Nini kifanyike kushinda kesi tunazoshtakiwa katika Mahakama za Kimataifa?

Nini kifanyike kushinda kesi tunazoshtakiwa katika Mahakama za Kimataifa?

Un
Ili kukomesha tatizo hili:-
1. Tuboreshe Mifumo yetu ya Elimu, iwe mifumo inayoendana na mahitaji ya kidunia ya Sasa, mifumo iliyo Bora na imara, yaani iwe mifumo yenye kutoa Elimu Bora inayweza kushindana kimataifa tofauti na mifumo iliyopo Sasa hivi ambayo inatoa 'Bora Elimu.'
2. Kuwepo na Demokrasia na Uwazi (Transparency) kwenye Michakato yote ya awali wakati Taifa au Serikali inapotaka kuingia Mikataba na Taasisi, Makampuni, au hata na Serikali nyingine ya nje. Mikataba yote kabisa iwekwe hadharani na Wananchi washirikishwe kikamilifu katika kutoa Maoni yao (Civilians or Public Participatory Approach) izingatiwe kikamilifu.
Ikiwezekana kuwe na Kifungu au Ibara maalumu kwenye Katiba ya nchi kinachozuia usiri kwenye suala hili la Mikataba ihusuyo Serikali na Makampuni binafsi.
3. Kuwepo na Sheria Kali sana za Kulinda Rasilimali za Nchi ili zisiuzwe hovyo hovyo kiholela. Kitendo Cha kuuza au Kuingia Mikataba ya kuuza au kubinafsisha rasilimali za nchi kwa Siri au kiholela ihesabike kuwa ni kosa kubwa zaidi sawasawa na kosa la UHAINI katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kuuza au kubinafsisha kiholela rasilimali muhimu za nchi ihesabiwe Kama ni kitendo kiovu Cha Usaliti dhidi ya Nchi hii na dhidi ya Watanzania wenzako. Hii itasaidia Watu kuheshimu rasilimali muhimu za nchi zilizopo ambazo zinatumika kwa maslahi mapana ya wananchi wote.
Unaporesha mifumo ya elimu sawa,lakin hii mikataba kwanza ni Siri na pili , mikataba inasukwa kwa njia ya kifisadi. Kuna wahuni ambao hao wazungu wakilipwa na wao wanapata mgao.
 
Hatuwezi kushinda sababu tuliingia kichwa kichwa kwenye mikataba.

Wenzetu wanazingatia hadi coma, na wanajua namna ya kujivua lolote likitokea na namna ya kutukamua tukizingua
Siyo tatizo la mikataba- na hatua zetu za kutaifisha wakati hatuko tayari kulipa fidia
 
Je kuna watu ambao wako vizuri kufanya negotiating,je tuna mawakili ambao wako vizuri wakikaa meza na mawakili wa huko wanawatoa jasho ???

Ova
 
Utajiri wa nchi yetu ni mkubwa ktk rasilimali mbalimbali kama misitu,madini,Mafuta na Gesi.

Mikataba ya siri mingi tulioingia na wawekezaji mingi imekuwa na matobo ya kutuadhibu inapotokea tumevunja,kusitisha ama vinginevyo..

Inavyoonekana mapungufu ya kimkataba yamekuwa yakichukuliwa kama kinga na siraha za wawekezaji kuendelea kunyonya au kutuumiza kiuchumi..

Nchi yetu imekuwa ikilipa mabilioni ya fedha kama fidia,adhabu na n.k na kutikisa uchumi wetu dhaifu na kusababisha maumivu makubwa.

Ni wakati wa kuweka mikakati sawa ya kuhakikisha tunakuwa na nguvu kubwa ya kupambana na ukoloni mamboleo.

Napendekeza hatua zifuatazo:-

1: Hatua kali zichukuliwe kwa wote wanaohusika kuingia mikataba isiyo na maslahi kwa taifa.Na hili lisiishie kwa wanasiasa pekee bali pia watendaji na maofisa wa umma wenye dhamana..

Mapana ya hatua yahusishe hata wakiwa wastaafu.

2: Mikataba inayohusisha rasilimali za nchi iwe wazi na ijadiliwe kwa kina na kwa uwazi

3: Vyuo vyetu viwezeshwe kimkakati kuwa na kozi mtambuka ktk masuala ya kisheria..Madini,Misitu,mafuta na gesi.

4: Makampuni yanayotushitaki kwa nia ovu ya kuendelea kutufanya maskini yawe blacklisted (Yenyewe,wabia,wanahisa,na watendaji wao wakuu)..Wawe maadui wa taifa letu.
Ni upigaji tu huo mpaka Nchi ifilisike !
 
Watu WEUPE wameshajua matanzania ni majinga.

Ndo maana wanahakikisha Mikataba inasainiwa kisiri Siri.

Kwa sababu wañajuaa, kwenye huo usiri, Serikali itapeleka Wanasheria uchwaraaa walopata kazi Kwa kujipendekezaaa.


Matokeo yake ndo hayo .

Nini kifanyike?.

MIKATABA yote kabla ya kusainiwa, ijadiliwe na werevu Kwa uwazi.. kama Mkataba ni Win-win.. kwann Mabeberu waogope kujadiliwa ?.


Na kama ni Wa Siri, basi SERIKALI ISWE INAONA AIBU KUWACHUKUA WATU KAMA MWABUKUSI, LISSU, N.K WANAOIJUA SHERIA KWA AKILI NA SIO MAKARATASI.
 
Utajiri wa nchi yetu ni mkubwa ktk rasilimali mbalimbali kama misitu,madini,Mafuta na Gesi.

Mikataba ya siri mingi tulioingia na wawekezaji mingi imekuwa na matobo ya kutuadhibu inapotokea tumevunja,kusitisha ama vinginevyo..

Inavyoonekana mapungufu ya kimkataba yamekuwa yakichukuliwa kama kinga na siraha za wawekezaji kuendelea kunyonya au kutuumiza kiuchumi..

Nchi yetu imekuwa ikilipa mabilioni ya fedha kama fidia,adhabu na n.k na kutikisa uchumi wetu dhaifu na kusababisha maumivu makubwa.

Ni wakati wa kuweka mikakati sawa ya kuhakikisha tunakuwa na nguvu kubwa ya kupambana na ukoloni mamboleo.

Napendekeza hatua zifuatazo:-

1: Hatua kali zichukuliwe kwa wote wanaohusika kuingia mikataba isiyo na maslahi kwa taifa.Na hili lisiishie kwa wanasiasa pekee bali pia watendaji na maofisa wa umma wenye dhamana..

Mapana ya hatua yahusishe hata wakiwa wastaafu.

2: Mikataba inayohusisha rasilimali za nchi iwe wazi na ijadiliwe kwa kina na kwa uwazi

3: Vyuo vyetu viwezeshwe kimkakati kuwa na kozi mtambuka ktk masuala ya kisheria..Madini,Misitu,mafuta na gesi.

4: Makampuni yanayotushitaki kwa nia ovu ya kuendelea kutufanya maskini yawe blacklisted (Yenyewe,wabia,wanahisa,na watendaji wao wakuu)..Wawe maadui wa taifa letu.
Unaongelea kesi zinazokuja au zilizopita?

Kama zinazokuja, point zako zinaweza kuwa na impact, hususan kwenye uwazi na uwajibikaji.

Lakini mikataba iliyopita, mingi sana tunachoweza kufanya ni kupunguza maumivu tu, kushinda kesi kwa mkataba mbovu ambao tushasaini wenyewe ni vigumu sana.

Kuna mkataba kama wa DP World unasema hata kama nchi ikigawanywa vipande, hii Tanzania isiendelee kuwapo (mfano muungano ukivunjika) mkataba utakuwa bado valid.

Na tumekubali kipengele hicho.

Sasa mkataba kama huo unauvunja vipi bila kupigwa faini kubwa?
 
Back
Top Bottom