Ninakubaliana na Rais hakuna vita ngumu kama ya uchumi, tushikamane

Ninakubaliana na Rais hakuna vita ngumu kama ya uchumi, tushikamane

Maisha ni uchumi na uhuru wa kweli ni uchumi. Wale waliosomea siasa Uchumi yaani political Economy wanajua uhusiano wa siasa na uchumi. Pia wanafahamu uhusiano wa binadamu juu ya uzalishaji.

Kimsingi mapambano yoyote ya kisiasa msingi wake ni uchumi ni nani apate nini na kwa wakati gani. Taifa letu linapita kwenye kipindi kigumu kutokana na jitihada za Rais wetu kuleta mageuzi ya kiuchumi ili kulifanya taifa kujitegemea na kwa kulinda raslimali zake.

Hivyo vita vya ndani na nje ya nchi kama taifa na Rais wetu ni matokeo ya jitihada hizo na matamanio ya kundi la ndani ya nchi kushirikiana na mataifa nyonyaji nje.

Kihistoria kuanzia wakati wa biashara ya utumwa, ukoloni na sasa ukoloni mambo leo Afrika imekuwa mhanga wa ukandamizwaji na mataifa makubwa kunufaika na raslimali ipatikanayo Afrika.

Fika Ulaya ujionee ilivyojengwa kwa raslimali zetu na biashara ya utumwa enzi hizo. Mataifa haya hayataacha kupigania kututawala kiuchumi yakijua raslimali iliyopo ni muhimu kwa mustakabali wa mataifa hayo.

Kelele tunazosikia kwenye siasa ndani na nje ya nchi ni vita ya kiuchumi. Hivyo watanzania tushikamane na Rais wetu dhidi ya unyonyaji huu.

Aidha vyombo vya dola, serikali na mifumo yote haina budi kujengwa upya kwa mwelekeo wa falsafa ya kizalendo na kujitegemea ili kukabiliana na vita hii ambayo hujitokeza katika sura na mbinu mbalimbali zisizo na kikomo.
Uchumi wa Marekani kweli ni wa kuja kupigana vita vya kiuchumi na nchi ambayo inasaidiwa kujengewa matundu ya vyoo?Nchi ambayo ina import wembe kwamba bado haina techinolojia ya kuunda wembe, nchi inayo import toothpick.

Tuna Techinolonia gani tunayo watishia Marekani au EU? si tunatumia Internet yao? hizi Facebook si za kwao?

Si tuna vaa mitumba kutoka kwao? how come tuvae mitumba yao then tuseme tuna vita na wao?

Ni hilo Bwawa la umeme? au Flyover ya Ubungo? ndo vitu tishio kwa Wazungu?

Katika Majimbo yote ya Marekani hakuna hata moja ambalo tunalikaribia na hatutarajii kulikaribia hata kwa miaka 200 ijayo, Jimbo kama California GDP yake ni kubwa kuliko nchi zote za Africa combined.

How come nchi ambayo inazidiwa pato na makampuni ndo ije ipigwe vita? BP wana turn over kubwa kuliko GDP yetu.

Marekani ana vita ya Kiuchumi na nchi kama China, EU na hao wakina Russia ila si chi kama Tanzania ambayo bado techinolojia ya kuuda pini bado hatuna.

Ulaya wana vita vya kiuchumi na nchi kama China, Russia na kadhalika na hata hivyo sio vita bali wanapambana kuhakikisha wanafaidika, China inapambana kuhakikisha inafaidika na EU na EU nao hivyo hivyo.

CCM wakisema tuna vita vya kiuchumi na nchi kama Kenya nitawaelewa ila sio hao ambao huwa wanatujengea vyoo vya shule, wanatupatia ARV, wanatupa vyandarua.

Hizi Propaganda ni za kijinga na kuna wajinga wameaminishwa na wameamini, ni bahati mbay nchi ina kiwango kikubwa cha watu wasio weza kureason.
 
Tuko kwenye vita ya uchumi demokrasia inatumika kama mwamvuli tuu
Mna uchumi gani wa maana? Mngekuwa na uchumi kule chini kwenye list ya nchi maskini zaidi duniani mnafanya Nini? Acheni siasa rahisi kwenye Maisha ya watu kwa hizi propaganda mfu zisizo na sifa Tena duniani! Yaani ccm mpo madarakani miaka 50+ na mmeshindwa kuwatia wananchi kwenye umaskini uliopea na mnazidi kuwadanganya kila uchao!
Mwaka juzi mlikuja na Sera ya viwanda, vipo vingapi na wapi na vinazalisha Nini? Ati, Vita vya kiuchumi, vya wewe na Nani?
 
Mna uchumi gani wa maana? Mngekuwa na uchumi kule chini kwenye list ya nchi maskini zaidi duniani mnafanya Nini? Acheni siasa rahisi kwenye Maisha ya watu kwa hizi propaganda mfu zisizo na sifa Tena duniani! Yaani ccm mpo madarakani miaka 50+ na mmeshindwa kuwatia wananchi kwenye umaskini uliopea na mnazidi kuwadanganya kila uchao!
Mwaka juzi mlikuja na Sera ya viwanda, vipo vingapi na wapi na vinazalisha Nini? Ati, Vita vya kiuchumi, vya wewe na Nani?

Ndio, hii ni vita ya kiuchumi. Una hasira eeee😂😂😂😂😂
Pole wee usiyejua maana
 
Maisha ni uchumi na uhuru wa kweli ni uchumi. Wale waliosomea siasa Uchumi yaani political Economy wanajua uhusiano wa siasa na uchumi. Pia wanafahamu uhusiano wa binadamu juu ya uzalishaji.

Kimsingi mapambano yoyote ya kisiasa msingi wake ni uchumi ni nani apate nini na kwa wakati gani. Taifa letu linapita kwenye kipindi kigumu kutokana na jitihada za Rais wetu kuleta mageuzi ya kiuchumi ili kulifanya taifa kujitegemea na kwa kulinda raslimali zake.

Hivyo vita vya ndani na nje ya nchi kama taifa na Rais wetu ni matokeo ya jitihada hizo na matamanio ya kundi la ndani ya nchi kushirikiana na mataifa nyonyaji nje.

Kihistoria kuanzia wakati wa biashara ya utumwa, ukoloni na sasa ukoloni mambo leo Afrika imekuwa mhanga wa ukandamizwaji na mataifa makubwa kunufaika na raslimali ipatikanayo Afrika.

Fika Ulaya ujionee ilivyojengwa kwa raslimali zetu na biashara ya utumwa enzi hizo. Mataifa haya hayataacha kupigania kututawala kiuchumi yakijua raslimali iliyopo ni muhimu kwa mustakabali wa mataifa hayo.

Kelele tunazosikia kwenye siasa ndani na nje ya nchi ni vita ya kiuchumi. Hivyo watanzania tushikamane na Rais wetu dhidi ya unyonyaji huu.

Aidha vyombo vya dola, serikali na mifumo yote haina budi kujengwa upya kwa mwelekeo wa falsafa ya kizalendo na kujitegemea ili kukabiliana na vita hii ambayo hujitokeza katika sura na mbinu mbalimbali zisizo na kikomo.
Nadhani unachanganya mambo.
Mabeberu wameluwa wakitishia kutuwekea vikwazo sababu ya kukosekana utawala wa uwazi na demokrasia.
 
Acheni kuomba huruma kwenye jamii kwa kidingizio cha Vita ya uchumi.Na muda si mrefu mabeberu watawafarakanisha na raia wenu.
 
Huu utawala kwa kila mwenye akili na uzalendo lazima atauchukia
 
TANZANIA ni nchi huru na tuna natural resources nyingi tuu za kufanya tuwe self reliant kwahiyo porojo zenu za bei chee hazitatufanya tushindwe kusonga mbele kama Taifa.

Hii vita ya kiuchumi tutaishinda tuu kwa uwezo wa Mungu.
Tatizo Hawa Jamaa wakiamua kukomaa na wewe hata wateja wa Mali asili hutawapata, Venezuela wanamafuta lakini hayauziki na Iran pia
 
Maisha ni uchumi na uhuru wa kweli ni uchumi. Wale waliosomea siasa Uchumi yaani political Economy wanajua uhusiano wa siasa na uchumi. Pia wanafahamu uhusiano wa binadamu juu ya uzalishaji.

Kimsingi mapambano yoyote ya kisiasa msingi wake ni uchumi ni nani apate nini na kwa wakati gani. Taifa letu linapita kwenye kipindi kigumu kutokana na jitihada za Rais wetu kuleta mageuzi ya kiuchumi ili kulifanya taifa kujitegemea na kwa kulinda raslimali zake.

Hivyo vita vya ndani na nje ya nchi kama taifa na Rais wetu ni matokeo ya jitihada hizo na matamanio ya kundi la ndani ya nchi kushirikiana na mataifa nyonyaji nje.

Kihistoria kuanzia wakati wa biashara ya utumwa, ukoloni na sasa ukoloni mambo leo Afrika imekuwa mhanga wa ukandamizwaji na mataifa makubwa kunufaika na raslimali ipatikanayo Afrika.

Fika Ulaya ujionee ilivyojengwa kwa raslimali zetu na biashara ya utumwa enzi hizo. Mataifa haya hayataacha kupigania kututawala kiuchumi yakijua raslimali iliyopo ni muhimu kwa mustakabali wa mataifa hayo.

Kelele tunazosikia kwenye siasa ndani na nje ya nchi ni vita ya kiuchumi. Hivyo watanzania tushikamane na Rais wetu dhidi ya unyonyaji huu.

Aidha vyombo vya dola, serikali na mifumo yote haina budi kujengwa upya kwa mwelekeo wa falsafa ya kizalendo na kujitegemea ili kukabiliana na vita hii ambayo hujitokeza katika sura na mbinu mbalimbali zisizo na kikomo.
Ili askari aweze kupiga kwa ari anahitaji maneno mazuri na huduma stahili.
Kila siku kutukana askari,kuwakejeri,kuwatopokea ushauri wao,unawabagua
Unadhani utapata wapi ushirikiano vitani
Unataka askari wapigane huku umewashikia siraha nyuma yao!!

Kuanzia sasa tumieni neno ccm tushirikiane siyo watanzani.
 
Vita ya kiuchumi ni suala la kihistoria kwa nchi za magharibi kunufaika na raslimali zetu kwa bei nafuu, kuhamisha madini, biashara isiyo sawia na kwa mwendelezo wa kuifanya Afrika soko lao na sehemu ya kuchuma au kodi za tax holidays etc. Hivyo ukiweka mifumo ya kuwadhibiti au kujiimarisha mwenyewe mapema ki nchi lazima makampuni yao yapige kelele na hiyo ndiyo vita yenyewe inaanzia hapo. Huo ndio ukweli upende au usipende.
Ni kweli mkuu,lakini assume kusingekuwa na unyanyasaji wa vyama vya upinzani, uchaguzi uwe huru na haki hao watu wangetuingiaje? Na Kama taifa tungeshikamana kuwapiga vita
 
Back
Top Bottom