Ninapitia msongo mkali wa mawazo baada ya kusimamishwa kazi kisa vyeti feki. Naomba ushauri niweze kujikwamua

PGDE.
Ni mdogo wangu na si mwanangu.
Cha umuhimu ni kuwa nahitaji ajira na uhitaji.
Kama unaweza kunisaidia sawa ila kama utaona haikupendezi basi usinizibie riziki kwa wanaotaka kunisaidia.
 
Pole sana dadq,
Huna mtoto?

At 42 jitahidi usipate depression, kuanzia 35-55 usipoangalia depression itakumaliza sababu ni umri wa kusahihisha makosa, ikitokea ukakosea zaidi unaangukia kwenye depression.

Tafuta kazi halali, hata ndogo ya kuingiza kipato ufanye. Ukirudi kwenye kujiuza na umri huo ni hatari kwako.
 
Amina Manyanza ....yaani sihitaji kabisa kurudi nilikotoka.
Na wala sitaki kukumbuka maisha yangu ya nyuma.
Hat ushauri wenu pia unanipa moyo mno.
Nawashukuru sana.
 
Subira ni ibada usikate tamaa mambo yakuwa sawa mpaka hutoamini
 
P
Pole sana ndugu Mungu akutangulie waja wasikie kilio chako mama
 
Wewe ndo pia Miss Natafuta umeona ubadilishe kidogo jina? Halafu umejichanganya. Kuwa ulitumia cheti. Ulikuwa na cheti fake. Sasa unasema una Diploma ya Education toka UDSM. labda miaka yenu hii UDSM imeanza kutoa Diploma. Miaka yetu haikuwa inatoa Diploma. Upo hapa kutafuta watu wajiingize kuliwa.
 
PGDE.
Ni mdogo wangu na si mwanangu.
Cha umuhimu ni kuwa nahitaji ajira na uhitaji.
Kama unaweza kunisaidia sawa ila kama utaona haikupendezi basi usinizibie riziki kwa wanaotaka kunisaidia.
Post Graduate Diploma?

Unazidi kujichanganya Mkuu.

Mimi sikuzibii riziki, ila najaribu kukudadisi ili kuweka msawazo.

Maelezo yako yana ualakini mwingi.
 
Cheti kikichomwa moto si unaenda NECTA kutafuta kingine? Ulifanya hivyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…