Nini maana ya hii ndoto?

Nini maana ya hii ndoto?

Mimi ni Mkristo. Niaminivyo, chanzo cha ndoto inaweza ikawa:
1. Ujumbe kutoka kwa Mungu

2. Kazi ya Shetani kwa lengo la kuharibu

3. Uchovu wa mwili na aina ya mawazo uliyokuwa ukiyawaza kabla ya kulala.

Hivi karibuni, nimeota ndoto ambayo mpaka sasa bado sijapata tafsiri yake.

Niliota natembea njiani na vijana wawili, na ghafla , nikaona noti ya sh 1,000/= mbele yangu.

Nilipoiona, nilijisemea kuwa kama nimetegeshewa kichawi, basi itakuwa "imekula" kwao walioitegesha kwa sababu nitaichukua na kuitakasa kwa Jina la Yesu na kuitumia bila madhara yoyote. Niliamua kuchukua, na mara tu baada ya kuiokota, niliziona zingine nyingi, noti za shilingi 1,000/= na za 2,000/=. Niliendelea kuziokota, na nikawaambia vijana wawili niliokuwa nao kuwa na wao waokote.

Baada ya kuiokota kiasi kikubwa, ziliisha na hatimaye tukaendelea na safari kila mmoja akiwa na noti zake. Muda wote nilikuwa makini kuzishikilia huku nikiendelea kuziombea ili kama zilikuwa na nguvu za giza zisiweze kuwa na athari kwangu.

Baada ya kutembea kidogo, tuliwakuta askari watatu wa usalama barabarani wakiwa wamesimama pembezoni mwa barabara. Mmoja wao, akiwa katika sare za kazi, alinifuata na kuniambia hela tuliyoiokota ni ya kwake hivyo nimrudishie.

Kwanza, nilitaka kukataa kumpa. Lakini aliponiambia kuwa walituona tokea tulipokuwa tunaokota hizo fedha, nilipatwa na mshutuko, nikagundua kuwa huyo trafiki si binadamu wa kawaida. Aliwezaje kutuona wakati tulikookotea ni mbali?

Pale pale nilianza kumkemea kwa Jina la Yesu, na ghafla yule trafiki akaanza kubadilika kuanzia sura, umbo mpaka na mavazi.

Mavazi yake ya utrafiki (meupe) yalipoteza uweupe na kufanania kwa mbali sare za wafungwa. Na umbile la huyo askari lilibadilika kutoka wa kiume na kuwa wa kike.

Nilipoendelea kumkemea, alidondoka chini na kuwa kama anayegugumia kwa maumivu.

Vijana wawili niliokuwa nao waliondoka kwa muda na kuniacha peke yangu nikiandelea kupambana na hicho kiumbe. Ni kama vile niliwaagiza kufuata kitu.

Wakati nikiendelea kumkemea, nilimhoji sababu ya kunitegeshea pesa, akasema walinipenda. Nilipomwuliza kama hiyo hela ingewaathiri na hao vijana wawili waliookota, alisema ingewaathiri kama wangekubaliana nao.

Baada ya kusema hivyo, nilikazana kuomba kwa bidii, lengo sasa likiwa hicho kiumbe kipotee kwa kuyeyuka.

Hiyo ndoto inamaanisha nini?

Nini chanzo chake?

Asanteni.
kuna mtu amekuelezea vizur hapo.
tafasiri ya ndoto yeyote inatoka kwa Roho wa Mungu ( ikiwa ni ndoto ya kiMungu)

rejea mifano mingi kwny biblia ya watu wengi walio ota ndoto tafasiri nzur ya ndoto wote walirejea kwa Mungu.

mfano. Daniel anamwambia nebukadnezza. tupe mda tutakukumbusha ndoto na tafasiri yake daniel anarejea kwa Mungu kumuuliza na badae anapata majibu yalio sawa na maana halisi ya ndoto.

nini chakufanya sasa unapoota ndoto?. either ni nzur au mbaya?.

Omba Omba Omba piga magoti mbele za Mungu utapata tafasiri na hatua zakuchukua.

namna ya kuomba.
approach ndoto vile ilivyo (kwa maana ndoto ni ishara ya jambo kutokea katika ulimwengu wa roho). kumbuka jambo lolote kabla halijaanza kwny ulimwengu wa mwili linaanza kwenye ulimwengu wa roho kupitia ndoto na maono.

kwahio vile ulivyoota step moja baada ya nyingine kwny kukataa jambo likatae ambalo halina baraka kwako kwny kulikubali mshukuru Mungu na kulikubali ulinene linakuja katika ulimwengu wa mwili

Kumbuka laana na baraka zito kwny ulimi wako
 
Kama ni tafsiri sahihi moyo utaridhia. Kuna namna amani ya moyoni itakupa uhakika kuwa hiyo ndiyo tafsiri sahihi.
Sasa je hiyo amani unayosema unaweza kuipata kweli kama tafsiri ya ndoto ni mbaya kwako kama ile kwenye bible aliyopewa King Nebukadneza.
 
kuna mtu amekuelezea vizur hapo.
tafasiri ya ndoto yeyote inatoka kwa Roho wa Mungu ( ikiwa ni ndoto ya kiMungu)

rejea mifano mingi kwny biblia ya watu wengi walio ota ndoto tafasiri nzur ya ndoto wote walirejea kwa Mungu.

mfano. Daniel anamwambia nebukadnezza. tupe mda tutakukumbusha ndoto na tafasiri yake daniel anarejea kwa Mungu kumuuliza na badae anapata majibu yalio sawa na maana halisi ya ndoto.

nini chakufanya sasa unapoota ndoto?. either ni nzur au mbaya?.

Omba Omba Omba piga magoti mbele za Mungu utapata tafasiri na hatua zakuchukua.

namna ya kuomba.
approach ndoto vile ilivyo (kwa maana ndoto ni ishara ya jambo kutokea katika ulimwengu wa roho). kumbuka jambo lolote kabla halijaanza kwny ulimwengu wa mwili linaanza kwenye ulimwengu wa roho kupitia ndoto na maono.

kwahio vile ulivyoota step moja baada ya nyingine kwny kukataa jambo likatae ambalo halina baraka kwako kwny kulikubali mshukuru Mungu na kulikubali ulinene linakuja katika ulimwengu wa mwili

Kumbuka laana na baraka zito kwny ulimi wako
Shukran mkuu🙏
 
Sasa je hiyo amani unayosema unaweza kuipata kweli kama tafsiri ya ndoto ni mbaya kwako kama ile kwenye bible aliyopewa King Nebukadneza.
Kuna namna fulani unakuwa na uhakika moyoni kuwa hiyo ndiyo tafsiri ya ndoto husika.
 
Nna ndugu yangu fulani hv nae ana pigo hizo, kila ndoto atakayoota lazima apate wenge kwamba kuna kitu Mungu anataka kumwambia 😂 ndoto zingine ni kutokana na maisha ya kawaida tuu mtu unayoyapitia em msichukulie mambo kigumu hvy
Hii si mara yangu ya kwanza kuota, ila ni mara yangu ya kwanza kuja humu jukwaani kuuliza tafsiri.

Nilishaota mara nyingi, baadhi nikazipuuzia na hazikuwa na madhara yoyote, lakini zingine zikatimia kama nilivyoota.

Kuna matukio nilishawahi kuyaota na yakatukia kama nilivyoyaota.

Kitendo cha kuamua kuja kuuliza ni kwa sababu nimejiridhisha kuwa si ndoto ya kawaida. Kuna "dots" nimeziunganisha zikanipa tafsiri fulani, na baadhi ya wachangiaji wameenda mwelekeo ule ule niliokuwa nikiufikiria. Niliwasilisha humu kwa lengo la kufanya "uhakiki".

Itoshe tu kusema si kila ndoto ni ya kupuuziwa. Nimejifunza hilo the "hard way". Sitaki kurudia kosa. Na kwa tafsiri niliyoipata, nimeshaanza kuchukua hatua stahiki.

Nafahamu ninachomaanisha.

Shukran mkuu🙏
 
naweza kutafsiri code ya pesa ni kitu kinachopendwa sana hivyo inaweza kuashiria ushetani umeuokota sana,wewe pamoja na wenzako ila ingelikuwa dhahabu au vito fulani au sent ingekuwa ni thamani haya tuendelee sasa kuna hao maaskari iliokutana nao,askari humaanisha code ya ulinzi na ana mamlaka katika mji au nchi hivyo ina maanisha kuna viumbe vilikupenda vikawa vinakupatia ushetani wa mambo mengi na walijifanya kuwa wema{usalama barabarani ni nguo nyeupe huashiria safi} ila ukawaombea wakageuka kuwa ni nguo za magereza{askari ambao wanafunga watu ina maana roho yako ilifungwa na wao} kwa kuwa walikupenda kuwa walikuwa wanaishi katika mwili wako.

lakini nguvu ya mungu ambayo ni energy ya kukemea imewaumbua na kuanza kuwachoma hivyo unatakiwa ufanye jitihada za kukemea ili uwadhoofishe na kuondoka hao viumbe unao na kama ungekuwa muislamu ungeambia ni rohani ambao ni viumbe wema ila siyo wema ni negative energy ambazo hukaa kwenye miili yetu,tambua mwili wa binadamu ni energy na hakuna energy inayoishi kufungamana na energy nyengine fight kwa jina la mola wako.
 
Hii si mara yangu ya kwanza kuota, ila ni mara yangu ya kwanza kuja humu jukwaani kuuliza tafsiri.

Nilishaota mara nyingi, baadhi nikazipuuzia na hazikuwa na madhara yoyote, lakini zingine zikatimia kama nilivyoota.

Kuna matukio nilishawahi kuyaota na yakatukia kama nilivyoyaota.

Kitendo cha kuamua kuja kuuliza ni kwa sababu nimejiridhisha kuwa si ndoto ya kawaida. Kuna "dots" nimeziunganisha zikanipa tafsiri fulani, na baadhi ya wachangiaji wameenda mwelekeo ule ule niliokuwa nikiufikiria. Niliwasilisha humu kwa lengo la kufanya "uhakiki".

Itoshe tu kusema si kila ndoto ni ya kupuuziwa. Nimejifunza hilo the "hard way". Sitaki kurudia kosa. Na kwa tafsiri niliyoipata, nimeshaanza kuchukua hatua stahiki.

Nafahamu ninachomaanisha.

Shukran mkuu🙏
Sawa Mkuu je ndoto unazoota ni kuhusu wewe binafsi au pia kuhusu matukio ya jamii inayokuzunguka au pia kuhusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Je unavyoona wewe kwa uzoefu wako ndoto je inaweza kuwa kama " taa ya oil" kukustua ili uchukue tahadhari?
 
Sawa Mkuu je ndoto unazoota ni kuhusu wewe binafsi au pia kuhusu matukio ya jamii inayokuzunguka au pia kuhusu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Je unavyoona wewe kwa uzoefu wako ndoto je inaweza kuwa kama " taa ya oil" kukustua ili uchukue tahadhari?
Chache ziliwahusu watu wengine, hasa ninaowafahamu. Sikumbuki kama nilishawahi kuota inayohusu nchi, labda kama sikuielewa tafsiri yake. Kwa hiyo nyingi zilinihusu mimi binafsi. Nitatoa mifano michache, alau miwili:

1. Kipindi nikisoma, nilihitaji suruali mpya ya "kutokea". Kutokana na hali ya nyumbani ya kifedha kipindi hicho kutokuruhusu mimi kuwa na nguo mpya, niliamua kuielekeza Imani yangu kwa Mungu. Niliomba.

Wakati nikiendelea na maombi, (nilikuwa nikiliombea hilo hitaji kila siku Asubuhi na Jioni), siku moja Usiku, niliota nimevaa suruali mpya. Nilihusianisha hiyo ndoto na maombi yangu, nikaamini nimeshajibiwa maombi. Kuanzia siku hiyo nilianza kushukuru badala ya kuomba.

Muda ulipita bila kuona matokeo. Hatimaye siku moja, nilitembelewa na ndugu yangu mmoja ambaye tulikuwa tukiishi naye mitaa ya karibu.

Wakati wa kuondoka, nilimsindikiza, na kwa sababu ya kunogewa na "story", nilijikuta nimefika mpaka kwake.

Kufika kwake, alifanya jambo ambalo sikulitegemea. Alichukua suruali yake mpya aliyokuwa ameishonesha siku chache zikizopita na kunipatia huku akinisihi nisiikatae. Alinihakikishia kuwa ni mpya na haina tatizo lolote, ila tu kwamba alipoichukua kwa fundi, alijikuta anaichukia sana.

Alipotaka ampatie mdogo wake, alikosa amani. Lakini siku hiyo nilipofika kwake, alipokumbuka kuwa ana suruali mpya asiyoipenda, alipata wazo la kunipatia, na alipolitafakari hilo, alijisikia amani sana.

Nililichukua hiyo suruali, na nilipoenda kuiijaribishia, ikinifiti vizuri sana, utafikiri nikivhukuliwa vipimo kabla ya kushindwa. Kama hilo haitosho, mwonekana rangi, na kila kitu ilifanana na suruali niliyoiona ndotoni.

Kwa tukio hilo, nilijua kuwa hata kutembelea na huyo ndugu yangu, na hatimaye mimi kumsindikiza hadi kwake, haikutokea kwa bahati. Ilipaswa kuwa hivyo ili kuikamilisha ndoto.

Hata yeye kujishonea suruali na kisha kuichukia, haikutokea kwa bahati mbaya. Aliishona kwa ajili yangu.

2. Miaka ya nyuma, niliota kuwa jirani yangu tuliyekuwa tukifanya naye kazi kampuni moja kafariki kwa ajali ya chombo cha moto. Nilipoamka, niliomba na kuvunja roho ya mauti dhidi yake.

Siku chache baadaye, alipata ajali sehemu ile ile niliyoota kuwa kapata ajali, na katika ajali hiyo, alivunjika mguu.

Inawezekana kama nisingeomba, matokea yangekuwa mabaya zaidi. Inawezekana pia ningefanya maombi ya kuzuia ajali, labda, asingevunjika mguu.
 
Chache ziliwahusu watu wengine, hasa ninaowafahamu. Sikumbuki kama nilishawahi kuota inayohusu nchi, labda kama sikuielewa tafsiri yake. Kwa hiyo nyingi zilinihusu mimi binafsi. Nitatoa mifano michache, alau miwili:

1. Kipindi nikisoma, nilihitaji suruali mpya ya "kutokea". Kutokana na hali ya nyumbani ya kifedha kipindi hicho kutokuruhusu mimi kuwa na nguo mpya, niliamua kuielekeza Imani yangu kwa Mungu. Niliomba.

Wakati nikiendelea na maombi, (nilikuwa nikiliombea hilo hitaji kila siku Asubuhi na Jioni), siku moja Usiku, niliota nimevaa suruali mpya. Nilihusianisha hiyo ndoto na maombi yangu, nikaamini nimeshajibiwa maombi. Kuanzia siku hiyo nilianza kushukuru badala ya kuomba.

Muda ulipita bila kuona matokeo. Hatimaye siku moja, nilitembelewa na ndugu yangu mmoja ambaye tulikuwa tukiishi naye mitaa ya karibu.

Wakati wa kuondoka, nilimsindikiza, na kwa sababu ya kunogewa na "story", nilijikuta nimefika mpaka kwake.

Kufika kwake, alifanya jambo ambalo sikulitegemea. Alichukua suruali yake mpya aliyokuwa ameishonesha siku chache zikizopita na kunipatia huku akinisihi nisiikatae. Alinihakikishia kuwa ni mpya na haina tatizo lolote, ila tu kwamba alipoichukua kwa fundi, alijikuta anaichukia sana.

Alipotaka ampatie mdogo wake, alikosa amani. Lakini siku hiyo nilipofika kwake, alipokumbuka kuwa ana suruali mpya asiyoipenda, alipata wazo la kunipatia, na alipolitafakari hilo, alijisikia amani sana.

Nililichukua hiyo suruali, na nilipoenda kuiijaribishia, ikinifiti vizuri sana, utafikiri nikivhukuliwa vipimo kabla ya kushindwa. Kama hilo haitosho, mwonekana rangi, na kila kitu ilifanana na suruali niliyoiona ndotoni.

Kwa tukio hilo, nilijua kuwa hata kutembelea na huyo ndugu yangu, na hatimaye mimi kumsindikiza hadi kwake, haikutokea kwa bahati. Ilipaswa kuwa hivyo ili kuikamilisha ndoto.

Hata yeye kujishonea suruali na kisha kuichukia, haikutokea kwa bahati mbaya. Aliishona kwa ajili yangu.

2. Miaka ya nyuma, niliota kuwa jirani yangu tuliyekuwa tukifanya naye kazi kampuni moja kafariki kwa ajali ya chombo cha moto. Nilipoamka, niliomba na kuvunja roho ya mauti dhidi yake.

Siku chache baadaye, alipata ajali sehemu ile ile niliyoota kuwa kapata ajali, na katika ajali hiyo, alivunjika mguu.

Inawezekana kama nisingeomba, matokea yangekuwa mabaya zaidi. Inawezekana pia ningefanya maombi ya kuzuia ajali, labda, asingevunjika mguu.
Mkuu kwa mitihani/changamoto/majaribu yaliyopo duniani inaelekea umepewa upendeleo fulani wa kujuzwa kitakachotokea mbele.

Bora uendeleze na kupanua hiyo karama
 
Back
Top Bottom