Kwa tunaomjua Mohamed hii ndiyo janja yake, kukwepa mada na kutumbukiza mambo yasiyhusiana.
Hoja hapa ni je, Abdul Sykes ndiye aliyempokea Nyerere Dar es Saalam
Rejea bandiko # 4 na #6 mimi na
Pascal Mayalla tukieleza Nyerere alivyokuja na kukanusha habari ya Mohamed. Kilichopaswa kufanywa na Mohamed ni kueleza upande wake akitetea hoja ambayo ameileta mwenyewe '' achilia mbali kwamba Abdul Sykes ndiye alimpokea Nyerere na kuishi naye....''
Tazama Mohamed anavyofanya wasomaji mazuzu na watu wapumbavu. Hebu rejea bandiko lake kama hakusema hayo maneno.
Mohamed anajua wajanja watasema sema , wasioelewa watamwelewa hasa anapo durusu uongo mara 1000.
Kwa msiojua, tangu 2010 tunamueleza huu uongo ambao anajua ni uongo lakini pia anajua kupitia uongo huo na kuurudia anapata kundi na kulielekeza anapotaka kifikra, si mjinga anajua anachofanya.Mohamed hatusomi vichwa vya habari, tunasoma maudhui na katika maudhui hatuchagui wewe unataka tusome nini.
Hapa unataka watu waache hoja ya Nyerere kupokelewa na Abdul kwavile unajua haikuwa hivyo, unatengeneza tu uongo na unaurudia sana kiasi cha kukaribia kuwa ukweli.
Hapana hatuhitaji majina ya watu.
Hoja iliyopo ni kuwa, je, Abdul Sykes alimpokea Nyerere Dar es Salaam.
Hoja zangu na Pasco ndizo mjadala uliopo.Usitake kuondoa watu kwenye mada, uongo!Nani kaukuuliza haya? Unataka watu waondoke katika hoja ya uongo! Nyerere hakupokelewa na Abdul ingawa unadai hivyo na huwezi kutihibitisha. Hoja si wazee ni Nyerere na Abdul hasa ujio wa Nyerere Dar Haya yanatoka wapi? Nani kaukuuliza haya?
Hoja ni moja tu, je, Abdul alimpokea Nyerere Dar es Salaam? Je, hoja za nguruvi na Pasco zina mapungufu yapi? Je, una ushahidi gani kwamba Abdul ndiye aliyempokea Nyerere?
Wanajamvi mnaweza kuona jinsi Mohamed anavyoweza kutunga uongo, kuuhadithia kwa nakshi na manemane akiupulizia ubani. Ni mtu anayeweza kupuliza udi uozo ukanukia jasmini.
Muulizeni kama Nyerere alipokelewa Dar na Abdul Sykes, kama hatawajibu huo ni sehemu ya uongo mwingi ambao kwa kutumia kipaji chake cha kueleza na kusimulia anaporudia mara saba sabin hugeuka kuwa ukweli.