Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hii njia ambayo nitaianika hapa si njia rasmi na si njia ya kuweza kutumiwa kichwakichwa. Hakikisha suala la ajira na sifa kedekede unazitupa mbali, let's say vitakuja automatically.
Ningefanya upelelezi kwa kina, ningeweza hata kufanya jambo kwa muda wa mwaka mmoja ili nikusanye taarifa za kweli na uhakika.
Ningefuatilia mtandao mmoja wa ujambazi kwa kina nipate details zao zote.
Kisha naandika barua kwa OCD, RC au kwa Afisa usalama wa wilaya au mkoa kuhitaji kuonana naye. Najua katika watu ambao hawakatai meeting na raia ni watu wa ulinzi na usalama.
- Ningemjua mkuu wao
- Center yao kuu
- Wanapoficha silaha
- Idadi kamili ya genge lao
- Muda na wakati wanaofanya matukio n.k, n.k
Unaweza kutaka kuonana na meneja mkoa TANROADS au dawasa ukazungushwa miezi na miezi ila kwa upande wa ulinzi na usalama haiko hivyo.
Siku nikikutana naye namweleza kukereka kwangu na vitendo vya uhalifu nchini hivyo kwa mapenzi ya dhati nimejitolea kuchunguza uhalifu kama jitihada za kusaidia dola.
Nitampa fuul information za hilo genge.
NB: Mweleze hatua hadi hatua ulizopitia katika investigation yako ili kumwondolea mashaka juu yako asije kuhisi ulihusika kwa namna moja au nyingine.
😂 😂 😂Blaza mwambie waiter asikuongeze bia, ushalewa wewe rudi home ukalale. Alafu nyie ndio mnasababisha bangi ionekane adui wa taifa.