Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Hasa majengo ya nane nane. Kwenye viwanja hivi ambavyo vipo karibu kila mkoa, utakuta taasisi nyingi zimejenga majengo mazuri na ya kudumu. majengo haya huwa hayatumiki na watu kwa mwaka mzima isipokuwa Kwenye sherehe za nane nane au sabasaba. Tunawezake kuyatumia majengo haya kwa faida kwa mwaka mzima?
Maoni yangu. Serikali za majiji zingeanzisha digital parks kwenye viwanja hivyo. Wasupply internet kwenye viwanja hivyo bure. Watu wenye kufanya kazi mtandaoni waende kutumia majengo na internet ya hapo. hili linawezekana kabisa, kuna miji kama Kinondoni, Mbeya na Dodoma yameanzisha timu na yanazihudumia. hawawezi shindwa kuweka internet ya bure kwenye viwanja hivyo.
Siku hizi mitandaoni kuna vikazi vingi sana vinavyoweza mpatia mtu kipato. kwa kufanya hivyo itakuwa ni hatua fulani kuelekea kutatua tatizo la ajira.
Unafikiri majengo hayo ambayo hukaa bure yanawezaje kutumika kwa faida.
Maoni yangu. Serikali za majiji zingeanzisha digital parks kwenye viwanja hivyo. Wasupply internet kwenye viwanja hivyo bure. Watu wenye kufanya kazi mtandaoni waende kutumia majengo na internet ya hapo. hili linawezekana kabisa, kuna miji kama Kinondoni, Mbeya na Dodoma yameanzisha timu na yanazihudumia. hawawezi shindwa kuweka internet ya bure kwenye viwanja hivyo.
Siku hizi mitandaoni kuna vikazi vingi sana vinavyoweza mpatia mtu kipato. kwa kufanya hivyo itakuwa ni hatua fulani kuelekea kutatua tatizo la ajira.
Unafikiri majengo hayo ambayo hukaa bure yanawezaje kutumika kwa faida.