Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Nini kilimfanya Benjamin Mkapa ashindwe kuchapa Taazia ya muasisi wa TANU Abdul Sykes katika magazeti ya chama?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KWA NINI BENJAMIN MKAPA ALISHINDWA KUCHAPA TAAZIA YA ABDUL SYKES KATIKA THE NATIONALIST BRENDON GRIMSHAW AKACHAPA "OBITUARY" YA ABDUL SYKES KATIKA SUNDAY NEWS (TANGANYIKA STANDARD)?

Mgogoro wa EAMWS nimeueleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Vyombo vilivyohusika katika mgogoro ule kuanzia gazeti la Uhuru na The Nationalist Mkapa akiwa Mhariri, Radio Tanzania Dar es Dalaam Martin Kiama akiwa Mkurugenzi, Polisi Geofrey Sawaya akihusika na Usalama wa Taifa alikuwapo Rashid Kayugwa.

Wote hawa walikuwa wakiamrishwa kutoka juu wengine wameyasema haya kwa kujuta kabla ya kufa kwao.

Hakika ni mkasa wa kusisimua.

Nataka nikupe mfano mmoja.

Kifo cha Abdul Sykes katikati ya mgogoro wa EAMWS maziko yake yalikuwa hayajapata kuonekana Dar es Salaam.

Mazishi yale yalikuwa habari kubwa kutokana na mchango wa Abdul Sykes katika TANU na uhuru wa Tanganyika achilia mbali kuwa yeye ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam na kuishinae nyumbani kwake Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Haya hakuna aliyekuwa hayajui na hii ndiyo ilikuwa sifa yake kubwa akitambulika kama mwezeshaji wa mambo yote ya TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Sasa jiulize vipi magazeti ya TANU chama alichounda Abdul yasimwandike inavyostahiki?

Mkapa kama mwandishi bila shaka alijua uzito wa stori iliyokuwa mbele yake na pengine kwa kufahamu uhusiano wa Abdul na Nyerere alimtaka Nyerere mwenyewe amwandikie rafiki yake taazia kwa mkono wake au amhoji (exclusive interview).

Yawezekana kuwa Mkapa aliyataka yote haya kwa Mwalimu na yeye akakataa?

Hapa ndipo panapoumiza kichwa.

Kuamini kuwa Mkapa kwa kutaka kwake tu aliamua kupuuza kifo cha Abdul Sykes huu ni muhali mkubwa sana.

Mwandishi mpumbavu peke yake ndiye anaeweza kuchagua uamuzi wa kijinga kama huu.

Benjamin Mkapa hakuwa mtu zuzu.

Kama ulivyohitimisha kuwa Allah ni mjuzi wa siri na dhahiri nami nasema hivyo hivyo.

Yapo mengi Mkapa aliyafanya hata alivyokuwa rais lakini kwa hali ya siasa zetu Tanzania, alijikuta mikono yake imefungwa na si kufungwa tu bali imefungwa nyuma ya mgongo wake.

Hapo chini ni taazia ya Abdul Sykes katika Sunday News la 20 October, 1968.

Lakini taazia hii ilileta mgogoro mkubwa ofisi ya TANU Lumumba.

Kuna baadhi ya viongozi ndani ya TANU walikerwa na taazia hii.

Hapo chini kuna Kumbukumbu ya Abdul Sykes kama zilivyochapwa na magazeti ya Chama na Serikali Uhuru na Daily News ya tarehe 12 Oktoba 1988.

Kumbukumbu hizi nazo zikafikwa na mkasa pia.

Wahariri walitishika na waliyoyasoma wakasema hawatachapa hadi wamepata kibali kutoka Dodoma.

Walipopewa ruhusa ya kuchapa Kumbukumbu ya Abdul Sykes yale yote muhimu katika kumuelewa Abdul Sykes yaliondolewa.
 
Mohamed Said,

Angalia picha:

Screenshot_20200731-063734.jpg
 
Mohamed Said,

Shukurani shehe wangu kwa hii ilimu. Najifunza misamiati mingi toka kwako.

Leo nimelinyaka neno "taazia" ingawa nilivyo search sikulipata badala yake nimelikuta neno "tazia" ambalo kama sikosei kwa muktadha wa bandiko lako linaonyesha kuwa na maana sawa na "taazia".

Halafu nikalinganisha na neno "tanzia" tunalotumia akina siye wa kutoka mrima.

"Tazia": means comfort, condolence or expression of grief.

ninaamini kwa definition hii, tazia = obituary.

OK.

"Tanzia": means death notice / announcement
 
Mohamed ana sifa moja kubwa miongoni mwa nyingi.
Ni mtu anayejua kuipeleka hadhra aliyoikusudia kule anakotaka.
Katika kufanisha mipango yake iwe kwa uzuri au ubaya kutegemea hoja, Mohamed hurudi jambo hata mara 1000. Mzee Said anafahamu, kurudia rudia uongo mara nyingi hugeuka kuwa ukweli.
Soma hapa chini
"Mohamed Said, post: 36184649, member: 12431"]Mazishi yale yalikuwa habari kubwa kutokana na mchango wa Abdul Sykes katika TANU na uhuru wa Tanganyika achilia mbali kuwa yeye ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam namkuishinae nyumbani kwake Mtaa wa Aggery na Sikukuu.
Kwa mtu anayesoma vitu juu juu, au asiye na ufahamu wa kina na mada au mwenye upungufu tu wa kibinadamu wa kuelewa, hoja ya Mohamed inasomeka tofauti lakini kwa mtazamo wa kusudio lake.

Msomaji ataamini kuwa Nyerere alitoka Butiama na kufikia kwa Abdul Sykes.
Na kwamba ujio wa Nyerere ilikuwa zao la juhudi za Abdul Sykes.
Hapo Mohamed atakuwa tayari amempa 'mbwa jina baya ili amuue''

Hapa ieleweke suala si uhusiano wa Nyerere na Abdul unaopingwa.
Nyerere alifika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza katika mkutano mwaka 1948 akitokea Tabora.

Baadaye Nyerere alikuja Dar kufundisha kama Mwalimu kule Pugu.

Alipoacha kazi ya Ualimu ndipo alipokwenda kuishi na Abdul

Mohamed hawezi kukueleza mahusiano ya kufahamiana japo kwa juu juu kati ya Nyerere na Abdul

Atakachokueleza ni Nyerere kuishi kwa Abdul na atarudia mara 1000 na inageuka kuwa ''ukweli ''

Tumemueleza Mohamed, haiwezekani Chama kikawa na makao makuu Dar es Salaam chini ya Abdul Kleist Syke Mbuwane, na mwenyekiti huyo asitambue uwepo wa tawi kubwa sana la Tabora likiongozwa na katibu Nyerere.

Haiwezekani kwamba Nyerere alizuka mwaka 1948 kuja katika mkutano ambao watu hawamjui na wala hawakutaka kumjua baada ya hapo.

Ikiwa ni hivyo huyu Abdul atakuwa kiongozi Mpumbavu sana.
Abdul hakuwa mpumbavu! wa kutambua wasomi wachache sana enzi hizo Nyerere akiwa miongoni!

Na ikiwa ilitokea haitakuwa ajabu, Abdul alikuwa Askari na aliwahi kuwafurumusha kwa makonde baba zake katika mapinduzi ya chama, seuse kumtambua Nyerere!

Sina tatizo na mtazamo wa Mohamed wala historia yake.

Nina tatizo na jinsi anavyotumia kalamu yake kuudurusu uongo mara 100 hata kuufanya uwe ukweli kwa sababu rahisi tu '' ukitaka kumuu mbwa mpe jina baya'' na hapa Nyerere hakwepi jina.

Masalaam, narudi viungani kuokota kumbaa !

JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
 
Mohamed ana sifa moja kubwa miongoni mwa nyingi.
Ni mtu anayejua kuipeleka hadhra aliyoikusudia kule anakotaka.
Katika kufanisha mipango yake iwe kwa uzuri au ubaya kutegemea hoja, Mohamed hurudi jambo hata mara 1000. Mzee Said anafahamu, kurudia rudia uongo mara nyingi hugeuka kuwa ukweli.
Soma hapa chini
Kwa mtu anayesoma vitu juu juu, au asiye na ufahamu wa kina na mada au mwenye upungufu tu wa kibinadamu wa kuelewa, hoja ya Mohamed inasomeka tofauti lakini kwa mtazamo wa kusudio lake.

Msomaji ataamini kuwa Nyerere alitoka Butiama na kufikia kwa Abdul Sykes.
Na kwamba ujio wa Nyerere ilikuwa zao la juhudi za Abdul Sykes.
Hapo Mohamed atakuwa tayari amempa 'mbwa jina baya ili amuue''

Hapa ieleweke suala si uhusiano wa Nyerere na Abdul unaopingwa.
Nyerere alifika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza katika mkutano mwaka 1948 akitokea Tabora.

Baadaye Nyerere alikuja Dar kufundisha kama Mwalimu kule Pugu.

Alipoacha kazi ya Ualimu ndipo alipokwenda kuishi na Abdul

Mohamed hawezi kukueleza mahusiano ya kufahamiana japo kwa juu juu kati ya Nyerere na Abdul

Atakachokueleza ni Nyerere kuishi kwa Abdul na atarudia mara 1000 na inageuka kuwa ''ukweli ''

Tumemueleza Mohamed, haiwezekani Chama kikawa na makao makuu Dar es Salaam chini ya Abdul Kleist Syke Mbuwane, na mwenyekiti huyo asitambue uwepo wa tawi kubwa sana la Tabora likiongozwa na katibu Nyerere.

Haiwezekani kwamba Nyerere alizuka mwaka 1948 kuja katika mkutano ambao watu hawamjui na wala hawakutaka kumjua baada ya hapo.

Ikiwa ni hivyo huyu Abdul atakuwa kiongozi Mpumbavu sana.
Abdul hakuwa mpumbavu! wa kutambua wasomi wachache sana enzi hizo Nyerere akiwa miongoni!

Na ikiwa ilitokea haitakuwa ajabu, Abdul alikuwa Askari na aliwahi kuwafurumusha kwa makonde baba zake katika mapinduzi ya chama, seuse kumtambua Nyerere!

Sina tatizo na mtazamo wa Mohamed wala historia yake.

Nina tatizo na jinsi anavyotumia kalamu yake kuudurusu uongo mara 100 hata kuufanya uwe ukweli kwa sababu rahisi tu '' ukitaka kumuu mbwa mpe jina baya'' na hapa Nyerere hakwepi jina.

Masalaam, narudi viungani kuokota kumbaa !

JokaKuu Pascal Mayalla Mag3
Mkuu Nguruvi3, asante kuni tag

P
 
Abdul Sykes yeye ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam namkuishinae nyumbani kwake Mtaa wa Aggery na Sikukuu.
Kati ya dhambi kubwa hapa duniani, ni dhambi ya kumsingizia marehemu, haisameheki!.

Huu urongo wa Abdul kumpokea Nyerere Dar es Salaam, ni urongo Mtakatifu wa mchana kweupe unaorudiwa na Mkuu Maalim Mohammed Said mara 100 ili uonekane ni ukweli!.

  1. Mwalimu Nyerere baada ya kumaliza Tabora School, amesoma St. Francis, Pugu, ni Dar es Salaam!, angalia ni mwaka gani, sio kuja kuongopa humu kuwa kuna Sykes ndio wamempokea Mwalimu Nyerere jijini DSM!.
  2. Baada ya Pugu, Mwalimu amekwenda Makekere, nchini Uganda na ameondokea Dar es Salaam na kurejea Dar es Salaam!, angalia ni mwaka gani?.
  3. Mwalimu Nyerere baada ya Makerere, amekwea pipa kwenda kusoma chuo kikuu cha Edinburgh nchini Uingereza!, hiyo ndege hakupandia Butiama!, alipandia Dar es Salaam!.
  4. Mwalimu amerudi Kufundisha Pugu, aliingilia Dar es Salaam na kuondokea Dar es Salaam.
  5. Mwalimu ndio alikuwa Katibu wa TANU wa Tabora, alikuja Dar kuhudhuria Mkutano Mkuu wa TAA mwaka 1948 wala hakupokelewa na Sykes!.
Kitu ambacho ni kweli, baada ya Mwalimu kuacha ualimu na kukitumikia chama full time, ni kweli yeye na Mama Maria, waliishi nyumbani kwa Sykes na ni kweli waliwahifadhi na kuwasaidia kwa kipindi kifupi kabla ya kuhamia Magomeni.

Mwaka 1996, nilisimuliwa na mjane wa Sykes, Mama Daisy aliyekuwa akiishi pale Opposite California Dreamer, na nilipelekwa na mjukuu wake, Mwamvua Mlangwa.

Kitu ambacho namkubali sana Maalim Mohammed Said ni uwezo wake wa uandishi, na umahiri wa kusimulia, he is gifted, ana kipaji, na kufuatia kipaji hicho, ni mtu wa kuaminiwa, hivyo ana agenda fulani hivyo kutunga uongo na kuu craft vizuri kabisa na kuonekana kama ukweli ili tuu kuitimiza hiyo agenda!.

Niliwahi kutoa angalizo humu kumhusu mtu huyu!.
Kwa Simulizi za Mwana JF, Maalim Mohammed Said, Sio Mtu wa Kubezwa, Mengine ni Ukweli Mchungu!, Ila Pia Sio Mtu wa Kupuuzwa!.

Sasa ni jana tuu tumetoka kumpumzisha Mkapa, hata siku 3 kaburini bado, leo anakuja kumzushia haya, tena kwa kutumia lugha ya kifedhuli kama hii
Yawezekana kuwa Mkapa aliyataka yote haya kwa Mwalimu na yeye akakataa?

Hapa ndipo panapoumiza kichwa.

Kuamini kuwa Mkapa kwa kutaka kwake tu aliamua kupuuza kifo cha Abdul Sykes huu ni muhali mkubwa sana.

Mwandishi mpumbavu peke yake.ndiye anaeweza kuchagua uamuzi wa kijinga kama huu.

Benjamin Mkapa hakuwa mtu zuzu.

Wewe Mkuu Maalim Mohammed Said ni mtu wa kutumia maneno haya kumzungumzia Mkapa?!, "Mwandishi mpumbavu peke yake ndiye anaeweza kuchagua uamuzi wa kijinga kama huu.

Benjamin Mkapa hakuwa mtu zuzu".

I think this is too much!.

Thanks God, Mkuu Maalim Mohammed Said ni mtu mwerevu anayejua vyema kusoma nyakati, anamjua vizuri JPM, naamini anazijua vyema sababu zilizopelekea "wale jamaa" waendelee kuhifadhiwa kule 'mahali salama', hivyo tangu baada ya kumtolea angalizo lile, sasa yuko makini kwa kupunguza kuipush ile agenda yake ambayo ndio the motive behind most of his writings, na by the time 'jamaa' anamaliza, "if at all atamaliza", the time left will be too little too late to keep pushing his agenda forward!.

Paskali
 
Kati ya dhambi kubwa hapa duniani, ni dhambi ya kumsingizia marehemu, haisameheki!.
P
Kaka yngu acheni unafiki kwenye ili Hali ya kuwa Ukweli unajurikana Mzee ameleta hoja jibu HOJA sio kuleta Maneno ya kwenye Kanga...narudia tna Nongwa tuachieni wenyewe Wazaramo. ukabila udini kutekena ndio kazini yenu.

Sent from my ANE-LX1 using JamiiForums mobile app
 
Mohamed Said,

Shukurani shehe wangu kwa hii ilimu. Najifunza misamiati mingi toka kwako.

Leo nimelinyaka neno "taazia" ingawa nilivyo search sikulipata badala yake nimelikuta neno "tazia" ambalo kama sikosei linaonyesha kuwa na maana sawa na "taazia".

Halafu nikalinganisha na neno "tanzia" tunalotumia akina siye wa kutoka mrima.

"Tazia": means comfort, condolence or expression of grief.

ninaamini kwa definition hii, tazia = obituary.

OK.

"Tanzia": means death notice / announcement
M...
Zamani nikiandika tanzia. Abdilatif Abdallah mtaalamu wa Kiswahili akaniambia hicho ni Kiswahili cha bara.

Sisi watu wa pwani tunasema "taazia," kwa kuwa neno lenyewe asili yake ni Kiarabu.
 
KWA NINI BENJAMIN MKAPA ALISHINDWA KUCHAPA TAAZIA YA ABDUL SYKES KATIKA THE NATIONALIST BRENDON GRIMSHAW AKACHAPA "OBITUARY" YA ABDUL SYKES KATIKA SUNDAY NEWS (TANGANYIKA STANDARD)?

Walipopewa ruhusa ya kuchapa Kumbukumbu ya Abdul Sykes yale yote muhimu katika kumuelewa Abdul Sykes yaliondolewa.

Mohamed ana sifa moja kubwa miongoni mwa nyingi.
Ni mtu anayejua kuipeleka hadhra aliyoikusudia kule anakotaka.
Katika kufanisha mipango yake iwe kwa uzuri au ubaya kutegemea hoja, Mohamed hurudi jambo hata mara 1000. Mzee Said anafahamu, kurudia rudia uongo mara nyingi hugeuka kuwa ukweli.

Sina tatizo na mtazamo wa Mohamed wala historia yake.

Nina tatizo na jinsi anavyotumia kalamu yake kuudurusu uongo mara 100 hata kuufanya uwe ukweli kwa sababu rahisi tu '' ukitaka kumuu mbwa mpe jina baya'' na hapa Nyerere hakwepi jina.

Masalaam, narudi viungani kuokota kumbaa !
This is getting better and better,
Soon we will find out who's telling the truth!
 
Mkuu Nguruvi3, asante kuni tag

P
Paschal,
Hayo uliyoleta hapa si maudhui niliyoandika.

Rejea kichwa cha habari la huamini haya niliyoandika kwangu si tatizo kwani kuna maelfu leo wameujua ukweli kupitia kalamu yangu.

Ikiwa unataka tujadili TAA Tabora nifahamishe nikukutanishe na Sheikh Abdallah na Maulidi Kivuruga, Chamng'anda Usingizi walioasisi TAA Gongoni huko mwaka 1945.

Nikukutanishe na babu yangu Salum Abdallah Popo na Bilali Rehani Waikela kwa kuwataja wachache na kwa akina mama nikufamishe kwa shangazi yangu Bi. Zarula bint Abdulrahmani.

Ipo Thesis (2019)nimetajwa mie pamoja na babu yangu Salum Abdallah katika ukurasa mmoja ukipenda nitakuwekea hapa.
 
Paschal,
Hayo uliyoleta hapa si maudhui niliyoandika.

Rejea kichwa cha habari la huamini haya niliyoandika kwangu si tatizo kwani kuna maelfu leo wameujua ukweli kupitia kalamu yangu.

Ikiwa unataka tujadili TAA Tabora nifahamishe nikukutanishe na Sheikh Abdallah na Maulidi Kivuruga, Chamng'anda Usingizi walioasisi TAA Gongoni huko mwaka 1945.

Nikukutanishe na babu yangu Salum Abdallah Popo na Bilali Rehani Waikela kwa kuwataja wachache na kwa akina mama nikufamishe kwa shangazi yangu Bi. Zarula bint Abdulrahmani.

Ipo Thesis (2019)nimetajwa mie pamoja na babu yangu katika ukurasa mmoja ukipenda nitakuwekea hapa.
Paschal,
Hao hapo Abdallah na Maulidi Kivuruga waasisi wa TAA Tabora 1945.

Hayo ya Nyerere ya 1948 hawa ndiyo waliomkaribisha kwenye chama yeye na Hamza Mwapachu.
Screenshot_20200731-090943.jpg
 
Kati ya dhambi kubwa hapa duniani, ni dhambi ya kumsingizia marehemu, haisameheki!.

Huu urongo wa Abdul kumpokea Nyerere Dar es Salaam, ni urongo Mtakatifu wa mchana kweupe unaorudiwa na Mkuu Maalim Mohammed Said mara 100 ili uonekane ni ukweli!.

  1. Mwalimu Nyerere baada ya kumaliza Tabora School, amesoma St. Francis, Pugu, ni Dar es Salaam!, angalia ni mwaka gani, sio kuja kuongopa humu kuwa kuna Sykes ndio wamempokea Mwalimu Nyerere jijini DSM!.
  2. Baada ya Pugu, Mwalimu amekwenda Makekere, nchini Uganda na ameondokea Dar es Salaam na kurejea Dar es Salaam!, angalia ni mwaka gani?.
  3. Mwalimu Nyerere baada ya Makerere, amekwea pipa kwenda kusoma chuo kikuu cha Edinburgh nchini Uingereza!, hiyo ndege hakupandia Butiama!, alipandia Dar es Salaam!.
  4. Mwalimu amerudi Kufundisha Pugu, aliingilia Dar es Salaam na kuondokea Dar es Salaam.
  5. Mwalimu ndio alikuwa Katibu wa TANU wa Tabora, alikuja Dar kuhudhuria Mkutano Mkuu wa TAA mwaka 1948 wala hakupokelewa na Sykes!.
Kitu ambacho ni kweli, baada ya Mwalimu kuacha ualimu na kukitumikia chama full time, ni kweli yeye na Mama Maria, waliishi nyumbani kwa Sykes na ni kweli waliwahifadhi na kuwasaidia kwa kipindi kifupi kabla ya kuhamia Magomeni.

Mwaka 1996, nilisimuliwa na mjane wa Sykes, Mama Daisy aliyekuwa akiishi pale Opposite California Dreamer, na nilipelekwa na mjukuu wake, Mwamvua Mlangwa.

Kitu ambacho namkubali sana Maalim Mohammed Said ni uwezo wake wa uandishi, na umahiri wa kusimulia, he is gifted, ana kipaji, na kufuatia kipaji hicho, ni mtu wa kuaminiwa, hivyo ana agenda fulani hivyo kutunga uongo na kuu craft vizuri kabisa na kuonekana kama ukweli ili tuu kuitimiza hiyo agenda!.

Niliwahi kutoa angalizo humu kumhusu mtu huyu!.
Kwa Simulizi za Mwana JF, Maalim Mohammed Said, Sio Mtu wa Kubezwa, Mengine ni Ukweli Mchungu!, Ila Pia Sio Mtu wa Kupuuzwa!.

Sasa ni jana tuu tumetoka kumpumzisha Mkapa, hata siku 3 kaburini bado, leo anakuja kumzushia haya, tena kwa kutumia lugha ya kifedhuli kama hii

"Mwandishi mpumbavu peke yake.ndiye anaeweza kuchagua uamuzi wa kijinga kama huu.

Benjamin Mkapa hakuwa mtu zuzu".

I think this is too much!.

Thanks God, Mkuu Maalim Mohammed Said ni mtu mwerevu anayejua vyema kusoma nyakati, anamjua vizuri JPM, naamini anazijua vyema sababu zilizopelekea "wale jamaa" waendelee kuhifadhiwa kule 'mahali salama', hivyo tangu baada ya kumtolea angalizo lile, sasa yuko makini kwa kupunguza kuipush ile agenda yake ambayo ndio the motive behind most of his writings, na by the time 'jamaa' anamaliza, "if at all atamaliza", the time left will be too little too late to keep pushing his agenda forward!.

Paskali
Bwana Paschal,
Hivyo vitisho vya nini ndugu yangu?

Hiyo fitna unayotengeneza kuwa nimetukana itakusaidia nini?

Rejea soma upya.

Mimi siwezi kukosa adabu nikawa na upumbavu wa kuandika matusi.

Una moyo wa kustahamili kalamu yangu na tujadiliane kwa adabu la huwezi nikwepe lakini usinitishe wala usinijengee fitna.
 
Kata...
Niamini ndugu yangu mimi hawa ninaowaandika ni baba na babu zangu hii elimu si kama nimekwenda mahali kujifunza la hasha nimeishi ndani ya historia hii.
Mzee wangu Mohamed,
Nyakati zimebadilika sana, naamini daima UKWELI hauwezi kujificha.
Hivyo siyo muda tutafahamu kati yako na Nguruvi3 nani anasema ukweli.
 
KWA NINI BENJAMIN MKAPA ALISHINDWA KUCHAPA TAAZIA YA ABDUL SYKES KATIKA THE NATIONALIST BRENDON GRIMSHAW AKACHAPA "OBITUARY" YA ABDUL SYKES KATIKA SUNDAY NEWS (TANGANYIKA STANDARD)?

Mgogoro wa EAMWS nimeueleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Vyombo vilivyohusika katika mgogoro ule kuanzia gazeti la Uhuru na The Nationalist Mkapa akiwa Mhariri, Radio Tanzania Dar es Dalaam Martin Kiama akiwa Mkurugenzi, Polisi Geofrey Sawaya akihusika na Usalama wa Taifa alikuwapo Rashid Kayugwa.

Wote hawa walikuwa wakiamrishwa kutoka juu wengine wameyasema haya kwa kujuta kabla ya kufa kwao.

Hakika ni mkasa wa kusisimua.

Nataka nikupe mfano mmoja.

Kifo cha Abdul Sykes katikati ya mgogoro wa EAMWS maziko yake yalikuwa hayajapata kuonekana Dar es Salaam.

Mazishi yale yalikuwa habari kubwa kutokana na mchango wa Abdul Sykes katika TANU na uhuru wa Tanganyika achilia mbali kuwa yeye ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Salaam namkuishinae nyumbani kwake Mtaa wa Aggery na Sikukuu.

Haya hakuna aliyekuwa hayajui haya na hii ndiyo ilikuwa sifa yake kubwa akitambulika kama mwezeshaji wa mambo yote ya TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.

Sasa jiulize vipi magazeti ya TANU chama alichounda Abdul yasimwandike inavyostahiki?

Mkapa kama mwandishi bila shaka alijua uzito wa stori iliyokuwa mbele yake na pengine kwa kufahamu uhusiano wa Abdul na Nyerere alimtaka Nyerere mwenyewe amwandikie rafiki yake taazia kwa mkono wake au amhoji (exclusive interview).

Yawezekana kuwa Mkapa aliyataka yote haya kwa Mwalimu na yeye akakataa?

Hapa ndipo panapoumiza kichwa.

Kuamini kuwa Mkapa kwa kutaka kwake tu aliamua kupuuza kifo cha Abdul Sykes huu ni muhali mkubwa sana.

Mwandishi mpumbavu peke yake.ndiye anaeweza kuchagua uamuzi wa kijinga kama huu.

Benjamin Mkapa hakuwa mtu zuzu.

Kama ulivyohitimisha kuwa Allah ni mjuzi wa siri na dhahiri nami nasema hivyo hivyo.

Yapo mengi Mkapa aliyafanya hata alivyokuwa rais lakini kwa hali ya siasa zetu Tanzania, alijikuta mikono yake imefungwa na si kufungwa tu bali imefungwa nyuma ya mgongo wake.

Hapo chini ni taazia ya Abdul Sykes katika Sunday News la 20 October, 1968.

Lakini taazia hii ilileta mgogoro mkubwa ofisi ya TANU New Street.

Kuna baadhi ya viongozi ndani ya TANU walikerwa na taazia hii.

Hapo chini kuna Kumbukumbu ya Abdul Sykes kama zilivyochapwa na magazeti ya Chama na Serikali Uhuru na Daily News ya tarehe 12 Oktoba 1988.

Kumbukumbu hizi nazo zikafikwa na mkasa pia.
Wahariri walitishika na waliyoyasoma wakasema hawatachapa hadi wamepata kibali kutoka Dodoma.

Walipopewa ruhusa ya kuchapa Kumbukumbu ya Abdul Sykes yale yote muhimu katika kumuelewa Abdul Sykes yaliondolewa.


Shk, Mohamed Said, your post is too late to be dealt with, as the concerned person is no more. You would have written it before his demise to see what he had to answer.

Ungeiandika pindi Mzee Mkapa akiwa hai ili tumsikie ingekuwa na faida kubwa lakini wasubiri afe ndipo waandika hiyo inakuwa ni hadithi tu isiyokuwa na uzito, a fruitless story.
 
Mohamed ana sifa moja kubwa miongoni mwa nyingi.
Ni mtu anayejua kuipeleka hadhra aliyoikusudia kule anakotaka.
Katika kufanisha mipango yake iwe kwa uzuri au ubaya kutegemea hoja, Mohamed hurudi jambo hata mara 1000. Mzee Said anafahamu, kurudia rudia uongo mara nyingi hugeuka kuwa ukweli.
Soma hapa chini
Kwa mtu anayesoma vitu juu juu, au asiye na ufahamu wa kina na mada au mwenye upungufu tu wa kibinadamu wa kuelewa, hoja ya Mohamed inasomeka tofauti lakini kwa mtazamo wa kusudio lake.

Msomaji ataamini kuwa Nyerere alitoka Butiama na kufikia kwa Abdul Sykes.
Na kwamba ujio wa Nyerere ilikuwa zao la juhudi za Abdul Sykes.
Hapo Mohamed atakuwa tayari amempa 'mbwa jina baya ili amuue''

Hapa ieleweke suala si uhusiano wa Nyerere na Abdul unaopingwa.
Nyerere alifika Dar es Salaam kwa mara ya kwanza katika mkutano mwaka 1948 akitokea Tabora.

Baadaye Nyerere alikuja Dar kufundisha kama Mwalimu kule Pugu.

Alipoacha kazi ya Ualimu ndipo alipokwenda kuishi na Abdul

Mohamed hawezi kukueleza mahusiano ya kufahamiana japo kwa juu juu kati ya Nyerere na Abdul

Atakachokueleza ni Nyerere kuishi kwa Abdul na atarudia mara 1000 na inageuka kuwa ''ukweli ''

Tumemueleza Mohamed, haiwezekani Chama kikawa na makao makuu Dar es Salaam chini ya Abdul Kleist Syke Mbuwane, na mwenyekiti huyo asitambue uwepo wa tawi kubwa sana la Tabora likiongozwa na katibu Nyerere.

Haiwezekani kwamba Nyerere alizuka mwaka 1948 kuja katika mkutano ambao watu hawamjui na wala hawakutaka kumjua baada ya hapo.

Ikiwa ni hivyo huyu Abdul atakuwa kiongozi Mpumbavu sana.
Abdul hakuwa mpumbavu! wa kutambua wasomi wachache sana enzi hizo Nyerere akiwa miongoni!

Na ikiwa ilitokea haitakuwa ajabu, Abdul alikuwa Askari na aliwahi kuwafurumusha kwa makonde baba zake katika mapinduzi ya chama, seuse kumtambua Nyerere!

Sina tatizo na mtazamo wa Mohamed wala historia yake.

Nina tatizo na jinsi anavyotumia kalamu yake kuudurusu uongo mara 100 hata kuufanya uwe ukweli kwa sababu rahisi tu '' ukitaka kumuu mbwa mpe jina baya'' na hapa Nyerere hakwepi jina.

Masalaam, narudi viungani kuokota kumbaa !

JokaKuu Pascal Mayalla Mag3

Huyu bwana sijui anataka nini? Taifa la kiislamu? Au viongozi waislamu tu?
 
Shk, Mohamed Said, your post is too late to be dealt with, as the concerned person is no more. You would have written it before his demise to see what he had to answer.

Ungeiandika pindi Mzee Mkapa akiwa hai ili tumsikie ingekuwa na faida kubwa lakini wasubiri afe ndipo waandika hiyo inakuwa ni hadithi tu isiyokuwa na uzito, a fruitless story.
Mokaze,
Hii ni taazia na taazia haiandikwi mtu akiwa hai.

Haya niliyoandika hapa wewe unayasoma leo.
Haya yote yamo katika kitabu cha Abdul Sykes toka mwaka wa 1998.
 
Mokaze,
Hii ni taazia na taazia haiandikwi mtu akiwa hai.

Haya niliyoandika hapa wewe unayasoma leo.
Haya yote yamo katika kitabu cha Abdul Sykes toka mwaka wa 1998.


Uncle Mohamed said, Hii sio taazia (tanzia) hata kidogo, kwani umeandika shortcomng ya Marehemu, katika taazia watu hatuandiki shortcomings za Marehemu, ndiyo maana nimesema ungeandika jambo hili humu ndani ya jf wakati huyo marehemu akiwa hai ili kama angeweza naye atoe majibu.

Kumbuka hili jambo limekaa kishutuma na Hadithi ya mtume (saw) inakataza kabisa kusema hadharani yale yanayodhaniwa ni mambo mabaya aliyofanya marehemu kipindi akiwa hai, the reason being he is not able to come back and defend himself on any charges against him.

Humu ndani jf, kuna watu zaidi ya 500,000, sijui wangapi wameshasoma hicho kitabu; "Abdul sykes"
 
Uncle Mohamed said, Hii sio taazia (tanzia) hata kidogo, kwani umeandika shortcomng ya Marehemu, katika taazia watu hatuandiki shortcomings za Marehemu, ndiyo maana nimesema ungeandika jambo hili humu ndani ya jf wakati huyo marehemu akiwa hai ili kama angeweza naye atoe majibu.

Kumbuka hili jambo limekaa kishutuma na Hadithi ya mtume (saw) inakataza kabisa kusema hadharani yale yanayodhaniwa ni mambo mabaya aliyofanya marehemu kipindi akiwa hai, the reason being he is not able to come back and defend himself on any charges against him.

Humu ndani jf, kuna watu zaidi ya 500,000, sijui wangapi wameshasoma hicho kitabu; "Abdul sykes"
Mokaze,
Zamani nikiandika tanzia.

Abdilatif Abdallah mtaalamu wa Kiswahili akaniambia hicho ni Kiswahili cha bara.

Sisi watu wa pwani tunasema "taazia," kwa kuwa neno lenyewe asili yake ni Kiarabu.

Rejea tena katika uzi uusome kwa makini utapata ujumbe ninaowasilisha.

Huko unakokwenda kwenye hadith hapa si pake kwani hajasemwa mtu mabaya yake.

Nakufamisha kuwa taazia inaweza pia ikaeleza ubaya wa marehemu.

Ukipenda naweza nikakuwekea taazia ya Thabit Kombo (Mlamali) na ya Martin Kayamba (Fiah).

Haya yote unayosoma hapa yamo katika kitabu cha Abdul Sykes toka 1998.
 
Back
Top Bottom