Nina mtaji wa milioni kumi; nifanye biashara ipi kati ya hizi nilizochagua?

Nina mtaji wa milioni kumi; nifanye biashara ipi kati ya hizi nilizochagua?

Biashara zote hapo zinawezekana kasoro ya vifaa vya ujenzi mtaji wako ni mdogo.
Ya vyombo vya nyumbani naikataa, haina mzunguko mkubwa inataka location nzuri zaidi kuliko hizo nyingine.

Ya small electronics, gadgets na accessories ina mzunguko mkubwa zaidi. Ila kila biashara inataka upewe codes zake kabla ya kuingiza mtaji mazima.
Hapo nmekupata japo kuna sehemu Dar hyo business ya vyombo vya ndani inafanywa na watu wengi kwny hilo eneo lakn wote wana mzunguko mzuri
 
Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu amfanyaye mwanadamu kuwa Kinga yakee....ushawahi jiuliza uyo mganga akifa utafanyaje...mganga mwenyew anategemea pumzi ya Mungu Mkuu kuishi
Huku kusini kulikuwa na daktari mmoja akiitwa mwambe huyu ndie alikuwa daktari bingwa wa mifupa kusini yote hii ilimtegemea yeye ila alipofariki wakatokea wengine na wanasaidia watu
 
Kuna bi mkubwa mstaafu Serikalini ameanzisha day care yake ya kihali ya chini, kutokana na muitiko wa ile idea yake pale mtaani kwa sasa ana uhakika wa kupata watoto 40 hadi 50 kwa siku, then hapo kila mtoto kwa siku anaenda na elfu 1 ya chakula na mwisho wa mwezi elfu 30 kama ada, bibi anakula pension yake kiurahisi mno
mwanzo hii sikuwahi kujua siri iliyo ndani mwake mpaka nilipoalikwa kwenye sherehe kama mbili hivi za daycare kama mgeni rasmi ndo nikajua tena baada ya kumkuta professor akaniambia na yeye anayo shule ya hivyo.
 
kwangu mimi ningekushauri ufanye biashara ya kwanza kwa haraka ndio naona nafsi yako inaitazama kwanza na ndio maana ni ya kwanza hata kuitaja.
biashara hii haihitaji mtaji mkubwa sana na hasa ukiuza vyombo vya watu wa kati na mama lishe hivyo mtaji wa m6 unaweza tosha kwa kuanzia.
katika vyombo vyako weka vyombo vya kawaida vingi na vile vya thamani vichache 70:30 itakaa sawa.
 
Habari ya muda huu wakuu, poleni na majukumu ya kila siku. Mimi kama kijana nimeamua rasmi kujikita kwenye kufanya Biashara maana ndiyo ndoto yangu ya siku nyingi sana.

Binafsi nimepambana hapa na pale nimebahatika kupata mtaji wa Tsh Milioni 10 hivyo nmeamua kujikita rasmi kwenye Biashara na kwa kufikiria nimepata mawazo ya Biashara 4 ambazo binafsi ninazipenda na kuzimudu..

1. BIASHARA YA KUUZA VYOMBO VYA MAJUMBANI
-Hapa nitahusisha uuzaji wa vyombo mbalimbali ambavyo vinatumika kwenye majukumu ya kila siku majumbani kama (Masufuria, Hotpots, Vijiko, Visu, Madeli, Ndoo za maji, Mabeseni, Chupa za Chai, Viti & Meza za plastic, Majaba etc)

2. BIASHARA YA NGUO NA PRODUCTS MBALIMBALI ZA WATOTO(0-3YEARS)
-Hapa itahusisha kuuza products mbalimbali za watoto wachanga hadi miaka mitatu(3) kama vile (Nguo, Nepi, Viatu, Kofia, Neti, Beseni za kuogea, Toys km Vigari & Midoli, Poda & Sabuni za watoto etc)

3. BIASHARA YA BIDHAA MBALIMBALI ZA UREMBO NA VIPODOZI VYA WANAWAKE
-Hapa nitahusisha bidhaa kama(Perfumes, Rasta, Lotions, Poda, Hereni, Lipstics, Cheni, Nguo za ndani,Madela etc)

4. BIASHARA YA VIFAA MBALIMBALI VYA UJENZI WA NYUMBA NA VIFAA VYA ELECTRONICS
Wakuu naombeni USHAURI kwa uzoefu wenu ni Biashara ipi hapo yenye return kubwa na bidhaa zake ni more Liquid (Rahisi kuuzika kwa haraka) na ni sehemu gani naweza kupata hzo bidhaa kwa urahisi na Bei nafuu kwa DAR ES SALAAM na changamoto pia za hyo biashara husika na kama itapendeza Location nzuri ya kufanya hyo biashara kwa DAR.

NINAWASILISHA KWENU WADAU KWA USHAURI.
Mkuu twende No.3 nina aunt yangu alimpandia mtu kariakoo pale mpaka kumtoa mil28 na kodi analipa 600k kwa mwezi.

Japo umetuwekea limit ila kuna biashara ya spare hii mkuu ukipata watu sahihi kutoboa ni 90%.
 
kitaaluma na kadri ya vimafunzo vyetu tulivyofundishwa vingine kwa kugoogle na vingine darasani unaweza kufanya yafuatayo kabla hujaamua kuchangua mradi:-
  1. uwezo muda na uzoefu wa biashara unayotaka kufanya
  2. kuna faida?
  3. soko likoje? hapa tunazungumza uhitaji na idadi ya wauzaji wengine?
  4. mtaji
  5. uchangiaji wa mahitaji ya familia ukoje?
 
kwangu mimi ningekushauri ufanye biashara ya kwanza kwa haraka ndio naona nafsi yako inaitazama kwanza na ndio maana ni ya kwanza hata kuitaja.
biashara hii haihitaji mtaji mkubwa sana na hasa ukiuza vyombo vya watu wa kati na mama lishe hivyo mtaji wa m6 unaweza tosha kwa kuanzia.
katika vyombo vyako weka vyombo vya kawaida vingi na vile vya thamani vichache 70:30 itakaa sawa.
Hapo nmekupata mkuu nahsi kwny uthamani wa vyombo itategemea zaidi na location ntayoipata na aina ya watu wanaopatikana hapo...
 
kitaaluma na kadri ya vimafunzo vyetu tulivyofundishwa vingine kwa kugoogle na vingine darasani unaweza kufanya yafuatayo kabla hujaamua kuchangua mradi:-
  1. uwezo muda na uzoefu wa biashara unayotaka kufanya
  2. kuna faida?
  3. soko likoje? hapa tunazungumza uhitaji na idadi ya wauzaji wengine?
  4. mtaji
  5. uchangiaji wa mahitaji ya familia ukoje?
Hakika hvi ni vitu muhmu sana ubongo inabdi utulie sana hapo
 
Mambo ya
Business proposal
SWOT
E.t.c
Naonaga ujinga tuuu...
Sawa niliyasoma chuo ila niliyakariri ili nifaulu darasani ila ukija mtaani ukitaka kutoboa....
1. Anzisha biashara
2. Weka bei kama ulizozikuta sokoni
3. Soma MCHEZO ukiwa mchezoni
4. Tafuta taarifa field
5. Tafuta waliokutangulia wakuongoze na kukupa hint

Makaratasi na mambo hayo ya darasani TUPA HUKOOOO

#YNWA
Ndioa maana vibiashara vyenu havidumu.. mnakuja kulia lia humu.

Kila kitu lazima ukifanyie tathmini na sio kwenda blindly..

Proposal na Biz plan ni muhimu. Hayo uliyoyataja maswala ya kutafuta taarif field, kwa waliotangulia etc ni moja ya feature za biz plan.

Pre assessment kwanza na sio ujitumbukize humo then uanze kulaumu watu labda kama hela sio yako, ila hela hizi za mikopo au za kukusanya muda mrefu kwa jasho na damu unatakiwa uende kwa umakini mno mno.
 
Ni sahihi Mkuu, ila kwa kiasi alichonacho cha milioni 10 nadhani haitatosha labda kama anaweza kuanza kuwa dealer wa Saruji na vifaa vichache vya Plumbing

Maana ukiagiza mifuko 300 ya Saruji utatakiwa kuwa na shilingi 4,576,000 hapo ukiagiza kiwandani
Anachotakiwa ni kuwa na connection na warehouses, ikitokea mtu kataka mifuko mingi kwa muda mdogo anavuta waya mifuko inakuja kwa haraka.

Cement, nondo, mbao, mabomba sio vitu vya kuumiza kichwa.

Hapo akili awekeze ktk vifaa vya Umeme aweke mzigo unaoeleweka.
 
Back
Top Bottom