Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
Huwezi kunikuta hata siku moja nikisema Asante Samia kwa kujenga hospitali, au barabara au shule.
Hata siku moja huwezi kuniona nikisema asante Samia kwa kupeleka maji sehemu ya Tanzania au umeme.
Haya ni majukumu ya msingi ambayo Serikali yeyote inapaswa kuyafanya na Wananchi hawapaswi kushukuru Serikali inapotimiza wajibu wake wa msingi. Pia haya yote yanafanywa kama majukumu ya msingi kwa kodi zetu sisi Watanzania! Hakuna kiongozi anayetoa fedha zake mfukoni kufanya haya.
Kuna maeneo machache ambayo mtu anapaswa kupewa sifa au shukrani binafsi.
Sote tunafahamu nafasi ya Tanzania kimataifa ilishuka sana awamu ya 5. Kuna fursa nyingi ambazo kama nchi tulianza kuzikosa kutokana na Magufuli kuharibu sana suala la Mahusiano ya Kimataifa.
Tuliona mikutano mikubwa ikienda kufanyika Rwanda huku Rwanda wakijibrand kimataifa kufikia hata kuizidi Tanzania na wakichukua fursa mbalimbali za Kiuchumi.
Kusema ukweli, Rais Samia amefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuinua tena nafasi ya Tanzania kimataifa.
Kufanyika kwa mikutano mikubwa kama huu wa Nishati sio tu kunaifanya Tanzania kujulikana zaidi ila kunaongeza fursa za Tanzania kiuchumi ikiwemo kuongeza wageni mbalimbali wanaotembelea nchi yetu na pia kuzidi kuipa nchi fursa zaidi za kiuchumi.
Vitu vya namna hii ndo watu wenye akili wanaweza sema tumpongeze Rais Samia maana masuala haya sio majukumu ya msingi ya Serikali bali ni juhudi binafsi za mhusika ndizo zinasababisha haya.
Bado nina shida kubwa na CCM ila kwa kuinyanyua hivi Tanzania Kimataifa, hongera Samia
Hata siku moja huwezi kuniona nikisema asante Samia kwa kupeleka maji sehemu ya Tanzania au umeme.
Haya ni majukumu ya msingi ambayo Serikali yeyote inapaswa kuyafanya na Wananchi hawapaswi kushukuru Serikali inapotimiza wajibu wake wa msingi. Pia haya yote yanafanywa kama majukumu ya msingi kwa kodi zetu sisi Watanzania! Hakuna kiongozi anayetoa fedha zake mfukoni kufanya haya.
Kuna maeneo machache ambayo mtu anapaswa kupewa sifa au shukrani binafsi.
Sote tunafahamu nafasi ya Tanzania kimataifa ilishuka sana awamu ya 5. Kuna fursa nyingi ambazo kama nchi tulianza kuzikosa kutokana na Magufuli kuharibu sana suala la Mahusiano ya Kimataifa.
Tuliona mikutano mikubwa ikienda kufanyika Rwanda huku Rwanda wakijibrand kimataifa kufikia hata kuizidi Tanzania na wakichukua fursa mbalimbali za Kiuchumi.
Kusema ukweli, Rais Samia amefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana kuinua tena nafasi ya Tanzania kimataifa.
Kufanyika kwa mikutano mikubwa kama huu wa Nishati sio tu kunaifanya Tanzania kujulikana zaidi ila kunaongeza fursa za Tanzania kiuchumi ikiwemo kuongeza wageni mbalimbali wanaotembelea nchi yetu na pia kuzidi kuipa nchi fursa zaidi za kiuchumi.
Vitu vya namna hii ndo watu wenye akili wanaweza sema tumpongeze Rais Samia maana masuala haya sio majukumu ya msingi ya Serikali bali ni juhudi binafsi za mhusika ndizo zinasababisha haya.
Bado nina shida kubwa na CCM ila kwa kuinyanyua hivi Tanzania Kimataifa, hongera Samia