Nini hatma ya Muba na John wa kipindi cha Mkasi?

Niliwahi kuandika uzi kuhusu hiki kipindi kifupi kilikua kipindi cha udaku na umbea. Maswali ya Salama yalikua predictable na repeatedly hata kwa wageni wa kariba tofauti. Sioni ajabu ratings za kipindi kwenda chini na kufungwa
 
Niliwahi kuandika uzi kuhusu hiki kipindi kifupi kilikua kipindi cha udaku na umbea. Maswali ya Salama yalikua predictable na repeatedly hata kwa wageni wa kariba tofauti. Sioni ajabu ratings za kipindi kwenda chini na kufungwa
hilo sio kweli.. miongoni mwa vipindi vilivyouza sana tanzania mkasi kilikua juu.. kilikua na ubunifu mwingi but kwa mtu overrated huwezi kujua.. corner angle mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii kama Youtube, twitter etc hao ndio miongoni mwa waanzilishi kwa Tanzania na video zao kwenye youtube ndio kipindi cha kwanza kupiga pesa ndefu na kupata views wengi wa youtube.. kuhusu kufunga biashara hiyo ni kawaida kama umepata biashara yenye manufaa kubadilisha ni kawaida, pia kila kitu na kipindi kina msimu wake ili ku maximize profit kwa wakati sahihi
 
Ulichoongea ni sahihi mkuu, lakini usimlaumu sana Salama juu ya kushindwa kumhoji vema Makamba before that judge kwanza interest yake kisiasa ipoje mfano utapata shida kidogo kumhoji mwanasheria wakati wewe taaluma ya sheria hujawa familiar nayo; na hata kipindi chake ki ktk mlengo upi? Yeye career yke ni intertainer though alitakiwa kusoma articles za kisiasa na hata kujiandaa kabla ya kumhoji. Lakini bado Salama anabaki kuwa most presenter talented Tz, ukitaka kuamini hili mfuatilie kwenye kipindi chake cha Ngaz kwa ngaz namna alivyo design, graphics and animation na hata anavokiendesha! Hakika mkasi team wanastahili pongezi.
 

Hujui nini unaongea. Mkasi ilianza kwa speed sababu kilikuwa ni kipindi kipya na watu walitegemea kuona kitu kipya, kilianza vizuri sababu ya umbea na udaku ambao kama ujuavyo ndiyo unaouza. Maswali yao ya kitoto mtu yeyote makini hawezi kuangalia mkasi isipokuwa kwa watu walio katika huo mlengo. Views za shows za mwisho zilipungua sana kulinganisha na zile za mwanzo. Watu wengi waliacha kufuatilia mkasi

Kipindi ni content sio camera angle tu. Salama alionyesha kupwaya sana pindi alipohoji watu makini kama Mo Dewji, Makamba na Zitto

Kama biashara inalipa kwanini ubadilishe? Mkasi ilikosa wadhamini ikabidi wabadilike
 
Kwani kipindi kikiwa cha udaku tatizo liko wapi?

Mbona hata TMZ wana kipindi kabisa kwenye runinga.

Tatizo liko wapi?

Mtu kama hupendi si usiangalie tu.

Mnataka wote tujadili mambo ya uchumi na siasa?

Maisha si uchumi na siasa tu.

Y'all need to loosen up.

Unataka siasa...mwangalie Jenerali Ulimwengu.

Geeez
 
1. Je vipindi vingapi vipya vimenza but havikua na attention kama mkasi...Nonsense 2. Hakuna mahali nimeandika camera angle nimeandika corner angles za social network.. naona unadandia gari kwa mbele na una speed ya light, tulia soma kwa makini 3. Biashara kubadilishwa ni kitu cha kawaida sana inategemea ni biashara gani iliyokujia mbele yenye manufaa maradufu kama umeshakua mfanya biashara wa vitendo utakua unanielewa but kama ni mfanya biashara wa mdomoni huwezi kuelewa kamwe..
 
Wewe ndio hujui unachoongea kwa taarifa yako mkasi tv walipata sponsors, hata kipindi chenyewe hakijaanza kurushwa yaani idea Ipo tu kwenye karatasi wadhamini wakatoa mpunga. Navofahamu Mimi Tz kuigana kwingi sana, mfano idea yote na content ya kipindi imeigwa na clouds ( zamaradi). That's why wamekuja na kipindi kipya ngaz kwa ngaz angalia ubunifu uliomo mle unajua mtu akifanya vizuri mpe hongera zake though mapungufu hayawez kukosena.
 
Wadhamini wakubwa wa Mkasi yani coca cola walikataa kuendelea na udhamini baada ya kipindi ratings za kipindi kuchukua nosedive ndiyo sababu ya mkasi kufungwa fuatilia.

Sijaona ngaz kwa ngaz yet. Wanaweka YouTube?
 


Coca cola wadhamini wakubwa wa mkasi waliacha kudhamini ule ujinga.
 
Savage
 

Salama ni mzuri sana kuwahoji watu wa kwenye burudani,watu wengi wa burudani walikuwa wameshahojiwa so alionyesha upungufu mkubwa alivyowahoji wataalamu kama Martin Chegere na Hilda Ringo
 
Ni kweli. Na huwa ananogesha habari kwenye kile kipindi cha Sam kwa sababu anapendelea sana zile za 'kimbea'
Like yule bwege wa clouds,some qns anahoj unapokuwa kwenye daladala unahis aibu kabisa,kwenye segment ya U heard
 
Ndiyo inatakiwa kuwa hivi, majadiliano yaliyosheheni mifano na uhalisia.

Nadhani wahusika na wanaoshughulika na haya mambo watakuwa wamejifunza vitu vipya.
Yeah, hawa jamaa mawazo Yao ni shule tosha, unaweza usinunue kitabu badala yake unasoma komenti tu za Kiranga na Ngabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…