Nina mwaka wa sita sijavaa pete ya ndoa, je ni kosa?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Kutokana na changamoto ya kunenepa vidole, imepelekea pete zetu kuwa ndogo, na kuonekana kama adhabu pale tunapo zivaa.

Kwa upande wangu, ni mwaka wa sita huu huwa sivai pete ya ndoa zaidi ya kuishi katika maadili ya ndoa tu.

Hii imepelekea wadada kujipitisha pitisha, wakiamini nipo singo; na wale waliobahatika kuonja mvinyo, hawataki kuniacha niende.

Je, kutokuvaa pete ya ndoa ni makosa?​
 
Sasa je makosa ni yetu au yenu
Makosa ya kunyima unyumba hiyo BIla kipingamizi ni yenu.Kuhusu makelele inategemea.

Kuhusu Tamaa ukimpa Mwanaume wako mapenzi yote sio kumnyima hata akipita huko mtaani amwone mwanamke mzuri vipi hawezi kuwaza kuzini.
 
Peleka sonara wakaitanue acha visingizio vya kuhalalisha zinaa

Sent from my SM-N975U using JamiiForums mobile app
 

Sisi waislam tunavaaa Pete za majini tuuu na hatuna shida mbona
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…