Nina wasiwasi na mke wangu...

Nina wasiwasi na mke wangu...

Sasa kama alijua anasafiri, ikawaje tena akachelewa kutoka mpk akalala dodoma.
Hapo kuna walakini

Ndo nasema shida sio anakokwenda sababu singida huko sina doubt nako shida ni Dodoma ndo ninamashaka napo wakuu mnielewe
 
"Watu wamefanya importation [emoji23][emoji23]"

[emoji3516][emoji3516] puuzia maneno hayo hapo juu , mkuu usiwe na mawazo hasi kila muda si vizuri kwa afya yako umefanya jambo la maana kutomuuliza maana inaweza kuwa unamuhukumu tu bure.

Yawezekana pia mkuu ni mawazo yangu lakini ndoivo wasiwasi ndo akili
 
Kama unampenda sana, na huwezi kumuacha; usiangaike kumuuliza chochote, wewe akija mpelekee moto maisha yaendelee.
Kwa sababu, itakuwa haina maana ya kumuhoji, huku ukiwa hauna uwezo wa kufanya maamuzi magumu itakuwa sawa na kupiga kelele tu.

Nikweli mkuu nimekuelewa ila siwez kulifumbia macho hili swala
 
Upo tayari kumuacha ukigundua ameliwa?

Kiukweli siwez ishi na mwamke ambae kanifanyia ujinga kiasi hicho mwisho nisije nikafaanya makubwa dunia inishangae mkuu nitapiga chini tu
 
Yaani Dar to Singida, kaitwa na dada zake then hajashinda hata siku moja kesho anageuza, safari ya karibu km 550, alafu kwenda na kurudi kashuka dodoma!!!!!!! Then gari zimejaa hakuna usafiri, ghafla inapatikana gari ya dodoma!!¡!!! Mbona ni rahisi ku predict kwamba hakusafiiri hakua mbali na hakua nje ya mkoa!!!!

Ainashida mkuu njia ya muongo ni fupi sana
 
Amini ninachokuambia huyo itakuwa kweli aliitwa ila hapo dodoma ndo alikuwa na mishe zake na uchafu wote alifanyia dodoma,

Yeah mkuu namimi ndo nina wasiwasi na Dodoma mi sina wasiwasi na kwa dadazake mkuu
 
Duh nasoma hadi nalia kwa hasira, bro huu uzi labda kama umeamua kuchangamsha jukwaa ila kama ni kweli umekosea sana ..huyo mimi ningemuua kbs

Mkuu maumivu yake ni makali sana ila mungu alete imani sana juu ya hili bhas
 
Ninayo but nilimuacha aende sikutaka complicated yoyote lakini ishu ya kulala Dodoma ndo tatizo lilipo anzia sababu hiyo ratiba haikuwepo
Wewe ni mwanaume mkuu head of the family!! You rule! You order Kama kiongozi wa familia inatakiwa uwe na sautiii inapobidi ukalii make wanawake akili zetu tunazijua wenyewe!
Hapo inaonesha kabisa mkeo kakupanda kichwani! Na anakuchukulia poa sanaa!!
 
Habar wana JF,
Naimani mko wazima.

Kiukweli nimekuwa na wasiwasi na safari ya wife, sijui kwanini lakini ni safari ambayo siielewi kabsa wakuu. Nina mashaka nayo coz naona mapicha picha tu.

Ni kwamba wife kasafiri juzi ijumaa kuelekea Singida lakini safari yake sielewi elewi kabisa, kwasabubu kwanza ni safari ya kushtukiza lakini pia mpaka now sielewi aim ya safari ni nini mpaka now.

Alhamisi amerudi kutoka kazini usiku tunalala ndiyo ananipa taarifa ya kuwa kesho Ijumaa anasafiri, nikamuuliza unaenda wap? Akaniambia kapigiwa simu na dada zake wamemuita ambao wanakaa Singida. Nikamuuliza kunatatizo akasema hapana, ila sijui wanashida gani na mimi ndiyo wamenipigia simu niende.

Kiukweli nilikuwa nimechoka nahitaji kupumzika, sikutaka ku complicate kitu, nikamjibu sawa nikalala. Then asubuhi nikajiandaa nikaenda kazini vizur. Niko job ananipigia simu kuwa ndiyo anatoka home anaelekea stendi kupanda bus. Iikuwa almost kama saa 7 hivi mchana nikamjibu haya na nikamuuliza kama kunakitu chochote anahtaji akasema hapana yuko powa.

Basi nikakata simu lakini kiukweli ghafla akili yangu ilishikwa na wasiwasi juu ya safari yake but sikutaka ku doubt anything nikapotezea. Baadaya kupita kama lisaa akanitumia message kuwa amepata basi but akifika Dodoma atashuka kuna ndugu yake anamchuka then wanaenda wote.

Daah, sikutaka pia ku doubt wala mambo mengi nikamjibu sawa, nikaachana naye nikaendelea na kazi zangu, but bado sikuona sababu ya yeye kushuka Dodoma. By saa 2 ndiyo ananiambia ndiyo wanaondoka Dodoma nikamjibu sawa safari njema tukaacha hivyo. Basi mi nikarud home usiku kwakuwa nilishapita somewhere nikapata chakula nikafika home niko good, nikaoga nikaingia kwa bed nikampigia ananiambia kashafika ila kachoka na safari nikamuacha nikapumzika.

Sasa leo Jpili tumeongea asubuh vizur tu na tukaagana baadae by saa 7 mchana ananiambia ndiyo anataka kurudi leo. Nikamuuliza mbona hukuniambia asubuhi na kwanini usingeondoka asubuhi? Sijaona cha maana anachonijibu, basi nikamwambia haya kama unarudi leo. Tuakaacha baada ya kama nusu saa ananipigia simu ananiambia kuwa yupo stendi, mara gari sijui hakuna, mara zimejaa, mara nimechoka nasikia usingizi, nikamwambia sasa siungebaki ili uondoke kesho asubuhi akasema sawa tukaacha.

Baadae ananitumia message eti amepata gari ila linaishia Dodoma kwaiyo atashuka Dodoma. Aloo nikasema kimoyomoyo hapo Dodoma hapo siyo bure, coz kwenda kashuka Dodoma kurudi baada arud kesho kama kweli kakosa usafiri na tumekubalina anarudi kesho mapema na sidhani kama kweli alikosa usafiri by that time ananiambia kuwa kapata usafiri.

Ila unaishia Dodoma so ataenda kulala Dom, sikutaka ku complicate nikamjibu sawa basi nikaachana nae. Ila cha ajabu baada ya hapo akawa kimya hakusema kama kafika au laa. Yaani ndo ananitumia text saa hii, saa 5 usiku kuwa alifika salama ila alishindwa kuniambia coz vidonda vya tumbo vilimshika akafikia kupumzika. Heheheh nacheka ila najua mwenyewe wakuu but sijamjibu na sitamjibu lakini namsubiri arudi kesho nikitoka kazini anieleze vizuri kuhusu hii safar yake.

Japokuwa mimi siyo mtu wa kumchunguza mwanamke na sipendi kabisa kuchunguza mtu sababu naelewa what’s gonna happen.

Wakuu kama kuna la kuniongezea karibuni sana, uwanja ni wenu.
wanawake walioajiriwa ni hatari sana

heri uingie gharama umfungulie biashara
 
Ungemwambia naomba niongee na dada zako waliokuita , inamana umeoa ufahamiani hata na ndugu zake

Ndugu nafaamiana nao vizur sababu ya kumwambia aende sikutaka mambo yawe mengi nilitaka aende then akirud ndo nimuweke chini anieleze kulikuwa na nini lakini singida alifika na nilihakikisha hilo ila doubt inakuja hapo Dodoma mkuu
 
Dada zake walipaswa kukupigia wewe kuomba ruhusa mdogo wao aende. Na akifika ujue ni kweli yuko na dada zake. Otherwise binafsi nakuona hauko imara, unapigiwa kizembe sana.

Sawa mkuu nimekuelewa
 
Duh nasoma hadi nalia kwa hasira, bro huu uzi labda kama umeamua kuchangamsha jukwaa ila kama ni kweli umekosea sana ..huyo mimi ningemuua kbs
Aiseee [emoji23][emoji23] watu wengine kama hamjaoa hata msioe.
 
Usioe,usioe tena usioe ili kuhepukana na Mambo Kama haya. Ona Sasa Mimi nimekaa kwa amani kabisa ila huyu bwana muda huu anateseka.

[emoji849][emoji849][emoji849]
 
Hapana mkuu ni mkewangu na niomemuoa
Sasa ndugu yangu kama mkeo mbona ndugu zake wanamchukulia kama anaishi na muhuni fulani how come kwa dharula hivyo usipewe taarifa wewe kwamba mkeo anahitajika na kama kuna tatizo, kwa maana wewe ndiyo mkuu wa kaya na unajua kama nauli ipo au haipo wewe ndiyo unapaswa kumsuport kwa kujua wapi upate pesa ya fasta, isije kuwa mkeo kakuzoea sana anaona hauna maamuzi yoyote juu yake.
 
Kutokana na makosa yako me naona uyo mwanamke usimuulize chochote tena mpokee kwa furaha na pole nyingi za safari

Kwa akiri yako ata ukisema umuache uyo mwanamke bado utapata mwingine nae utamuacha

Chakufanya ni wew kwanza kubadirika ujue unatakiwa kuishi nao vipi hawa viumbe maana naona ujui kuishi na mwanamke

Note: utakuwa umekosea sana kumuuliza mkeo kusiana na safari yake Kama ambavyo ukuona umuhimu wa kumuuliza kabla ajaondoka basi usione umuhimu wa kumuuliza atakaporejea

Wewe ndo unamakosa wew ndo dereva kwake wew ndo mlizi kwake wew ndo una mamlaka kwake ata akipata tatizo familia itakuoji wew
 
ungemkumbusha azingatie matumizi ya kondomu.
 
Back
Top Bottom