Nini mantiki ya Dkt. Magufuli kuikumbatia sera ya ubaguzi wa kimaendeleo?

Nini mantiki ya Dkt. Magufuli kuikumbatia sera ya ubaguzi wa kimaendeleo?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
11,550
Reaction score
40,697
"Mimi niwaambieni ukweli, nimechoka kuwabembeleza ,mkiniletea madiwani na wabunge wa kutoka upande mwingine(wapinzani), siwaletei maji na huu ndiyo ukweli sipendi kuwaficha, nimechoka kuwabembeleza"
Magufuli (1/Oktoba/2020, Tunduma)


Hisia za ubaguzi wa kimaendeleo zilianza mara tu Rais Magufuli alivyoapishwa mwaka 2015 ambapo majimbo, mikoa na nyanda zilizomnyima kura zikaonekana kutengwa kimakusudi katika mipango ya kimaendeleo na utekelezaji wa kibajeti. Kadri muda ulivyozidi kusogea hisia zikaanza kuonekana kuwa ni kweli baada ya JPM mwenye kukiri hivyo (kwa majivuno) wakati akifanya ziara za kitaifa.

Na sasa sio siri tena hii ni mojawapo ya sera yake rasmi ya kuombea kura katika uchaguzi huu mkuu 2020, maana karibu kila mahali ambapo CCM ilipoteza Ubunge mwaka 2015 amekuwa akirudia kuyasema hayo hayo.

Sina uhakika kama hii ni sera rasmi ya CCM au kama ipo kwenye ilani yake ya uchaguzi 2020, lakini kwa kuwa inasemwa na mwenyekiti wa CCM huku viongozi na wanachama wake wakikaa kimya au kushangilia ina maana ni sera ya CCM.

Nini mantiki ya Magufuli kuikumbatia sera ya ubaguzi wa kimaendeleo ?
 
Ni hali ya Mtawala tu kutofuata Katiba ya Nchi kama alivyo apishwa kuifuata na kuilinda ,pamoja na Ujinga wa baadhi ya Wananchi-Watanzania kuendelea kukubali kuukumbatia Mfumo huu ulio undwa na uano endelea kuundwa wa Chama cha Mapinduzi CCM.

Kama Tanzania ingekuwa na Wananchi wenye maamuzi sahihi ,hii ni Sababu tosha ya kuikataa CCM kwa Hali na Mali ikibidi kwa kuvuja Damu.

Pemba 2001 wlaijitahidi sana hata Mh Mkapa (R.I.P.) alikiri kuzembea kwa Vifo vya hawa Binadamu ,kinyume na hapo tuta endelea kutawaliwa mpaka tukome.
 
Huo ndio wanauita ulevi wa madaraka. Akili ya huyu mtu ni kuwa anauchukulia uraisi kuwa kama ni biashara yake binafsi na wala siyo taasisi nyeti yenye dhamana ya kuongoza nchi.

Napata mashaka juu ya mtu huyu, kuwa anahitaji kwa nguvu zote "quorum" fulani ya namba ya wabunge bungeni ili apate kutimiza malengo yake binafsi yaliyojificha. Pengine anatamani apate kufanana na Kagame ama Museveni.
 
Sababu kuu ni hana Sera zaidi ya ubabe na vitisho,anafikiri watanzania wote ni ng'ombe wake wa kule Chato.

Kwanza uchaguzi wenyewe hashindi maana hapo anawahutubia wanafunzi wa chekechea,shule za msingi na sekendory waliosombwa kwa malori na mabasi ili waje kushuhudia tamasha la wasanii.
 
Na kodi wasilipe sasa,huu ujinga unataka kuota mizizi sasa maendeleo ya nchi ni matokeo ya kodi zetu
 
Huo ndio wanauita ulevi wa madaraka. Akili ya huyu mtu ni kuwa anauchukulia uraisi kuwa kama ni biashara yake binafsi na wala siyo taasisi nyeti yenye dhamana ya kuongoza nchi.

Napata mashaka juu ya mtu huyu, kuwa anahitaji kwa nguvu zote "quorum" fulani ya namba ya wabunge bungeni ili apate kutimiza malengo yake binafsi yaliyojificha. Pengine anatamani apate kufanana na Kagame ama Museveni.
Yaani kwa mtu kama huyu usitegemee upinzani ushinde hata wakipata 100% atageuza matokeo yote, watanzania tujiandae kutumia nguvu kupata haki yetu.
 
Yaani anavyoongea huyu mzee anathibitisha kabisa kwamba mikakati ya wizi wa kura ameshaikamilisha! Anaongea kama vile yeye hagombei, anaudharau sana uchaguzi ambao ni kipimo kikuu cha demokrasia, pia anatudharau sana sisi wapigakura.

Kwanza haeleweki! Mara apige magoti kuomba kura, mara afoke! Tabu tupu.
 
........................Mimi nadhani ingepitishwa sheria kuwapima akili kwa nguvu watake wasitake wagombea uongozi hasa kwa nafasi kubwa na nyeti kama za urais ili kujua back ground zao kiakili na kimaisha.

Vyovyote ilivyo huyu mzee kichwani siyo mzima hajatokea bado mtu mwenye ujasiri wa kusema maneno ya kipumbavu hadharani kama haya akawa timamu kichwani mwake japo kwa 65%,inajenga picha gani kwa hata viongozi wenzako majirani kusikia ukitamka haya?ndiyo hataki kuwe na mpinzani Tanzania ila alitakiwa akae kimya kisha aonyeshe kwenye vitendo siyo kufungua kinywa kuongea akasikika,kwani hajui au hatujui unafiki unavyofanya kazi jamani???

Nilikuwa sitaki kwenda kukaa foleni kupiga kura ila kwa huu ujinga unaondelea napandwa na hasira nitaenda kupiga kura ya kumkataa hata aki-force kupita nisiwe mmoja wa wale waliokubali kukumbatia umaskini huu wa akili.
 
Huyu hafai kushika madaraka makubwa kama haya kumbe Ngombale Mwiru (Rip) alikuwa na busara.

Utaongeaje ujinga kama huo kwa watu wanaolipa kodi, mbona usiache kukusanya kodi kwao. This is very stupid.

Kumbe ndio maana watu wanalipa kodi yeye anachukua kwenda kujengea kiwanja cha ndege kwao ilhali hata hiyo ndege kwa sababu za kiafya yeye huipanda mara chache tu.
 
Ni mbaguzi sana, Itoshe kusema Watanzania si tu kuwa tusichague wabunge na madiwani wa CCM, tuanze na yeye tuungane tumnyime kura ili nchi hisije kutumbukia katika ubaguzi mzito.
 
Amepotosha, unapowanyima watu maendeleo kwa msingi wa vyama wala huwafanyi wakupende au wakipende chama chako. Unawaongezea chuki tu dhidi yako ni kama walivyoamua kuwabinya upinzani wote kwa miaka mitano unafikiri ndio watu wamezidi kukipenda chama chake ?
 
Back
Top Bottom