Nina wasiwasi na mke wangu...

Pasipo na wivu hapana mapenzi. Usiniambie kuwa unaweza kuvumilia na kuchukulia kawaida pindi ukimuona mkeo kasimamishwa kichochoroni na mwanaume usiyemuelewa au uchukulie kawaida pindi mkeo anapokuwa busy kuchat na watu kwenye simu yake wakati upo nae ndani.
 
Nasema kwamba tegemea lolote kutoka kwa mwanamke sababu siyo mali yako, ni binadamu kama wewe mliyekubaliana kuwa atafanya ngono na wewe tu, sasa pale atakapofanya lolote linalovuka mipaka ya mikataba mliyojiwekea vunja mahusiano usijimilikishe kuwa huyo ni wako sijui umemtolea mahari, huwezi miliki binadamu, ukilikubali hilo siku akifanya mambo yasiyokupendeza utakuwa mwepesi kuheal kuliko ukijiambia uongo kuwa huyu ni mali yangu hakuna wa kutembea nae. Ni pua yangu hii nampengea kamasi mie tu.
 
Mwanamke umleavyo ndivyo aishivyo na wewe,

Hizo taabu umezitengeneza mwenyewe, maana kwenye ndoa inabidi WEWE NDIO UWE MUAMUZI WA MWISHO, NA WEWE NDIO WA KUMRUHUSU AENDE AU ASIENDE
Mkuu inaonyesha mwanamke ana uchumi mkubwa pamoja na dada zake sasa huyu ndugu yetu kapuku inaonyesha anadharauliwa sana upande wa mke wake.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Haya mambo hayanaga mjanja; ni rahisi kuzungumza, ila mkionana uso kwa uso, kuna mawili uwe mpole uendelee kupelekea moto au upandishe mabega juu na ujikute umefanya maamuzi yasiyo sahihi.
 
Busara ni kujua unajua ulifichwa na ukaendelea kukaa kimya. Huna haja ya kuhoji hoji kila kitu. Potezea!!!
 
Kipindi chote hicho ulijaribu kuwasiliana na na ndugu zake kujua kama ameitwa kweli?
Pia kwanini iwe ghafla? Wewe kama mume ilitakiwa wakushirikishe.
 
Mambo mengine ni afadhali ubaki nayo mwenyewe au uombe ushauri kwa watu wachache wa karibu.
Unaweza kuta labda hata wife hajaliwa ( ingawa uwezekano ni mdogo)
Balaa lake huko wanaweza wakauana kwasababu ya hizi comments hapa
Yani mambo ni moto
 
Ukute wala hafanyi hivyo unavyomuwazia sema fanya hivi muulize tu vizuri huku unamtazama machoni hawezi kukuficha kitu ukashindwa kujua
 
Mkuu nilimruhusu sababu yakusema ameitwa na dadazake but haijulikani nini shida kwakuwa ni familia yake nikamruhu aende ili tujue nini shida huko
Acha kuishi hvyo mkuu kua na msimamo usipende kuzoeleka kirahisi hivyo na mashemeji.Kama Aliitwa na dada zake ilipaswa wakupigie wewe simu na kuomba kuonana na ndugu yao na sio kuwasiliana na mkeo kimyakimya eti wamemuomba! mkuu utajuaje kama Alisafiri kweli!? Usikute alifichwa maeneo flan mjini hapo.
USHAURI
-Wasiliana na dada zake ili kuhakiki kama alienda singida .
  • Akirudi chukua simu kwa kumshitukiza kaa nayo kwa masaa kama kumi, lazma atapigiwa na kutumiw sms na wezi wenzie.
  • Badili mfumo wa maisha sometimes unakua mtemi usisomeke mkuu usije ukapandwa kichwani.
 
Nadhani huu ndio wakati wa kumuwekea application za kuhack mawasiliano yake. Usimuulize chochote, tengeneza mazingira upate uhakika wa Yale unayoyahofia. Mwanamke ni mjanja Sana kwanza hatakubali kwa hayo unayomhisia, atakupiga chenga Sana huta ondoa doubts. Lkn pia akihisi unamashaka ataongeza umakini utasalitiwa kwa muda mrefu baadae.

Ila pia kuwa makini kuletewa mimba za nje pamoja na ukimwi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…