Nina Tsh. milioni 200, niweke benki gani yenye 'Fixed Interest' nzuri?

Nina Tsh. milioni 200, niweke benki gani yenye 'Fixed Interest' nzuri?

Nilikuwa nafuatilia suala kama lako miezi miwili imepita yaani kabla huu ugonjwa ( corona ) haujashika kasi duniani niliambiwa kuwa rate zinatofautiana kutoka na muda utaoweka mfano ikiwa ni miaka miwili rate ni tofauti na mwaka mmoja, niliambiwa postal bank wanatoa 7% kwa mwaka na 9% kwa miaka miwili ukianzia 100m na bank nyingine niliambiwa BankABC wanatoa asililimia 10 % kwa mwaka mpaka 11% kwa sasa sjui hali ikoje maana corona imevuruga kila kitu.

Wadau walinishauri pia bank mpya zina risk ikifilisika inachukua mda kupata pesa yako na inaweza kupotea kabisa ila wakashauri bank kongwe kama NMB, CRDB na Postal bank
Intrest rates za bank ya Nmb zikoje? Mkuu na mimi nina shida kama ya kwenu,nilienda crdb wao wakaniambia riba yao ni asilimia 5 tu mpaka mwili ukachoka
 
Intrest rates za bank ya Nmb zikoje? Mkuu na mimi nina shida kama ya kwenu,nilienda crdb wao wakaniambia riba yao ni asilimia 5 tu mpaka mwili ukachoka
Pia wana bonus account ambayo hukatwi na interest ni 3.5 mpaka 5.5 kutegemea hela unayoweka. Unapata interest quarterly na sharti ni utoe hela mara moja tu katika miezi mitatu. Tofauti na fixed hii unaweza toa hela muda wowote japo ni lazima uende dirishani
 
Ushauri wangu nenda makao makuu ya benki hizi kubwa then negotiate nao kuhusu interest rate. Usiende kwenye matawi nenda kwa watunga sera wanaweza kukupa special rates. Hiyo hela ni nyingi unakuwa na power ya ku negotiate

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Intrest rates za bank ya Nmb zikoje? Mkuu na mimi nina shida kama ya kwenu,nilienda crdb wao wakaniambia riba yao ni asilimia 5 tu mpaka mwili ukachoka
Nenda BankABC kama unaamini kuwa the higher the risk the higher the return mim nimesaini this morning their rate is above 10% and is negotiable.
 
Mkuu hajasema hana uwezo wa kuitunza ila anatafuta mahali ambapo anaweza kuongeza hicho kiasi kuliko kukaa nayo nyumbani wakati anafikiria afanye nini?
Pia angesema ameipataje hiyo 200m. Zaidi ya hapo ni swaga tu. Huwezi kumiliki 200m pasipo kujua kuziendeleza huenda kama ni za kiinua mgongo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
So far, nyote mnazunguka, hamjamjibu swali la mleta uzi.

Anauliza ni bank gani yenye Fixed Interest nzuri? Hajaomba ushauri wa jinsi ya kuinvest.

Mnaweza kuanzisha uzi wenu wa ushauri kama alivyofanya mkuu OEDIPUS na tutakuja kuchangia.

Kwenye huu uzi, ni vema kama mtajikita kujibu swali husika.
Yaani badala ya kujibu swali wanapandikiza mawazo yao na hivyo kupotosha wazo la mtoa mada, FIXED DEPOSIT.
 
Mkuu salute!

Seriously fanya haya kwa pamoja baada ya miaka 5 utakuja kunishukuru hapa.

1.Nunua hisa za millioni kumi tu uweke malengo ya miaka 5, mfano hisa za CRDB bado ziko chini na zinaweza kupanda sana tu hata mara tano baada ya miaka hiyo mitano.

2.Chagua kuwekeza kwenye UTT au hatifungani za serikali. Napo unaweza kuwekeza hata million 40.(utt +hatifungani)

3.millioni 100, weka fixed account..tafuta benk hizi ambazo ni global.banclays kwa sasa inaitwa Absa,fnb,bankABC interest zake ni kubwa kuliko hizi local banks.

4.millioni 25 weka kwenye biashara ya nafaka...mfano mpunga ,au ndegu,au choroko...hutajuta wala usiogope.(niulize nitakuogonza)

5.Millioni 25 njoo tufanye biashara ya pamoja,Mimi Nina wazo.very productive wewe una pesa,...Mimi ndo nitalisimamia na biashara itaenda vizur kwa sababu ujuzi na uzoefu wa hiyo biashara.(makubaliano ya kisheria tutaweka ili kulindana na kuaminiana)

Kamwe usikubali kuweka fixed accouts hiyo pesa yote mkuu, itakuwa ni uoga na ufinyu wa maarifa sana hata kama unazo nyingi hizo million 200 ila bado kuna namna ya kuzizalisha zaidi. Usibweteke ukasema unazo nyingi ukaanza kufanya biashara ya mwendo wa kinyonga, hakuna tajiri duniani ametajirika kwa kwa savings accounts au hizo fixed accounts, matajiri wote wanafanya investments.


Hizo million 100 utakazoweka fixed accounts ni kwa tahadhari tu kuwa biashara ikishashika mizizi unaongeza mtaji kwemye biashara kutoka fixed accounts ndo watu wenye jicho la tatu wanavyofanya.

Bahati nzuri biashara zote hizo juu nilizo kuorodheshea nina ujuzi nazo na zingine nazifanya...ukiacha hati fungani ndo sijawahi kufanya, kwa hiyo wewe kama uko tayari fanya hayo niliyokushauri, ingawa ushauri sio lazima ufatwe.

Najua watu wana pesa ila hawana mawazo ya biashara au wanaogopa kufanya biashara. Wenye pesa za mitaji msiogope kufanya biashara frankly speaking mimi nipo nitakushauri, mwanzo hadi mwisho kwenye biashara yako kama ukinikaribisha niwe mshauri wako usitishwe na watu waoga wa kuthubutu.

Dunia ya sasa inataka taarifa sahihi ndo muhimu sio uoga na hadithi za kukatisha watu tamaa.

Ni hayo tu Mkuu wa million 200/= karibu sana kwa ushauri na vitu kama hivyo.
dylm.mashauri@gmail.com 0762742349


Sent using Jamii Forums mobile app
Watu wataogopa kuona kuwa wewe
Ni member wala sio jf expert wanataka platinum members
 
Bank gani chief
Ilikua barclays, for now sijui kutokana na mabadiliko ya kibenki. By the way, 15m unaweza invest katika business unaweza tengeneza that amount monthly as a profit not sales, monthly.
 
Weka benki robo ya pesa , nyingine zungusha kwenye biashara , ama vipi wekeza kwenye ardhi . Ardhi ni benki inayozalisha sana ili mradi ardhi isiwe na mgogoro . Nilinunua kiwanja miaka 5 iliyopita kwa 4m leo nauza 8m na mteja yupo !

Sent using Jamii Forums mobile app

Duh ! Kaka miaka mitano iliyopita ungeanza biashara na ukaisimamia vyema ungekuwa umepata mara 100 ya hiyo 8 M.

kweli sijawahi kuthamini biashara ya kununua viwanja now na kuuza baadae kwa lengo la kupata faida. Kama unafanya hivyo kwa lengo la urith sawa.

mfano unasikia magomeni kiwanja ni Mil 150, but wengi wanaopata hizo hela sio wamiliki, ni wajukuu.

Wamiliki walishakufa zamani . It is not not good business to start.


Mk54
 
Najua lengo lako la kuitia yote hyo mbal na faida ila n sehemu salama 100%... Ila mkuu ikikupendeza unaweza toa fungu hapo ukanunua hisa za crdb hutokuja jutiaaa..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama lengo ni kuhifadhi basi weka Bank yoyote ila kama unahitaji kupata faida sikushahuri kuweka Fixed, weka NMB Bonus Account. Lakini kama unategemea kuanzisha mradi basi weka akaunti yoyote utakayoweza kutoa pindi utakapohitaji fedha zako.
 
Back
Top Bottom