Nyaka-One
JF-Expert Member
- Oct 27, 2013
- 4,730
- 6,736
Wana JF,
Poleni na majukumu mliyonayo.
Ni kwamba mimi ninaishi Dar es Salaam. Umbali kutoka yalipo makazi yangu hadi city centre ni wastani wa kilometer 18. Nimeajiriwa sehemu ambako kwa maisha yetu ya kitanzania nadiriki kusema kwamba mshahara si mbaya kivile. Kutokana na ajira hii niliyonayo nimeweza kujenga nyumba ya kisasa kiasi fulani na pia kufungua miradi kadhaa hapa hapa jijini.Kwa kiasi kikubwa hii miradi inasimamiwa na mke wangu akisaidiwa na watu wengine tuliowaajiri.
Sasa kutokana na faida iliyopatikana kutokana na miradi hii ambayo imedumu kwa muda wa miaka minne napia saving yangu inayotokana na ajira yangu tuliweza kugawa hiyo faida katika mafungu makubwa mawili. Fungu la kwanza ikiwa ni kukuza mtaji kwa kila mradi uliopo na fungu la pili likiwa ni kufungua mradi mwingine mpya ambapo tuliutengea jumla ya Tshs. 45,000,000/=. Mradi huo mpya tulilenga kuufanyia nyumbani ili kuwa na usimamizi wa karibu (kwa maana ya kuuona kila siku) lakini usiohitaji uwepo wa mimi na mke wangu muda wote (kati ya saa moja na nusu asubuhi na saa kumi jioni)
Baada ya kutenga kiasi hicho chapesa tulifanya investment portfolio analysis na tukaona kwamba tungeweza kuwekeza pesa hiyo kwenye mradi wa ufugaji wa kuku wa kisasa wa mayai (2,000),kuku wa kienyeji (2,000) na pia kanga (1,000) na pia kununua vifaa mbalimbali kwa ajili ya ufugaji huo kama incubator, generator, n.k. Maamuzi ya kufanya mradi huo pamoja na factors zingine yalizingatia taarifa tulizokuwa nazo kuhusu faida nzuri ya ufugaji huo na pia eneo tulilo nalo nyumbani ambalo ni mita za mraba 2,600 na liko liko fenced.
Sasa taarifa nilizo nazo hivi karibuni soko la mazao ya ufugaji huu hasa kwa upande wa mayai ya kuku wa kisasa siyo zuri kutokana na uingizwaji wa mayai kutoka nchi jirani ambayo uuzwa kwa bei ya chini ukilinganisha na bei ya wafugaji wa hapa Dar. Pia gharama za ufugaji wa hao kuku na kanga kuonekana kuwa kubwa kulinganisha na hali ya soko kwa sasa. Hali hii imetufanya tusite kuwekeza kwenye mradi huu wa ufugaji (kwa ujumla wake) kwa sasa ili kuepuka hasara ambayo inaonekana kuwa wazi kwa macho ya haraka haraka.
Sasa ndugu zangu nikaona si vibaya kuja hapa JF ili ikiwezekana basi kupata ushauri wa mawazo mbadala ambayo tutayafanyia kazi na kuweza kuwekeza kiasi hicho cha pesa lakini wakatiwa kutoa ushauri naomba mzingatie kwamba mradi huo mpya unatakiwa ufanyikie katika eneo la nyumbani ninapoishi.
Natanguliza shukurani zangu kwenu wana JF.
Poleni na majukumu mliyonayo.
Ni kwamba mimi ninaishi Dar es Salaam. Umbali kutoka yalipo makazi yangu hadi city centre ni wastani wa kilometer 18. Nimeajiriwa sehemu ambako kwa maisha yetu ya kitanzania nadiriki kusema kwamba mshahara si mbaya kivile. Kutokana na ajira hii niliyonayo nimeweza kujenga nyumba ya kisasa kiasi fulani na pia kufungua miradi kadhaa hapa hapa jijini.Kwa kiasi kikubwa hii miradi inasimamiwa na mke wangu akisaidiwa na watu wengine tuliowaajiri.
Sasa kutokana na faida iliyopatikana kutokana na miradi hii ambayo imedumu kwa muda wa miaka minne napia saving yangu inayotokana na ajira yangu tuliweza kugawa hiyo faida katika mafungu makubwa mawili. Fungu la kwanza ikiwa ni kukuza mtaji kwa kila mradi uliopo na fungu la pili likiwa ni kufungua mradi mwingine mpya ambapo tuliutengea jumla ya Tshs. 45,000,000/=. Mradi huo mpya tulilenga kuufanyia nyumbani ili kuwa na usimamizi wa karibu (kwa maana ya kuuona kila siku) lakini usiohitaji uwepo wa mimi na mke wangu muda wote (kati ya saa moja na nusu asubuhi na saa kumi jioni)
Baada ya kutenga kiasi hicho chapesa tulifanya investment portfolio analysis na tukaona kwamba tungeweza kuwekeza pesa hiyo kwenye mradi wa ufugaji wa kuku wa kisasa wa mayai (2,000),kuku wa kienyeji (2,000) na pia kanga (1,000) na pia kununua vifaa mbalimbali kwa ajili ya ufugaji huo kama incubator, generator, n.k. Maamuzi ya kufanya mradi huo pamoja na factors zingine yalizingatia taarifa tulizokuwa nazo kuhusu faida nzuri ya ufugaji huo na pia eneo tulilo nalo nyumbani ambalo ni mita za mraba 2,600 na liko liko fenced.
Sasa taarifa nilizo nazo hivi karibuni soko la mazao ya ufugaji huu hasa kwa upande wa mayai ya kuku wa kisasa siyo zuri kutokana na uingizwaji wa mayai kutoka nchi jirani ambayo uuzwa kwa bei ya chini ukilinganisha na bei ya wafugaji wa hapa Dar. Pia gharama za ufugaji wa hao kuku na kanga kuonekana kuwa kubwa kulinganisha na hali ya soko kwa sasa. Hali hii imetufanya tusite kuwekeza kwenye mradi huu wa ufugaji (kwa ujumla wake) kwa sasa ili kuepuka hasara ambayo inaonekana kuwa wazi kwa macho ya haraka haraka.
Sasa ndugu zangu nikaona si vibaya kuja hapa JF ili ikiwezekana basi kupata ushauri wa mawazo mbadala ambayo tutayafanyia kazi na kuweza kuwekeza kiasi hicho cha pesa lakini wakatiwa kutoa ushauri naomba mzingatie kwamba mradi huo mpya unatakiwa ufanyikie katika eneo la nyumbani ninapoishi.
Natanguliza shukurani zangu kwenu wana JF.