Nina wazo la kufungua kiwanda cha kugandisha barafu feri

hp4510

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
7,235
Reaction score
7,392
Habari za Mchana

Nina wazo la kuanzisha kiwanda cha kugandisha mabarafu pale soko la Feri

Naitaji muongozo na ushauri Kwa mtu yoyote ambae aliwahi kufanya au ana uzoefu kidogo na biashara hii


Na pia napenda kupata ushauri au mawazo ya jinsi ya kurent sehemu ya soko na kuweka kampuni yangu hapo

Hapa nalenga kujua ishu ya vibali na utaratibu wote wa kufata

Ahsante Sana
 
Wazo zuri sana na hiyo ni pesa tupu shida ipo kwenye upinzani utakaopata kutoka kwa matycoon wa sasa walioshikilia hiyo biashara
 
Wazo zuri sana na hiyo ni pesa tupu shida ipo kwenye upinzani utakaopata kutoka kwa matycoon wa sasa walioshikilia hiyo biashara
 
Kwani hakuna hiyo bizness pale?
barafu zipo pale ila demand na supply ni tofauti kwani uhitaji ni mkubwa kuliko upatikanaji na sio feri tt wewe ukienda maeneo yote yenye uhitaji wa barafu mfano pale mbagala,kariakoo,buguruni,gmboto,tandika kuanzia pale tmk hospital kuja sudan,majaribio,sokoni hadi Devis corner uhitaji ni mkubwa.
Pale feri barafu kama unafanikiwa kupata mashine ya kuweza kutengeneza barafu zile kubwa unaweza kuuza @6,000 na zile ngalawa za uvuvi zenye kutumia mashine wanachukua matofali ya barafu kuanzia 70-100 ambapo wanapoenda baharini wanakaa uko kuvua hadi wiki ndio warejee,sasa piga hayo matofali mara hyo bei,ni biashara nzuri sana ila kwenye mzunguko popote lazima ujipange
Mimi kwa ushauri wangu usiende kuweka mashine pale feri ila tafuta eneo upande wa kigamboni hata maeneo ya kutokea daraja la Nyerere tafuta eneo uwe unazalisha bidhaa zako uko na unakwenda pale kwa kuanzia tafuta japo wateja wako watatu wa ngalawa na wawili wakuuza vipande vipande kwa wanunuzi wadogo wadogo
 




barafu zipo pale ila demand na supply ni tofauti kwani uhitaji ni mkubwa kuliko upatikanaji na sio feri tu wewe ukienda maeneo yote yenye uhitaji wa barafu mfano pale mbagala,kariakoo,buguruni,gmboto,tandika kuanzia pale tmk hospital kuja sudan,majaribio,sokoni hadi Devis corner uhitaji ni mkubwa.
Pale feri barafu kama unafanikiwa kupata mashine ya kuweza kutengeneza barafu zile kubwa unaweza kuuza @6,000 na zile ngalawa za uvuvi zenye kutumia mashine wanachukua matofali ya barafu kuanzia 70-100 ambapo wanapoenda baharini wanakaa uko kuvua hadi wiki ndio warejee,sasa piga hayo matofali mara hyo bei,ni biashara nzuri sana ila kwenye mzunguko popote lazima ujipange
Mimi kwa ushauri wangu usiende kuweka mashine pale feri ila tafuta eneo upande wa kigamboni hata maeneo ya kutokea daraja la Nyerere tafuta eneo uwe unazalisha bidhaa zako uko na unakwenda pale kwa kuanzia tafuta japo wateja wako watatu wa ngalawa na wawili wakuuza vipande vipande kwa wanunuzi wadogo wadogo
 
Hapo ferry bei ya barafu ikoje bro.....
 
 
 

Attachments

  • Anza_biashara_na_sisi_njoo_tukutengenezeemashine_bora_zakugandisha_barafu_choyo_cool_078933870...mp4
    3.6 MB
Hapo ferry bei ya barafu ikoje bro.....
kuna video nimetuma ambapo kama una pesa yako ya ndani ya milioni 3 ni bora ukatengeneza mashine kama hyo ambapo barafu za ukubwa huo unauza buku buku na haina ulazima wa kwenda feri kikubwa ni ubunifu na kukaza buti kama utaenda maeneo niliyoyaorodhesha ktk post zilizopita na ukawa na toyo lako au lakukodi hzo barafu pisi 100 unapiga fasta ni ukifika saa 1 asubuhi hadi saa 3 asubuhi unarudi unapiga miruzi tu
 
Hiyo mashine nnayo, ila ni ndogo yake inagandisha zile barafu size ndogo za kupoza vinywaji..... Na mara moja inatoa barafu 100

Hiyo umetuma ni XL
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…