Nini maana ya pesa?

Nini maana ya pesa?

Joined
Apr 19, 2018
Posts
83
Reaction score
115
Je, pesa ni bahati? hasa ya kuzaliwa nayo?

Je, pesa ni kitu kinachotafutwa?

Je, pesa ina thamani ile ile tunayoiamini?

Je, ni kwa nini walio wachache wanamiliki kiasi kikubwa cha pesa na kutuacha wengine tuking`ang`aniana “Vijisenti” vilivyobaki?

Hayo ni maswali yaliyowahi na yanaendelea kupita vichwani mwa watu wengi, hasa vijana wa kizazi hiki, ambao ndiyo nguvu kazi ya taifa.

Pesa ni bahati?
Wengine wanaamini kuwa na pesa ni bahati, na ndiyo maana wanakukuruka huku na kule, kucheza bahati nasibu mbalimbali kama betting, forex, n.k wakijaribu bahati zao; lakini wapo wengine wanaamua kwenda kusafishwa nyota zao kwa njia mbalimbali, wakiamini kuwa njia hizo zitawasafisha na kuwaletea hizo bahati.

Wengine wanafikiri kuwa pesa ni bahati ya kuzaliwa, kwa hiyo kama familia yenu hamko vizuri kifedha, basi maisha yako vile vile hayatabadilika, unaweza ukajitahidi kutafuta elimu au kufahamiana na kujiungamanisha na mtu aliyetoka kwenye familia kama hizo za wenye nazo na ndipo maisha yako yanaweza kuwa na unafuu.

‘Mindset’ hii ndiyo inayopelekea mtu kufanya juu chini ili aoe au aolewe na mtu mwenye nazo, la sivyo maisha yake hayawezi kufanikiwa.

Pesa inatafutwa?
Kundi lingine la watu wanaamini kuwa pesa inatafutwa, kwa hiyo wao wanaamini kuwa ni lazima mtu ujishughulishe na kujibidiisha na ndipo anaweza kuwa na pesa kibao kama waliofanikiwa wengine. Na ndiyo maana utamkuta mtu mwenye mtazamo wa aina hii yuko bize kweli kweli, mpaka kuna wakati anasahau ratiba ya kula, ili mradi tu, afanye kazi kwa bidii ili afanikiwe na kuwa na pesa nyingi.

Waliojiriwa na wana mtazamo wa aina hii, utawakuta wanajibidiisha kweli kweli, wengine wanarudi mashuleni na kuongeza elimu zao, wengine wanafanya kazi mpka masaa ya ziada. Yote hayo yanafanyika ili mradi wapande cheo na kuweza kukuza vipato vyao.

Maswali yanayofuata baada ya swali hili la pili, ndiyo haswaa yanayoibua mkanganyiko, kwenye “Mindset” hii. Kwa sababu licha ya kujibidiisha, watu wengi wa kundi hili bado wana “Struggle” kimaisha, mpaka wengine wanakata tamaa na kurudi kwenye kundi la kwanza kabisa hapo juu, la wale wanaowaza kuwa “Pesa ni bahati”.

Je, pesa ina thamani ile ile tunayoiamini? Pesa inalinganishwa na nini haswaa mpaka inakuwa ngumu kupatikana kiasi hiki? Bidii na jasho ndiyo vinavyotupatia pesa? Bahati ndiyo inayotupatia pesa?

Kabla ya kuendelea na Maada yetu, nataka nipate maoni yako, wewe unafikiri kipi ni kipi kuhusu pesa?
 
Pesa ni MOJA ya matokeo unayopata baada ya KUTOA kitu fulani chenye THAMANI katika maisha ya MTU fulani.

Hicho unachotoa hutegemeana na kitu ulichonacho.

Una ujuzi fulani, utautoa ujuzi huo na matokeo yake utayapata kulingana na tafsiri au mtazamo wako juu yake. Yaani kama unaamini mimi ni mtu wa IT na nakutengenezea security system ili unilipe pesa, maana yake ni kwamba ujuzi huo umeupa THAMANI ya pesa, japo unaweza lipwa kingine tofauti na pesa.


Kwa mfano huo, wapo wanaopata pesa kiulaini na wapo wanao angaika sana kuipata hiyo pesa.

Kutokana na uhitaji mkubwa wa pesa, zipo dhana nyingi zimejengwa kuhusu upatikanaji wake na ndiyo matokeo ya wengine kwenda kwa waganga na wengine kujiunga katika makundi fulani ili kuzipata.


Naomba nikupe jibu lako kwa mtazamo wangu na imani yangu.

Pesa haitafutwi. Pesa inakufuata wewe kutegemeana na THAMANI ya kile ulichonacho.

Wengi waliofanikiwa katika maisha ni wale waliotatua matatizo fulani ya watu katika jamii.

Wale watu walitumia muda na nguvu kufanyia kazi changamoto za watu au kundi fulani baada ya hapo walipata MATOKEO kulingana na THAMANI ya KITU walichokitoa kwa watu, ndiyo maana hapo mwanzo nimesema pesa ni MOJA ya MATOKEO.

Watu hao hawakupata pesa tu, kuna vingine vingi walipata kupitia kutatua changamoto hizo za watu, heshima, uwepo wao kutambulika na hata thamani ya kile walichonacho kupewa kipao mbele katika jamii husika.

Ukijua thamani yako, ukatambua uwezo halisi ulio nao, na ukaanza kutatua changamoto za watu katika jamii kwa kutumia uwezo wako binafsi pesa zitakufuata na hutokaa utafute pesa.


Sent from my E2333 using JamiiForums mobile app
 
Kuna mifumo imewekwa inayowazuia watu wengi kupata pesa kama unabisha angalia hatua zinazochukuliwa na Central bank hasa US,Australia, Japan nk kudhibiti infration
 
Pesa ni MOJA ya matokeo unayopata baada ya KUTOA kitu fulani chenye THAMANI katika maisha ya MTU fulani.

Hicho unachotoa hutegemeana na kitu ulichonacho.

Una ujuzi fulani, utautoa ujuzi huo na matokeo yake utayapata kulingana na tafsiri au mtazamo wako juu yake. Yaani kama unaamini mimi ni mtu wa IT na nakutengenezea security system ili unilipe pesa, maana yake ni kwamba ujuzi huo umeupa THAMANI ya pesa, japo unaweza lipwa kingine tofauti na pesa.


Kwa mfano huo, wapo wanaopata pesa kiulaini na wapo wanao angaika sana kuipata hiyo pesa.

Kutokana na uhitaji mkubwa wa pesa, zipo dhana nyingi zimejengwa kuhusu upatikanaji wake na ndiyo matokeo ya wengine kwenda kwa waganga na wengine kujiunga katika makundi fulani ili kuzipata.


Naomba nikupe jibu lako kwa mtazamo wangu na imani yangu.

Pesa haitafutwi. Pesa inakufuata wewe kutegemeana na THAMANI ya kile ulichonacho.

Wengi waliofanikiwa katika maisha ni wale waliotatua matatizo fulani ya watu katika jamii.

Wale watu walitumia muda na nguvu kufanyia kazi changamoto za watu au kundi fulani baada ya hapo walipata MATOKEO kulingana na THAMANI ya KITU walichokitoa kwa watu, ndiyo maana hapo mwanzo nimesema pesa ni MOJA ya MATOKEO.

Watu hao hawakupata pesa tu, kuna vingine vingi walipata kupitia kutatua changamoto hizo za watu, heshima, uwepo wao kutambulika na hata thamani ya kile walichonacho kupewa kipao mbele katika jamii husika.

Ukijua thamani yako, ukatambua uwezo halisi ulio nao, na ukaanza kutatua changamoto za watu katika jamii kwa kutumia uwezo wako binafsi pesa zitakufuata na hutokaa utafute pesa.


Sent from my E2333 using JamiiForums mobile app
Good! nimevutiwa sana na narrative yako.
 

AINA KUU TATU YA NJIA ZA KUTAFUTA PESA

Kuna njia kubwa tatu zilizotawala duniani, ambazo watu wanatumia kutafuta au kuzalisha pesa. Ili tuelewane vizuri, juu ya njia hizi, nitatumia majina matatu kwa lugha ya picha;

  1. Njia ya waenda kwa miguu
  2. Njia ya foleni (polepole)
  3. Njia ya mwendokasi

Kila moja ya njia hizi ina sifa, kanuni na taratibu zake, nimeamua kutumia lugha ya picha ili mtanzania mwenzangu unielewe kwa sababu njia hizo tatu (halisi) umeziona kwa macho yako, na inawezekana zote umewahi kuzipita, kuanzia ukiwa kwa mguu mpaka ukiwa umepanda chombo cha usafiri, lakini pia kwa mwendokasi.

Vigezo vinavyozitofautisha njia hizo tatu viko vitano(Machujio);

  1. Mahitaji ya njia hizo
  2. Namna ya uingiaji kwenye njia hizo
  3. Muda
  4. Uendeshaji wa maisha kwenye njia hizo
  5. Skeli (Ukubwa) wa njia hizo

Tunakwenda kuvitumia vigezo hivyo kwenye njia moja mpaka nyingine, taratibu ili tujifunze kwanini wapo matajiri wakubwa duniani, kama asilimia 1 tu ya watu wote, lakini wachache hao ndiyo wanaomiliki utajiri karibu asilimia 50 ya dunia nzima?



NJIA YA KWANZA: WATEMBEA KWA MGUU

Njia ya watembea kwa mguu ni njia inayoongoza kwa kuwa na watu wengi duniani. Watu hawa hawana, chombo chochote cha kusafiria, kuelekea kwenye ukwasi. Wao wanaamini kuwahi kwa mguu ni afadhali kuliko kusubiri muda mrefu inaweza ikawa miezi au miaka, ili kukiandaa chombo cha usafiri kuelekea utajiri.

Vyombo vya usafiri wa kuelekea kwenye ukwasi ni kama vile ajira au biashara. Ili mtu apate vyombo hivi ni lazima atumie muda mrefu kutafuta elimu na maarifa, pia awekeze nguvu zake na uvumilivu mwingi mpaka pale atakapopata chombo kinachoeleweka na kinachotembea. Hivyo basi unaweza kuona kuwa ni gharama kubwa inatumika mpaka mtu anakuja kupata ajira inayoeleweka au biashara inayoeleweka, inayoweza ikamsafirisha kwa miaka kadhaa mpaka anakuja kuufikia utajiri.

Watembea kwa mguu, hawataki kabisa habari za kujishugulisha; wanaogopa sana mchakato (process), bali siku zote wanataka matokeo (results), hasa kwa njia za short-cut.

Dalili 10 zinazoonesha kuwa uko kwenye njia ya watembea kwa mguu kwenye safari ya kuelekea kwenye ukwasi

  1. Unaanzisha vitu vingi iwe ni masomo au biashara lakini humalizi vitu hivyo au mambo yako mpaka mwisho.
  2. Unachojiuliza kichwani mwako ni “Njia gani rahisi ya kupiga pesa, itakayoniwezesha kulala maskini kuamka tajiri”
  3. Unataka kufanya kila kitu lakini, hakuna hata kimoja ulichobobea nacho. Vivyo hivyo kwenye kutoa hoja na michango, huwa unachangia hata kama hauna uelewa mzuri na wa kutosha wa masuala hayo.
  4. Uko tayari kuwasifia watu wakiwepo, lakini wakigeuza tu migongo yao unawasengenya
  5. Ni mwepesi sana kupokea kutoka kwa wengine, lakini kutoa kwako ni shughuli nzito
  6. Unalaumu sana serikali
  7. Unaamini kuwa ndugu, jamaa, mpenzi, wazazi au walezi, wanawajibika kabisa (kihalali) kukusaidia majukumu yako hata kama umefikia umri wa kujitegemea au una familia kabisa.
  8. Kuweka akiba kwako ni mtihani
  9. Ukipata tatizo hata dogo tu, mara nyingi unalaumu ‘Mungu’
  10. Malengo yako ni ya siku kwa siku, sidhani kama una malengo ya miezi, mwaka au muongo ujao.



Tukutane sehemu ijayo ili tuichuje, njia hii ya watembea kwa mguu kwa kutumia vigezo vyetu vitano, tulivyoviorodhesha hapo awali.
 
Pesa ni MOJA ya matokeo unayopata baada ya KUTOA kitu fulani chenye THAMANI katika maisha ya MTU fulani.

Hicho unachotoa hutegemeana na kitu ulichonacho.

Una ujuzi fulani, utautoa ujuzi huo na matokeo yake utayapata kulingana na tafsiri au mtazamo wako juu yake. Yaani kama unaamini mimi ni mtu wa IT na nakutengenezea security system ili unilipe pesa, maana yake ni kwamba ujuzi huo umeupa THAMANI ya pesa, japo unaweza lipwa kingine tofauti na pesa.


Kwa mfano huo, wapo wanaopata pesa kiulaini na wapo wanao angaika sana kuipata hiyo pesa.

Kutokana na uhitaji mkubwa wa pesa, zipo dhana nyingi zimejengwa kuhusu upatikanaji wake na ndiyo matokeo ya wengine kwenda kwa waganga na wengine kujiunga katika makundi fulani ili kuzipata.


Naomba nikupe jibu lako kwa mtazamo wangu na imani yangu.

Pesa haitafutwi. Pesa inakufuata wewe kutegemeana na THAMANI ya kile ulichonacho.

Wengi waliofanikiwa katika maisha ni wale waliotatua matatizo fulani ya watu katika jamii.

Wale watu walitumia muda na nguvu kufanyia kazi changamoto za watu au kundi fulani baada ya hapo walipata MATOKEO kulingana na THAMANI ya KITU walichokitoa kwa watu, ndiyo maana hapo mwanzo nimesema pesa ni MOJA ya MATOKEO.

Watu hao hawakupata pesa tu, kuna vingine vingi walipata kupitia kutatua changamoto hizo za watu, heshima, uwepo wao kutambulika na hata thamani ya kile walichonacho kupewa kipao mbele katika jamii husika.

Ukijua thamani yako, ukatambua uwezo halisi ulio nao, na ukaanza kutatua changamoto za watu katika jamii kwa kutumia uwezo wako binafsi pesa zitakufuata na hutokaa utafute pesa.


Sent from my E2333 using JamiiForums mobile app
Comment Bora kwangu
 
Sasa imekuwaje uarabun wamekubali mafuta yao yanunuliwe kwa dola.
 
Back
Top Bottom