MUSHEKY
JF-Expert Member
- May 9, 2014
- 2,812
- 2,760
Moja kwa moja kwenye mada,
Toka kutolewa kwa hukumu iliyomfungia aliyekua msemaji wa klabu ya yanga ndugu Haji Sunday Manara kumekua na makundi mawili ama moja linahisi Manara ameonewa ama jingine linahisi TFF wapo sahihi
Nirudi nyuma kidogo kuwakumbusha mashabiki wa mpira kua sheria yoyote ya taasisi yoyote ile ndani ya Tanzania haikinzani na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa mantiki hiyo katiba yetu ndio sheria mama ya sheria zote hapa nchini
Kwa kua sheria na kanuni za TFF zilitumika kumuadhibu kiongozi huyu wa kabumbu hapa nchini sanjali na zile zilizotumika pia kuwaadhibu kocha Mbwana Makata wa Dodoma jiji na mtangazaji Shafi Dauda ni kanuni hizo hizo za TFF
Kwa heshima na taadhima nimshauri ndugu yangu Haji Manara afuate sheria na kanuni zile zile za TFF kuitafuta haki yake kama anahisi ameonewa
Ipo wazi na ifahamike mlalamikaji baada ya hukumu kupita alipewa fursa ambayo ni haki yake kimsingi kukata rufaa ndani ya muda uliowekwa kisheria na yeye mwenyewe anajua kua muda huo ukipita hakuna cha ziada kwake zaidi ya watoa hukumu kukoleza wino wa hukumu hiyo
Jambo ambalo wanafamilia ya mpira wanapaswa kumshauri haji ni kwamba malumbano anayoyaendeleza kwenye media na kutafuta uungwaji mkono na followers wengi ni kupoteza muda tu kusiko na msingi wowote
Aidha ipo hoja ya msingi ya Manara kwamba Karia alimtukana n.k, kama Sunday anaona iko hivyo anapaswa kutumia sheria zile zile kumshtaki Karia na kwa kua sheria ni msumeno karia ataitwa mbele ya jopo na ushahidi wa Manara utasikilizwa na hukumu itatolewa ikishindikana atakata rufaa kwenye vyombo vyenye mamlaka zaidi n.k
Mwisho kabisa nimeona mahali Haji manara anamtaka waziri wa michezo kuingilia kati suala lake na TFF akiamini kwamba mwanasiasa huyu atainfluence maamuza ya TFF dhidi yake
Nimuombe Manara aachane na majaribio ya namna hiyo kwani sheria za mpira Duniani "FIFA" zinaharamisha kabisa masuala ya hukumu za kisoka kuingiliwa na wanasiasa na moja ya adhabu ni kuifanya nchi husika kufungiwa kushiriki michuano yoyote inayotambulia na chombo jicho cha kuendesha kandanda la Dunia
Niseme tu watanzania tunaupenda mpira na hatupo tayari kwa hilo na nawashauri watanzania tuufunge mjadala wa Manara kwa kumshauri asitafute suluhu ya jambo "lake" kwa kuitisha press za mara kwa mara ama kulalamika juu ya maamuzi fulani bali afuate taratibu za kisheria hata ikiwezekana kimya kimya akate rufaa ama vinginevyo
Hayo ndio yanafanyika hata kwenye hukumu za raia kwenye mahakama za kiraia, hutapata haki yako kwa kurandaranda huku na kule kudai uamuzi wa mahakama si sahihi
Nawasilisha
Toka kutolewa kwa hukumu iliyomfungia aliyekua msemaji wa klabu ya yanga ndugu Haji Sunday Manara kumekua na makundi mawili ama moja linahisi Manara ameonewa ama jingine linahisi TFF wapo sahihi
Nirudi nyuma kidogo kuwakumbusha mashabiki wa mpira kua sheria yoyote ya taasisi yoyote ile ndani ya Tanzania haikinzani na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa mantiki hiyo katiba yetu ndio sheria mama ya sheria zote hapa nchini
Kwa kua sheria na kanuni za TFF zilitumika kumuadhibu kiongozi huyu wa kabumbu hapa nchini sanjali na zile zilizotumika pia kuwaadhibu kocha Mbwana Makata wa Dodoma jiji na mtangazaji Shafi Dauda ni kanuni hizo hizo za TFF
Kwa heshima na taadhima nimshauri ndugu yangu Haji Manara afuate sheria na kanuni zile zile za TFF kuitafuta haki yake kama anahisi ameonewa
Ipo wazi na ifahamike mlalamikaji baada ya hukumu kupita alipewa fursa ambayo ni haki yake kimsingi kukata rufaa ndani ya muda uliowekwa kisheria na yeye mwenyewe anajua kua muda huo ukipita hakuna cha ziada kwake zaidi ya watoa hukumu kukoleza wino wa hukumu hiyo
Jambo ambalo wanafamilia ya mpira wanapaswa kumshauri haji ni kwamba malumbano anayoyaendeleza kwenye media na kutafuta uungwaji mkono na followers wengi ni kupoteza muda tu kusiko na msingi wowote
Aidha ipo hoja ya msingi ya Manara kwamba Karia alimtukana n.k, kama Sunday anaona iko hivyo anapaswa kutumia sheria zile zile kumshtaki Karia na kwa kua sheria ni msumeno karia ataitwa mbele ya jopo na ushahidi wa Manara utasikilizwa na hukumu itatolewa ikishindikana atakata rufaa kwenye vyombo vyenye mamlaka zaidi n.k
Mwisho kabisa nimeona mahali Haji manara anamtaka waziri wa michezo kuingilia kati suala lake na TFF akiamini kwamba mwanasiasa huyu atainfluence maamuza ya TFF dhidi yake
Nimuombe Manara aachane na majaribio ya namna hiyo kwani sheria za mpira Duniani "FIFA" zinaharamisha kabisa masuala ya hukumu za kisoka kuingiliwa na wanasiasa na moja ya adhabu ni kuifanya nchi husika kufungiwa kushiriki michuano yoyote inayotambulia na chombo jicho cha kuendesha kandanda la Dunia
Niseme tu watanzania tunaupenda mpira na hatupo tayari kwa hilo na nawashauri watanzania tuufunge mjadala wa Manara kwa kumshauri asitafute suluhu ya jambo "lake" kwa kuitisha press za mara kwa mara ama kulalamika juu ya maamuzi fulani bali afuate taratibu za kisheria hata ikiwezekana kimya kimya akate rufaa ama vinginevyo
Hayo ndio yanafanyika hata kwenye hukumu za raia kwenye mahakama za kiraia, hutapata haki yako kwa kurandaranda huku na kule kudai uamuzi wa mahakama si sahihi
Nawasilisha