Ninatoa dollar $1000 kwa atakaenifanikishia Visa hii

Ninatoa dollar $1000 kwa atakaenifanikishia Visa hii

Daah yaani bado mnasumbuka kwenda ulaya njia rahisi tafuta visa ya Hungary au Nchi yeyote ambayo ina masharti mepesi ukifika huko entry visa ya kwenda sehemu ingine kirahisi ila hii ilikua kabla ya Corona wale wa USA walikua wanaenda Mexico hata hiki kipindi cha Trump kwa wale wanaotaka kujilipua huko Ila kwa mwendaji na kurudi ukiwa na familia bongo USA ukienda kama mchungaji ni njia rahisi ila awepo mtu wa kanisa kule...
Biden mwanetu
 
Tulikuwa tunawaambia Jiwe ameshavuruga kwa mabeberu na Covidiots mindset yake
Huendi popote sasa hivi, utaliwa hela tu
Wabongo mna variants nyingi mno ........
 
Daah yaani bado mnasumbuka kwenda ulaya njia rahisi tafuta visa ya Hungary au Nchi yeyote ambayo ina masharti mepesi ukifika huko entry visa ya kwenda sehemu ingine kirahisi ila hii ilikua kabla ya Corona wale wa USA walikua wanaenda Mexico hata hiki kipindi cha Trump kwa wale wanaotaka kujilipua huko Ila kwa mwendaji na kurudi ukiwa na familia bongo USA ukienda kama mchungaji ni njia rahisi ila awepo mtu wa kanisa kule...
Hiyo njia waachie wasomali na waarabu ndio wanaiweza, unadhani hiyo mchezo kama unavyoona kwenye TV, nani aliwambia ukifika huko utapata visa kirahisi? unajua kwamba watu wanajicha kwenye difu na exel ya lorry?
Wabongo nyoso tu, South inawatosha kupitia Mozambique
 
Daah yaani bado mnasumbuka kwenda ulaya njia rahisi tafuta visa ya Hungary au Nchi yeyote ambayo ina masharti mepesi ukifika huko entry visa ya kwenda sehemu ingine kirahisi ila hii ilikua kabla ya Corona wale wa USA walikua wanaenda Mexico hata hiki kipindi cha Trump kwa wale wanaotaka kujilipua huko Ila kwa mwendaji na kurudi ukiwa na familia bongo USA ukienda kama mchungaji ni njia rahisi ila awepo mtu wa kanisa kule...
Maelezo mazuri mkuu! Kanisa nadhani Ni easiest way.
 
Hiyo njia waachie wasomali na waarabu ndio wanaiweza, unadhani hiyo mchezo kama unavyoona kwenye TV, nani aliwambia ukifika huko utapata visa kirahisi? unajua kwamba watu wanajicha kwenye difu na exel ya lorry?
Wabongo nyoso tu, South inawatosha kupitia Mozambique
Mimi Kuna mshkaji alitumia hii njia tena kipindi hiki cha corona aliomba Norway sijui Spain ila yupo kwenye Nchi aliyotaka kwenda yeye hapo bongo hakupata ushirikiano akaamua kudivert njia...hao wa maroli hawana karatasi wala chochote
 
Mimi Kuna mshkaji alitumia hii njia tena kipindi hiki cha corona aliomba Norway sijui Spain ila yupo kwenye Nchi aliyotaka kwenda yeye hapo bongo hakupata ushirikiano akaamua kudivert njia...hao wa maroli hawana karatasi wala chochote
Usiseme Norway sijui Spain
eleza vizuri tukuelewe au umepigiwa stori kijiweni.......
na kama ni Norway au Spain hizo ni Shenghen viza.....unapita tu lakini pia sio sasa hivi na corona
Tatizo linarudi palepale la kuipata hiyo Shenghen viza ndio hapo sasa.........
 
Usiseme Norway sijui Spain
eleza vizuri tukuelewe au umepigiwa stori kijiweni.......
na kama ni Norway au Spain hizo ni Shenghen viza.....unapita tu lakini pia sio sasa hivi na corona
Tatizo linarudi palepale la kuipata hiyo Shenghen viza ndio hapo sasa.........
Yan mm nakulewa vijana humu wanapigiwa story tu,wanazani kupata visa ni kama kwenda chooni mavi yanapokubana unakunya,unachamba then unatoka zako

Kama hujawah kutembea kwenda nchi yeyote Africa au Europe nakushauri anza na nchi ambazo ni free visa waiver kama Singapore, HK,Malaysia etc
 
Na flight iternary
Health insurance
Visa fee 60€
Bank statement wanawapigiaga simu bank husika so any counterfeit there is severely penalt

Tushajadili sana mambo ya visa humu jukwani. Mleta uzi ajaribu kusearch atapata majibu yake.

Ipo hivi, ubalozi haupigi simu bank yeyote na bank haiwezi toa taarifa za mteja wake kama sio takwa la mahakkama. Hiyo ni sheria sio hisani.

Hizo ni story za mitaani tu, watu hii michezo tushaifanya sana.
 
Usiseme Norway sijui Spain
eleza vizuri tukuelewe au umepigiwa stori kijiweni.......
na kama ni Norway au Spain hizo ni Shenghen viza.....unapita tu lakini pia sio sasa hivi na corona
Tatizo linarudi palepale la kuipata hiyo Shenghen viza ndio hapo sasa.........
Mkuu mbona unaongea kama ni kitu ambacho ni kigumu mno wakati tunasafiri kawaida tuu Mzee..mimi nimetumia mkwaju wa Tanzania bandika bandua,malawi,msumbiji,SA na sasa hivi nimerudi nyumbani na mkwaju huu usiochezewa tena mtoa uzi kashaelewa mimi kusafiri sio ishu toka miaka hiyo popote pale nikitaka kwenda nakwenda....
 
Ahahahaha!! Mbona Kiranga anaonekana mstaarabu!
Nimesoma huu uzi tangu awali, nafikiri jana, kwa kuwa nimekuwa tagged, na pia kwa kuwa napenda kuchangia habari za kusafiri sehemu tofauti duniani.

Nimepata shida sana kuujibu kutokana na misimamo yangu ya kifalsafa inayopingana na jambo la msingi kabisa la maudhui ya uzi huu. Rushwa.Hadaa.Kutofuata utaratibu.Kutumia fedha vibaya.

Nlitaka kuanza kujibu, nikaahirisha kwa kuogopa kutoa maoni ambayo kwa Kiingereza yanaitwa "blaming the victim", na sasa nimekuwa tagged mara ya pili. Hivyo naona ni wakati muafaka kujibu.

Kwanza kabisa nataka kusema kwamba, nina mshikamano na watu wote ambao wakiona sehemu moja haiwatoshi kujiendeleza mambo yao, wana haki ya kutalii , kusoma, kufanya kazi, biashara au kutembelea tu sehemu nyingine ya dunia. Hii kwangu ni haki ya msingi kabisa ya watu wote wenye uwezo na nia nzuri. Mimi mwenyewe ni mfano wa watu hao waliosafiri na kuanza maisha sehemu nyingine duniani.

Pili, mimi nataka niseme kwamba, napenda sana kuishi ndani ya sheria, na nataka sehemu yoyote ninayoshurutishika kuvunja sheria, sheria yenyewe ionekane kuwa ni ya kidhalimu na kuifuatilia kunavunja maadili makubwa zaidi. Hapa unaweza kuweka mifano kama ya sheria za ubaguzi wa rangi za enzi ya ukaburu Afrika Kusini au Marekani, na sheria za kikoloni zilizopinga watu kujitawala wenyewe.

Miaka yote zaidi ya ishiri niliyoishi ughaibuni, kosa kubwa kabisa nililofanya ni kwamba siku moja nilisahau kuondoa gari langu upande mmoja wa barabara uliokuwa unasafishwa, nikapata adhabu ya faini kwa kuwa sikuondoa gari upande huo. Na nililipa $35 kwa kosa hilo mara moja mtandaoni.Hilo ndilo kosa moja na pekee lililo katika rekodi yangu kwa muda wote huu. Naheshimu sana kuishi nje ya sheria mpaka muhasibu wangu alikuwa ananiambia kwamba tunaweza kupata "tax returns" zaidi kwa kubadili mambo madogo tu kwenye taarifa zangu za kodi, ambayo hayawezi kujulikana na mamlaka za kiserikali na yatanizidishia pesa sana, lakini nilikuwa nakataa, kwa sababu sijazoea kuishi kwa ujanja ujanja wa njia za panya.

Tatu, naheshimu sana taifa la Tanzania na nataka kuwa sehemu ya watu wanaopeleka mbele juhudi za kuondoa mawazo ya kuchochea rushwa, kufanya mambo kwa njia za panya na mkatomkato, na kiujumla kutofuatilia utaratibu uliowekwa.

Nimepata tabu sana kutoa msaada katika jambo ambalo linaonekana kuwa linakwendana na hadaa kama si jinai kabisa.

Nilitaka kusema kwa nini watu wanataka kusafiri muda huu wa mlipuko mkubwa wa ugonjwa wa Covid-19, lakini inawezekana safari zikawepo na haja ya kutulia ninayoiona mimi ikawa si sawa na ya mwingine.

Lakini pia, kama mtu ana shida ya kumfanya atake kusafiri kwenda nje, kwa nini hafuati matakwa ya visa yaliyowekwa na nchi hizo na kusafiri kihalali kama tulivyosafiri wengine? Kwa nini aanze kwa kutaka kutoa rushwa kwa kitu ambacho ukiwa umekamilisha masharti unakipata kwa visa fee ndogo tu? Mbona Watanzania wenye sababu nzuri na uwezo wanasafiri kila siku bila kutoa rushwa?

Ni kwamba huyu mwenzetu ni muoga/mvivu tu anataka kutumia fedha kama fimbo ya kutatua matatizo yote? Yani, anaweza kutimiza masharti, ila ni muoga/ mvivu tu, anataka kurahisisha mamabo kwa fedha? Kama ni hivyo, mimi nina matatizo na watu wanaotaka kutumia fedha kuruka utaratibu na siwezi kumsaidia.

Au ni kwamba huyu mtu anataka kusafiri kwenda nchi za nje bila ya kuweza kutimiza masharti yanayotakiwa? Kama ni hivyo, mimi pia nina matatizo na watu wanaotaka kusafiri kwenda nchi za nje huku hawajafikisha masharti yanayotakiwa, pengine hawana pa kufikia, hawana mpango wa kazi, hawana kitu kinachoeleweka wanachoenda kufanya, wanajiweka katika nafasi kubwa ya kukutwa na matatizo au hata kufa.

Au ni kwamba huyu mtu ana sababu mbaya, biashara haramu kama ya madawa ya kulevya, ugaidi, etc., na anaogopa kufuatilia mlolongo uliowekwa wa kupata visa, anataka kutumia njia za mkato ili mambo yake haramu yasigunduliwe? Hilo nalo mimi ninajiweka mbali nalo na siwezi kumsaidia mtu.

Mimi sina tatizo la kumsaidia mtu kusafiri, hususan upande wa Marekani. Maana huku ndiko niliko.Tena naweza kumsaidia mtu mpaka barua ya mualiko na akafikia nyumbani kwangu asilale hoteli. Kuna Mzee mmoja Profesa wa Chuo Kikuu alitaka kuja Marekani nikamuandikia hivyo barua ya mualiko akaja Marekani.Mtu mzima na heshima zake. Hata hapo ubalozi wa Marekani walivyomuangalia huyu Profesa wa Chuo Kikuu anaenda Marekani, na huyu anayemualika mtu wetu Marekani tunamjua nyendo zake siku nyingi hana kosa la hata speeding ticket na anatengeneza mkwanja wa maana kila mwaka ana kwake, hawezi kushindwa kumkarimu huyu Profesa, hawakuwa na shida. Walimpa visa.

Ila, nitakuwa mjinga nikimsaidia mtu simjui, sijui anataka kusafiri kwa sababu gani, na sijui amejikita kufanya nini. Nikimsaidia halafu kesho akikutwa na kesi ya ugaidi au madawa ya kulevya nikasema "huyu simjui, nilikutana naye online tu nikamsaidia", wakati naonekana nimempa msaada mkubwa sana, watu watanielewa kweli? Au wataniona mpango wangu na yeye ni mmoja?

Kibongobongo hili ni jambo rahisi tu kusaidiana bila kujuana, lakini huku tunavyoishi hakuna kitu kama hicho. Siku moja nilikuwa kwenye treni natoka mji wangu naenda mji wa state ya pili, sasa nikawa nimesahau kuweka full charge kwenye simu, nakaribia kufika ninakoenda.Natakiwa niwapigie simu wenyeji wangu waje kunichukua train station.Nikakuta simu haina charge. Nikamuomba mtu wa pembeni yangu, kijana Mmarekani mweusi, nikamwambia "kaka, nakuomba simu yako mara moja niwapigie wenyeji wangu waje kunipokea train station, kwani simu yangu imekwisha chaji".

Niliona ni ombi dogo tu. Kibongobongo.

Yule jamaa alinijibu kwamba yeye hawezi kunipa simu yake, kwa sababu alisema "I am flying under the radar".

Yani inaonekana alishapata matatizo na vyombo vya sheria, au anaogopa sana kupata matatizo na vyombo vya sheria, kiasi kwamba, anaogopa hata kumpa mtu baki simu yake apige, kwa sababu, ikitokea tu simu yake imeonekana kupiga kwenye network mbaya kama ya wauza madawa ya kulevya au magaidi, anaweza kupata tabu sana

Hayo ndiyo maisha tunayoishi huku. Na kipindi cha nyuma tumesaidia sana wasafiri wa Kitanzania. Kuna watu walikuwa wanakuja US hata hatuwajui tunakaa nao, wengine wameenda Canada, wengine mpaka leo tumejenga undugu.

Lakini, hapa kati, lazima niseme ukweli, biashara ya ngada imeharibu sana trust kati yetu Watanzania. Mtu kumsaidia mtu, hata kumpa hela tu, inabidi umjue, ama sivyo umpe hela cash ambayo haina track record.Kwa sababu unaweza kumsaidia mtu kwa roho nzuri tu, akapata matatizo, watu wakaangalia nani yupo kwenye mtandao wake wa kumsaidia.

Kuna mtu kapata kesi mpaka karudishwa Tanzania kwa kisa cha kumnunulia Mtanzania tiketi ya ndege tu, tena ile ya "ebwana mimi sina credit card ninunulie tiketi nakulipa hela yako cash hapa". Ikaonekana huyu amefanya biashara ya ngada, wewe umemnunulia tiketi, mna lenu moja mnajuana nyie. Wkamuunganishia na mambo mengine ya uongo na kweli, wakamrudisha Bongo.

Hivyo, mimi watu legit, hususan ninaowajua mwenyewe, sina tatizo kuwasaidia.

Ila hizi habari za kukutana mitandaoni tu, sanasana kama hujui process nitakuambia tu process ni hii, kinachoptakiwa ni passport na bank statement na sababu ya kusafiri na barua ya kazi au chuo au mualiko au reservation ya hoteli etc, mambo ambayo yote unaweza kuyapata online.

Waswahili walisema, mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba.

Nishaona watu wakipata tabu sana kwa kuendekeza tabia za Kibongobongo za kusaidia "watu wasiojulikana".

Huo ndio msimamo wangu kuhusu hili jambo.
 
Nimesoma huu uzi tangu awali, nafikiri jana, kwa kuwa nimekuwa tagged, na pia kwa kuwa napenda kuchangia habari za kusafiri sehemu tofauti duniani.

Nimepata shida sana kuujibu kutokana na misimamo yangu ya kifalsafa inayopingana na jambo la msingi kabisa la maudhui ya uzi huu. Rushwa.Hadaa.Kutofuata utaratibu.Kutumia fedha vibaya.

Nlitaka kuanza kujibu, nikaahirisha kwa kuogopa kutoa maoni ambayo kwa Kiingereza yanaitwa "blaming the victim", na sasa nimekuwa tagged mara ya pili. Hivyo naona ni wakati muafaka kujibu.

Kwanza kabisa nataka kusema kwamba, nina mshikamano na watu wote ambao wakiona sehemu moja haiwatoshi kujiendeleza mambo yao, wana haki ya kutalii , kusoma, kufanya kazi, biashara au kutembelea tu sehemu nyingine ya dunia. Hii kwangu ni haki ya msingi kabisa ya watu wote wenye uwezo na nia nzuri. Mimi mwenyewe ni mfano wa watu hao waliosafiri na kuanza maisha sehemu nyingine duniani.

Pili, mimi nataka niseme kwamba, napenda sana kuishi ndani ya sheria, na nataka sehemu yoyote ninayoshurutishika kuvunja sheria, sheria yenyewe ionekane kuwa ni ya kidhalimu na kuifuatilia kunavunja maadili makubwa zaidi. Hapa unaweza kuweka mifano kama ya sheria za ubaguzi wa rangi za enzi ya ukaburu Afrika Kusini au Marekani, na sheria za kikoloni zilizopinga watu kujitawala wenyewe.

Miaka yote zaidi ya ishiri niliyoishi ughaibuni, kosa kubwa kabisa nililofanya ni kwamba siku moja nilisahau kuondoa gari langu upande mmoja wa barabara uliokuwa unasafishwa, nikapata adhabu ya faini kwa kuwa sikuondoa gari upande huo. Na nililipa $35 kwa kosa hilo mara moja mtandaoni.Hilo ndilo kosa moja na pekee lililo katika rekodi yangu kwa muda wote huu. Naheshimu sana kuishi nje ya sheria mpaka muhasibu wangu alikuwa ananiambia kwamba tunaweza kupata "tax returns" zaidi kwa kubadili mambo madogo tu kwenye taarifa zangu za kodi, ambayo hayawezi kujulikana na mamlaka za kiserikali na yatanizidishia pesa sana, lakini nilikuwa nakataa, kwa sababu sijazoea kuishi kwa ujanja ujanja wa njia za panya.

Tatu, naheshimu sana taifa la Tanzania na nataka kuwa sehemu ya watu wanaopeleka mbele juhudi za kuondoa mawazo ya kuchochea rushwa, kufanya mambo kwa njia za panya na mkatomkato, na kiujumla kutofuatilia utaratibu uliowekwa.

Nimepata tabu sana kutoa msaada katika jambo ambalo linaonekana kuwa linakwendana na hadaa kama si jinai kabisa.

Nilitaka kusema kwa nini watu wanataka kusafiri muda huu wa mlipuko mkubwa wa ugonjwa wa Covid-19, lakini inawezekana safari zikawepo na haja ya kutulia ninayoiona mimi ikawa si sawa na ya mwingine.

Lakini pia, kama mtu ana shida ya kumfanya atake kusafiri kwenda nje, kwa nini hafuati matakwa ya visa yaliyowekwa na nchi hizo na kusafiri kihalali kama tulivyosafiri wengine? Kwa nini aanze kwa kutaka kutoa rushwa kwa kitu ambacho ukiwa umekamilisha masharti unakipata kwa visa fee ndogo tu? Mbona Watanzania wenye sababu nzuri na uwezo wanasafiri kila siku bila kutoa rushwa?

Ni kwamba huyu mwenzetu ni muoga/mvivu tu anataka kutumia fedha kama fimbo ya kutatua matatizo yote? Yani, anaweza kutimiza masharti, ila ni muoga/ mvivu tu, anataka kurahisisha mamabo kwa fedha? Kama ni hivyo, mimi nina matatizo na watu wanaotaka kutumia fedha kuruka utaratibu na siwezi kumsaidia.

Au ni kwamba huyu mtu anataka kusafiri kwenda nchi za nje bila ya kuweza kutimiza masharti yanayotakiwa? Kama ni hivyo, mimi pia nina matatizo na watu wanaotaka kusafiri kwenda nchi za nje huku hawajafikisha masharti yanayotakiwa, pengine hawana pa kufikia, hawana mpango wa kazi, hawana kitu kinachoeleweka wanachoenda kufanya, wanajiweka katika nafasi kubwa ya kukutwa na matatizo au hata kufa.

Au ni kwamba huyu mtu ana sababu mbaya, biashara haramu kama ya madawa ya kulevya, ugaidi, etc., na anaogopa kufuatilia mlolongo uliowekwa wa kupata visa, anataka kutumia njia za mkato ili mambo yake haramu yasigunduliwe? Hilo nalo mimi ninajiweka mbali nalo na siwezi kumsaidia mtu.

Mimi sina tatizo la kumsaidia mtu kusafiri, hususan upande wa Marekani. Maana huku ndiko niliko.Tena naweza kumsaidia mtu mpaka barua ya mualiko na akafikia nyumbani kwangu asilale hoteli. Kuna Mzee mmoja Profesa wa Chuo Kikuu alitaka kuja Marekani nikamuandikia hivyo barua ya mualiko akaja Marekani.Mtu mzima na heshima zake. Hata hapo ubalozi wa Marekani walivyomuangalia huyu Profesa wa Chuo Kikuu anaenda Marekani, na huyu anayemualika mtu wetu Marekani tunamjua nyendo zake siku nyingi hana kosa la hata speeding ticket na anatengeneza mkwanja wa maana kila mwaka ana kwake, hawezi kushindwa kumkarimu huyu Profesa, hawakuwa na shida. Walimpa visa.

Ila, nitakuwa mjinga nikimsaidia mtu simjui, sijui anataka kusafiri kwa sababu gani, na sijui amejikita kufanya nini. Nikimsaidia halafu kesho akikutwa na kesi ya ugaidi au madawa ya kulevya nikasema "huyu simjui, nilikutana naye online tu nikamsaidia", wakati naonekana nimempa msaada mkubwa sana, watu watanielewa kweli? Au wataniona mpango wangu na yeye ni mmoja?

Kibongobongo hili ni jambo rahisi tu kusaidiana bila kujuana, lakini huku tunavyoishi hakuna kitu kama hicho. Siku moja nilikuwa kwenye treni natoka mji wangu naenda mji wa state ya pili, sasa nikawa nimesahau kuweka full charge kwenye simu, nakaribia kufika ninakoenda.Natakiwa niwapigie simu wenyeji wangu waje kunichukua train station.Nikakuta simu haina charge. Nikamuomba mtu wa pembeni yangu, kijana Mmarekani mweusi, nikamwambia "kaka, nakuomba simu yako mara moja niwapigie wenyeji wangu waje kunipokea train station, kwani simu yangu imekwisha chaji".

Niliona ni ombi dogo tu. Kibongobongo.

Yule jamaa alinijibu kwamba yeye hawezi kunipa simu yake, kwa sababu alisema "I am flying under the radar".

Yani inaonekana alishapata matatizo na vyombo vya sheria, au anaogopa sana kupata matatizo na vyombo vya sheria, kiasi kwamba, anaogopa hata kumpa mtu baki simu yake apige, kwa sababu, ikitokea tu simu yake imeonekana kupiga kwenye network mbaya kama ya wauza madawa ya kulevya au magaidi, anaweza kupata tabu sana

Hayo ndiyo maisha tunayoishi huku. Na kipindi cha nyuma tumesaidia sana wasafiri wa Kitanzania. Kuna watu walikuwa wanakuja US hata hatuwajui tunakaa nao, wengine wameenda Canada, wengine mpaka leo tumejenga undugu.

Lakini, hapa kati, lazima niseme ukweli, biashara ya ngada imeharibu sana trust kati yetu Watanzania. Mtu kumsaidia mtu, hata kumpa hela tu, inabidi umjue, ama sivyo umpe hela cash ambayo haina track record.Kwa sababu unaweza kumsaidia mtu kwa roho nzuri tu, akapata matatizo, watu wakaangalia nani yupo kwenye mtandao wake wa kumsaidia.

Kuna mtu kapata kesi mpaka karudishwa Tanzania kwa kisa cha kumnunulia Mtanzania tiketi ya ndege tu, tena ile ya "ebwana mimi sina credit card ninunulie tiketi nakulipa hela yako cash hapa". Ikaonekana huyu amefanya biashara ya ngada, wewe umemnunulia tiketi, mna lenu moja mnajuana nyie. Wkamuunganishia na mambo mengine ya uongo na kweli, wakamrudisha Bongo.

Hivyo, mimi watu legit, hususan ninaowajua mwenyewe, sina tatizo kuwasaidia.

Ila hizi habari za kukutana mitandaoni tu, sanasana kama hujui process nitakuambia tu process ni hii, kinachoptakiwa ni passport na bank statement na sababu ya kusafiri na barua ya kazi au chuo au mualiko au reservation ya hoteli etc, mambo ambayo yote unaweza kuyapata online.

Waswahili walisema, mtaka nyingi nasaba, hupata mwingi msiba.

Nishaona watu wakipata tabu sana kwa kuendekeza tabia za Kibongobongo za kusaidia "watu wasiojulikana".

Huo ndio msimamo wangu kuhusu hili jambo.
Kuna jamaa aliniambia una matatizo saan sikuamini Hadi Sasa. Naona Kama umeishia kujinadi tu na kujivika utukufu na utakatifu.

Lakini ungekua ni mtu mwema na gentleman ungenifuata inbox na kuniomba taarifa zangu na details zangu muhimu ili Kama nitakidhi na kuaminika Basi unisaidie kwa vyovyote unavyoweza nitimize ndoto zangu unfortunately umetoa accusations na imbecille allegations kuhusu Watanzania.

Kusafiri ni haki ya mtu, Ni heri ungetoa ushauri tu na kuondoka zako kuliko kutoa accusations.

Kiukweli, umedhirisha upumbavu saana Ni Bora ungekaa kimya tu sababu even silence is an answer.
 
Kuna jamaa aliniambia una matatizo saan sikuamini Hadi Sasa. Naona Kama umeishia kujinadi tu na kujivika utukufu na utakatifu.

Lakini ungekua ni mtu mwema na gentleman ungenifuata inbox na kuniomba taarifa zangu na details zangu muhimu ili Kama nitakidhi na kuaminika Basi unisaidie kwa vyovyote unavyoweza nitimize ndoto zangu unfortunately umetoa accusations na imbecille allegations kuhusu Watanzania.

Kusafiri ni haki ya mtu, Ni heri ungetoa ushauri tu na kuondoka zako kuliko kutoa accusations.

Kiukweli, umedhirisha upumbavu saana Ni Bora ungekaa kimya tu sababu even silence is an answer.
Ndiyo maana nikasema kwamba nimepata tabu sana kuujibu uzi huu, na nilikataa kuujibu nikawa napewa tags kuujibu.

Nilijua kwamba nikiujibu ni lawama (majibu yangu hayataeleweka kwa wengine) na nisipoujibu ni lawama (Kiranga tunamuita ajibu na kusaidia kwenye uzi anaringa).

Ila ukae ukijua kitu kimoja, mimi siko hapa ili wewe unione mtu mzuri sana.

Ukinitag kutaka maoni yangu, nakupa maoni yangu.

Na siogopi kuonekana mpumbavu, naogopa kuogopa kuonekana mpumbavu.

Nimetoa majibu kwa hoja, umerudi kunishambulia kwa kitu kinachoitwa "ad hominem" kwa kilatini.

An ad hominem attack, yani, kuacha kujibu hoja za mtu na kuanza kumshambulia mtu mwenyewe kibinafsi, ni attack fulani za watu mufilisi wa hoja ambao wameshindwa kujadili hoja wanatukana mtu.

Sasa mimi kusema sitaki kumsaidia mtu kusafiri nje kwa njia za mkato, kwa kuwa njia sahihi zinajulikana nimefanya kosa gani?

Au mimi kusema sipendi watu wanaotumia fedha kupindisha utaratibu nimekosea nini?

Au mimi kusema sitaki kusaidia rushwa na hadaa nimekosea nini?

Au mimi kusema siku hizi kuna watu wengi wanafanya uhalifu wa biashara za madawa ya kulevya na ugaidi, na hivyo kumsaidia mtu nisiyemjua ni jambo hatari nimekosea nini?

Jifunze siku nyingine usiwa tag watu kuwaomba msaada katika mambo ambayo hawayafagilii, wasije kukukatalia halafu ukawalaumu wao kwa kusimamia misimamo yao na kukueleza kuhusu misimamo hiyo, wakati umewaomba msaada wewe mwenyewe.

Wewe unataka nikufuate inbox wakati wewe hujanifuata inbox, sawa hiyooo?


Haaaaaata, hiyo si sawa LaRosa, wacha vitukoo.
 
Ndiyo maana nikasema kwamba nimepata tabu sana kuujibu uzi huu, na nilikataa kuujibu nikawa napewa tags kuujibu.

Nilijua kwamba nikiujibu ni lawama (majibu yangu hayataeleweka kwa wengine) na nisipoujibu ni lawama (Kiranga tunamuita ajibu na kusaidia kwenye uzi anaringa).

Ila ukae ukijua kitu kimoja, mimi siko hapa ili wewe unione mtu mzuri sana.

Ukinitag kutaka maoni yangu, nakupa maoni yangu.

Na siogopi kuonekana mpumbavu, naogopa kuogopa kuonekana mpumbavu.

Nimetoa majibu kwa hoja, umerudi kunishambulia kwa kitu kinachoitwa "ad hominem" kwa kilatini.

An ad hominem attack, yani, kuacha kujibu hoja za mtu na kuanza kumshambulia mtu mwenyewe kibinafsi, ni attack fulani za watu mufilisi wa hoja ambao wameshindwa kujadili hoja wanatukana mtu.

Sasa mimi kusema sitaki kumsaidia mtu kusafiri nje kwa njia za mkato, kwa kuwa njia sahihi zinajulikana nimefanya kosa gani?

Au mimi kusema sipendi watu wanaotumia fedha kupindisha utaratibu nimekosea nini?

Au mimi kusema sitaki kusaidia rushwa na hadaa nimekosea nini?

Au mimi kusema siku hizi kuna watu wengi wanafanya uhalifu wa biashara za madawa ya kulevya na ugaidi, na hivyo kumsaidia mtu nisiyemjua ni jambo hatari nimekosea nini?

Jifunze siku nyingine usiwa tag watu kuwaomba msaada katika mambo ambayo hawayafagilii, wasije kukukatalia halafu ukawalaumu wao kwa kusimamia misimamo yao na kukueleza kuhusu misimamo hiyo, wakati umewaomba msaada wewe mwenyewe.

Wewe unataka nikufuate inbox wakati wewe hujanifuata inbox, sawa hiyooo?


Haaaaaata, hiyo si sawa LaRosa, wacha vitukoo.
Hata sijaisoma ndefu saana hii mkuu wangu kiranga. [emoji41]
 
Back
Top Bottom