Nini kimetokea mpaka kufa kwa uzalishaji wa Ngano hecta 350,000 kule Bassotu Manyara?

Nini kimetokea mpaka kufa kwa uzalishaji wa Ngano hecta 350,000 kule Bassotu Manyara?

Umekumbusha mbali sana. Ni maeneo yaliyokuwa mazuri sana miaka ya mid 80 hadi mwishoni mwa miaka ya 90. Kulichangamka sana kwa biashara, watu toka kila pembe ya nchi n.k.

Ngano iikuwa inalimwa sana, kama sikosei mashamba ya Basuto yaliongoza Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Kuna Setcheti, Basuto, Gawali, Murijanda, Gidagamowdi, Mulbadow n.k. Kateshi ilichangamka haswa, hata Mwagitu, Kendabi, Nangwa n.k.

Kuna mameneja/meneja wasaidizi kama Mzee Mndeme, Kimaro, Shetui, Koopa n.k walikuwa wanachapa kazi sana.

Jandu plumbers ndio aliyevuta maji kutoka Kindabi (mlima Hanang) na kuyasambaza kwenye hayo mashamba.

Wengi waliokuwa mameneja na wasaidizi wao walisoma Canada.

Ila wengi walikufa na ukimwi sana. Halafu wengi wao hawakuwekeza , ukikutana nao sasa hivi wamepigika kimaisha na utawaonea huruma. Walipenda sana starehe maeneo ya Arusha, Katesh, Babati na Basuto Central.

Kulikuwa na wanawake wengi sana wazuri kutoka kila pembe ya Tanzania ukijumlisha na dada wa Kiiraq, ilikuwa burudani haswa.

Karibuni Katesh, Kindabi, Mwagitu, Hydom, Masakta, Endasaki, Dareda Centre na Mission, Balang'ida Lalu na Dirima, Milima ya Logia, Gendii, Bonga, Managha, Galapo, Maweni, Maisaka, Murara, Magugu n.k.

Saitaaaaa/Gabaseyuuu.
Mkuu bado unakaa huko? Niliishi bonga kipindi Fulani hivi
 
Kwa nchi kama Tanzania, kusema tuna uhaba wa ngano au hata pengine mafuta ni aibu. Tuna ardhi bora sana ya kilimo. Tatizo hatujawekeza sana huko. Kuna kipindi kilimo kilipewa kipaumbele, kabla kilimo hakijaimarika tunavuka kwenye viwanda.

Nafikri watunga Sera wetu wanatakiwa kua makini na kutambua nini kinatakiwa kupewa kipaumbele, kwa wakati gani na kwa nini.

Kwa hesabu za haraka haraka, viwanda huja baada ya kilimo kuimarika.
 
Kuna wazungu wamechukua hilo shamba la basuto wanafukua barabara zote za shamba ili kuanza kilimo cha ngano,bila shaka mwaka kesho wataanza kilimo....shamba limeharibika sana mpka waweke miundombinu sawa
80% hapa tz inatoka Ukraine, Sasa hii vita wazungu wanaona mbali wanajua watapiga hela acha sisi tuendelee kufungua nchi.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Cha ajabu zaidi hiyo report ya CAG haifanyiwi kazi yoyote ile.

Nimeamini rasmi wakoloni weusi ni hatari sana kuliko hao mabeberu.

Trump alikuwa sahihi kabisa kuwa "inabidi wakoloni weupe(mabeberu) warudi upya kututawala maana tangu tumepata uhuru tumeshindwa kujitawala"
Ndo maana upigaji KILA mwaka na mwakani watazipiga zaidi,Ningepata namna ya kukwepa kodi ningefurahi sana.
Ripot ya CAG ni SAwa na ngonjera zisomwazo KILA mwaka kuwaumiza wananchi.
Hakuna mtu amewahi fungwa eti kapiga.Wanafungwa vibaka wa kuiba kuku sababu hawana pesa za kuhonga,jela ni kwa ajili ya watu masikini tu sababu hawana pesa ya kununua UHURU wao.
 
Kwa nchi kama Tanzania, kusema tuna uhaba wa ngano au hata pengine mafuta ni aibu. Tuna ardhi bora sana ya kilimo. Tatizo hatujawekeza sana huko. Kuna kipindi kilimo kilipewa kipaumbele, kabla kilimo hakijaimarika tunavuka kwenye viwanda.

Nafikri watunga Sera wetu wanatakiwa kua makini na kutambua nini kinatakiwa kupewa kipaumbele, kwa wakati gani na kwa nini.

Kwa hesabu za haraka haraka, viwanda huja baada ya kilimo kuimarika.
Ukinunua ndege utapata kiki zaidi kuliko kuinua kilimo, mwanasiasa anaangalia kiki kwa maumivu ya kodi zetu
 
Ili shamba lina zaidi ya miaka 45 na mpaka reli ilijengwa kwenda maeneo yale.

Tungekuwa tumeliendeleza huu uhaba wa ngano sasa ingwekuwa kuna ahaueni.

Nadhani ni mda muafaka wadau sector binafasi kwa kushiriana na serikali kufufua kilimo cha Ngano aya maeneo.

Pata habari kamili kuhusu ili shamba la ngano ndo ujue kwenye miti hakuna wajenzi.

======

When the Canadians in co-operation with the TZ Government embarked on the big wheat production project about 45 years ago, more than 350 000 ha of the best land was taken away from the pastoralists using it for grazing cattle. The Canadian extensive strategy of wheat production, without using fertilizers, produced annually between 25 000 and 50 000 tons of wheat, depending on the rains.

By then it contributed to about 10 % or less of the demand for high quality wheat in Tanzania. The best wheat farmers in Europe, or Zambia, are getting yields 5 times or more per ha. This is equivalent to 125 000 tonnes or more from an area as big as all the seven “Canadian” wheat farms in Hanang.

Why are these facts important?

At present, the total demand for wheat in Tanzania stands at about one million tons. The Tanzanian production is about 100 000 tons, or 10 % of the demand. The deficit of 900 000 tons is imported, using huge amount of foreign exchange. It makes good sense to invest in food production in Tanzania and save foreign exchange by closing the gap between demand and supply by food produced locally.

The big challenge is to use land more efficient; doubling or more the yields per ha of cereals and to establish more sustainable and productive food productions systems.

Efficient use of land - higher yields per ha

Many factors might influence the yield. Water and plant nutrients; - fertilizers or manure - are among the more important ones if the farmer has good and disease resistant varieties of the crops. Looking at the yields at Mulbadaw, Murjanda, Setchet and ..... farms, the average yields are not different from the yields obtained 40 years ago. The main production strategy is still rather extensive. There has been none or only negligible efforts in making the land more productive.

These farms are all owned and run by non-citizens through shareholder companies registered as “Tanzanian” companies. The mode of production is large-scale monoculture of wheat, using big tractors and aeroplanes for spraying pesticides.

One of the main objectives of HDC was to improve yields from the historic average yields in the area of less than 1,5tons/ to 3 tons/ha. The company hired a senior Tanzanian wheat specialist in breeding and production and established a research and development program addressing soil fertility and variety challenges.

The late Dr. Ole Hallgrim Evjen Olsen at Haydom Lutheran Hospital (HLH) suggested already in 2004, when the process of buying Mulbadaw was initiated, to construct shallow dams at Mulbadaw for harvesting of rain water and to use this for securing better yields of the crops. In 2006, HDC hired the services of Ingar Kvia and the soil moving equipment he brought to HLH to construct one shallow dam, in order to gain practical experiences with shallow dams at Mulbadaw.

The main wheat growing areas in Australia has a rolling landscape similar to that of the wheat growing areas of Hanang. HDC received a team of three Australian irrigation specialists from the wheat growing area in Australia where rain harvesting has become an important strategy for higher and more reliable yields of wheat.

The team concluded that the landscape and rainfall pattern of Mulbadaw and Bassotu is ideal for rain harvesting. There is experience from Zambia indicating that rain harvesting and irrigation is profitable. One company investing in irrigation of wheat there had an ambition of getting 6 tons/ha from irrigated and fertilized fields. They got 10 tons/ha, - same yield as the best wheat growers in Europe are getting with similar inputs.

Sustainable production systems

There is much to be wanted in form of sustainability from what I see at present.

Water management

Much of the rain falling over the Basotu farms is lost from the production fields, flooding Lake Basotu in years of heavy rains. There is soil erosion and hence silting of Lake Basotu. Even in years with a high rainfall, crops might suffer during long dry spells and impede growth and development of the crops. Rain harvesting and irrigation contributes to sustain yield at high levels. Same amount of wheat can be produced using less land. Water harvesting might thus be a sustainable strategy for diversification of agricultural production systems, including other crops for proper crop rotations, livestock and useful trees.

Soil fertility and soil productivity
After more than 45 years with wheat, the infection pressure from wheat diseases and pests is high. Noxious weeds have been combated by spraying large amounts of glyphosate (‘Round Up’) on the fields before planting. Pests and diseases are sprayed from the air, using chemicals that might be harmful for the people living in the vicinity of the farm. Run off from the fields pollute drinking water for cattle and man. Crop rotation and proper soil cultivation might be a more sustainable strategy for obtaining sufficient control with some weeds and harmful diseases and pests.

Source :Haydom Development Company

The erratic and often insufficient rainfall cause low efficiency of fertilizers in most years, using conventional methods of application. Trials conducted by HDC at Mulbadaw in 2006 and at Setchet in 2007 demonstrated the tremendous effect of adding fertilizers to the soils of these farms, providing that the crop gets sufficient water[3].

A crop getting sufficient “food” in the form of fertilizer is much more competitive towards competition from weeds and damage by wheat diseases and pests.
Halina mchango wa kura wakati wa uchaguzi mkuu, kipaumbele chetu ni kuchukua madaraka na hilo shamba lingekuwa na wapiga kura ungeziona nguo za kijani hapo mwaka mzima zikipishana.
 
Mkuu awali ya yote pongezi kwa uzi huu
Si basutu pekee kule west Kilimanjaro kuna ngano pia inalimwa na serekali imekaa kimya
Swala la PSRC ile ya Nkapa kuhusu ubinafsishaji wa mali za uma ndio tatizo na sera zetu za ubabaishaj
 
Umekumbusha mbali sana. Ni maeneo yaliyokuwa mazuri sana miaka ya mid 80 hadi mwishoni mwa miaka ya 90. Kulichangamka sana kwa biashara, watu toka kila pembe ya nchi n.k.

Ngano iikuwa inalimwa sana, kama sikosei mashamba ya Basuto yaliongoza Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Kuna Setcheti, Basuto, Gawali, Murijanda, Gidagamowdi, Mulbadow n.k. Kateshi ilichangamka haswa, hata Mwagitu, Kendabi, Nangwa n.k.

Kuna mameneja/meneja wasaidizi kama Mzee Mndeme, Kimaro, Shetui, Koopa n.k walikuwa wanachapa kazi sana.

Jandu plumbers ndio aliyevuta maji kutoka Kindabi (mlima Hanang) na kuyasambaza kwenye hayo mashamba.

Wengi waliokuwa mameneja na wasaidizi wao walisoma Canada.

Ila wengi walikufa na ukimwi sana. Halafu wengi wao hawakuwekeza , ukikutana nao sasa hivi wamepigika kimaisha na utawaonea huruma. Walipenda sana starehe maeneo ya Arusha, Katesh, Babati na Basuto Central.

Kulikuwa na wanawake wengi sana wazuri kutoka kila pembe ya Tanzania ukijumlisha na dada wa Kiiraq, ilikuwa burudani haswa.

Karibuni Katesh, Kindabi, Mwagitu, Hydom, Masakta, Endasaki, Dareda Centre na Mission, Balang'ida Lalu na Dirima, Milima ya Logia, Gendii, Bonga, Managha, Galapo, Maweni, Maisaka, Murara, Magugu n.k.

Saitaaaaa/Gabaseyuuu.
Mulbadwa vs nafco
 
Hatuna dhana ya uwongozi ndani mwetu hili ndiyo tatizo la msingi. Kiongozi anatakiwa afahamu kila kitu juu ya anacho kiongoza, iwe ni chama, kiwanda, taasisi nk.

Kiongozi anapaswa ajue uongozi wote wa siku unavyofanyika na uwezo wa kila mtendaji. Asilale mpaka pitied ripoti zote na azifanyie tathmini.

Wazungu huwa wanaandaa viongozi kwa muda mrefu. General manager ana nature vijana watakao mrithi kwa muda mrefu.

Mfano wa jambo hili ni Mbowe na Chadema, Mbowe anaijua Chadema tangu akiwa Bavicha. Anajua Idara zote muhimu na watendaji wake. Ndiyo maana si rahisi Chadema kuyumba.
Huo mfano wa Mbowe na bavicha ndo matatizo ya waafrika hayo.
Watu wanaongelea uchumi wewe unatuletea mambo ya mabakuli.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Ninakumbuka wa Canada walitoa mchango mkubwa sana katika kukiendesha kilimo hiki. Enzi zile kulikua na mabasi ya Mtei kutoka Arusha mpaka Katesh. Katesh ulikua ni mji kabisa watu walikwenda kula starehe na kupata mahitaji.
Ni kweli. Wadada wazuri wa nchi hii walidhuru eneo hilo na kutoa burudani. Nadhani hata wewe wakati ukiwa mbichiiii ulikuja huku.

[emoji38][emoji38][emoji3][emoji3]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Njowepo umeleta mada nzuri sana, Jamii Forums tunahitaji mada kama hizi ambazo mjadala wake unaweza kuleta tija katika kutatua changamoto zilizopo na kuleta impact katika uchumi wa nchi yetu. Ni seme tu huu ni mmoja ya miradi ambayo kama nchi ni wakati muafaka sasa Waziri wa Kilimo na team yake waangalie namna ya kufufua miradi hii mikubwa ya kilimo ya kimkakati kwa njia ya PPP (Public-Private Partnership) kwa mazao ya Ngano, Alizeti, Mpunga n.k. Ukiacha maeneo haya ya Hanang, pia kuna haja ya kufufua mashamba makubwa ya Ngombe wa Maziwa kule West Kilimanjaro, Pia Ngano inaweza kulimwa maeneo hayo, pamoja na Mufindi, Njombe n.k
 
Unaweza kutoa chozi ukisoma wadau humu wanavyochambua mambo.

Kuna pahala sisi huku Africa nafikiri hatuko sawa licha ya kutaliwa.

Ni kwa kiasi gani Serikali inakimbilia kujenga Miundombinu ya Kisasa mijini kwa gharama kubwa ikiwa kuna sehemu kama Kigoma , Ulanga-Mahenge na kote ambako watu wanazalisha mazao mengi lakini kutokana na kutofikika kwa urahisi , watu wamekata tamaa wameamua kulisha tu matumbo yao.

Vijana hawaogopi kutumia fursa ,tatizo kwenye Kilimo kwa hapa kwetu kumesahaulika na sidhani kama kuna Mwanasiasa ana muda na Kilimo.Ni ujuha wa hali ya juu Nchi kamaa hii kukosa mafuta ya kupikia..huo ni uchawi wa mchana kweupe sana.

Nenda West Kilimanjaro kuna vijana wanalima Karoti ,Nyanya na viazi Ulaya lakini katazame Barabara ya West to Bomang'ombe ni lami lakini ni uozo ule..Barabara nyembamba kama uzi.Sehemu kama hizo na zingine ambazo ndio kabisa hazina hata nukta ya lami zilipaswa kusambazwa Barabara na za kiwango cha lami na Reli pia ili kutufanya tuhame huko mijini tujikite na Kilimo.

Ukitaka kujua sisi tunashida angalia Mkoloni alipeleka Reli kila pahala pailipokuwa na mazao na uzalishaji maligahfi. Lakini njoo utazame akili zetu sis wenye Uhuru.

NSSF ,PSSF wanajenga majengo kiwizi wizi kwa fedha zetu za michango wanaacha kwenda kuwekeza kwa Vijana..majengo marefu na hakuna watu wanakaa humo.

Wanajijengea njia zao Baharini wapite wakati wa jioni wakiwa wamechoka,thamani ya hizo barabara ni umejenga Barabara za kutosha kuunganisha miji yenye uzalishaji bila ubabaishaji.

Vijana tuamke tujikite huko taratibu ..japo kuna ugumu.Serikali haiwezi komboa mtu.
 
Back
Top Bottom