Nina Tsh. milioni 200, niweke benki gani yenye 'Fixed Interest' nzuri?

Nina Tsh. milioni 200, niweke benki gani yenye 'Fixed Interest' nzuri?

Kama lengo ni kuhifadhi basi weka Bank yoyote ila kama unahitaji kupata faida sikushahuri kuweka Fixed, weka NMB Bonus Account. Lakini kama unategemea kuanzisha mradi basi weka akaunti yoyote utakayoweza kutoa pindi utakapohitaji fedha zako.
Hiyo Bonus Account ikoje ndugu yangu!
 
Duh ! Kaka miaka mitano iliyopita ungeanza biashara na ukaisimamia vyema ungekuwa umepata mara 100 ya hiyo 8 M.
Kuanzisha biashara ni kitu kimoja na kuisimamia vyema ni kiti kingine na kupata mafanikio ni kitu kingine kabisa. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kama angekuwa ameanzisha biashara na kuisimamia vizuri leo asingekuwa na hata senti tano iliyobakia.
 
Kuanzisha biashara ni kitu kimoja na kuisimamia vyema ni kiti kingine na kupata mafanikio ni kitu kingine kabisa. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kama angekuwa ameanzisha biashara na kuisimamia vizuri leo asingekuwa na hata senti tano iliyobakia.

Na ndio maana nikasema kama akisimamia vyema. Biashara yoyote sio porojo ; ni usimamizi.

Kununua maviwanja kwa lengo la faida ni uoga wa maisha.




Mk54
 
Kama lengo ni kuhifadhi basi weka Bank yoyote ila kama unahitaji kupata faida sikushahuri kuweka Fixed, weka NMB Bonus Account. Lakini kama unategemea kuanzisha mradi basi weka akaunti yoyote utakayoweza kutoa pindi utakapohitaji fedha zako.
Hii bonus account intrest yake ikoje kwa kiasi hicho cha pesa
 
Mkuu salute!

Seriously fanya haya kwa pamoja baada ya miaka 5 utakuja kunishukuru hapa.

1.Nunua hisa za millioni kumi tu uweke malengo ya miaka 5, mfano hisa za CRDB bado ziko chini na zinaweza kupanda sana tu hata mara tano baada ya miaka hiyo mitano.

2.Chagua kuwekeza kwenye UTT au hatifungani za serikali. Napo unaweza kuwekeza hata million 40.(utt +hatifungani)

3.millioni 100, weka fixed account..tafuta benk hizi ambazo ni global.banclays kwa sasa inaitwa Absa,fnb,bankABC interest zake ni kubwa kuliko hizi local banks.

4.millioni 25 weka kwenye biashara ya nafaka...mfano mpunga ,au ndegu,au choroko...hutajuta wala usiogope.(niulize nitakuogonza)

5.Millioni 25 njoo tufanye biashara ya pamoja,Mimi Nina wazo.very productive wewe una pesa,...Mimi ndo nitalisimamia na biashara itaenda vizur kwa sababu ujuzi na uzoefu wa hiyo biashara.(makubaliano ya kisheria tutaweka ili kulindana na kuaminiana)

Kamwe usikubali kuweka fixed accouts hiyo pesa yote mkuu, itakuwa ni uoga na ufinyu wa maarifa sana hata kama unazo nyingi hizo million 200 ila bado kuna namna ya kuzizalisha zaidi. Usibweteke ukasema unazo nyingi ukaanza kufanya biashara ya mwendo wa kinyonga, hakuna tajiri duniani ametajirika kwa kwa savings accounts au hizo fixed accounts, matajiri wote wanafanya investments.


Hizo million 100 utakazoweka fixed accounts ni kwa tahadhari tu kuwa biashara ikishashika mizizi unaongeza mtaji kwemye biashara kutoka fixed accounts ndo watu wenye jicho la tatu wanavyofanya.

Bahati nzuri biashara zote hizo juu nilizo kuorodheshea nina ujuzi nazo na zingine nazifanya...ukiacha hati fungani ndo sijawahi kufanya, kwa hiyo wewe kama uko tayari fanya hayo niliyokushauri, ingawa ushauri sio lazima ufatwe.

Najua watu wana pesa ila hawana mawazo ya biashara au wanaogopa kufanya biashara. Wenye pesa za mitaji msiogope kufanya biashara frankly speaking mimi nipo nitakushauri, mwanzo hadi mwisho kwenye biashara yako kama ukinikaribisha niwe mshauri wako usitishwe na watu waoga wa kuthubutu.

Dunia ya sasa inataka taarifa sahihi ndo muhimu sio uoga na hadithi za kukatisha watu tamaa.

Ni hayo tu Mkuu wa million 200/= karibu sana kwa ushauri na vitu kama hivyo.
dylm.mashauri@gmail.com 0762742349


Sent using Jamii Forums mobile app
Uyu jamaaaa ni tapeli ogopa sama watu ksma haea ni bora uombe ushauri kwa ndugu wa damu
 
Mmh mkuu....tunatishana
Kama ni ushauri kuhusu pesa my friend its better ukaomba ushauri kwa ndugu zako tena wa damu hawa wahun from no where my brother utaliaa angalia alivo na maneno mengi kama vile yeye ni mjukuu wa jeff benzos vile kumbe ni kapuku tuuu angalia hapo alivochomekea et hio biashara ya mill 25 mfanye woote atakulamba huyo usimsogelee washirikishe wana familia tu hakuna binadam wa bongo wenye roho nzur hivo
 
Duh ! Kaka miaka mitano iliyopita ungeanza biashara na ukaisimamia vyema ungekuwa umepata mara 100 ya hiyo 8 M.

kweli sijawahi kuthamini biashara ya kununua viwanja now na kuuza baadae kwa lengo la kupata faida. Kama unafanya hivyo kwa lengo la urith sawa.

mfano unasikia magomeni kiwanja ni Mil 150, but wengi wanaopata hizo hela sio wamiliki, ni wajukuu.

Wamiliki walishakufa zamani . It is not not good business to start.


Mk54
Mie pia naona time value for money haikai mzuka maana payback period ya miaka 5 ni kubwa sana. Wakati hio million 4 ungeweza kui invest kwenye biashara tofauti ikawa 10 times more.

Kuwekeza hio pesa ili izae million 3 tu kama faida kwa miaka 5 ni uzembe.
 
Kama ni ushauri kuhusu pesa my friend its better ukaomba ushauri kwa ndugu zako tena wa damu hawa wahun from no where my brother utaliaa angalia alivo na maneno mengi kama vile yeye ni mjukuu wa jeff benzos vile kumbe ni kapuku tuuu angalia hapo alivochomekea et hio biashara ya mill 25 mfanye woote atakulamba huyo usimsogelee washirikishe wana familia tu hakuna binadam wa bongo wenye roho nzur hivo
Kama una mjua uyo mtu ni Sawa ila kama sio Dah mkuu umemsemea makubwa sana..

U know kuna watu kweli humjui ila wana weza wakakusaidia na ukafika mbali sana bila ya wewe kutegemea so sometimes ni Umakini mkubwa unahitajika na Risk taking labda angeonana nae alafu alate mrejesho..ili tuangalie
 
Wakishindwa kukushauri, kuna pub mpya hapa inaitwa click point,mademu wazuri hutojuta kutumia hela yako.
kula bia wewe
 
k
Ilikua barclays, for now sijui kutokana na mabadiliko ya kibenki. By the way, 15m unaweza invest katika business unaweza tengeneza that amount monthly as a profit not sales, monthly.
Biashara kama ipi chief?Naomba ,mawazo
 
Kwa 8% kwa mwaka itamtolea 16M! Sasa kwa pesa hio mie nahangaika na Risky business za nini?
Kuna mzee mmoja alishinda kesi àkalipwa 450mil, akakimbilia kujenga gesti na kununua vidaladala vibovu. Right now naambiwa ana msongo wa mawazo na sometimes akikaa anaongea peke ake.
Pesa kama iyo gvt bonds za miaka 10 unakula asilimia 0.975% kama net profit kila mwezi, ingawa ndo ivyo utalipwa baada ya miezi 6 ila ni pesa nzuri mno.
Tatizo wabongo tamaa+ ujuaji.
 
Kwa 8% kwa mwaka itamtolea 16M! Sasa kwa pesa hio mie nahangaika na Risky business za nini?
Ofcourse, tamaa imewacost.
Kutengeneza faida ni kazi ngumu sana. Unaweza ukawa unafurahia let's say mapato ya 7.2mil kwa mwezi toka kwenye lori ila hii si faida, na mtaji wako ni almost 120m. Ni heri niweke kwenye financial markets nipate iyo 8%-income tax, kama faida tena bila kuhangaika kupiga piga simu kwa dereva kila siku.
 
Kuna mzee mmoja alishinda kesi àkalipwa 450mil, akakimbilia kujenga gesti na kununua vidaladala vibovu. Right now naambiwa ana msongo wa mawazo na sometimes akikaa anaongea peke ake.
Pesa kama iyo gvt bonds za miaka 10 unakula asilimia 0.975% kama net profit kila mwezi, ingawa ndo ivyo utalipwa baada ya miezi 6 ila ni pesa nzuri mno.
Tatizo wabongo tamaa+ ujuaji.
Samahani mkuu unaweza zieleza vizuri hizo government bond na nama unavyoweza pata faida?
Na pia nimeona kama kuna T bill na kuna T bond, tafadhali kama unaweza fafanua zaidi hapa , asante.
 
Back
Top Bottom