Nini kilikuwa chanzo cha mapato ya Bwana Yesu?

kwa ufupi sana eleza vyanzo. unaeleza matumizi lakini huonyeshi vyanzo vya fedha. Sipingi ila naomba kujua
Hadi sasa tumegundua.

Alikuwa na savings za shughuli zake za uselemala aliifanya zaidi ya miaka 20. Na hakuwa na Mke wala Mtoto hivyo hakuwa na majukumu makubwa.

Zawadi zake aliletewa na majusi akiwa Mtoto. Madhahabu na fedha nyingi sana.

Matajiri wenzake waliappreciate huduma yake na kumsupport.

Alikuwa ametunz Pesa nyingine matumboni mwa samaki maana hakukuwa na ATM, hiyo ndio ulikuwa ATM yake na ndoano aliyotumia Petro ni Password.

Alikuwa na uwezo wa kushusha vitu kwa imani. Japo alikuwa anafunga muda msingi lakini alhakikisha kundi kubwa watu zaidi ya 5000 bila kuhesabu wanawake na watoto wengi zaidi. Walikuwa kila Siku anawalisha hadi akawakolomea waache kumfuatafuata ili wale mikate. Waanze kuconcentrate na neno.
 
Sasa ushasikia Nabii, mnamjadili uchumi tena uku ni kukosa nidhamu kabisa.
Usiseme hiyo. Nyamaza Mkuu.
Kuna nabii mmoja aliishi nje ya principles hizi za kiungu akaishia kuwa na madeni hadi akafa.

Elisha nabii ilibidi aingilie kati kufanya miujiza mjane na Mtoto wake wapate mafuta wauze walipe madeni ya marehemu nabii wasijekuuzwa wao.


Ndio Siku hizi MTU a naona sifa eti kuwa mfuasi wa Yesu masikini. Utakufa uache watoto wanateseka.

Bora uforce hata kumtoa pepo Tajiri mmoja mkubwa 'dongota' na umuamuru alete sadaka ya kukombolewa kwake.

Yesu alikuwa na Mamlaka. Akiamua anaamuru tu watu wanamkimbizia Punda wao (Sasa Punda Leo ni kama Hammer) anatumia.

Ukiwa nabii wa kuungaunga hunamamlaka kwa hawa matajiri na maskini, huwezik kusema tu Mungu akashusha vitu maisha yakaenda, huwezi kurun mambo na idea kubwa kubwa kama Yesu alikuwa na project ya furniture center. Inakula kwako.
 
Na fedha pia umemsahau mamajusi walimpelekea Yesu fedha na dhahabu alipozaliwa umemsahau fedha

Yesu alipewa fedha na matajiri mamajusi toka nje ya nchi
Mk
Na fedha pia umemsahau mamajusi walimpelekea Yesdhahabu na dhahabu alipozaliwa umemsahau fedha

Yesu alipewa fedha na matajiri mamajusi toka nje ya nchi
Mkuu Baba yetu wa imani Elder IBRA alianza kumiliki dhahabu. Sasa sisi watoto wake wa imani tunatakiwa angalau kuwa na kamgodi au ndani unawakia kadhaa za dhahabu kutrade kwenye masoko ya ndani.

Huyu ndio Mtoto wa Ibrahim, mfuasi wa Yesu.
 
We jamaa comments zako ni hatari sana unacheka huku unapata points.
Mtumishi Tuko vzr. Angekuwa enzi za Yesu , Bwana angempa usupervisor wa wale mitume. Maana walikuwa wazito kuelewa na wepesi kusau, hadi Yesu akaambia Hawana akili, walipomboa.

Mkuu yuko vzr
 
Utajiri wa zamani ilikuwa wa kumiliki mali kama mifugo, dhahabu, mashamba nk
Na dinari Mkuu.
Kujua hata Paulo hakuwa cha Mtoto.
Aliporudi Yerusalem rais wa Yuda Festo alimuomba Rushwa. Sasa kuomba rushwa na wakuu lazima utakuwa vzr.


Aliwahi kuchoma mavitabu ya kichawi efeso yenye thamani ya dinari 50K ambayo kwa sasa nikama Milioni 750.

Wale wakristo wa awali walikuwa sio wa mchezo. Hawezi kubabaishwa na Pesa. ila wao ndio waliozibabaisha.


Mfano Filemoni alikuwa tajiri mwenye mahouseboy wengi sana na mtandao mkali wa kiintellijensia kiasi kwamba ukimuibia inabidi uhame Baraka sio nchi.

Jamaa anaitwa onesmo anamfahamu vzr huyu Bosi.
 
Kutokomea kweli na minunio juu [emoji53][emoji53][emoji53][emoji53]
 
Watu ndo walifinance huduma ya Yesu . Waliomuamini walihusika na kula kwake na mahitaji yake.

Basically alipoanza full time ministry alikua busy Sana kuzunguka miji mingi kuhubiri injili. Zaidi ya yote alikua na maisha simple Sana, hakutaka nyumba , kumiliki usafiri vitu vinavyofanya watumishi wa Leo kushindwa kubalance mambo na kujikuta wanaanza kuwalemea watu.

Pia Jesus aliishi maisha ya maombi sana. Ilikua kawaida Sana jioni kujitenga na wafuasi wake then anaingia kwenye maombi usiku kucha. Maisha ya namna hii hayana gharama Sana.

Ni vizuri kutambua Jesus was the King . Kanuni ya ufalme ni kuwa vyote vilivyoko ndani ya milki ya mfalme ni vyake. Ndo maana huwa inawapa shida na kumuona Jesus kama alikua mkorofi Sana, unawezaje kuwatuma watu wakuletee punda wake bila kumuomba afu unawaambia mwenye punda akikuuliza unampeleka wapi mjibuni Bwana ana haja nae , just that ...!

He was the king ...ndo maana watu walitoa vyote kumfanya aendelee na huduma yake just like tunavyolipa Kodi Leo ili president na Crue yake yote waishi comfortable na aendelee kutoa huduma.
 
Mkuu umesisitiza point kubwa sana.
Yesu alikuwa mfalme, ndio maana alikuwa anafukuza wawekezaji kanisani na hakuna Kesi ya madai kwenye mahakama za Jerusalem.

Hata ile Kodi aliyoifuata kwenye Samaki Petro.Yesu alianza kugoma. Akamwambia Petro, ni halali maana wa ufalme kulipa kodi?

Inabidi atoe tu ili aepushe maneno.


Vipi waliompokea. Anasema amewafanya kula Ufalme na ukuhani nao wanatawala juu ya nchi.


Je na sisi tunaweza kukwapua magari ya watu, na majumba kama Yesu Kifalme?
 
Nashukuru Mungu umeupata ufunuo halisi . Jesus is the King . Na alikuja duniani kurejesha ufalme mwanadamu aliopoteza. Ni kweli kabisaa wote waliomwamini ni Wana wa ufalme ...Prince and princess.

Kwa msingi huo waliomwamini wanapaswa kuishi maisha ya ndani ya falme . Shida ni uelewa TU that's why Bible inasema mwana mrithi ataendelea kuwa chini ya muangalizi hadi atapokua na kujitambua.

Hakuna watu ambao walipaswa kuenjoy maisha kama watu waliomuamini Jesus na kuupokea ufalme Kwa Imani. Changamoto hawazijui kanuni na funguo za ufalme, yaani how things works!!

Sio kwa kukwapua , Bali unaishi ubundant life, maisha yenye utele. Sio kwamba uwe unamiliki majumba makubwa, gari expensive and the like !!!! Bali ukihitaji huduma zote hizo unazipata ndani ya ufalme without any straggling .

Jesus was simple Yet kila alipolala jioni aliandaliwa part ( Karamu nyie huiita hivyo)
Alipohitaji usafiri alipatiwa Boti na mashua na mwanapunda.
Alivarishwa mavazi ya kifalme toka day one anazaliwa.
Ata kaburi lake, sanda aliyozikiwa, uturi uliotumika vyote ni vya kifalme.

Jesus is the king ....and that's why all is message he wanted people to understand about the Kingdom of God.
 
Mkuu umeandika siri kubwa. Na hii ndio nataka kila mfuasi wa Yesu ajue.

Tunaiita siri ya Ufalme.

Afrika wakoloni, na walokole wa sasa hawakuuleta ufalme aliouleta Yesu ili sisi tuwe watoto wa mfalme. Walileta dini. Yangu zamani wangeleta concept hizi za Kifalme kwanza tungekuwa na raha sana. Kila MTU angetamani kuwa mkristo.

Yesu alizungumzia ufalme zaidi ya kitu kingine katika hotba zake.

Umeandika siri kubwa.

Asante Mkuu.
 
Mathayo 6

24 Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.

25 Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
 
Aka. UPLOAD Sio DOWNLOAD

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
We jamaa kumbe hujui kitu, yule jamaa alipomwambia Yesu aondoke sio kwamba alimaanisha ametosheka ila ni kwamba alikuwa anajiona ni mdhambi sana kiasi kwamba hafai kabisa kuwa karibu na Yesu, angalia Luka5:8-10

Halafu msipende kuandika kimihemko...unamuita Simon Petro Lofa!? Hebu kuwa serious kidogo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…