Nina wasiwasi idadi ya wasiojua kusoma na kuandika inazidi kuongezeka nchini Tanzania

Nina wasiwasi idadi ya wasiojua kusoma na kuandika inazidi kuongezeka nchini Tanzania

MamaSamia2025

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2012
Posts
14,588
Reaction score
32,361
Kulingana na UNESCO hadi mwaka 2015, kiwango cha watu wazima kusoma na kuandika cha ni 77.89% nchini Tanzania. Wakati kiwango cha wanaume kusoma na kuandika ni 83.2%, kwa wanawake ni 73.09%, kuonyesha pengo kati ya jinsia.

Kwa mujibu wa taarifa nyingi zilizopo ni kwamba Tanzania imeshuka kwa zaidi ya 10% kulinganisha na kiwango kilichokuwepo miaka ya 70. Ripoti zinasema Tanzania ilikuwa na literacy rate ya kwenye 90% ambacho ni kiwango cha juu sana kwa nchi. Kwa ufupi bongo kwa miaka hiyo watu karibu wote walikuwa wanajua kusoma na kuandika. Hakika serikali ya Mwalimu iliupiga mwingi.

Nimeanza na utangulizi huo uliokaa kisomi ili sasa nieleze kwanini nimeandika huu uzi. Kwa muda mrefu kuna nimekuwa nikikerwa mno na jinsi watu wengi wanavyoshindwa kuandika vizuri maandishi yao bila kukosea. Matumizi yasiyo sahihi herufi "L" na "R" yamekuwa changamoto kubwa. Isitoshe mtaani tunamoishi kuna watu wengi sana wasiojua kuandika kabisa wala kusoma. Wala halihitaji sana utafiti kujua kwamba kuna hili tatizo.

Mitandao ya kijamii imesaidia sana kujua ukubwa wa tatizo. Watu wengi mno ukisoma comments na captions zao utapandwa na jazba mno. MwanaJF FaizaFoxy huuliza kwamba huko shuleni ulienda kusomea ujinga? 🤣🤣. Watu maarufu wengi hasa wanamuziki na wanafilamu/maigizo (Bongo movie) wamekuwa vinara wa maandishi yaliyokosewa kuandikwa, iwe Kiswahili au kiingereza. Ukitembelea mtandao wa Facebook ndo utaona maajabu mengi hadi unatamani watu wanyang'anywe simu na kurudishwa darasani kwa lazima.

Mimi nashauri wazazi wawafuatilie watoto wao toka wakiwa wadogo ili kujenga mtanzania ambaye hatatia aibu kwa kushindwa hata kuandika na kusoma lugha ya kiswahili. Waalimu nao wasiwe nyuma kutimiza wajibu wao. Wale waalimu wa zamani wa mwandiko darasa la kwanza na la pili bado wapo? Serikali nayo ifuatilie kila kitu kwa karibu sana kwa sababu kwa ninayoyaona mtandaoni huenda tumeshashuka tena.
 
Ukisema kwalifikesheni ya walimu wa sasa ndo chanzo, utagundua kuwa kipindi cha Mwalimu, UPE ndo walishika hatamu.

Zaidi, kama ni kansa imeshasambaa kila sehemu, kule mjengoni unaona wengine wanashindwa hata kutaja namba zikiwa kwenye maelfu na mamilioni tu!

Tunasubiri ufafanuzi wa 23.3% mwezi Julai, maana kilichoandikwa kwenye tangazo pia kimeleta mjadala, maana sio selfu eksiplanatori
 
Ukisema kwalifikesheni ya walimu wa sasa ndo chanzo, utagundua kuwa kipindi cha Mwalimu, UPE ndo walishika hatamu.

Zaidi, kama ni kansa imeshasambaa kila sehemu, kule mjengoni unaona wengine wanashindwa hata kutaja namba zikiwa kwenye maelfu na mamilioni tu!

Tunasubiri ufafanuzi wa 23.3% mwezi Julai, maana kilichoandikwa kwenye tangazo pia kimeleta mjadala, maana sio selfu eksiplanatori
Kweli ndugu. Kwenye elimu kuna matatizo mengi mno.
 
Hapo inamaanisha Mkoloni aliwasomesha watu kuliko toka tupate uhuru. Simpo. Maana mtu mzima wa mwaka 70 alisomeshwa mwaka gani? "Obviously" ni kabla ya Uhuru.

Tena waweke wazi, kila mtu aelewe kuwa, wengi wao hao watu wazima walioweza kusoma na kuandika ilikuwa ni kwa kutumia hati za Kiarabu.

Madrasssa hoyeee.
 
Hapo inamaanisha Mkoloni aliwasomesha watu kuliko toka tupate uhuru. Simpo. Maana mtu mzima wa mwaka 70 alisomeshwa mwaka gani? "Obviously" ni kabla ya Uhuru.

Tena waweke wazi, kila mtu aelewe kuwa, wengi wao hao watu wazima walioweza kusoma na kuandika ilikuwa ni kwa kutumia hati za Kiarabu.

Madrasssa hoyeee.
Hapa sasa utaharibu thread
 
Hapo kwenye facebook ndo umegusa penyewe, yaan watu wengi wanaotumia sana facebook wanachekesha sana. Kwenye R anaweka L kwenye L anaweka R karibu sentensi yote
 
Hili na vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi ilikua miongoni mwa Mambo ambayo Lipumba akiyasema kampeni za 2000-2010, nyie mkavutiwa na helikopta na breaking nyuzi za chadema
 
Baada ya Uhuru UPE na Elimu ya watu wazima vilisaidia sana kupandisha idadi ya wanaojua kusoma na kuandika. Msaada mkubwa tuliupata kutoka Cuba ambako hii ilikua sera ya Fidel Castor.

Katika kuendeleza Elimu Castro alijenga shule ya Kibiti Girls na Ruvu. Cuba ilifikisha 99% ya raia wAke kujua kusoma na kuandika.

Cuba inaongoza kuwa na udadi ya madaktari na wahandisi duniani.
 
Hati kwa Kiingereza ni nini? Hand writing?
Sipo hapa kufanya tafsiri, kama hujaelewa nilichokiandika, basi elewa kuwa maandiko yangu si kwa ajili yako ni kwa ajili ya wenye kunielewa ninavyoandika.
 
Hapo inamaanisha Mkoloni aliwasomesha watu kuliko toka tupate uhuru. Simpo. Maana mtu mzima wa mwaka 70 alisomeshwa mwaka gani? "Obviously" ni kabla ya Uhuru.

Tena waweke wazi, kila mtu aelewe kuwa, wengi wao hao watu wazima walioweza kusoma na kuandika ilikuwa ni kwa kutumia hati za Kiarabu.

Madrasssa hoyeee.

Unaushahidi na unachokisema au unazungumza kujifurahisha,..

Ukongea mambo unapaswa uwe na ushahidi.

Unaweza kutaja shule au chuo chochote kilichojengwa na waarabu wakati wa ukoloni?
 
Back
Top Bottom