Nini maana ya msemo 'Mwenda tezi na omo marejeo ngamani'

Nini maana ya msemo 'Mwenda tezi na omo marejeo ngamani'

Mkuu, hii maana yake ukienda mbele au nyuma lazima utarejea nyumbani. Kama mdau hapo juu alivyofafanua, kuwa "tezi" ni mbele ya chombo na "omo" ni nyuma ya chombo, na "ngamani" ni katikati ya chombo. Kwa hiyo, ili uweze kwenda mbele ya chombo, lazima upite katikati ya chombo [ngamani], na ukitaka kwenda nyuma ya chombo, utapita pia katikati ya chombo [ngamani].
 
Nijuavyo mie ni kuwa: Ngamani ni kule kambini mnapoishi mkiwa ziwani au baharini , sasa tafsiri ya methali hiyo ni kuwa kila jambo unalofanya lazima lina matokeo either hasi au chanya pale unapoishi.
 
Upwa ni sehemu ya bahari na mgaagaa ni mtu anayezurula maeneo ya upwa, maana yake ni kuwa mgaagaa hawezi kosa samaki hata wa kupewa ndio maana hali wali mkavu. Tafsiri yake ni kuwa MTU anayejishughulisha hawezi kosa chochote hata Kama ni kidogo.
Kiswahili kigumu kweli....mgaagaa na upwa hali wali mkavu.
 
Tezi ni upande wa mbele, Omo ni upande wa nyuma, na Ngamani ni katikati ya chombo.

Haya, chukulia bahari imechafuka, ni lazima kuangaika kwenda mbele na nyuma au kuchota maji yaliyoingia kwenye chombo. Lakini mwisho wa yote, bahari ikitulia au kuwa shwari, unarudi mahali sahihi, yaani Ngamani au katikati ya chombo. Kwa mfano, wewe ni nahodha wa mtumbwi, boti, na kadhalika.
 
Mkimaliza hiyo kuna hii 'Kata pua uhunge wajihi' sina uhakika kama nimepatia 'spelling' za kila neno ila ndiyo sielewagi kabisaa
 
Upwa ni sehemu ya bahari na mgaagaa ni mtu anayezurula maeneo ya upwa, maana yake ni kuwa mgaagaa hawezi kosa samaki hata Wa kupewa ndio maana hali wali mkavu. Tafsiri yake ni kuwa MTU anayejishughulisha hawezi kosa chochote hata Kama ni kidogo.
[emoji122][emoji122]
 
Mkimaliza hiyo kuna hii 'Kata pua uhunge wajii' sina uhakika kama nimepatia 'spelling' za kila neno ila ndiyo sielewagi kabisaa

" Kata pua uunge wajihi "
Chagua moja kati ya mawili / mengi lililosahihi ili ulifanye. Mfano , unataka kufanya biashara Ila mzee wako anaumwa , itabidi ukate pua na kuunga wajihi .....
Nahisi itakuwa umefahamu kidogo Gaspare Mbile
 
Upwa ni sehemu ya bahari na mgaagaa ni mtu anayezurula maeneo ya upwa, maana yake ni kuwa mgaagaa hawezi kosa samaki hata Wa kupewa ndio maana hali wali mkavu. Tafsiri yake ni kuwa MTU anayejishughulisha hawezi kosa chochote hata Kama ni kidogo.
Wengi wanadhani UPWA linatokana na neno MPWA ambalo unaweza kulitafsiri kama MTOTO WA NDUGU. Hivyo ukihangaika kulea watoto wa ndugu, hawatakutupa au hawatakusahau na vijizawadi.
 
Back
Top Bottom