Ningekuwa Mkuu wa Wilaya ningetatua tatizo la ajira kwa watu wote wanaoishi wilayani kwangu

Ningekuwa Mkuu wa Wilaya ningetatua tatizo la ajira kwa watu wote wanaoishi wilayani kwangu

Wahitimu tumieni ujuzi mliopata vyuoni katika utatuzi wa changamoto zinazoikuta jamii na watu wanao wazunguka kwa kufanya hivyo jamii mnayoisaidia haitowaacha bila kuwalipa fadhila za mchango wenu huku moyoni mwenu mkiwa na moyo wa kutoa msaada mtajikuta mnaona faida ya elimu zenu lakini mambo ya kujiona msomi unajitenga na watu upo bize kuangalia matangazo ya ajira mitandaoni ukishinda ndani ukitoka upo na bahasha mkononi faida ya elimu utachelewa sana kuiona.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚Mkuu hii mikakati nadhani kuna wakuu wawilaya humu wananote saivi. Wanadhani ukuu wa wilaya ni kutakua kero za maji tu.
Hhahahhaa...! Maji na umme ni sera za kitaifa. Kama mkuu wa wilaya inabidi ujiongeze uwe na mambo ya mfano ambayo hayaharibu mfumo uliowekwa
 
Wahitimu tumieni ujuzi mliopata vyuoni katika utatuzi wa changamoto zinazoikuta jamii na watu wanao wazunguka kwa kufanya hivyo jamii mnayoisaidia haitowaacha bila kuwalipa fadhila za mchango wenu huku moyoni mwenu mkiwa na moyo wa kutoa msaada mtajikuta mnaona faida ya elimu zenu lakini mambo ya kujiona msomi unajitenga na watu upo bize kuangalia matangazo ya ajira mitandaoni ukishinda ndani ukitoka upo na bahasha mkononi faida ya elimu utachelewa sana kuiona.
Mkuu usirahisishe hivo ukadhani mambo ni rahisi kama enzi zile za Maisha Bora kwa kila Mtanzania....! Hapo katikati mambo yalivurugika...
 
Wakuu wa wilaya hawa hawa ambao criteria kuu ni kuwa kada mtiifu wa CCM?

Huku niliko kwa sasa Mayor ni kiongozi mkubwa na anatosha kabisa kuendesha shughuli nyingi za kiutawala ....

Achana na level nyingine ya wawakilishi kwenye bunge ! Wote hawa hupitia michakato yenye mchujo na uwazi hadi mtu anachaguliwa hawezi kuwa 'okota okota'

Kwanini wenzetu wa wanaweza ni rahisi sana kila kitu kiko wazi na mtu yuko chini na sio juu ya sheria!

Tanzania kuna watu wako juu ya sheria na hata walio juu ya sheria wanawalinda wengine wengi !

Je ukibisha basi naomba uje na jibu kuwa Rais wa Tanzania akifanya makosa atashitakiwa na mahakama gani hata ni watu gani wanaweza kumshitaki...

Mwisho tu niseme kwa cheo na mfumo wa UDC kwa Tanzania uliyoyapanga hayawezakani hata kidogo...
 
Ningekuwa ndio mkuu wa wilaya ningetatua tatizo la ajira kwa watu wote wanaoishi wilayani kwangu.

Hizi ni hatua ambazo ningechukua.

Kwanza ningetambua idadi ya wahitimu wote wanaotokea wilayani kwangu.

Ningehakikisha kama hawana kazi za kufanya nawatafutia kampuni, taasisi na viwanda vya kufanyia mazoezi ya vitendo (internship) kipindi wanasubiria ajira zao.

Nisingekubali wahitimu wanaotokea wilayani kwangu kukaa bila kitu cha kufanya huku wakipoteza maarifa yao waliojifunza vyuoni bila kuyafanyia chochote.

Pili ningehakikisha natambua idadi ya wanafunzi wanaoendelea na masomo vyuoni. Hawa wangekuwa wanajiunga kufanya field moja kwa moja kwenye kampuni, taasisi na viwanda vilivyopo wilani kwangu.

Ningeanzisha wakala wa kuajiri kwa kazi zote zinazotangazwa na kampuni za binafsi katika wilaya yangu. Hivyo ningetambua nafasi zote zilizowazi katika kampuni, taasisi na viwanda binafsi kisha zingetangazwa kupitia wakala hiyo wilayani kwangu.

Tatu ningeanzisha vikundi mbalimbali kwaajili ya ujasiriamali ambavyo ningevidhamini mikopo ya riba nafuu. Vikundi hivi vingefanya ujasiriamali mbalimbali mfano ufugaji, kilimo, biashara za bidhaa, usafirishaji n.k. Haya yote yangekua chini ya uangalizi wa wilaya yangu.

Kwakweli mambo yangekua ni moto kwenye wilaya yangu.

Kwenye wilaya kuna matatizo mengi lakini nadhani tatizo la ajira ndio kubwa kuliko matatizo yote Tanzania. Ni tatizo gumu linalohitaji ushirikiano na akili ya ziada ili kuweza kulitatua.

Wewe kama mkuu wa wilaya unatumia mbinu zipi kutakua tatizo hilo.

Karibuni kwa maoni.
we mwenyewe huna ajira
 
Mimi nashauri wahitimu wasio na kazi wakamatwe wafunguliwe kesi za uhujumu uchumi. Wamefuja fedha za walipa kodi kwa kusomeshwa na serikali halafu wanamaliza anakaa bila ya kufanya chochote? How? Walienda shule kulemaa ama kupata mbinu za kujitafutia riziki??.
Wewe raia wa wapi?!!! Wamesomeshwa au wamekopeshwa hizo pesa ?, Kwahio wakamatwe na wafungwe ili waende kulishwa kwa pesa za walipa kodi ?

Ofcourse ili suala likiendelea kujibiwa kwa majibu mepesi kama yako in the end, hao watu hawatakaa bure bali ndio wale watakaokuingilia usiku nyumbani kwako ili kugawana chako kiwe chenu
 
Kwahio wakamatwe na wafungwe ili waende kulishwa kwa pesa za walipa kodi ?
Wakienda jela watalimishwa na kuzalisha kwa mijeledi mpk hela yetu itakapo rudi yote. Miaka ya kukaa jela itategemea kiwango cha mkopo mhitimu alichopewa.

Na usiwe na wasi wasi kwamba Hawa wahitimu wanaweza kuanza kuwa majambazi. Hawana uwezo huo. Watu ambao wamekosa uthubutu kiasi cha kukosa cha kufanya, hawawezi ujambazi maana unahitaji uthubutu mkubwa.

Wahitimu wa aina hii ni mzigo kwa taifa.
 
Wakienda jela watalimishwa na kuzalisha kwa mijeledi mpk hela yetu itakapo rudi yote. Miaka ya kukaa jela itategemea kiwango cha mkopo mhitimu alichopewa.

Na usiwe na wasi wasi kwamba Hawa wahitimu wanaweza kuanza kuwa majambazi. Hawana uwezo huo. Watu ambao wamekosa uthubutu kiasi cha kukosa cha kufanya, hawawezi ujambazi maana unahitaji uthubutu mkubwa.

Wahitimu wa aina hii ni mzigo kwa taifa.
Kindly that's not good solution. We don't solve problems like that
 
Kindly that's not good solution. We don't solve problems like that
Usiwaonee huruma. Wahenga wanasema "uvivu nyumba ya njaa". Tukiwaonea huruma wavivu hawa wa kufikiri taifa litaangamia kwa njaa.

Nchi ina kila aina ya rasilimali msomi anakosaje kazi ya kufanya baada ya kumaliza masomo? Inaudhi Sana.

Acha niishie hapa nitapandwa na hasira nitukane tena.
 
Mimi nina kazi zangu nafanya mkuu nimeajiri watanzania. Ila 2025 nagombea ubunge ili kusaidia watanzania. Naingia bungeni kwenda kuwasemea watanzania. Nadhani umenipata mkuu.
Ukishakuwa petty bourgeoisie habari ya kuwasemea watanzania itakuwa ndoto. Utakumbuka maneno yangu.
 
Back
Top Bottom