Nina mtaji wa milioni kumi; nifanye biashara ipi kati ya hizi nilizochagua?

Nina mtaji wa milioni kumi; nifanye biashara ipi kati ya hizi nilizochagua?

Kama siyo rahisi kwako usidhani kwa wengine pia yatakuwa ni magumu. Kaa na ujifunze kwa wale wenye pesa ili nawe upate kujua njia za kuipata pesa.
Sijui niseme unachekesha au unasikitisha.

Boss,10m haikupi faida ya 4m achilia mbali 8m.

Labda kama tumeamua kutaniana hapa.
 
Chief, mimi nilikuwa mwajiriwa wa company moja ya mauzo apa mjini, nafasi niliyokuwepo ilikuwa inamezewa mate na watu wengi mno.

Fitina nyingi aisee, nilipigiwa simu mpaka na waganga, wananiambia wanafuatwa na watu wafanye mpango ning'olewe kazini.

Nimekuja kustuka sina hamu na kazi plus uvivu uvivu, sijakaa sawa nikalizwa mamilioni ya pesa aisee.

Haya mambo we acha tu
Hahahah wew ulichezewa mchezo wa kitapeli na wahuni,

Yan mganga atafute namba yako et watu wanataka kukutoa kazini? Labda kama ni mganga huyo huyo ndio alikupa cheo
 
Shukrani kwa maoni,, niende na ipi hapo sasa.?
Boss fuata oder hii utapo fanya maamuzi ...
3
2
1
4

Biashara inayohusu wanawake utatoboa mkuu ... wanaume tunakomaa huko kwenye makazi na maBiashara mengine ..tunatuma na yakutolea ..kwaajili ya kusuka ... wanakuja kununua rasta kwako ...na wanabadili mitindo kila siku ..leo bambucha kesho sijui yeboyebo ...kazi kweli kweli
 
Back
Top Bottom