Ninachojua kuhusu kesi ya ugaidi inayomkabili Mbowe

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Wanabodi, ninajua wengi tunashangaa sana imekuwaje mfanyabiashara na mwanasiasa Freeman Mbowe kufunguliwa kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi.

Ukweli ni kwamba, mwaka 2017 baada ya jaribio la kumuua Lissu kushindikana, target ya pili alikuwa ni Mbowe baada ya TISS kumshauri Magufuli, "mwengine atakayefanya usitawale kwa utulivu ni Mbowe". Magufuli alisema, "muueni tu" lakini Usalama wakamwambia, "hapana, italeta taswira mbaya kimataifa, huyu mfunge tu". Toka hapo mchakato wa kumfunga Mbowe ulianza na ilikuwa ukamilike mara tu baada ya Uchaguzi wa 2020. Rais Samia amekuta faili hilo likiwa juu kabisa mezani akiambiwa, "haya ni maamuzi ya Usalama wa Taifa". Samia angefanyaje? Mnadhani binafsi haumii kumuona binti wa Mbowe akilia kortini?
 
Thibitisha hili
 
Hii kesi ya Mbowe inaonekana toka mwanzo ni mpango uliosukwa na wasaidizi wa ikulu, na mkuu wa nchi amejikuta hana ujanja tena.

Ila muda ni jawabu tosha naamini kabisa kesi ya Mbowe ni feki iliyotengenezwa makusudi ili kumfunga mdomo asiendeleze movement ya Katiba Mpya.

Kumuachia sasa wanaona atarudi kuendeleza kile wasichokitaka, kwao ni bora aendelee kukaa lockup kwa muda mpaka hali itakapotulia ndio wamuachie, thats why tunaona mambo ya ajabu yaliyofanywa na yule jaji aliejiondoa.
 
Acha hadithi za vijiweni.Mm nilifikiri una ushahidi kibao.Kumbe huna lolote zaidi ya hadithi za kutunga.Kichwa cha habari kikubwa unatuandikia utopolo tupu.Usipende kutupotezea muda kwa vihadithi feki feki vya kuunga unga.
 
Rais Samia amekuta faili hilo likiwa juu kabisa mezani akiambiwa, "haya ni maamuzi ya Usalama wa Taifa". Samia angefanyaje? Mnadhani binafsi haumii kumuona binti wa Mbowe akilia kortini?[emoji2827][emoji848][emoji2827][emoji848][emoji2827][emoji848][emoji2827]
 
Hayo lazima yatakuwa ni maamuzi ya makada wahafidhina, UVCCM na GREEN GUARDS waliovishwa koti na kutaka watambulike kama 'Usalama wa Taifa".

Hii ndiyo sababu kubwa inayowafanya watu makini waamini ya kuwa kuna mstari mwembamba sana ambao unatenganisha mipango ya kidhalimu na kifedhuli ya INTERAHAMWE ni hii ambayo SA inayothibitishwa na makada wa CCM.
 
MUNGU atayajibu haya yote..
MUNGU NI MWEMA.
 
Chama Cha Madhalimu kamwe hakitaacha kutenda udhalimu. Ila haya yote yana mwisho mchungu kwa Madhalimu wote
 
Yaani kweli anashindwa kumuagiza mkurugenzi wa mashitaka aifunge kesi hiyo na kumwachia MBOWE huru?
 
Rubbish of the year, pathetic!
 
Yaani kweli anashindwa kumuagiza mkurugenzi wa mashitaka aifunge kesi hiyo na kumwachia MBOWE huru?
Chief Hangaya afunge jalada hiyo kesi ni aibu......aibu aibu sibu pia Mama hutapata haki mvele Mungu sababu hutendi haki.....kisa utawala wa duniani? Katiba ni mali watanzania wote mil 60 lazima ije itengenezwe mpya leo kesho keshokutwa lazima.....hata ukimuua Mbowe katiba its a must
 
Kesi ya Mbowe inawavua nguo viongozi wetu hadharani. Ipo siku tutaona utosi ule uliofichwa na ile baibui.
 
Kesi ya MBOWE,kwanza mashtaka yalikosewa jaji luvanda akaamrisha yarekebishwe Kisha akajitoa.

Akateuliwa jaji Siyani naye akapokea kielelezo kilichopatikana kwa njia haramu Kisha naye akajitoa.

Sasa Leo yupo Jaji Tiganga hatujui na yeye anakuja kufanya lipi ili ajitoe,kiufupi MBOWE anakwenda kufungwa mchana kweupe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…