Nini kifanyike kuisafisha CCM ili iliongoze taifa kwa ufanisi maana bado wapowapo sana

Nini kifanyike kuisafisha CCM ili iliongoze taifa kwa ufanisi maana bado wapowapo sana

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Kwa namna upepo wa kisiasa unavyovuma hapa nchini inaonyesha wazi kwamba uwezekano wa wapinzani kuchukua nchi kwa miaka ya karibuni ni mdogo sana, ingawa sijasema haiwezekani ila dalili zinaonyesha kwamba hawana huo ubavu Kwa sababu zifuatazo:

1. Kubadilibadili hoja
2. Kuvurugana kama ilivyotokea chadema, cuf, act, na sasa nccr mageuzi. Hii mifarakano inavidhoofisha sana vyama vyetu vya upinzani na kuwakatusha tamaa wafuasi wao.
3. Kuwa na viongozi wa kudumu na wamiliki wa vyama husika
4. Kukosa upendeleo toka kwenye dola/vinakuwa kama watoto yatima.
5. Tamaa ya madalaka miongoni mwa viongozi wenye we.
6. Kukosa fedha za kuendeshea siasa.

Kwa mtazamo wangu haya ni baadhi ya mambo yanayoudidimiza upinzani hapa nchini kwa kiwango ambacho hakuna namna wakashinda uchaguzi siku za karibuni.

Njia pekee iliyobakia kwetu kama watanzania ni kuangalia namna ya kuifanyia ukarabati CCM yenyewe ili ituvushe. Maana Kwa jinsi ilivyojizatiti sidhani kama inawaza kukubali tonge liiponyoke kirahisi.

Nitoe wito tuje na maoni kuitengeneza CCM ili ilifae taifa na isiwe mzigo Kwa taifa.
 
Back
Top Bottom