kuliko kutumia neno kujamiiana heri ungetumia "kuhusiana!".
Kwangu mimi nilipata chombo haswa hata sikujutia, baada ya mazoea kwa takribani wiki mbili penzini nikaamua nimuombe mchezo!.
tukapanga siku yakwenda kutufuana vizazi, siku ilipofika ndo nilijua nimeopoa kisu badala ya jokeri kama ingekuwa ni mchezo wa karata!.
mtoto pamoja na uzuri wake kumbe anamajini!, si yakampanda ghafla... kile chumba nilikuwa nakiona kikubwa hapo awali lkn yalivyompanda tu ndo nilijua nimeingia kwenye shimo la sungusungu!.
ile nataka kutimua niwahi mlangoni alinikwatua mguu nikaanguka chini!, hapo nipo uchi maana ndo nilikuwa naelekea kumaliza cha kwanza can you imagine aliyapandisha madude yake hata sijamaliza!.
akasimama mkabala namimi hapo nipo chini, kumcheki macho yake yamekuwa mekundu huku anaongea kiarabu mi hata sielewi!.
kiukweli alikuwa hana nia ya kunidhuru isipokuwa mimi ndo nilikuwa sijazoea hiyo hali na majini yake yalikuwa hayataki nikimbie, yalikuwa yanataka kuzungumza namimi man to man!.
Mimi sasa sielewi nikiwa pale chini nikakurupuka tena!, mara hii akanishika kichwa nikampush! ohoo! si yakasala ile naukaribia tu mlango nahangaika kuufungua ili nitokomee nje nikatoe burudani ya kuonyesha uchi!, kabla hata sijaufungua alikuja mzima mzima akanikumbatia kwa nguvu na jini lake hapo likawa linacharanga kiarabu haswa limesala kwelikweli!!.
nikawa najilazimisha kujitoa kwa nguvu ndo akazidi kunibana zaidi na ubovu lilikuwa na nguvu!. likanisokota mpk kwenye kona ya ukuta nikaona leo nafwa!. ikabidi nitulie kidogo jicho hapo limenitoka natamani kupiga kelele nashindwa!.
ikapita kama dk moja hivi kaning'ang'ania tu, ikabidi nilegee nilivyoanza kuona hana madhara tena ndo nalenyewe likatulia mpk likamuondoka!.
alivyorudi kwenye utimamu wake mtoto wa watu akawa ananionea aibu maana anajijua!, akanipa sorry kibao lkn mimi na mood ya tendo ndo ikawa imekata, tukasepa na ndio ukawa mwanzo na mwisho wa kumtafuta niliona isiwe tabu tusije pelekana oman bure!.
Sina hamu tena na wadada wa Facebook, huyo alitosha kunionyesha maana ya face halafu book!.