Nini kifanyike kwenye bongo fleva ya Sasa?

Wewe unaongelea kwa kipindi hiki mimi naongelea tangu muziki ulivyokuwa mpaka umekuja kubadilika, hilo suala kwa kiasi flani prodyuza wamechangia kuwabadilisha wasanii, ukiangalia hapo nyuma wasanii wengi walikuwa kwenye labels ambazo prodyuza anamlazimisha msanii kufanya kile anachoona yeye kinafaa at the moment, sijui umenipata vizuri...?
 
Kama ulikua una maamuzi haya au mtazamo huu,kwanini umefungua thd na kutaka maoni ya pande zote mbili? i meant wapenda mziki wa zamani na wa sasa?
Kwa sababu nimeanza kutengeneza program ya kusample sound ya zamani na ya Sasa na kuwachanganya wanamuziki wasasa na wazamani ,
Na tayari nimeshaanza kwa marioo na mr nice
 

Attachments

Sisi hatujawabadilisha wasanii bali ukweli usiopingika ni kuwa now msanii ananguvu kubwa kuliko producer sababu wanatulipa pesa nyingi na ma producer tumekuwa wengi
Kwahiyo ukikataa kumfanyia anavyotaka anaenda kwa producer mwingine kwahiyo wasanii ndiyo waaribifu wenyewe ,
Kiufupi pesa ndy inabadilisha industry
 
Ukisikiliza kwenye radio na live inakuwa vitu viwili tofauti
Exactly!
Kwasababu sikuhizi kuingia studio hakutegemei uwezo wa msanii ,
We lipa pesa njoo studio nakupa Dogo anakuandikia nyimbo na kukuelekeza namna ya kuimba ,unafanya mazoez ,unaingia booth unaimba ,nakurekebishia saut yako hata kama inamikwaruzo itaisha then nakupa ngoma yako ,siku ukiitwa uimbe live ndy utajua mwenywe😁😁
Yaan nyimbo studio unatengenezwa mfano wa wale jamaa wa photostudio wanavyo tengeneza picha mbaya kuwa nzur.
 
Aaaah 😆🤣 kweli zombie mtu mbadi yaani kumbe mimi naweza kuja studio sahv nikachagua hit song nitengenezewe na kuanza kuruka hewani duuh
 
Mziki wa mashetani zaidi ya kupromote ngono ushoga kudanga pombe bangi ufuksa una kipi cha kuboresha.
Ukiimba mistari ya uhanarakati basati na police Wana wewe
Yaan hizi ndo nyimbo za wasafi, wasipoongelea ngono bac ni pombe, bangi na umalaya.
 
Nini kinaitambulisha bongo Flava ?

Instrument zipj ? Kivipi?

Mfano mtindo wa amapiano, ukisikia midundo wake unajua tayari ni amapiano, ukisikia singeli midundo wake unajua ni singeli


Sasa bongo Flava ni nini?

Maana sielewi au ni jumuiko la nyimbo zozote za bongo au ni genire.


Hata best za nyimbo za zamani hazina midundo sawa labda kama zilifanya na stidio moja
Ila akifanya producer mwingine huwa na vionjo tofauti mno.


Angalia amapiano inafanywa na producer tofauti lakini hukosi common vyombo.

Hata singeli.


Je vingi Flava ni kitu gani sielewi?
 
Genre ya Tanzania ni singeli,michiriku ,taarabu na ngoma za kikabila,
Ila bongo flava ni mjumuiko wa ngoma zote zinazoimbwa na wasanii wa Tanzania tu.
 
Singeli iboreshwe haya mambo yakuiga wanaija na wa south matokeo yake nyimbo ikihit dunian wanajisifia wao wanaponda wasanii wa kibongo kwakucopy afu walivyowapuuzi zile video za wanawake wakibongo wakicheza singeli wanasema Africa 😂hawataji ni from Tanzania
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…