, watu wengi waliokulia mazingira ya wasomi wasomi au waliosoma sana (hata degree ya kwanza ni kusoma sana pia) na mazingira hayo yakawa hayana hata mfanyabiashara au mjasiriamali tunakosa uzoefu wa kufanya kitu nje ya ajira.

Namba 1 na 2 vinaweza kuwa matokeo ya namba 3 na 4.

Mtu muoga anaogopa kuanza.
Mtu muoga anawaza hasara kwanza badala ya faida
Mtu muoga hataki usumbufu
Mtu muoga hataki kukosana na watu

Kwenye biashara hivyo vitu HAVIKWEPEKI!

Hakuna biashara isiyo na hasara
Hakuna biashara isiyo na changamoto
Hakuna biashara isiyo na usumbufu
Na biashara nyingi lazima kuna kutofautiana hata na mteja tu achilia mbali uliowaajiri

Ukishajihisi ni muoga wa kupoteza, muoga wa usumbufu, muoga wa kukosana na watu achana na biashara zinazohusisha watu kwasababu kwanza sio lazima kila mtu afanye biashara na wala si kila mmoja anaweza kufanya biashara

Ni kweli kabisa tunahitaji kuwa na kipato cha ziada ila kuna vitu havifanywi na kila mtu.

Ushauri wangu kwako

Kwasababu angalau mwenzetu unauwezo wa kupata mamilioni yote hayo, kuna uwekezaji ambao unaweza kufanya usio na usumbufu

Mimi huwa naamini uwekezaji ni tofauti kidogo na biashara japo vinashabihiana

Unaweza kufanya moja kati ya vifuatavyo:

1. Tafuta kampuni inayopata faida kanunue hisa huko

2. Tafuta eneo (sio lazima iwe dsm), jenga stoo (sijui ndo godown) ambapo wakulima watakuwa wanatunza mazao yao huko kwa kulipia ushuru

3. Nunua mashine ya kusaga na kukoboa weka kwenye hiyo stoo kupanua wigo wa mapato

Katika hivyo vitatu sio rahisi kuibiwa pesa kizembe, hazina stress, hazina purukushani wala hazikuhitaji kuwepo kila siku japo kwenye mashine hapo utahitajika kuweka ndugu yako au mtu unayemuamini atukuibia ila hatakuibia sana
Umemueleza vyema sana muomba ushauri, hakuna biashara isiyo na changamoto hapa duniani,

Mtoa mada fuata ushauri wa huyu mwamba hapa
 
Back
Top Bottom