Nini kimetokea mpaka kufa kwa uzalishaji wa Ngano hecta 350,000 kule Bassotu Manyara?

Nimekusoma,nakumbuka enzi zile unakuta mjinga mmoja anawapiga biti wawekezaji Ili kutafuta kiki.Mtu kama sabaya,hapi wanampiga biti wawekezaji mbele ya macamera Ili kumfurahisha jiwe eti kodi ilipwe ndani ya siku saba, wawekezaji wakijitetea ndo wameanza uwekezaji wapewe mda watalipa. Wanasiasa pia ni changamoto kwenye uwekazaji maana sera zetu hazitabiriki. Kuwekeza afrika ni risk Sana angalau wahindi ndio wanamudu nao walijifunza Waliyofanyiwa na Nyerere ( utaifishaji) na Iddi Amin ( kufukuzwa) hivyo hawawekezi nchi moja kama ni ndugu wanasambaa nchi hata zaidi ya nne mfano Ghana, senegal, zambia, TANZANIA na awajengi wanakodi wakiona dalili za upepo wa siasa umeyumba nchi fulani wanawahi fasta kukimbiza Mitaji yao nchi zingine walipo ndugu zao ukitulia wanarudi.
 
Viwanda vilivyokufa baada ya Tanganyika kupata uhuru

1. Kiwanda cha matairi general tyre cha Arusha
2. Kiwanda cha viberiti Moshi/kilimanjaro
3. Kiwanda cha tambi za majiko na vibatari dar es salaam
4. Viwanda vya pamba mwanza,singida na shinyanga

Na vingine vingi sana

Katika haya wafuatao ni wakulaumiwa vikali

1. Mwinyi
2. Mkapa
3. Msoga
 
Waafrika tuliwahi sana kujitawala, bora ukoloni ungeendelea mpaka miaka ya 2000 pengine tungekua mbali
Hatuna dhana ya uwongozi ndani mwetu hili ndiyo tatizo la msingi. Kiongozi anatakiwa afahamu kila kitu juu ya anacho kiongoza, iwe ni chama, kiwanda, taasisi nk.

Kiongozi anapaswa ajue uongozi wote wa siku unavyofanyika na uwezo wa kila mtendaji. Asilale mpaka pitied ripoti zote na azifanyie tathmini.

Wazungu huwa wanaandaa viongozi kwa muda mrefu. General manager ana nature vijana watakao mrithi kwa muda mrefu.

Mfano wa jambo hili ni Mbowe na Chadema, Mbowe anaijua Chadema tangu akiwa Bavicha. Anajua Idara zote muhimu na watendaji wake. Ndiyo maana si rahisi Chadema kuyumba.
 
Kwa upande wa wazungu nakubaliana na wewe 100% , wazungu bwana unakuta kijana wa miaka 36 ni general manager, experience yake ni 15 years kwenye same field sio kwa kusoma tuu hata kufanya kazi, maajabu yetu weusi majukumu yanakuja kwa connection bila kujali education background, work experience, uadilifu, uaminifu

Angalia taasisi nyingi walipoondoka wazungu, wabongo wakakaimu hata kwa miezi 6 mambo yalikua hovyo zaidi ya hovyo

Kwa swala la bwana mbowe hapo ni 50/50
 
Ukweli ni kwamba wafanya biashara walikifisidi ili waweze kuagiza ngano nje ya nchi na kisha wajipangie bei wa mlaji na mwisho wapige pesa maradufu.
Viberiti - kenya, india
Matairi - kenya, Germany
Nguo - ulaya, Asia

Cha kushangaza kila kitu tajwa hapo juu kilikua kinatengenezwa hapa hapa nchini
 
Historia ya hii ilianzia babu zetu walipoanza kuchukuliwa utumwani. Watu waliokua na ujuzi wa kufua vyuma, kujenga, na waliokua na nguvu za kulima na kufuga waliuzwa utumwani. Uzalishaji ulishuka na hakukuwa na watu wa kurithisha vizazi vinge ujuzi.

Dysfunctional society ilianzia hapa, babu zetu walianza kuuzana utumwani wenyewe kwa wenyewe ili wapate angalau chakula.

Hata walipokuja kutwaa makoloni tayari tulikua na dysfunctional society. Ilikuwa rahisi kwao kututawala. Kipindi chote cha Ukoloni tulikuwa ni watu wa kupokea amri. Hatujawahi kujifunza uwongozi.
 
Chakula..? Hapana labda kwa jamii chache ambazo zilikuwa masikini, lakini kwa wale waliofanikiwa kugundua chuma mapema hawakuwa masikini maana production yao ya chakula ilikua juu, sema walitaka vizawadi vya kishenzi kutoka huko ulaya in exchange of manpower, raw materials na vito.
 
Cha ajabu zaidi hiyo report ya CAG haifanyiwi kazi yoyote ile.

Nimeamini rasmi wakoloni weusi ni hatari sana kuliko hao mabeberu.

Trump alikuwa sahihi kabisa kuwa "inabidi wakoloni weupe(mabeberu) warudi upya kututawala maana tangu tumepata uhuru tumeshindwa kujitawala"
 
Unajua biashara ya utumwa iliendelea kwa miongo mingi, watu waliingiwa na woga hata wa kufanya shughuli za uzalishaji kwa hofu ya kukamatwa utumwani. Matokeo yake jamii zilianza kuwa na uhaba wa chakula.
 
Hoja nzuri sana.
 
Inasikitisha sana, hadi inafikia hatua unajiuliza kwanini ni Afrika tu [emoji848][emoji30]
 
Gharama ya kulima Tanzania ni kubwa kuliko kununua mazao nje,ukitaka kuamini hvyo angalia mafuta ya alizeti yanayotengenezwa Tanzania na mafuta ya alizet yanayokuwa import bei zake
Hizo gharama zinasababishwa na kodi kubwa.
Wangeweza kuondoa baadhi ya kodi uzalishaji ungekuwa rahisi sana.Watu wangepata ajira na biashara ingefanyika kwa wingi sana.
Mungu atujaalie akili
 
Gharama ya kulima Tanzania ni kubwa kuliko kununua mazao nje,ukitaka kuamini hvyo angalia mafuta ya alizeti yanayotengenezwa Tanzania na mafuta ya alizet yanayokuwa import bei zake
Umeongelea zao moja tuu alizeti, tena hata hilo nakupinga.

Fikiria serikali ingewekeza vya kutosha kwenye mashamba ya alizeti pale singida kuwe na plantation kubwa kungekuwa na uhaba wa malighafi..?

Unataka kutuaminisha kuwa tukinunua mahindi, maharage, ngano, mchele, nchi za nje bei itakua chini kuliko kununua hapa kwetu..? , Hizo ndo sababu za wafanyabiashara wapumbavu wabinafsi wasiojali wengine na kuangalia matumbo yao wenyewe
 
Bongo hii hata kama Mtu ana kipaji cha kuongoza nchi "charismatic power" bado tu itamlazimu awe na connection la sivyo ataendelea kuwa mpenzi mtazamaji tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…