Ningepata nafasi ningemshauri haya Rais Samia

Ningepata nafasi ningemshauri haya Rais Samia

Chambusiso

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2007
Posts
2,592
Reaction score
4,640
Wanabodi,

Mama Samia ni Rais na kiongozi wa taifa letu, ni msikivu na mnyenyekevu sana, mwenye subira na utulivu sana wa kusikiliza na kuchambua mambo kabla hajafanya maamuzi na anapofanya maamuzi yake anayasimamia, huku akitoa nafasi ya kukosolewa sana bila kuwa jazba wala kutumia manguvu makubwa aliyonayo. Kumbukeni kwa katiba iliyopo angekuwa mtawala kama waliotangulia leo hii na mijadala migumu inayoendelea tungeshaanza kusikia wakosoaji wanakutana na matokeo hasi tena gizani.

Nimefungua uzi huu kwa watu positive tu wanaoweza kusema mambo yanayojenga watupie hapa, najua sisi ndio wananchi wenyewe na wawakilishi wetu wanajiwakilisha wenyewe tu (kule bungeni) na matumbo yao, lakini mama huyu alisema anapita JF mara kwa mara, so tukiweka mawazo positive hapa naamini yeye na team yake wataokota machache na watachagua ya kufanyia kazi (hatuna bunge), so bila jazba wadau karibuni tushauri mambo makubwa yanayoweza kuleta "transformation" sio ya kutibu njaa, fikiria nchi yako baada ya miaka 30-50 itakuwa wapi kama mawazo yako yatafuatwa au kutumika hata asilimia ndogo tu. Vijana wenye mihemko wanaweza kwenda kwenye nyuzi zingine tu sio lazima wachangie hapa.

Langu nalosema, ningepata nafasi ya kumshauri Mama Samia, Mheshimiwa Rais, ningemwambia apeleke vijana kusoma nje - hata kama uchumi wetu ni mgumu kiasi gani mama rudisha utaratibu wa zamani kupeleka vijana hata 100 kila mwaka wakapate exposure na elimu ya kuja kubadilisha mindset zetu, tumekuwa watanzania tunaofanana wote, hamna msomi wala asiyesoma wote tuna mawazo yanayofanana 100% peleka watu waje na upeo mpya, kama Nyerere alivyofanya miaka ya nyuma, watu waje wawe wataalam, waalimu, viongozi etc. warudi na maarifa mapya, hautapata matokeo mwaka huu au ndani ya uongozi wako lakini miaka 20-30 ijayo kama wamesoma watu angalau watu 3000-5000 nje ya mfumo wa elimu wa kwetu, tutapata mabadiliko makubwa. Ulisema unafungua nchi, fungua sasa na kwenye maarifa. Yaje maarifa mapya na yatumike kwa vizazi vijavyo achana na chawa wanaongalia leo tu!

Wewe ungepata nafasi ungemshauri nini?

Karibuni sana wadau.
 
Wazo zuri sana ila changamoto ni kwamba kwa huo mfumo anaotumikia naona wangepelekwa watoto na wajukuu wa viongozi waandamizi. Kwa hiyo tunakuwa kwenye vicious cycle
 
" Ni Rais na kiongozi wa taifa letu, ni msikivu na mnyenyekevu sana, mwenye subira na utulivu sana wa kusikiliza na kuchambua mambo kabla hajafanya maamuzi na anapofanya maamuzi yake anayasimamia, huku akitoa nafasi ya kukosolewa sana bila kuwa jazba wala kutumia manguvu makubwa aliyonayo" Sidhani kama ni kweli ila kama hujuwi kaa ukijuwa wapo wanaompa maelekezo..,
 
Wazo zuri sana ila changamoto ni kwamba kwa huo mfumo anaotumikia naona wangepelekwa watoto na wajukuu wa viongozi waandamizi. Kwa hiyo tunakuwa kwenye vicious cycle

Ni kweli itaanzia kwao, lakini ikifanyika consistently kwa miaka say 10 mfululizo, watachanganya tu na hata kama ni wao kuwe tu na sharti na kurudi, wakirudi wataanza kudilute hawa watu wanaosomea manzese primary, kinondoni secondary, then chuo UD! So akili yake itakuwa ni flyovers tu za magu ndo kaona na kuexperience na pia hana confidence kwa sbb mfumo wetu wa elimu ni wa vitisho levels zote na pia kwa wazazi wetu, tunaishi maisha ya kutishana muda wote na matokeo yake tunaua vipaji vya watoto wetu wote. So something has to start somewhere.
 
" Ni Rais na kiongozi wa taifa letu, ni msikivu na mnyenyekevu sana, mwenye subira na utulivu sana wa kusikiliza na kuchambua mambo kabla hajafanya maamuzi na anapofanya maamuzi yake anayasimamia, huku akitoa nafasi ya kukosolewa sana bila kuwa jazba wala kutumia manguvu makubwa aliyonayo" Sidhani kama ni kweli ila kama hujuwi kaa ukijuwa wapo wanaompa maelekezo..,

Ndio maana nimeshauri tusio kwenye kundi la kumuelekeza tuseme hapa, ndio jukwaa letu, sidhani kama thread ikienda mbele sana itapuuziwa, watamficha hadi lini? Na yeye anakuja hapa personally kasema! Tusijudge tuwe open minded
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Ndio maana nimeshauri tusio kwenye kundi la kumuelekeza tuseme hapa, ndio jukwaa letu, sidhani kama thread ikienda mbele sana itapuuziwa, watamficha hadi lini? Na yeye anakuja hapa personally kasema! Tusijudge tuwe open minded
Usemayo ni kweli Mkuu., ila kuna mambo tu yakujiuliza hivi huyo mam anauwezo kabisa wakuamua jambo yeye kama yeye bila wale wanaompa muongozo., I don't think so. Kuna vitu vinafikirisha sana, na mfano mzuri ni hili swala la bandari kila chawa amekuwa msemaji wa serikali, na ukiangalia kwa makini hata wao pia wanatofautiana kimaelezo, unategemea raia wa kawaida ataelewa nin.
 
Mbona kashaanza kupitia Samia scholarship?
Wanaopata division One ya 3-4 form 6 ndo wanapelekwa Kila mwaka kusomea Uhandisi na afya.
 
Watapelekwa watoto wa vigogo wa CCM kwenda kutumbua bata kwa gharama ya fedha za mlipakodi masikini and nothing will change.

Dawa ni Katiba bora na mpya ikibidi tuwe na coalition government.
 
Ningemshauri pia aachane na mawazo anayopewa na mstaafu mmoja hivi ambae qnampeleka pabaya kabisa.

Kama kaanza ni jambo jema sana, ili liwe na impact angalau wasipungue 100, kama wanakwenda 30-40 watakwenda na kurudi kushibisha matumbo yao tu, angalau malengo ya kati yawe graduates 5000 hadi 10000 ndio unaweza kuona transformation, level ndogo hizo wazazi wengi tu wanapeleka watoto wao. Hii inatakiwa iwe ni mkakati wa kisera na ulenge maeneo mahususi, yenye mahitaji makubwa. Kwa mfano tukiwa na wahadhiri wenye exposure kubwa, wanavyuo wetu hawataenda chuo kudesa na kurudi mtaani kufanya deals, ningemshauri badala ya kupeleka pesa JKT kuzichoma na kuchezea, peleka watoto shule nje affirmatively. Itakuwa na impact sana kuliko huo uchafu unaofanyika makutupora, bulombora, mafinga etc!
 
Watapelekwa watoto wa vigogo wa CCM kwenda kutumbua bata kwa gharama ya fedha za mlipakodi masikini and nothing will change.

Dawa ni Katiba bora na mpya ikibidi tuwe na coalition government.

Ikifanyika miaka 20 mfululizo hata hao wa CCM wataisha na kama wanarudi wataleta tu mawazo mapya na huenda baada ya exposure watakuwa na ujasiri wa kuona CCM inavyodanganya na kutumia udhaifu wa elimu yetu! Kila kitu lazima kianzie mahali, kumbuka wakienda nje hawatasomeshwa na wanaitikadi wa CCM lakini wakisomea hapa for sure watamkuta Palamagamba (MCCM wa jalalani) so risk ni ndogo nje kuliko ndani!
 
Wishfully thinking, CCM wameshajiapiza kutufanya watumwa wao milele.

Yes inawezakuwa wishfull thinking, but haijafanyiwa practice au inaweza kuboreshwa, ni mawazo tu kwa sababu hata hao maCCM ni watanzania, wakienda na wakapata exposure wakarudi na elimu (kuwe na standards za kupima) bado watakuwa ni sehemu ya jamii yetu. Kiongozi kipi bora hii ya sasa kuwa na UVCCM viazi kama hawa tunaowaona au wakasomeshwe? Huoni kwamba wa sasa hivi ni vipofu kabisa wakirudi huenda watapata mwanga kiasi, to me naona bora nusu hasara kuliko hawa wa leo ambao haogopi kusema akija Mange watamgawana, kwa msomi atajua hiyo ni criminal hawezi kutamka, suppose imetokea aliyetajwa kafa muda mfupi uliofuata? Ingekuwa nchi inayofuata sheria si kapata murder hapo? Just thinking loud.
 
Yes inawezakuwa wishfull thinking, but haijafanyiwa practice au inaweza kuboreshwa, ni mawazo tu kwa sababu hata hao maCCM ni watanzania, wakienda na wakapata exposure wakarudi na elimu
Watoto wa Vigogo wamejaa Ulaya na Marekani kazi yao kubwa kutafuta Wanawake wa Kizungu na kuwaoa kujenga status kuongea slang na kuvaa designer clothes.
 
Watoto wa Vigogo wamejaa Ulaya na Marekani kazi yao kubwa kutafuta Wanawake wa Kizungu na kuwaoa kujenga status kuongea slang kuvaa designer clothes.

Kwa sababu wamepelekwa na wazazi wao, kukiwa na affirmative action na issue nzima ikabebwa na serikali kwa makubaliano ya serikali na serikali naamini kutakuwa na matokeo baada ya muda, kwa mfano akaamua kufanya maboresho ya wahadhiri tu akahakikisha ndani ya miaka 10 vyuo vikuu vyote vina wahadhiri waliosoma elimu halisi na kupata exposure, nina uhakika tutakuwa na maprofesa wasiofukuzia uteuzi wa ukuu wa wilaya ambao hata wasanii wa maigizo wanaweza! Watasimamia profession na watafanya tafiti wakiwa na network za waliosoma nao Ulaya na nchi zingine, huku wakishirikiana!
 
1. Jambo jema ni kumwambia Samia atoe waiver kwa kijana yoyote wa kitanzania mwenye kitambulisho cha taifa apewe Passport free of charge.

2. Samia atoe rai kwa mabalozi wote walio ughaibuni kuangalia fursa za kazi na kurahisisha makampuni katika nchi husika yanaingia mikataba ya kuja chukua wafanyakazi Tanzania.

3. Zoezi liendelee hadi Samia atavyohakikisha ametoa vijana zaidi ya laki 5 ndani ya nchi. Vijana hawa wataenda huko watapata ujuzi wa kimataifa, watapata fedha za kimataifa ambazo zikitumwa nyumbani ni faida kwa nchi, na siku wakirudi nyumbani wataweza tranfer knowledge waliyoipata huko nje kuileta Tanzania.

Raisi hapo atakumbukwa kwa Mengi.
 
Ushauri mbovu. Vijana wanaosoma nje wapo wengi kweli, mamia kwa maelfu kila mwaka wanaenda.

Mawaziri na top officials wa serikali wengi degree za pili wamesomea nje ya nchi.

Hakuna jipya
 
1. Jambo jema ni kumwambia Samia atoe waiver kwa kijana yoyote wa kitanzania mwenye kitambulisho cha taifa apewe Passport free of charge.

2. Samia atoe rai kwa mabalozi wote walio ughaibuni kuangalia fursa za kazi na kurahisisha makampuni katika nchi husika yanaingia mikataba ya kuja chukua wafanyakazi Tanzania.

3. Zoezi liendelee hadi Samia atavyohakikisha ametoa vijana zaidi ya laki 5 ndani ya nchi. Vijana hawa wataenda huko watapata ujuzi wa kimataifa, watapata fedha za kimataifa ambazo zikitumwa nyumbani ni faida kwa nchi, na siku wakirudi nyumbani wataweza tranfer knowledge waliyoipata huko nje kuileta Tanzania.

Raisi hapo atakumbukwa kwa Mengi.

Wazo jema sana, na kuongeza akaanzisha vituo vya elimu vya kujifunza mambo ya kimataifa, the anaweza pia kuanzisha sera ya kuuza ujuzi nje, yani vijana waliosoma wenye potential ya kuuzika nje wakawezeshwa say na recuiters na kuachwa wakatafute ingebadilisha sana mtazamo! Tatizo kubwa sana la wasomi wa kitanzania ni kukosa confidence na hii inatoka na kuivishwa nusunusu vyuoni!
 
Ushauri mbovu. Vijana wanaosoma nje wapo wengi kweli, mamia kwa maelfu kila mwaka wanaenda.

Mawaziri na top officials wa serikali wengi degree za pili wamesomea nje ya nchi.

Hakuna jipya

Wewe ungemshaurije kiongozi? Ndo maana ya kuwepo mjadala huu!
 
Ushauri mbovu. Vijana wanaosoma nje wapo wengi kweli, mamia kwa maelfu kila mwaka wanaenda.

Mawaziri na top officials wa serikali wengi degree za pili wamesomea nje ya nchi.

Hakuna jipya

Wapo wangapi? Any data? Kwa mujibu wa data zilizopo online watanzania wenye degree hawajafika 60,000 au wapo juu kidogo, mawaziri ni wangapi? Concept hapa ni kwamba watu wenye exposure wawepo wengi, mazingira yatawaforce kuwajibika tu awe ni CCM, au mwengine yeyote, sio watunga sera wanakuwa ni hawa ambao wameona flyover kwa mara ya kwanza za magufuli. So kila anachosema na kuplan anatumia mfano huohuo kila siku, kwa kuwa hajaona zaidi ya hapo, kila siku wanaongelea SGR, Stiglers gorge, kijazi flyover, basi ndio mwisho wa ufahamu wao! Exposure ya watu wengi ya makusudi kabisa itabadilisha mtazamo wa jamii ya watanzania.
 
Back
Top Bottom