Nina siku tatu Mbeya, katika kuzunguka mitaani tayari nimeshuhudia kina mama watano wakiporwa handbag na waendesha pikipiki!

Nina siku tatu Mbeya, katika kuzunguka mitaani tayari nimeshuhudia kina mama watano wakiporwa handbag na waendesha pikipiki!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kitu kimoja nimeona Mbeya tofauti na mikoa mingine ni wingi wa Bajaji hizi na bodaboda. Ni nyingi hadi zinakera. Naambiwa kwamba wingi wake umeletwa na Tulia Foundation ya spika wa Bunge ambaye amekuwa akiwawezsha vijana hapa mkoani, yote haya yakiwa ni katika kuungwa mkono dhidi ya Sugu!

Sawa. ni jambo zuri Tulia alifanya. Lakini sasa ameleta kero nyingine, maana sasa hawa watu waliokuwa na lengo la kufanya biashara ya bajaji na bodoboda, wamejikuta wako kwenye ushindani mwingi wa kupata abiria na sasa bajaji na bodaboda havilipi tena. Hawa waendesha pikikipi wameanza kukwapua mifuko ya watu barabarani, na hasa handbag za kina mama! Siku tatu tu hapa tayari nimeona matukio matano ya ukwapuaji handbag za wanawake! Nadhani baada ya muda mfupi Mbeya itakuwa inaongoza kwa aina hii ya wizi.

Natoa tahadhari kwa wakazi wa Mbeya na mnaokuja kutembea kama mimi - chunga begi lako au handbag yako. La sivyo utakuta umeporwa, kutia ndani laptop bags. Usitembee barabarani kwa madoido ukiwa umening'iniza begi au handbag begani hapa, watakuliza!
 
Hao Vishandu wakwapuaji ndiyo waliomtukana Zuchu nini Jukwaani!...piga moto hao madogo aisee.
 
Mbeya sehemu gani mbeya kubwa Kuna
Kabwe
Mama John
Soko matola
Mbalizi
Mafiati kwa wauza utamu
Sido.nk
Sijui majina ya mitaa ya Mbeya. Kwa nini hilo ni muhimu?

Ila moja ilikuwa kwenye hii kona ya karibu na Hosptali iliyo karibu ja JKT. Mara tatu ilikuwa hii mitaa ya barabara kuu maeneo ya CRDB. Nyingine ilikuwa tunaenda airport, jamaa kanyakua begi kakiwasha kama anaenda airport!
 
Zamu ya Mkoa wa Mbeya na watu wake kuwa trendini,,mikoa mingine wamepumzishwa sasa.
 
Kitu kimoja nimeona Mbeya tofauti na mikoa mingine ni wingi wa Bajaji hizi na bodaboda. Ni nyingi hadi zinakera. Naambiwa kwamba wingi wake umeletwa na Tulia Foundation ya spika wa Bunge ambaye amekuwa akiwawezsha vijana hapa mkoani, yote haya yakiwa ni katika kuungwa mkono dhidi ya Sugu!

Sawa. ni jambo zuri Tulia alifanya. Lakini sasa ameleta kero nyingine, maana sasa hawa watu waliokuwa na lengo la kufanya biashara ya bajaji na bodoboda, wamejikuta wako kwenye ushindani mwingi wa kupata abiria na sasa bajaji na bodaboda havilipi tena. Hawa waendesha pikikipi wameanza kukwapua mifuko ya watu barabarani, na hasa handbag za kina mama! Siku tatu tu hapa tayari nimeona matukio matano ya ukwapuaji handbag za wanawake! Nadhani baada ya muda mfupi Mbeya itakuwa inaongoza kwa aina hii ya wizi.

Natoa tahadhari kwa wakazi wa Mbeya na mnaokuja kutembea kama mimi - chunga begi lako au handbag yako. La sivyo utakuta umeporwa, kutia ndani laptop bags. Usitembee barabarani kwa madoido ukiwa umening'iniza begi au handbag begani hapa, watakuliza!
Ujumbe kwa Tulia Ackson umeuficha kwenye ukwapuaji wa bodaboda sivyo?
Kwanza Mbeya si yako, wewe ni lipita njia tu. Waache wenyie wenye Mbeya na Mbeya yao.
Eti Tulia Foundation ndiyo chanzo,research ya wapi inakuwa ya kifala hivyo?
Kenge wewe
 
airport njia ya kuingia terminal one dar es salaam nimeshuudia na naendelea kushuudia watu wakiporwa na waendesha piki piki
 
no cap mbeya
imeanza kuwa na magumashi hivi kuna mwanangu aliniambia daah

ndugu yangu watoto wa dar wengi sana siku hizi uku ata mashoga wameanza kusogea

kuna club yangu pendwa inaitwa mbeya pazuri

mashoga kibao siku hizi kila kitu kinabadilka siku hizi
 
Sijui majina ya mitaa ya Mbeya. Kwa nini hilo ni muhimu?

Ila moja ilikuwa kwenye hii kona ya karibu na Hosptali iliyo karibu ja JKT. Mara tatu ilikuwa hii mitaa ya barabara kuu maeneo ya CRDB. Nyingine ilikuwa tunaenda airport, jamaa kanyakua begi kakiwasha kama anaenda airport!
Kona ya karibu na hospitali iliyo karibu na JKT-SIMIKE,META,KADEGE.CRDB-mjini,airport -SONGWE-nilikuwa najiwazia kwa sauti tuuu🤣🤣
 
Back
Top Bottom