Nini maana ya neno kuokoka?

Nini maana ya neno kuokoka?

Walokole ndio huokoka
Sio walokole pekee, yeyote anaweza kuokoka, akishamkiri tu Yesu kuwa ndiye mwokozi wa maisha yake..

Hapa anakuwa ameokoka, na nguvu za Roho Mtakatifu zinaanza kufanya kazi ndani yake ..
 
Nimeuliza kiimani, kwa sababu huwasikia wengi hususan wasio waislam wakisema "nimeokoka, ameokoka, wameokoka" likihusika na imani zao.

Ndiyo nauliza ni nini maana ya kuokoka?
Hao wote unaowasikia wakisema hivyo ni wanafki wakidini... Mistari inayozungumzia wokovu iliyopo katika biblia inalizingumzia suala hilo katika hali yawakati Ujao...

Mimi ni Muumini wa dini ya Kristo na katika wokovu naamini Nitakuja Kuokoka wakati ambao wengine watakua wameangamizwa kwa kukosa kwao maharifa.

Duniani hakuna aliyeokoka kwa mujibu wa maandiko ila wapo watakaookoka.

So wanaoamini wameokoka sasa katika nyakati hizi... waje na maandiko yanayouthibitisha kuokoka katika wakati uliopo.

Nilitaka tulikwepe swali lako maana kuzama sana kwenye dini ni aina ya uchizi ndio maana katika jamii wanaoongoza kuchukiana ni wale walio deep sana katika imani zao za kidini. Chunguza!
 
Ww hujauliza kwa nia ya kujifunza ni unafiki tu unakusumbua ww ya wakristo yana kuhusu nn maana hata wakikueleza kwa ulivo mdini wanatwanga maji kwenye kinu.KUOKOKA NI KUACHA UISLAM NA KUJA KWA MUNGU WA KWELI.
Kumbe unaacha uislam kwanza cyo? Kuokoka:Ni kitendo cha kuwa huru kutoka kwenye dhambi yaani mtu aliyeokoka ni yule asiye na dhambi ambapo mpaka sasa hatuna mtu huyo zaidi ya kuwa na wazinzi tu

Sent from my SM-G950U using JamiiForums mobile app
 
Ww hujauliza kwa nia ya kujifunza ni unafiki tu unakusumbua ww ya wakristo yana kuhusu nn maana hata wakikueleza kwa ulivo mdini wanatwanga maji kwenye kinu.KUOKOKA NI KUACHA UISLAM NA KUJA KWA MUNGU WA KWELI.
Atuambie kwanza ..kuhusu bikira 72,mito ya pombe na uhalali na uharamu wa nguruwe katika muktadha tofauti!?
 
Ww hujauliza kwa nia ya kujifunza ni unafiki tu unakusumbua ww ya wakristo yana kuhusu nn maana hata wakikueleza kwa ulivo mdini wanatwanga maji kwenye kinu.KUOKOKA NI KUACHA UISLAM NA KUJA KWA MUNGU WA KWELI.
Nimeweka sababu ya kuuliza, labdahujnisoma vizuri, Soma tena kuhusu mafundisho yangi ya Kiislam:

Qur'an 3:64. Sema: Enyi Watu wa Kitabu! Njooni kwenye neno lilio sawa baina yetu na nyinyi: Ya kwamba tusimuabudu yeyote ila Mwenyezi Mungu, wala tusimshirikishe na chochote; wala tusifanyane sisi kwa sisi kuwa Waola Walezi badala ya Mwenyezi Mungu. Na wakigeuka basi semeni: Shuhudi- eni ya kwamba sisi ni Waislamu. 64
 
Walokole na wakristo ni kitu kimoja isipokuwa unaweza ukajiita wa Kristo ila sio wa kristo kwa kuwa hujaokoka...

Wengi hujiita tu hivyo kimwili ila kiroho hawajampokea Yesu kuwa Bwana wa maisha yao
Unapiga chenga kaali sana lakini hujajibu swali:

Kwani "walokole" siyo wakristo?

Nini maana ya kuokoka?
 
Yesu anawezaje kuwa "mwokozi" wakati yeye mwenyewe aliomba aokolewe? Mpaka akalalamika "mbona unaniwacha?".

Kivipi anayelia kuokolewa awe "mwokozi"?
Yesu Kristo ni mwanadamu kweli kweli na Mungu kweli kweli...

Yesu Kristo ni mwanadamu...hivyo aliishi kama mwanadamu hivyo alipopigwa aliumia kama mwanadamu..

Yesu ni MUNGU, alipokufa na kufufuka hapa ndio inadhihirisha kuwa yeye ni Mungu kweli kweli...

Mungu ni Roho

Zingatia Yesu Kristo na Yesu ni vitu viwili tofauti ..
 
Ww hujauliza kwa nia ya kujifunza ni unafiki tu unakusumbua ww ya wakristo yana kuhusu nn maana hata wakikueleza kwa ulivo mdini wanatwanga maji kwenye kinu.KUOKOKA NI KUACHA UISLAM NA KUJA KWA MUNGU WA KWELI.
"Mungu wa kweli" ni yupi?
 
Mimi ni mkristo... Nimejitahidi sana kutafuta mstari unaonipa uhakika wakuwa nikifanya hivyo nimeokoka ila nimeukosa... Yote inayoelezea wokovu ipo katika wakati ujao...
Sina mtego wowote hapo. Nimeuliza kiukweli kabisa na nimeeleza kwanini nimeuliza. Kanisome tena.
 
Sio walokole pekee, yeyote anaweza kuokoka, akishamkiri tu Yesu kuwa ndiye mwokozi wa maisha yake..

Hapa anakuwa ameokoka, na nguvu za Roho Mtakatifu zinaanza kufanya kazi ndani yake ..
Samahani...Nilichomaanisha ni kuwa walokole ndio huamini hivi
 
Mimi ni mkristo... Nimejitahidi sana kutafuta mstari unaonipa uhakika wakuwa nikifanya hivyo nimeokoka ila nimeukosa... Yote inayoelezea wokovu ipo katika wakati ujao. Je, Ni Mstari gani au andiko gani linalotuthibitishia.. nikifanya hivi au vilw nitakua nimeokoka na sio nitakuja kuokoka?

Namaanisha... Kwanini tuseme tumeokoka wakati maandiko yanatuambia Tutaokoka.?

Halafu tusipende kulazimisha udini katika mada zilizo wazi. Swali ni nini maana ya Kuokoka. wewe imekuja na habari za Wokovu... kitu ambacho nakuona umenasa kwenye mtego wa mtoa mada.
Ulichokiandika sio sahihi kwa 100% kibiblia. Nitaweka ufafanuzi hapa.

Kwanza, huwezi kutenganisha Wokovu na kuokoka, kama usivyoweza kutenganisha Imani na kuamini, kifo na kufa, maisha na kuishi, ufufuo na kufufuka, chakula na kula nk. Wokovu ndio unazaa kitendo cha kuokoka.

Pili, Kibiblia, kiujumla, Kuokoka ni kumwamini Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako. (MATENDO YA MITUME 16:30-31 (.....Yanipasa nifanye nini ili nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako)

Tatu, yapo maandiko mengi kwenye Biblia yenye kueleza tukio la kuokoa katika wakati uliopita, na hapa kwa uchache nitakuwekea kwa mifano.
-ISAYA 45:20 (Jikusanyeni mje, na kukaribia pamoja, ninyi wa mataifa MLIOOKOKA)

-WAEFESO 2:5 (Hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu, alituhuisha pamoja na kristo, yaani, TUMEOKOLEWA kwa neema)

-WAEFESO 2:8 (Kwa maana MMEOKOLEWA kwa neema, kwa njia ya amani, ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu)

Nne, kuweka kumbukumbu sawa hawa JF, kimsingi tukio la wokovu (kuokoka) ni sasa (2Korintho 6:2) ukiwa unaliendea (bado hujaokoka) litakuwa kwa wakati ujao na ukiwa ulishafikia (tayari umeokoka) utalizungumzia katika wakati uliopita.

Mwisho,kibiblia hakuna wokovu (kuokoka) nje ya Yesu kristo (MATENDO YA MITUME 4:12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwako)
 
Unapiga chenga kaali sana lakini hujajibu swali:

Kwani "walokole" siyo wakristo?

Nini maana ya kuokoka?
Umeshajibiwa lakini unaleta ubishi tu.
Umeambiwa kuwa wafuasi wa Yesu kristo hapa duniani wanaitwa wakristo regardless wamempokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wao (wameokoka) ama la.
 
Samahani...Nilichomaanisha ni kuwa walokole ndio huamini hivi
Haijarishi unaamini hivyo ama la, ukweli unabakia hivyo hivyo kimaandiko. Ukimpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako maana yake umeokoka kwa mujibu wa maandiko (Matendo ya Mitume 16:30-31)
 
Back
Top Bottom