Nini huathiri ukuaji bora wa ng'ombe wa nyama? Nini kifanyike?

Nini huathiri ukuaji bora wa ng'ombe wa nyama? Nini kifanyike?

Idrissou02

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2018
Posts
354
Reaction score
656
Habarini ndugu wa JF,

Tupeane mawazo hapa kwenye hii mada tafadhali. Kwann jamii zetu nyingi zinashindwa kuzalisha ng'ombe nyama wa kutosha? Je, tuchukue hatua gani maana ng'ombe nyama wanalipa bana kama ukifankiwa kuwakuza.
 
Mi napinga si kweli kwamba wafugaji wameshindwa kuzalisha ng'ombe/ Nyama ya kutosha. Tatizo ni ubora. Tuna ng'ombe wengi sana ila changamoto ni malisho au lishe duni inayopelekea kuwa nyama isiyokuwa na viwango hasa kwa masoko ya kimataifa. Na sio kwamba wafugaji hawana elimu,wana elimu sana tu ila wanaamua kufuga kwa mazoea na kupenda njia rahisi. Pia wengine hawataki kabisa kuachana na njia zao za asili.

Tutafika huko kwenye kuzalisha ng'ombe na nyama yenye ubora endapo tu km sisi vijana wasomi tutaingia kwenye ufugaji seriously badala ya kuwaachia Wamasai na Wasukuma pekee.

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
 
Wafugaji wengi mnategemea nyasi zinazo jiotea zenyewe.

Tafuta shamba andaa aina ya majani au nafaka ambazo ng'ombe anaweza kula mwaka mzima.

jifunze kupanda aina miti ambayo ukisaga majani yake mabichi ng'ombe anakula.

jifunze kulime mazao ambayo yatakuwa pande mbili kwenye biashara na mifugo kwenye ulishaji.
 
Shida serikali ya ccm haitaki wafugaji waendeleaje..karne hii waancha watu wanazurura hovyo na ngombe..wakiharibu mazingira na kukausha vyanzo vya maji.

Inapaswa wapewe vitalu vya ufugaji..wapewe wataalamu katika maeneo husika..wapewe mbegu bora..malisho bora...soko la nyama lipo na haliwezi kuisha ndani na nje ya nchi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Shida serikali ya ccm haitaki wafugaji waendeleaje..karne hii waancha watu wanazurura hovyo na ngombe..wakiharibu mazingira na kukausha vyanzo vya maji.

Inapaswa wapewe vitalu vya ufugaji..wapewe wataalamu katika maeneo husika..wapewe mbegu bora..malisho bora...soko la nyama lipo na haliwezi kuisha ndani na nje ya nchi.

#MaendeleoHayanaChama
Malalamiko hayatakufikisha popote. Wakati wewe unalalamika na CCM, Kuna wenye malisho Yao binafsi. Hakuna anayekatazwa kumiliki Shamba lake la ufugaji. Pia Kuna wanaoomba vitalu vya ufugaji kwenye ranch za Taifa. Nenda Kibebe Farm ana ekari 4,000, nenda pale Ndiwiri-Kilolo, nenda kwa Mtanga Farm kaone. Sehemu nyingi tu kwa Sasa watu wanafanya unenepeshaji wa mifugo.
 
Malalamiko hayatakufikisha popote. Wakati wewe unalalamika na CCM, Kuna wenye malisho Yao binafsi. Hakuna anayekatazwa kumiliki Shamba lake la ufugaji. Pia Kuna wanaoomba vitalu vya ufugaji kwenye ranch za Taifa. Nenda Kibebe Farm ana ekari 4,000, nenda pale Ndiwiri-Kilolo, nenda kwa Mtanga Farm kaone. Sehemu nyingi tu kwa Sasa watu wanafanya unenepeshaji wa mifugo.
Wewe ndio hujaja na solution..umekula kulalamika pia..sio ngelei hao wenye hiyo mitaji..naongelea wasukuma..wamasai na wamangati wanaozurula nchi nzima kusaka malisho..je hao serikali yako ya ccm imewasaidiaje.?

#MaendeleoHayanaChama
 
Wewe ndio hujaja na solution..umekula kulalamika pia..sio ngelei hao wenye hiyo mitaji..naongelea wasukuma..wamasai na wamangati wanaozurula nchi nzima kusaka malisho..je hao serikali yako ya ccm imewasaidiaje.?

#MaendeleoHayanaChama
Kwa Nini unakazana na "kusaidiwa"?

Wao wanajisaidiaje?

Wewe unaona wasukuma Hawana mitaji!! Hao ng'ombe sio mitaji?

Kila siku wamasai, wasukuma na hao wamang'ati wanauza ng'ombe kwenye minada, kwa Nini hawatengi pesa za kununua mashamba wakafugia humo?

Hivi wewe unajua kwamba bado Kuna maeneo unapata ekari ya mita 70 kwa 70 kwa shilling 50,000 tu?

Hivi unajua kwamba mfugaji anaweza kukopa TADB kwa kutumia dhamana ya mifugo?

Kijana wa kiume kwa Nini unapenda Sana kulalamika usaidiwe?
 
Malalamiko hayatakufikisha popote. Wakati wewe unalalamika na CCM, Kuna wenye malisho Yao binafsi. Hakuna anayekatazwa kumiliki Shamba lake la ufugaji. Pia Kuna wanaoomba vitalu vya ufugaji kwenye ranch za Taifa. Nenda Kibebe Farm ana ekari 4,000, nenda pale Ndiwiri-Kilolo, nenda kwa Mtanga Farm kaone. Sehemu nyingi tu kwa Sasa watu wanafanya unenepeshaji wa mifugo.
Asante Kwa mawazo yako mazuri,ni kweli kulalamika hakutufikishi popote.

Nataka kujua hayo mashamba Ndiwiri Kilolo,Kibebe na Mtanga yapo wapi yaani kijiji gani na wilaya gani,je wanahusika na unenepeshaji tu au na ngombe wa maziwa?

Pia nimelisikia shamba la mzungu lipo Kilolo anafuga ng'ombe wa maziwa unalifahamau?nalo lipo kijiji gani.
 
Asante Kwa mawazo yako mazuri,ni kweli kulalamika hakutufikishi popote.

Nataka kujua hayo mashamba Ndiwiri Kilolo,Kibebe na Mtanga yapo wapi yaani kijiji gani na wilaya gani,je wanahusika na unenepeshaji tu au na ngombe wa maziwa?

Pia nimelisikia shamba la mzungu lipo Kilolo anafuga ng'ombe wa maziwa unalifahamau?nalo lipo kijiji gani.
Vyote unenepeshaji na ng'ombe wa maziwa. Kilolo mashamba ya wazungu yapo mengi hasa wilaya za Kilolo na Iringa vijijini.
 
Vyote unenepeshaji na ng'ombe wa maziwa. Kilolo mashamba ya wazungu yapo mengi hasa wilaya za Kilolo na Iringa vijijini.
Sawa hayo mashamba uliyoyataja yapo vijiji gani na wilaya gani, nataka nitembelee kujifunza.
 
Sawa hayo mashamba uliyoyataja yapo vijiji gani na wilaya gani, nataka nitembelee kujifunza.
Kibebe farm ipo Iringa nje kidogo ya Ipogoro. Ndiwiri ipo njia ya kuelekea Kilolo kutokea ipogoro. Mtanga fika mtanga butcher uhindini Iringa utaelekezwa. Kikongoma Kalenga kwa akina MT. Nduli kwa Asas......kama utapata appointment. Unaweza kukuta hata huko ulipo, yapo mashamba ya wafugaji. Watu wamewekeza kila mahali.
 
Kibebe farm ipo Iringa nje kidogo ya Ipogoro. Ndiwiri ipo njia ya kuelekea Kilolo kutokea ipogoro. Mtanga fika mtanga butcher uhindini Iringa utaelekezwa. Kikongoma Kalenga kwa akina MT. Nduli kwa Asas......kama utapata appointment. Unaweza kukuta hata huko ulipo, yapo mashamba ya wafugaji. Watu wamewekeza kila mahali.
Nashukuru.
 
Malalamiko hayatakufikisha popote. Wakati wewe unalalamika na CCM, Kuna wenye malisho Yao binafsi. Hakuna anayekatazwa kumiliki Shamba lake la ufugaji. Pia Kuna wanaoomba vitalu vya ufugaji kwenye ranch za Taifa. Nenda Kibebe Farm ana ekari 4,000, nenda pale Ndiwiri-Kilolo, nenda kwa Mtanga Farm kaone. Sehemu nyingi tu kwa Sasa watu wanafanya unenepeshaji wa mifugo.
Yeye anajua kuilalamikia CCM tu utafikiri imembebea kichwa....
 
Yeye anajua kuilalamikia CCM tu utafikiri imembebea kichwa....
Raisi Mkapa aliwahi kusema "Lawama ni tamu sana ikiwa inatoka kinywani mwako". Ni rahisi Sana kulaumu na kulalamika kuliko kuchukua hatua
 
Binafsi naona serikali aijaweka kiupambele swala la wafugaji kama sector ya kukuza uchumi wa ndani na nje kuna changamoto nyingi kubwa zaidi ni ukosefu wa elimu kwa wafugaji sjaona serikali ikiweka mpango mkakati wa kuweka wataalamu kuwaelimisha wafugaji ufugaji wenye tija mfano jinsi ya kupanda malisho ,kupunguza idadi kubwa ya wanyama katika eneo moja au athari za kimazngira zinazosababishwa na overstocking /overgrazing
Pili kuna ukosefu wa breed za ngombe wa nyama wenye tija ukiangalia ngmbe wa mmasai anatumia miaka mingi kufikia uzito wa kuchinjwa ambapo aileti faida zaida yankuaribu mazingira .
Tatu ukosefu wa malisho wa kutosha pamoja na kua na ardhi kubwa hapa tz lakini bado kuna changamoto ya uhaba wa malisho hasa kipindi cha kiangazi matokea yake kunakua idadi kubwa ya vifo vya wanyama kila mwaka

Mwisho naweza kusema wafugaji wangepatiwa elimu juu ufugaji wa kisasa na kuachana na ufugaji wa zamani wajue kupanda malisho mbali mbali kwenye maeneo yao ili kupunguza kuhama hapa na pale kufuata malisho hata pia jinsi ya kutunza vyanzo vya maji ,kuzalisha malisho na kuyastore kama silage na hay kuhakikisha upatikanaji wa tiba za wanyama pia
Habarini ndugu wa JF,

Tupeane mawazo hapa kwenye hii mada tafadhali. Kwann jamii zetu nyingi zinashindwa kuzalisha ng'ombe nyama wa kutosha? Je, tuchukue hatua gani maana ng'ombe nyama wanalipa bana kama ukifankiwa kuwakuza.
 
Binafsi naona serikali aijaweka kiupambele swala la wafugaji kama sector ya kukuza uchumi wa ndani na nje kuna changamoto nyingi kubwa zaidi ni ukosefu wa elimu kwa wafugaji sjaona serikali ikiweka mpango mkakati wa kuweka wataalamu kuwaelimisha wafugaji ufugaji wenye tija mfano jinsi ya kupanda malisho ,kupunguza idadi kubwa ya wanyama katika eneo moja au athari za kimazngira zinazosababishwa na overstocking /overgrazing
Pili kuna ukosefu wa breed za ngombe wa nyama wenye tija ukiangalia ngmbe wa mmasai anatumia miaka mingi kufikia uzito wa kuchinjwa ambapo aileti faida zaida yankuaribu mazingira .
Tatu ukosefu wa malisho wa kutosha pamoja na kua na ardhi kubwa hapa tz lakini bado kuna changamoto ya uhaba wa malisho hasa kipindi cha kiangazi matokea yake kunakua idadi kubwa ya vifo vya wanyama kila mwaka

Mwisho naweza kusema wafugaji wangepatiwa elimu juu ufugaji wa kisasa na kuachana na ufugaji wa zamani wajue kupanda malisho mbali mbali kwenye maeneo yao ili kupunguza kuhama hapa na pale kufuata malisho hata pia jinsi ya kutunza vyanzo vya maji ,kuzalisha malisho na kuyastore kama silage na hay kuhakikisha upatikanaji wa tiba za wanyama pia
Bwana salmin siraj Mimi napingana na wewe. Serikali imefanya mengi tu kwenye sekta ya kilimo na ufugaji. Miradi ya ASDP ipo tangu miaka ya 2008 kuwaelimisha kilimo na ufugaji wa kibiashara. SAGCOT, MIVARF yote imekuja miaka takribani 10 iliyopita. Kuna mabwana mifugo kila halmashauri mpaka kwenye majiji. Kuna kata Zina bwana/bibi mifugo. Ulitaka serikali ifanye nini la ziada?

Tangu enzi na enzi (ukiacha mwaka Jana 2021) huwa Kuna maonesho ya nanenane, unajua lengo lake ni Nini??
Pale kuna wakulima wakubwa na wadogo, wafugaji wakubwa mpaka ranch, Kuna vyuo vya kilimo na ufugaji, Kuna VETA/SIDO. Pale unakuta mbegu Bora za ng'ombe, mbuzi, kondoo, kanga, Bata, hata malisho. Shamba la mifugo la Mafinga wanazalisha mbegu za nyasi nzuri kwa ajili ya malisho, uliwahi kuzitafuta ukakosa?
Mfugaji gani anazitafuta elimu anaikosa?

Mimi mwenyewe nimewahi kwenda kuonesha ufugaji wa Bata bukini pale John Mwakangale Uyole nikanunua na mbegu za lucina.

Swali ni je Hawa wafugaji wanahudhuria sehemu kama hizi?
Wafugaji wanawekeza kwenye elimu?
Acheni Lawama za kipuuzi. Ngozi nyeusi wengi hatuzingatii maarifa na technology. Tunafanya ili mradi. Hata umwelimishe vipi anarudia Mambo yake vilevile. Unless soko limwekee masharti ndipo atalazimika kuyafuata mfano kwenye tumbaku na Parachichi.
 
Back
Top Bottom