Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,713
- 6,121
Habari na poleni sana kwa msiba.
Niseme tu kwamba wengi wanaweza kusema mengi kuhusu Msiba huu ila mimi naweza kusema Jambo Moja. Maisha ni zawadi, tuyaenzi. ujifunze kutoka katika maisha ya Magufuli; Maisha ambayo yaliacha alama.
Mwaka 2010 mara baada ya uchaguzi mama yangu mzazi aliniuliza "Sasa akitoka Kikwete nani atakuwa Rais" Nilimtazama nikamwambia hata wewe unaweza kuwa Rais au hata mimi pia naweza kuwa Rais. Raia yeyote wa Jamhuri ya Tanzania anayo haki na wajibu wa kuwa RAIS wa nchi hii. Pamoja na hayo nilimchokoza kwani wewe ungependa nani awe RAIS. Mama yangu kwa nguvu kabisa akasema "MAGUFULI" Kwa kuwa nilimfahamu Magufuli vyema nilimwambia Jambo moja tu. Magufuli atakuwa RAIS ila utamkataa. Nikamwambia Magufuli anafanya kazi nzuri ila nafasi ya urais hasa kwa nchi yetu inahitaji zaidi ya mtu anayefanya kazi nzuri. Nilimwambia kwamba kuongoza taifa sio kazi Rais. Ni kazi ambayo inahitaji neema na huruma ya Mungu ili uweze kuifanya katika ukamilifu wake.
Kazi ya kuongoza nchi ambayo ina watu wa silka, tabia, tabaka, historia, matarajio, matamanio, maono, mitazamo tofauti huku nchi ikiwa na changamoto mbalimbali. Vipaumbele mbali mbali inahitaji karama ya kimungu ili kuweza kuindesha kikamilifu. Nchi hio inapokuwa katika dunia ambayo nayo ina mataifa ambayo nayo yana mirengo tofauti tofauti basi ujue kabisa kwamba kazi ya urais inakuwa ngumu zaidi.
Kazi ya urais inakuwa ngumu zaidi pale unapokuwa na cheo ambacho kina mamlaka makubwa sana kikatiba,nguvu kubwa sana kijeshi na uwezo mkubwa sana huku ukiwajibika kwa Mungu tu na kwa dhamira yako inakuwa ni ngumu zaidi. Hivyo basi anayetamani kuwa Rais anatamani kitu chema lakini kuwa RAIS wa nchi ni jambo gumu sana. Unapokuwa rais wa nchi unawajibika kwa kila jambo, kila mtu na kila hali. Watu wote wanakutazama wewe.
Ikafika mwaka 2015 na Magufuli akawa Rais na ndani ya MIEZI 6 yake ya mwanzo MAMA YANGU akamkataa. Sitaeleza sababu ila najua kwamba mengi yalitokea na labda yalikuwa tofuati na matarajio yake lakini alimkataa. Mimi nikamwambia MAMA hata kama mimi ningekuwa RAIS wa nchi hii ningefanya aliyofanya Magufuli ingawa ningefanya tofauti kidogo. Ningetumia nguvu kubwa zaidi katika kujenga mifumo kuliko kubomoa mifumo. Ningetumia nguvu nyingi katika kujenga uwazi badala ya kufichua siri. Ningejenga zaidi uwajibikaji wa kimfumo kuliko kuwajibisha watu. Ningejenga zaidi uzalendo wa kimfumo na sio uzalendo wa kiimla. Ningetaka nikumbukwe kama kiongozi niliyewainua watanzania. Hata hivyo binafsi nilijua kwamba Magufuli hakuwa mtaalamu wa kujenga mifumo ila hakuwa anapenda mifumo mibovu pia.
Hakuwa anapenda kuona mambo hayaendi. Hakutaka kuona watu wanateseka. Kwa sababu hio alijikuta akivunja mifumo na taratibu nyingi na kujikuta tunaingia katika zama ambazo taifa halikuwa na mifumo. Mifumo iliheshimiwa pale tu ambapo ilimpendeza yeye ila pale ambapo haikumpendeza aliikataa na kuweka amri yake.
Sio kila mtu alipenda tabia yake kwani kuna watu ambao walinufaika na mifumo hiyo mibovu na alipoikataa waliona maslahi yao kutishiwa. Na pia kuna waliopenda tabia yake ya kutokuheshimu mifumo kwa ni iliwawezesha wao kuneemeka kwa kutumia udhaifu wake katika kutaka mambo yaende bila kujali mfumo hasa mfumo unapochelewesha mambo. Huyo Ndiye Magufuli niliyemfahamu Tangu akiwa Mwanafunzi, Mwalimu, Mbunge, Naibu waziri, Waziri na Rais.
Hakuwa comformist. Udhaifu wake mkubwa ulikuwa na katika uwezo wake wa kutengeneza mifumo.Simlaumu kwani katika historia ya nchi yetu mtu pekee ambaye alikuwa fundi wa kutengeneza Mifumo alikuwa na hayati Benjamini Mkapa. Ndio. Mkapa alikuwa na uwezo wa kutengeneza mifumo, kuisimamia na kuiheshimu. Hata hivyo pamoja na uwezo wake huo hakuwana na uwezo wa kujenga nidhamu kwa wengine kuheshimu na kuisimamia mifumo. Hii ni kwa sababu watanzania tumekuwa na kasumba ya kuheshimu mifumo pale tu inapotufaa.
Naandika haya kama mtu ambaye nafuatilia sana historia ya chi yetu na watu. Kama mtu ambaye ninayo access ya kuzungumza na watu wenye nafasi nyeti serikalini na ambaye pia ninayo access ya kuzungumza na watu wa chini kabisa katika magenge na vijwe. Siandiki kwa ushabiki wala kwa ajili ya kutaka kumtukuza mtu au kumkejeli mtu bali ninaandika huku nikimlilia Magufuli.
Magufuli hakuwa adui yangu alikuwa ni rais wangu.Tangu aingie madarakani nimekuwa mkosoaji wake. Hata nisipomkosoa kwa uwazi ila ndani ya moyo kuna mambo sikukubaliana naye lakini nilimheshimu kama rais wa nchi.Nilitambua kwamba kama mwanadamu hakuwa mkamilifu. Nilitambua pia kwamba kuna uwezekano pia kwamba mimi ndio mwenye kasoro na sio yeye. Hivyo basi namjua Rais wangu.
Rais Magufuli alitaka kufanya mengi na amefanya mengi.Kwa kadiri ya uwezo na nafasi yake amefanya mengi. Ameonesha uthubutu na ujasiri ila pia kuna mengine ambayo hayakwenda sawa.Kuna ambao walimwangusha katika uongozi na kuna ambao walisababisha ashindwe kufikia malengo yake. Kuna ambao hawakumwelewa na kuna ambao walimchukia bila sababu na kuna ambao walimchukia wakiwa na sababu. Hata hivyo ukweli utabaki kuwa ukweli. Ukimtoa Nyerere Magufuli ni mmoja kati ya viongozi bora wa zama hizi. Kwa kipindi cha miaka 6 tu ameweza kuthibitisha kwamba INAWEZEKANA kuwa na ndoto kubwa na kuanza safari ya kuzifikia.
Naumia sana nikifikri kwamba Magufuli pamoja na Katibu mkuu wake KIJAZI sasa hawapo tena. Katika wilaya ya UBungo imesimama kumbukumbu,Kijazi Interchange na Magufuli International Bus Terminal. Miradi ambayo kwa hakika ni alama ya Nyakati hizi zao.
Nataka sasa niseme tu kwamba nitamlilia Magufuli kwamba hatakuwepo wakati tutakapopanda TRENI yetu ya kwanza ya SGR, hatakuwepo wakati tutakapowasha umeme wetu wa Bwawa la Nyerere. Namlilia sana Magufuli kwa sababu nilitamani sana aendelee kuwepo. NIlitamani sana atimze ndoto zake kwa taifa letu kwa nyakati zetu.
Mungu Mpokee mja wako John Joseph Pombe Magufuli na uendelee kutulinda na kutubariki Watanzania wote
Raha ya milele umpe Ee Bwana; Na mwanga wa milele umwangazie, apumzike kwa aman
Niseme tu kwamba wengi wanaweza kusema mengi kuhusu Msiba huu ila mimi naweza kusema Jambo Moja. Maisha ni zawadi, tuyaenzi. ujifunze kutoka katika maisha ya Magufuli; Maisha ambayo yaliacha alama.
Mwaka 2010 mara baada ya uchaguzi mama yangu mzazi aliniuliza "Sasa akitoka Kikwete nani atakuwa Rais" Nilimtazama nikamwambia hata wewe unaweza kuwa Rais au hata mimi pia naweza kuwa Rais. Raia yeyote wa Jamhuri ya Tanzania anayo haki na wajibu wa kuwa RAIS wa nchi hii. Pamoja na hayo nilimchokoza kwani wewe ungependa nani awe RAIS. Mama yangu kwa nguvu kabisa akasema "MAGUFULI" Kwa kuwa nilimfahamu Magufuli vyema nilimwambia Jambo moja tu. Magufuli atakuwa RAIS ila utamkataa. Nikamwambia Magufuli anafanya kazi nzuri ila nafasi ya urais hasa kwa nchi yetu inahitaji zaidi ya mtu anayefanya kazi nzuri. Nilimwambia kwamba kuongoza taifa sio kazi Rais. Ni kazi ambayo inahitaji neema na huruma ya Mungu ili uweze kuifanya katika ukamilifu wake.
Kazi ya kuongoza nchi ambayo ina watu wa silka, tabia, tabaka, historia, matarajio, matamanio, maono, mitazamo tofauti huku nchi ikiwa na changamoto mbalimbali. Vipaumbele mbali mbali inahitaji karama ya kimungu ili kuweza kuindesha kikamilifu. Nchi hio inapokuwa katika dunia ambayo nayo ina mataifa ambayo nayo yana mirengo tofauti tofauti basi ujue kabisa kwamba kazi ya urais inakuwa ngumu zaidi.
Kazi ya urais inakuwa ngumu zaidi pale unapokuwa na cheo ambacho kina mamlaka makubwa sana kikatiba,nguvu kubwa sana kijeshi na uwezo mkubwa sana huku ukiwajibika kwa Mungu tu na kwa dhamira yako inakuwa ni ngumu zaidi. Hivyo basi anayetamani kuwa Rais anatamani kitu chema lakini kuwa RAIS wa nchi ni jambo gumu sana. Unapokuwa rais wa nchi unawajibika kwa kila jambo, kila mtu na kila hali. Watu wote wanakutazama wewe.
Ikafika mwaka 2015 na Magufuli akawa Rais na ndani ya MIEZI 6 yake ya mwanzo MAMA YANGU akamkataa. Sitaeleza sababu ila najua kwamba mengi yalitokea na labda yalikuwa tofuati na matarajio yake lakini alimkataa. Mimi nikamwambia MAMA hata kama mimi ningekuwa RAIS wa nchi hii ningefanya aliyofanya Magufuli ingawa ningefanya tofauti kidogo. Ningetumia nguvu kubwa zaidi katika kujenga mifumo kuliko kubomoa mifumo. Ningetumia nguvu nyingi katika kujenga uwazi badala ya kufichua siri. Ningejenga zaidi uwajibikaji wa kimfumo kuliko kuwajibisha watu. Ningejenga zaidi uzalendo wa kimfumo na sio uzalendo wa kiimla. Ningetaka nikumbukwe kama kiongozi niliyewainua watanzania. Hata hivyo binafsi nilijua kwamba Magufuli hakuwa mtaalamu wa kujenga mifumo ila hakuwa anapenda mifumo mibovu pia.
Hakuwa anapenda kuona mambo hayaendi. Hakutaka kuona watu wanateseka. Kwa sababu hio alijikuta akivunja mifumo na taratibu nyingi na kujikuta tunaingia katika zama ambazo taifa halikuwa na mifumo. Mifumo iliheshimiwa pale tu ambapo ilimpendeza yeye ila pale ambapo haikumpendeza aliikataa na kuweka amri yake.
Sio kila mtu alipenda tabia yake kwani kuna watu ambao walinufaika na mifumo hiyo mibovu na alipoikataa waliona maslahi yao kutishiwa. Na pia kuna waliopenda tabia yake ya kutokuheshimu mifumo kwa ni iliwawezesha wao kuneemeka kwa kutumia udhaifu wake katika kutaka mambo yaende bila kujali mfumo hasa mfumo unapochelewesha mambo. Huyo Ndiye Magufuli niliyemfahamu Tangu akiwa Mwanafunzi, Mwalimu, Mbunge, Naibu waziri, Waziri na Rais.
Hakuwa comformist. Udhaifu wake mkubwa ulikuwa na katika uwezo wake wa kutengeneza mifumo.Simlaumu kwani katika historia ya nchi yetu mtu pekee ambaye alikuwa fundi wa kutengeneza Mifumo alikuwa na hayati Benjamini Mkapa. Ndio. Mkapa alikuwa na uwezo wa kutengeneza mifumo, kuisimamia na kuiheshimu. Hata hivyo pamoja na uwezo wake huo hakuwana na uwezo wa kujenga nidhamu kwa wengine kuheshimu na kuisimamia mifumo. Hii ni kwa sababu watanzania tumekuwa na kasumba ya kuheshimu mifumo pale tu inapotufaa.
Naandika haya kama mtu ambaye nafuatilia sana historia ya chi yetu na watu. Kama mtu ambaye ninayo access ya kuzungumza na watu wenye nafasi nyeti serikalini na ambaye pia ninayo access ya kuzungumza na watu wa chini kabisa katika magenge na vijwe. Siandiki kwa ushabiki wala kwa ajili ya kutaka kumtukuza mtu au kumkejeli mtu bali ninaandika huku nikimlilia Magufuli.
Magufuli hakuwa adui yangu alikuwa ni rais wangu.Tangu aingie madarakani nimekuwa mkosoaji wake. Hata nisipomkosoa kwa uwazi ila ndani ya moyo kuna mambo sikukubaliana naye lakini nilimheshimu kama rais wa nchi.Nilitambua kwamba kama mwanadamu hakuwa mkamilifu. Nilitambua pia kwamba kuna uwezekano pia kwamba mimi ndio mwenye kasoro na sio yeye. Hivyo basi namjua Rais wangu.
Rais Magufuli alitaka kufanya mengi na amefanya mengi.Kwa kadiri ya uwezo na nafasi yake amefanya mengi. Ameonesha uthubutu na ujasiri ila pia kuna mengine ambayo hayakwenda sawa.Kuna ambao walimwangusha katika uongozi na kuna ambao walisababisha ashindwe kufikia malengo yake. Kuna ambao hawakumwelewa na kuna ambao walimchukia bila sababu na kuna ambao walimchukia wakiwa na sababu. Hata hivyo ukweli utabaki kuwa ukweli. Ukimtoa Nyerere Magufuli ni mmoja kati ya viongozi bora wa zama hizi. Kwa kipindi cha miaka 6 tu ameweza kuthibitisha kwamba INAWEZEKANA kuwa na ndoto kubwa na kuanza safari ya kuzifikia.
Naumia sana nikifikri kwamba Magufuli pamoja na Katibu mkuu wake KIJAZI sasa hawapo tena. Katika wilaya ya UBungo imesimama kumbukumbu,Kijazi Interchange na Magufuli International Bus Terminal. Miradi ambayo kwa hakika ni alama ya Nyakati hizi zao.
Nataka sasa niseme tu kwamba nitamlilia Magufuli kwamba hatakuwepo wakati tutakapopanda TRENI yetu ya kwanza ya SGR, hatakuwepo wakati tutakapowasha umeme wetu wa Bwawa la Nyerere. Namlilia sana Magufuli kwa sababu nilitamani sana aendelee kuwepo. NIlitamani sana atimze ndoto zake kwa taifa letu kwa nyakati zetu.
Mungu Mpokee mja wako John Joseph Pombe Magufuli na uendelee kutulinda na kutubariki Watanzania wote
Inna Lillahi wa inna ilaihi raji'un
Bwana Ametoa na Bwana Ametwaa Jina la Bwana Libarikiwa-Apumzike kwa AmaniRaha ya milele umpe Ee Bwana; Na mwanga wa milele umwangazie, apumzike kwa aman