Nina tabia ya kumuamini kila mtu

Nina tabia ya kumuamini kila mtu

LA7

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2019
Posts
655
Reaction score
2,369
Yaani iko hivi mimi hua namwamini mtu yeyote ili mradi tu hajawahi nifanyia ubaya lakini cha kustaabisha watu wabaya siku hizi hawaji tena kwangu yaani wanakuja watu wema tu na hata nikiwafanyia kazi za kudaiana wananilipa kati ya watu 10 ni wawili tu ndo wanaweza kunidhulumu au kusiwepo kabisa.

Namshukuru mungu kwa kuwa amenipa moyo wa kutohofia kudhulumiwa na kila mtu🙂
 
Wako njiani watakuja na atakuja mmoja tu atakupiga tukio moja tu utanyooka.
 
Yaani iko hivi mimi hua namwamini mtu yeyote ili mradi tu hajawahi nifanyia ubaya lakini cha kustaabisha watu wabaya siku hizi hawaji tena kwangu yaani wanakuja watu wema tu na hata nikiwafanyia kazi za kudaiana wananilipa kati ya watu 10 ni wawili tu ndo wanaweza kunidhulumu au kusiwepo kabisa,

Namshukuru mungu kwa kuwa amenipa moyo wa kutohofia kudhulumiwa na kila mtu🙂
Kwahiyo Wana JF tufanyeje sasa ikiwa wewe mwenyewe umeona ni vyema?

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Nimewahi kupigwa matukio makubwa mawili (Nasisitiza MAKUBWA) ndani ya week na watu wawili tofauti. Hayo matukio yalinipeleka mpaka polisi Nikaharibu uhusiano na watu wengi na kupoteza pesa nyingi mno na kupoteza utulivu wa akili.

Aisee mi nimekoma kuamini watu haraka.
.
Sio kila mtu ana roho nzuri kama yako.
 
Nimewahi kupigwa matukio makubwa mawili (Nasisitiza MAKUBWA) ndani ya week na watu wawili tofauti. Hayo matukio yalinipeleka mpaka polisi Nikaharibu uhusiano na watu wengi na kupoteza pesa nyingi mno na kupoteza utulivu wa akili.

Aisee mi nimekoma kuamini watu haraka.
.
Sio kila mtu ana roho nzuri kama yako.

Tueleze mkuu ilikuwaje tujifunze .
 
Siwezi kumuamini mtu hata kwa Dakika Moja
Pia Huwa nina mazoea kidogo sana na watu nisiowajua...
Usiwaamini hata muwe mmekaa muda mrefu vipi
Watu hubadilika kulingana na mahali pia wakati
 
Nakumbuka mzee wangu pia aliniambia siku za nyuma kuwa

“TRUST NO ONE”

Huwa siamini mtu kbsaaa hata wife mwenyew mwanzoni nilikuwa nakaa naye kimachale, baada ya miaka ndo uaminifu upo.
 
Subiri ipo siku, mimi nilikuwa hivyo hivyo na huruma ....kuna siku jamaa mmoja alinikuta nimekaa sehemu akaja anatia huruma sana ana nihadithia ana siku ya 3 hajala chochote , anasema alikuwa anaishi na mama yke wa kambo huko Mwanza baba yke alipo alifariki sasa baba yke alipo fariki tu mama wa Kambo akamfukuza , kwakweli alinihadithia vitu vingi ambavyo vinatia imani na huruma na huyu kijana alikuwa na umri wa miaka kama 17 hivi , kwanza nilimnunulia chakula, alishukuru sana tena alikuwa anataka kupiga magoti nikamkatza , yule dogo kutokana na muonekano wake na jinsi anavyotia huruma nikaona nimsaidie...
Nikaamua niishi nae geto....tulikaa sana yapata mwaka 1 mpk nikaanzisha biashara akawa ana simamia vzr kwa uaminifu tu na mimi nikazid kumwamini .....sasa kutokana na mishe zangu zingine ilibid kijana nimtume kwenda kufungasha mzigo ..mara ya kwanza, pili na ya tatu alienda akarud vzr tu biashara ikakua, nikazid kumwamini ilibid tuongeze mzigo uwe mkubwa kwani wateja wamekuwa wengi .....ilibid nimtume akachukue mzigo tena kibunda cha kutosha ...nilimpatia ....yaani tangu siku hiyo tarehe 17.06.2014 mpk leo huyo kijana hajawah kurud na sijui alienda wapi...nimemtafuta mpk nimekata tamaa , isitoshe aliondoka mpk na vitu vingine pale geto ...kwn siku hiyo anaondoka mimi nilikuwa job. Sasa watu hawaaminiki jombaa
 
Back
Top Bottom