Nina mtaji wa Tsh. 200 Milioni, ninataka kuwekeza katika biashara ya mbao kule Mafinga

Bwenyenye254

Member
Joined
Mar 13, 2021
Posts
52
Reaction score
85
Habari Wana JF,

Mimi ni mwanabiashara kutoka Nairobi, Kenya. Ninafanya biashara katika sekta za Ujenzi na Real Estate.

Katika pilka pilka za kibiashara, nimekuja kuugundua mji wa Mafinga. Mji wa Mafinga unajulikana kama mji wenye mbao na miti mingi zaidi Tanzania. Kwa sekta yangu ya Ujenzi hapa kenya, kuna demand kubwa sana ya Mbao kwa hivyo soko itakuwa ni hapa Kenya.

Kama nilivyosema kwenye mada, nina mtaji wa millioni mia mbili pesa za Tanzania.

Ningependa kuwekeza katika hii sekta ya mbao kwa kuweka sawmill hapo mafinga.

Je, ni kweli kwamba miti iko available easily?

Biashara hii wakenya tunaruhusiwa kujihusisha nayo pia?

Ninaweza kupata shamba la ku-lease ili niweke hiki kiwanda? Kulease kiwanda itagharimu pesa ngapi hivi per acre.

Mapato ya hii sekta hukuwa vipi?

Bei ya sawmill kule Tanzania ni pesa Ngapi? Hapa Kenya inaanzia Tsh. 60 million kuendelea.

Bei ya miti mafinga ni ngapi hivi?

Nikifanya biashara Mafinga nitaishi wapi? Ningependelea mji ambao ni upper-middle class kwendelea.

Kuna Ndege zinazokwenda route ya Mafinga au Iringa to Arusha?

Kuna taratibu nyingine maalamu kwenye hii biashara ambazo ninafaa kuzijua?

Je, hii biashara inalipa?

Ninaomba ushauri wenu.

Ninashukuru.
 
Ni kweli mji wa mafinga, na mufindi yote kwa ujimla pia mkoa wa njombe kuna miti mingi sana mbao nyingi sana za kutosha.

Kuhusu makazi pindi utakapo kua Tanzania kama uta chagua mafinga tafuta nyumba hapo hapo huwezi kukosa, pia mafinga hakuna kiwanja cha ndege hata iringa sidhani labda uchukue ndege ya arusha Dar mbeya ukitua mbeya uchukue costa mpaka mafinga sio mbali ni mwendo wa saa moja na nusi au saa moja tu kuhusu kibali cha kusafirisha Kenya sifahamu na menginyo wanakuja.
 
200000000 dah aisee siku nikizipata hizi kwanza nanunua gari ambalo juu liko wazi.pili nanunua nyumba tatu naweka fixed account nabaki na million 20 tu za biashara ya kunipa wese route za singida dodoma dar masasi songea mtwara ...ni full unyama
 
Iringa uwanja upo ,,halafu mbeya-mafinga sio saamoja Ni masaa manne mpaka tano kwa coaster
 
Kiwanja kipo kwenye marekebisho hapo Iringa, kwa sasa atapanda Kapricon bus mpaka Arusha.
 
Ingia ground ufanye research yako mwenyewe ukiweza hata piga camp mwezi mzima ukifuatilia na kujua facts zote kuhusu hiyo biashara ya mbao na Mafinga kwa ujumla, ukianza business never ever take a short cut , fungua kampuni na fuata sheria zote inavyotakiwa lasivyo wabongo watakugeuza fursa na utaondoka kurudi kenya bila hata senti tano huku ukitukana matusi non stop
 
Aise hyo hbr za kuchukuwa Costa uje mafinga kutokea mbeya siyo lzm muda wowote unakula mbanga na lorry za kutosha


Bwana mk fanya namna uje dm tuyajenge Kama upo serious tuende nikupeleke huko tufanye reseach yetu Kisha ukajipange sas kwa kuanza kazi

Andaa tz 2 million for research only
 
Mtaji mkubwa sana huo hongera Bwanyenye.
Nakushauri kule Mafinga usiende kama mwekezaji utapigwa, nenda kama unazuga unataka kuishi halafu anza kuchukua ardhi "grabbing" utapata ardhi kubwa kwa bei ndogo ndani ya mwaka ndio uanze uwekezaji wako. Ukienda kama investor itakugharimu mkuu.
Kila la kheri
 
Nicheki DM!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…