Nina mtaji wa milioni kumi; nifanye biashara ipi kati ya hizi nilizochagua?

Nina mtaji wa milioni kumi; nifanye biashara ipi kati ya hizi nilizochagua?

Ingawa hujaipendekeza, biashara ya chakula inalipa sana. Maana kula hakuna option Mkuu. Ila tafuta sehemu yenye mzunguko mkubwa wa watu. Vilevile, unaweza kuspecialize kwa kuuza product fulani tu e.g supu ya kuku wa kienyeji, nyama choma ya kuku wa kienyeji etc.
Anhaaa pamoja sana kiongozi
 
Mkuu
Biashara ya vyombo vya nyumbani ina faida nzuri ya mpaka 45% ila changamoto yake ni mzunguko
Kwahiyo hapo lazima uzingatie sana location Mf. Eneo ambalo lina hostel za wanachuo, au kambi ya jeshi au eneo lenye mwingiliano mkubwa wa watu wanao enda na kutoka majumbani mwao

Vile vile inategemea utakuwa umewalenga watu wa aina gani kwahiyo aina ya vyombo utaleta kutokana na aina ya wateja wako kama ni changanyikeni vyombo plastic vinatoka zaidi kuliko glass na udongo ila kama ni ushuan glass na udongo ndio zinatoka zaidi

Uzuri wa duka la vyombo unaweza kuweka bidhaa zingine kama fane, mafagio, kapeti, mito, Net, stand za mikoba na viatu, mapazia N.k unaweza kuwa unaongeza aina za bidhaa kulingana na uhitaji wa wateja wako.
Karibu vyomboni.
machimbo take wapi
 
Habari ya muda huu wakuu, poleni na majukumu ya kila siku. Mimi kama kijana nimeamua rasmi kujikita kwenye kufanya Biashara maana ndiyo ndoto yangu ya siku nyingi sana.

Binafsi nimepambana hapa na pale nimebahatika kupata mtaji wa Tsh Milioni 10 hivyo nmeamua kujikita rasmi kwenye Biashara na kwa kufikiria nimepata mawazo ya Biashara 4 ambazo binafsi ninazipenda na kuzimudu..

1. BIASHARA YA KUUZA VYOMBO VYA MAJUMBANI
-Hapa nitahusisha uuzaji wa vyombo mbalimbali ambavyo vinatumika kwenye majukumu ya kila siku majumbani kama (Masufuria, Hotpots, Vijiko, Visu, Madeli, Ndoo za maji, Mabeseni, Chupa za Chai, Viti & Meza za plastic, Majaba etc)

2. BIASHARA YA NGUO NA PRODUCTS MBALIMBALI ZA WATOTO(0-3YEARS)
-Hapa itahusisha kuuza products mbalimbali za watoto wachanga hadi miaka mitatu(3) kama vile (Nguo, Nepi, Viatu, Kofia, Neti, Beseni za kuogea, Toys km Vigari & Midoli, Poda & Sabuni za watoto etc)

3. BIASHARA YA BIDHAA MBALIMBALI ZA UREMBO NA VIPODOZI VYA WANAWAKE
-Hapa nitahusisha bidhaa kama(Perfumes, Rasta, Lotions, Poda, Hereni, Lipstics, Cheni, Nguo za ndani,Madela etc)

4. BIASHARA YA VIFAA MBALIMBALI VYA UJENZI WA NYUMBA NA VIFAA VYA ELECTRONICS
Wakuu naombeni USHAURI kwa uzoefu wenu ni Biashara ipi hapo yenye return kubwa na bidhaa zake ni more Liquid (Rahisi kuuzika kwa haraka) na ni sehemu gani naweza kupata hzo bidhaa kwa urahisi na Bei nafuu kwa DAR ES SALAAM na changamoto pia za hyo biashara husika na kama itapendeza Location nzuri ya kufanya hyo biashara kwa DAR.

NINAWASILISHA KWENU WADAU KWA USHAURI.
Namba 2 ni best kwako Kwa kuzingatia yafuatayo,mtaji wako si mkubwa,ni biashara yenye uhakika wa mauzo Kila cku na hii itakusaidia kwenye mahitaji,vifaa vya ujenzi yes ni biashara nzuri ila kama huna capital nzuri itakufrastate na usitamani Tena biashara,Anza na simple business Kisha mtaji ukikua wekeza kwenye biashara zinazohitaji mtaji mkubwa
 
Namba 2 ni best kwako Kwa kuzingatia yafuatayo,mtaji wako si mkubwa,ni biashara yenye uhakika wa mauzo Kila cku na hii itakusaidia kwenye mahitaji,vifaa vya ujenzi yes ni biashara nzuri ila kama huna capital nzuri itakufrastate na usitamani Tena biashara,Anza na simple business Kisha mtaji ukikua wekeza kwenye biashara zinazohitaji mtaji mkubwa
Thanks boss,, vp ushawahi ifanya hyo no.2
 
No2. No 3. Hizi ndo za kufanya moja wapo lakini yenye kipao mbele zaidi ni No 3. Pkj
1. Tafuta eneo ambalo ni chipkizi, means eneo ambalo limeanzishwa kukua wilaya ama kijiji. Sababu watu asilimia 90 hawatokuwa wakienda mjini lazima watanunua kwako tu. NB. Bei ya bidhaa iwe sawa na ile ya mjini na hata kama itapanda ipande sio zaidi ya 500. Kwajili ya usafiri no.
2.uwe na pesa ya kadi, TRA, na halimashauli nje na mtaji walau kwa mwaka, then unapoendelea kufanya biashara itakuwa includi taratibu.
3.weka bidhaa zenye mzunguko zinazonunuliwa kwa wingi.
4. Epuka wanawake kama wewe ni mwanaume.
5. Tafuta sehem unapoweza nilunua bidhaa zako kwa jumla ikiwezekana nunua bidhaa tokea kiwandani ili uwe na access ya kuuza kwa jumla ama leje leja.
7. Zingatia mda wa kufungua na kufunga .
8. Lugha ya biashara na uchangamfu kwa wateja.

Asante.
 
No2. No 3. Hizi ndo za kufanya moja wapo lakini yenye kipao mbele zaidi ni No 3. Pkj
1. Tafuta eneo ambalo ni chipkizi, means eneo ambalo limeanzishwa kukua wilaya ama kijiji. Sababu watu asilimia 90 hawatokuwa wakienda mjini lazima watanunua kwako tu. NB. Bei ya bidhaa iwe sawa na ile ya mjini na hata kama itapanda ipande sio zaidi ya 500. Kwajili ya usafiri no.
2.uwe na pesa ya kadi, TRA, na halimashauli nje na mtaji walau kwa mwaka, then unapoendelea kufanya biashara itakuwa includi taratibu.
3.weka bidhaa zenye mzunguko zinazonunuliwa kwa wingi.
4. Epuka wanawake kama wewe ni mwanaume.
5. Tafuta sehem unapoweza nilunua bidhaa zako kwa jumla ikiwezekana nunua bidhaa tokea kiwandani ili uwe na access ya kuuza kwa jumla ama leje leja.
7. Zingatia mda wa kufungua na kufunga .
8. Lugha ya biashara na uchangamfu kwa wateja.

Asante.
Shukrani sana kiongozi somo kubwa sana hili
 
BIASHARA YA VIFAA MBALIMBALI VYA UJENZI WA NYUMBA na Biashara ya hoteli kuuza chakula hizo ndio Biashara nzuri zitakayo kuletea pesa kwa haraka kuliko biashara nyingine ulizo zitaja. Swali langu umezaliwa tarehe gani na mwezi gani?yaani unajijuwa wewe ni mtu wa nyota gani? ukinijibu swali langu nitakwambia kitu chakufanya kizuri zaidi.
Mim nimezaliwa tarehe 8 mwez WA 11
 
Naludia tena kama ww ni Bible mkononi na rozali shingon hutanielewa nikizungumzia chuma ulete ila wajanja wanajua hii kitu.chuma ulete,chuma ulete kua makini sana kabla mlango wabiashara hujaufungua siku yakwanza funga geti lachuma ulete.utanikumbuka haya.
Tupe elimu na mbinu hzo kiongozi
 
Back
Top Bottom