Nini hatma ya Ubunge wa Mbunge wa Ngorongoro baada ya wapiga kura wake kuhamishiwa Handeni?

peno hasegawa

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2016
Posts
14,255
Reaction score
23,949
Ninajiuliza huyu mbunge atapigiwa kura na nani huko Ngorongoro baada ta wapiga kura wake kuhamishiwa Handeni?

Sijasikia familia ya huyo Mbunge imehamishiwa Handeni kutoka Ngorongoro.

Pili baada ya Wamaasai kuhamishwa Ngorongoro hiyo wilaya itafutwa kiutawala au nini hatima yake?
 
Jimbo la Ngorongoro ni kubwa kuliko sehemu inayohamishwa.
Wanaohamishwa ni wale walio ndani ya hifadhi, kuna sehemu kubwa sana inabaki ni pamoja Wasso Loliondo na viunga vyake
 
Huelewi chochote na hutakaa uelewe chochote kuhusu NGORONGORO.
 
Nchi hii ina vijana wa hovyo sana. Yaani mleta mada unajaribu kusema eneo wanaloondoshwa ndio jimbo zima? Kuwa wananchi wote wa jimbo wamehamishwa au kwenda kwenye maeneo ambayo ni majimbo mengine??

JF imekuwa sehemu ya kuandika tu ili mradi kuna namna na njia, sio kwa sababu kuna hoja!
 
Kwani jimbo lote lilimezwa na mbuga?Kama kuna maeneo yalikuwa nje na waliyopo wanakidhi atakuwa na hao.
 
Umesikia wapi kwamba wilaya nzima wanahama?
 
Anahama nao🏃.Situmesha Ina mifano,vipi wale wa michongo wa Mzee wa gereji.🤔
 
kwani yeye anasemaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…