Nina mtaji wa Tsh Milioni 20, nataka kufanya biashara ya ng'ombe

Nina mtaji wa Tsh Milioni 20, nataka kufanya biashara ya ng'ombe

Ipi hiyo boss?
Kwa pesa hiyo sio ndogo kwamaana kuna watu wananunua ngo'mbe 10 wanakuja wanawauza kisha wanafuata wengine na maisha yanakwenda vizuli . Unaweza kuanza lkn kabla ya yote fanya kwanza ujue soko nk . Nimekupa wazo la biashara yako, sasa tutoke hapo boss

Bonafsi sikushauli kufanya biashara hiii kwa maana ina changamoto nyingi sana, kama unataka biashara ya kusafili , nenda kanunue mahindi, maharage lete dar , utauza, peleka manze pale madalali wanakupa mteja unaenda unauza, maharade unaweza peleka tandika nk ..

Lkn kuna biashara nyingi ambazo kwa mtaji wako unaweza fanya tu, kuna jamaa ana mtaji wa milion 10 , tigo pesa, m-pesa, nmb wakala ,crdb wakala nk , kwa mwezi anapata faida ya milioni 2. Kuna mtu ana mtaji wa milioni 4 anafanya biashara ya kuuza vinywaji lain julma na reja reja, soda maji, juic nk kwa mwezi anapata faida ya laki 9.

, nimekupa mchanganuo huo, lkn kuna biashara moja siwezi weka hapa njoo mp nikulishe madini,
Ng'ombe watakufilisi
 
Mkuu karibu.
Nilishafanya ya mbuzi mwaka 2018 na hao kidogo.
Hiyo pesa kwa ng'ombe halitoshi labda uanze kwa kuunga kwa mzoefu.
Kuna gharama nyingi kama:
-Kupiga kambi ya manunuzi(Centre)
-Ukusanyaji na uswgaji toka minadani(Wapo unawalipa)
-Kuzunguka kwenye minada(Wasaidizi utawakuta huko)
-Malisho ya hao ambao ushawanunua(Utanunua nyasi au mashudu)
-Malipo ya uhifadhi na mlinzi
-Matibabu kwa watakaopata homa
-Upakiaji na Usafirishaji
-Ushuru na vibali vingine
-Machawa nao wamo(watoa miongozo)
NB:Nenda pale mabibo mwisho mtafte tajiri mmoja anaitwa Halubu
Nipe ABC ya mbuzi mkuu.
 
Nipe ABC ya mbuzi mkuu.
Uwe na mtaji.
Manunuzi kwa mbuzi wengi ni dodoma minadani.
Uwe na mtu anaeifahamu minada na anafahamika na magalagaja wa minadani.
Manunuzi yanaanza asubuhi mpaka mchana kazi imeisha.
Baada ya manunuzi ataachumiwa mshagaji atapakia kwenye gari kuwaleta mjini kwenye kituo cha uhifadhi.
Gari utalipia,mswagaji na kituo cha utunzaji.
Utazunguka minada kadhaa kukusanya,ukitimiza idadi kulingana na mtaji wako utakodi gari kama unao wachache utaunga gari na wengine ila lazima mbuzi wako uwawekee alama maalumu.
Kituo kikuu cha mauzo ni pugu.
Pia waweza andaa wateja wako.

WAKATI NAFANYA 2018
Mnadani kwa kila mbuzi ushuhuru 2000
Pungu kwa kila mbuzi ushuru 2000
Maji na majani ya kulishia utanunua
Wapakiaji na washushaji utawalipa ww
 
Hakuna biashara rahisi hata kidogo nashangaa kuona watu wengi wakitoka negative sana kwenye hii biashara ila cha kushangaza kila siku ng'ombe zinachinjwa na nyama inalika. Kwani wao wanaofanya sio watu na swali la msingi nikujua jinsi yakupambana na changamoto hizo za biashara full stop. Muomba ushauri anzia pugu pata ABC za biashara then ingia mzigoni usikatishwe tamaa eti kwa sababu flani alifanya akashindwa na ww ukifanya utashindwa hiyo ni BiG NO. Kushindwa kwake ni kushindwa kuhandle changamoto hiyo biashara. Utamu wa ngoma ingia kati ucheze mwenyewe bro. Ukitaka kujua kuwa hakuna biashara rahisi. Andaa uzi mwingine wa hizo biashara ambazo umeambia ni bora ufanye kuliko hiyo ya ng'ombe alafu utaona wadau watakavyokuambia changamoto zake na mwisho watakupa mawazo mengine ya biashara zingine. Nawasilisha
 
Mkuu kabla ya yote nenda Mnada wa Ngombe pugu Ujuwe Bei ya kuuzia Then njoo Utembelee minda ya Wilayani KITETO husisani Mnada wa Dosi Dosi tarehe 01/14 Kwa mwezi mara mbili na Mnada wa Kibaya 02/15. Bei za Ngombe kipindi hichi zipo chini sana, Nakushauri ununue Ng'ombe 50 Kwa laki 4 Kwa Moja, unawanenepisha Hadi mwezi wa Tisa/(09) Unawauza Kwa Milioni Hadi Milioni na laki nne,
Bei ya kukodi eneo la malisho haezidi laki Tano, Mchumgaji ni Elfu sabini Kwa mwezi unaweka wawili,. Kwanzia mwezi wa Saba unanunuwa mabua masjambani unawalisha wanenepe, mabua ekari mia ni laki Saba, wanakula Hadi mwezi wa kumi.
Siwezi kueleza yote , wewe njoo ujifunze kwanza then ndio ufanye biashara. Njoo na nauli tu na gharama za lodge, ujifunze tutakupa watu wanaofanya hiyo kazi uone ugumu na changamoto zake zilivyo nyingi
Mkku nami naitaji muongoz nimekufata inbox!
 
Mkuu kabla ya yote nenda Mnada wa Ngombe pugu Ujuwe Bei ya kuuzia Then njoo Utembelee minda ya Wilayani KITETO husisani Mnada wa Dosi Dosi tarehe 01/14 Kwa mwezi mara mbili na Mnada wa Kibaya 02/15. Bei za Ngombe kipindi hichi zipo chini sana, Nakushauri ununue Ng'ombe 50 Kwa laki 4 Kwa Moja, unawanenepisha Hadi mwezi wa Tisa/(09) Unawauza Kwa Milioni Hadi Milioni na laki nne,
Bei ya kukodi eneo la malisho haezidi laki Tano, Mchumgaji ni Elfu sabini Kwa mwezi unaweka wawili,. Kwanzia mwezi wa Saba unanunuwa mabua masjambani unawalisha wanenepe, mabua ekari mia ni laki Saba, wanakula Hadi mwezi wa kumi.
Siwezi kueleza yote , wewe njoo ujifunze kwanza then ndio ufanye biashara. Njoo na nauli tu na gharama za lodge, ujifunze tutakupa watu wanaofanya hiyo kazi uone ugumu na changamoto zake zilivyo nyingi
Hii imetoa mwanga sana sana
 
Msaada nenda Pugu utapata ABC kwa hao wauzaji. Sidhani kama wamo humu.

Siyo kejeli ila ni ukweli.

Ni biashara inalipa kama utavumilia nakushauri kachukue msukuma mmoja anayenunua mikoani uungane naye. Ni waaminifu .
Sahihi
 
Kwa mtaji wako tafuta biashara nyingine labda ingekuwa m200
Mbona mnapenda kukatisha tamaa watu, ml 20 ni ndogo wakati ng'ombe mkubwa ana range 400000-1500000. Ukichukua 15 tu wa kusimamia ml 1 na utabakiza 500000 ambayo mtachanga na wafanga biashara wenzio nauli ya gari coz huoakii peke ako.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Hao ng'ombe unaowaona hapo pugu wakubwa na wanono ni process mkuu...... Hununuliwa wakiwa wadogo au wamekonda na kulishwa vizuri kwa kipindi fulani kabla ya kuuzwa tena au kusafirishwa kuja hapo pugu........ Kwa kawaida kununua ng'ombe aliyekamilika ni ghali na ngumu kuwapata kwani wafugaji huuza ng'ombe dhaifu na wadogo na mara chache wazuri kwa dharura!!! Biashara hii ni nzuri kama utakuwa na reliable source ya kuwapata kwa bei poa..... Obheja nkwela!!!
 
Mbona mnapenda kukatisha tamaa watu, ml 20 ni ndogo wakati ng'ombe mkubwa ana range 400000-1500000. Ukichukua 15 tu wa kusimamia ml 1 na utabakiza 500000 ambayo mtachanga na wafanga biashara wenzio nauli ya gari coz huoakii peke ako.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Tena siku hizi wala hakuna kuhangaika kupeleka huko
Ukipata wanunuzi wa Dar wanakuja hapo hapo na kubeba mzigo na faida yako unaiona tayari
Unaingia tena kutafuta
Mbona inalipa vizuri
 
Back
Top Bottom